dudus
JF-Expert Member
- Feb 28, 2011
- 22,126
- 49,384
- Kukutana Diamond Ijumaa
- Mikoa Yote Nchini Kushiriki
- Abas Syskes, Masheikh Kuunguruma
Kongamano la Kitaifa la Uzinduzi wa Jukwaa la Katiba la Waislamu nchini linatarajiwa kufanyika Ijumaa ya wiki hii katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Habari za kuaminikia ..... zinafahamisha kuwa, kongamano hilo la siku moja linaloelezwa kuwa la kihistoria litafunguliwa na Abbas Syskes ambaye amewahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini, ...
Pia wanasheria, masheikh mbalimbali wa jijini Dar es Salaam na vitongoji vyake, pamoja na ujumbe kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na visiwani watashiriki.
Akithibistihs habari hizo, ...., Sheikh Ponda Issa Ponda, alisema hatua zote za maandalizi ya shughuli hiyo zimekamilika. ...
Akizungumzia maudhui ya kongamano hilo, Sheikh Ponda alisema kuwa ni pamoja na kuzindua rasmi chombo kitakachojishughulisha na utoaji elimu ya katiba kwa jamii ya Waislamu nchini.
"Chombo hicho ambacho tumekubaliana kitaitwa Jukwaa la Katiba la Waislamu, kitakuwa na jukumu la kuhakikisha Waislamu kote nchini wanakuwa na kauli moja juu ya masuala yanayohusu dini na maisha yao amabayo wangependa yawemo kwenye katiba mpya", alisema.
Akifafanua namna Jukwaa hilo litakavyofanya kazi hiyo, Sheikh Ponda alisema kuwa, kabla ya kutazama yanayohitajika kuwemo kwenye katiba mpya, watatangulia kutoa elimu juu ya katiba ya sasa ...
"Baada ya hapo ndipo Jukwaa litaketi na kutafakari kwa kina mahitajio ya waislamu tunayodhani ni muhimu yakaainishwa ndani ya katiba ya nchi", alizungumza Sheikh Ponda.
...
Wakuu kwa muhtasari ni hayo - full stori, tafadhali pata nakala yako ya LULU.