Waislamu wazindua Jukwaa la KATIBA

"Chombo hicho ambacho tumekubaliana kitaitwa Jukwaa la Katiba la Waislamu, kitakuwa na jukumu la kuhakikisha Waislamu kote nchini wanakuwa na kauli moja juu ya masuala yanayohusu dini na maisha yao ambayo wangependa yawemo kwenye katiba mpya", alisema.

Hapo kwenye red inanipa tabu:-

Chombo hicho kitaitwa JUKWAA LA KATIBA LA WAISLAMU

Kitahakikisha Waislamu wanakuwa na kauli moja juu ya masuala yanyohusu DINI ambayo wangependa YAWEPO KWENYE KATIBA

Kitahakikisha Waislamu wanakuwa na kauli moja juu ya masuala yanyohusu MAISHA YAO ambayo wangependa YAWEPO KWENYE KATIBA

KATIBA inayozungumziwa hapa sio ya BAKWATA au Taasisi nyinge ya Kiislamu bali KATIBA YA NCHI. Ni lazima kuwa makini baadhi yetu wanapoanza kutaka DINI ZAO ziwepo kwenye KATIBA.

Kwenye suala la MAISHA kila mtu anahitaji maisha bora kwanini mjadala usijikite kwenye MAISHA YA WANANCHI WOTE badala ya MAISHA YA WAISLAMU TU? Nashindwa kuwaelewa hawa jamaa.
 
Acha kashfa za kidini, kama huna jema la kusema kaa pembeni, waislamu hatuhitaji hiyo special treatment kinachotakiwa ni chombo chenye kutoa miongozo sahihi kwa waumini, Bakwata ilianzishwa kwa nia njema tu lakini ukweli imeshindwa kutekeleza majukumu yake kama chombo, huu ni mwanzo mzuri tu, naamini waislamu wakieleshwa haki zao msingi mabadiliko makubwa ya kisiasa yatatokea Tanzania, kumbuka baadhi ya wanasiasa wetu wameanza kupandikiza chuki za kidini kwa maslahi yao binafsi.

Chama
Gongo la Mboto DSM.
Waislamu kupata chombo chenye kutoa miongozo sahihi kwa Tanzania hii hatutakuja kukiona mpaka tutakapo tangulia mbele ya haki ....labda Allah awashushie chombo hicho ndipo wote kwa pamoja mtaweza kufuata miongozo yake...sorry , hili jukwaa la katiba ni chombo kingine kinachoongeza chaos zaidi kwenye utitiri wa vyombo vingi vinavyowakilisha makundi makundi tu ya waislam badala ya waislam wote kitaifa.
 
Waislamu kupata chombo chenye kutoa miongozo sahihi kwa Tanzania hii hatutakuja kukiona mpaka tutakapo tangulia mbele ya haki ....labda Allah awashushie chombo hicho ndipo wote kwa pamoja mtaweza kufuata miongozo yake...sorry , hili jukwaa la katiba ni chombo kingine kinachoongeza chaos zaidi kwenye utitiri wa vyombo vingi vinavyowakilisha makundi makundi tu ya waislam badala ya waislam wote kitaifa.

Mkuu bandiko lako likiangaliwa kwa jicho makini ni kama lina ka-ukweli fulani vile. Tatizo kuu ninaloliona kwa hawa ndugu zetu ni UBAGUZI dhidi ya wasio waislamu; yaani too much u-sisi. Laiti kwenye mijadala yao hasa inayohusu maslahi ya kitaifa ingelenga utaifa (wananchi wote) zaidi badala ya wao tu. Fikiria kitu kama MAISHA eti watajadili MAISHA (bora) YA WAISLAMU na siyo ya WATANZANIA WOTE yaweje kwenye KATIBA MPYA.

Inasikitisha kwamba kwao katika masuala ya kawaida na ya msingi ya kila mwananchi kuna mwislamu na asiye mwislamu; inasikitisha sana. Dhambi ya UBAGUZI ni mbaya mno.
 
hapa lazima MOU iondoke ndani ya katiba
Wishful thinking. Imagine serikali irudishe vyuo,hospitali, visima nk kwa kanisa ili kanisa liviendeshe lenyewe....na nyinyi mrudishe yale majengo ya tanesco ya kile chuo chenu cha Kiislam Morogoro...unafikiri ni nani atakaye umia zaidi? Unafikiri serikali itaweza kuziba kwa haraka hilo pengo la huduma za jamii zitakazo rudishwa chini ya kanisa? Hizo ndoto zako za MOU kundoka ni kama vile kukata mbuyu mkubwa kwa kutumia kiwembe kidogo...mwisho wa siku utajichanja tu mwenyewe.
 
Waislam wako wengi kuliko wakristu TZ, lakini wanavyolalama, utasea ni minority:(

Hivi kama hiyo MOU ikifutwa, ndiyo itaondoa matatizo yote ya Waislamu nchini?
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Ngoja tuone.Ila nawashauri waislam mtumie busara na hekima ya hali ya juu sana katika hili mnalotaka kufanya. Naomba msikurupuke kabisa jaribu kutumia wataalam wenu hasa wanasheria katika hili. Angalieni mwisho wa siku msije mkaumbuka.
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Hawa waislamu walishangilia sana wakati JK anasaini hiyo sheria ya marekebisho ya katiba,
wakifikiri wanaikomoa CDM. Matokeo ya kushangilia DHAMBI sasa itaanza kuwatafuna wao.

Sheria aliyoisani JK hairuhusu, NGOs, vyama vya kiraia, vyama vya Siasa, vyama vya kidini,
etc kuandaa makongamano ya katiba mpya. Ukifanya hivyo ni kosa la jinai na adhabu yake
imeaanishwa kwenye sheria hiyo, fani 5 mil(?), kifungo mwaka mmoja(?) jela au vyote viwili kwa pamoja.

Hayo ndiyo matokeo ya kushangilia DHAMBI. Ninajua serikali inaweza kuwafumbia macho
hao waislamu kwasababu inafahamu from the word GO ajenda zao ni Mahakama ya kadhi,
Tanzania kujiunga na OIC na Serikali inawapendelea wakiristu, Ubalozi wa Vatican Tanzania etc.
Madai kama hayo kulingana na sheria aliyosaini JK anaweza kuyaweka kapuni bila hata kuyasoma
na asiulizwe ni mtu because he is ALPHA & OMEGA.
 
  • Kukutana Diamond Ijumaa
  • Mikoa Yote Nchini Kushiriki
  • Abas Syskes, Masheikh Kuunguruma
Gazeti la LULU la leo Jumanne - 03 Januari 2012 linaripoti:

Kongamano la Kitaifa la Uzinduzi wa Jukwaa la Katiba la Waislamu nchini linatarajiwa kufanyika Ijumaa ya wiki hii katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Habari za kuaminikia ..... zinafahamisha kuwa, kongamano hilo la siku moja linaloelezwa kuwa la kihistoria litafunguliwa na Abbas Syskes ambaye amewahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini, ...

Pia wanasheria, masheikh mbalimbali wa jijini Dar es Salaam na vitongoji vyake, pamoja na ujumbe kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na visiwani watashiriki.

Akithibistihs habari hizo, ...., Sheikh Ponda Issa Ponda, alisema hatua zote za maandalizi ya shughuli hiyo zimekamilika. ...

Akizungumzia maudhui ya kongamano hilo, Sheikh Ponda alisema kuwa ni pamoja na kuzindua rasmi chombo kitakachojishughulisha na utoaji elimu ya katiba kwa jamii ya Waislamu nchini.

"Chombo hicho ambacho tumekubaliana kitaitwa Jukwaa la Katiba la Waislamu, kitakuwa na jukumu la kuhakikisha Waislamu kote nchini wanakuwa na kauli moja juu ya masuala yanayohusu dini na maisha yao amabayo wangependa yawemo kwenye katiba mpya", alisema.

Akifafanua namna Jukwaa hilo litakavyofanya kazi hiyo, Sheikh Ponda alisema kuwa, kabla ya kutazama yanayohitajika kuwemo kwenye katiba mpya, watatangulia kutoa elimu juu ya katiba ya sasa ...

"Baada ya hapo ndipo Jukwaa litaketi na kutafakari kwa kina mahitajio ya waislamu tunayodhani ni muhimu yakaainishwa ndani ya katiba ya nchi", alizungumza Sheikh Ponda.

...


Wakuu kwa muhtasari ni hayo - full stori, tafadhali pata nakala yako ya LULU.



Bravo MUSLIMS
 
Waislam wako wengi kuliko wakristu TZ, lakini wanavyolalama, utasea ni minority:(

Hivi kama hiyo MOU ikifutwa, ndiyo itaondoa matatizo yote ya Waislamu nchini?

hawako wengi mkuu jumla yao ni milion 13 na usheh kati ya watu 42 milioni
 
Hawa waislamu walishangilia sana wakati JK anasaini hiyo sheria ya marekebisho ya katiba,
wakifikiri wanaikomoa CDM. Matokeo ya kushangilia DHAMBI sasa itaanza kuwatafuna wao.

Sheria aliyoisani JK hairuhusu, NGOs, vyama vya kiraia, vyama vya Siasa, vyama vya kidini,
etc kuandaa makongamano ya katiba mpya. Ukifanya hivyo ni kosa la jinai na adhabu yake
imeaanishwa kwenye sheria hiyo, fani 5 mil(?), kifungo mwaka mmoja(?) jela au vyote viwili kwa pamoja.

Hayo ndiyo matokeo ya kushangilia DHAMBI. Ninajua serikali inaweza kuwafumbia macho
hao waislamu kwasababu inafahamu from the word GO ajenda zao ni Mahakama ya kadhi,
Tanzania kujiunga na OIC na Serikali inawapendelea wakiristu, Ubalozi wa Vatican Tanzania etc.
Madai kama hayo kulingana na sheria aliyosaini JK anaweza kuyaweka kapuni bila hata kuyasoma
na asiulizwe ni mtu because he is ALPHA & OMEGA.
Nadhani hata JK alishawahi kuwahimiza viongozi wa dini pamoja na waumini wao kutoa mchango wao kwenye katiba mpya ila wasiingize mambo ya dini maana yataleta mafarakano...sasa wenzetu sijui wanatumia viungo gani vya mwili kufikiria!?
 
Sheikh Ponda asituletee matatizo, kauli zake mara kwa mara ni kama BOKO HARAM

Naam! Unajua maana ya Boko Haram? Kwa asiyejua maana yake ni neno la Kihausa (Hausa ni kabila fulani linalopatikana zaidi huko Kaskazini mwa Nigeria) lenye maana hii:

Boko - Elimu ya Magharibi
Haram - Haramu

Hivyo Boko Haram = Elimu ya Magharibi Haramu.
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Hawa waislamu walishangilia sana wakati JK anasaini hiyo sheria ya marekebisho ya katiba,
wakifikiri wanaikomoa CDM. Matokeo ya kushangilia DHAMBI sasa itaanza kuwatafuna wao.

Sheria aliyoisani JK hairuhusu, NGOs, vyama vya kiraia, vyama vya Siasa, vyama vya kidini,
etc kuandaa makongamano ya katiba mpya. Ukifanya hivyo ni kosa la jinai na adhabu yake
imeaanishwa kwenye sheria hiyo, fani 5 mil(?), kifungo mwaka mmoja(?) jela au vyote viwili kwa pamoja.

Hayo ndiyo matokeo ya kushangilia DHAMBI. Ninajua serikali inaweza kuwafumbia macho
hao waislamu kwasababu inafahamu from the word GO ajenda zao ni Mahakama ya kadhi,
Tanzania kujiunga na OIC na Serikali inawapendelea wakiristu, Ubalozi wa Vatican Tanzania etc.
Madai kama hayo kulingana na sheria aliyosaini JK anaweza kuyaweka kapuni bila hata kuyasoma
na asiulizwe ni mtu because he is ALPHA & OMEGA.

Kaka tafadhali usiseme mambo usiyoyajua waisilamu wangapi unajua tulishangilia hiyo kitu au

ni kikundi gani kwa mfano unachokijua kilishangilia....ndugu acha udini utatumaliza.
 
Wataalam mbali mbali, very good. Naunga mkono 100%. Nachotia shaka ni msimamo wa Waislamu, je wanapenda maoni ya watu wengine, hususan wataalam? Hotuba ya Mh.Dokta pale Masjid Gadaffi, kwenye baraza la idi iligusia jambo moja la mahakama ya kadhi na hapo nilisikia Mh.Dokta akiongelea ushiriki wa Prof....(simkumbuki jina) ambaye ni mtaalamu wa sheria na sharia. Hilo waislamu hawakulipenda na ndio hasa msingi wa kufanywa kongamano hili ambalo dhahiri litaendeshwa kwa hisia na si hali halisi.

Mimi nachoona hapa ni kama wanataka kuwa wa kwanza kuhukumiwa na sheria ambayo waliishangilia juzi juzi tu hapa iliposainiwa na Mh.Dokta. Unaposhangilia mvua milimani kumbuka maji huelekea bondeni, sasa tuliodhani itawabana CDM kufanya harakati sasa ndio tuone ugumu wa kuchekelea dhambi.

Na mwisho nikukosoe kidogo (hapo kwenye red). Nature ya Uislamu ni kinyume kabisa na maoni yako. Utanibishia kisiasa au kwa kuchelea usionekane mbaya lkn ukweli hubakia kuwa ukweli. Soma Quran 9:5

Ofcourse waislam wanakubali ushauri wa watu wengine kwani kawaida ya ushauri hua unakubalika au kukatalika. Usijaribu kubadilisha malengo ya kongamano kwa dhana yako binafsi kwani malengo ya kongamano yametajwa kwa ufasaha kabisa.

Umejaribu kukosoa kua nature ya uislam sio amani na badala yake ukaleta Quran 9:5 Nimejaribu kuulizia kwa wataalam maana ya hizo verse nikafahamishw kua zilishushwa ktk mazingira maalum. Kwahiy kama unaona mazingira hayo yapo Tz basi ni wewe kuamua.

Au unataka democrasia ya Cameron na capitalism ya europe. Wacha waislam wapange mambo yao kwani hilo halina maslahi kwa Tanzania tu bali kwa dunia.
 
nawapongeza waislamu kwa hatua hii thabiti walioichukua, maana ni jukumu lao pia katika kuisaidia serikali kwenye suala zima la kupata katiba mpya.
ila tu natoa angalizo, mkutano huu uwe kweli wa kujadili katiba na kutafuta suluhisho hasa kwa matatizo ya nchi na yale ambayo yanawasumbua waislamu kwa ujumla ambayo wangependa serikali iyashughulikie ikiwa tu hayaingilii uhuru wa dini nyingine, naomba mkutano huu usiwe wa kuwanyooshea vidole watu wengine wa imani tofauti, mana unaweka kukuta mada ni katiba lakini yatajkayozungumzwa ni ya ukristu, pengo au kakobe kupendelewa na serikali. ikiwa hivo hilo lengo lenu litakuwa halijatimia
ila kama kweli itakuwa ni juu ya katiba ni vizuri.. pia kama ninyi mnafanya hivi, kesho au keshokutwa mkisikia wakristu wanafanya sawa nanyi basi yasitoke yale maneno au malalamiko ya kusema wanaiongoza serikali au wanaiamrisha serikali, wanaipangia serikali, kumbukeni nao wanayo haki kama ninyi.
My take: kama waislamu wataendelea na utamaduni huu wa kuandaa utamaduni chanya wa kuyatazama mambo ya msingi kwa taifa kama wanavyokusudia basi kwa hakika watapiga hatua kubwa, mi nadhani ile dhana ya kuwanyooshea vidole wengine saizi ingewekwa pembeni nanyi ndugu zetu, sasa ni wakati wa kujitazama nyinyi kama nyinyi na serikali yetu.
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Back
Top Bottom