Baija Bolobi
JF-Expert Member
- Feb 25, 2009
- 1,093
- 1,726
Serikali imelifungia gazeti la MWANAHALISI. Wiki hiyo hiyo Rais Kikwete akawaalika wahariri kwenda kuongea nao Ikulu. Akawaagiza waandike maswali na kuyatuma mapema. Wakatii na kuyatuma. Orodha ya waalikwa ikachambuliwa. Ni sawa na kusema, ili uwe mhariri ni lazima ikulu ikubali kuwa wewe ndiye mhariri. Haya tuyaweke pembeni, tujikumbushe yaliyowahi au kutabiriwa/ kusemwa kuhusu waandishi wa Tanzania.
-Kwamba, ni wavivu wa kufikiri
-Kwamba, hawajui kuuliza maswali ya maana,
-Kwamba, hawajui kufanya uchunguzi na kuandika vizuri habari za uchunguzi,
-Kwamba, ni "vijibwa" vya watawala na wenye fedha,
-Kwamba, ni "makanjanja" wanaochafua tasnia ya habari, n.k.
Kwa kitendo cha wahariri kutii kwenda Ikulu na kukubali kuandaa maswali na kuyatuma mapema, wakati gazeti mojawapo limefungiwa kibabe, kimewadhalilisha sana wahariri wetu. Kimedhihirisha kwa dhati kuwa waandishi hawana umoja wala mshikamano na kwa hiyo ni ruksa kwa dola kuwafanyia itakavyo.
Hata katika nchi zilizoendelea, marais na viongozi wa nchi hizo, wakiitisha mikutano na wahariri au waandishi, huwapa uhuru wa kuulizwa maswali hata kama wanaweza kufanya mbinu ya kuwainua na kuwapa fursa ya kuuliza wale ambao hurusha "friendly fire" kwa watawala. Huu utaratibu wa wahariri wetu kukubali "kuandikiana barua za mapenzi" na rais ukome maana unaidhalilisha tasnia ya habari. Kama rais anataka maswali yaliyoandikwa, basi na yeye ajibu kwa maandishi na awatumie waliouliza.
Kukosekana kwa umoja na mshikamano miongoni mwenu, kunawafanya muishi kwa matumaini ya kuteuliwa ua kuingia katika siasa ili muendeleze michezo michafu mnayoipiga hivi sasa mkiwa mmevaa glovu. Jamani mnashindwa kumwuliza Rais, ikiwa serikali haikumteka Dr. Ulimboka kwa nini haichunguzi utekaji huo? Mnakubaliana na kujiumauma kwake kuwa "maneno yako mengi na yataendelea kuwapo"!
MMENISIKITISHA SANA.
-Kwamba, ni wavivu wa kufikiri
-Kwamba, hawajui kuuliza maswali ya maana,
-Kwamba, hawajui kufanya uchunguzi na kuandika vizuri habari za uchunguzi,
-Kwamba, ni "vijibwa" vya watawala na wenye fedha,
-Kwamba, ni "makanjanja" wanaochafua tasnia ya habari, n.k.
Kwa kitendo cha wahariri kutii kwenda Ikulu na kukubali kuandaa maswali na kuyatuma mapema, wakati gazeti mojawapo limefungiwa kibabe, kimewadhalilisha sana wahariri wetu. Kimedhihirisha kwa dhati kuwa waandishi hawana umoja wala mshikamano na kwa hiyo ni ruksa kwa dola kuwafanyia itakavyo.
Hata katika nchi zilizoendelea, marais na viongozi wa nchi hizo, wakiitisha mikutano na wahariri au waandishi, huwapa uhuru wa kuulizwa maswali hata kama wanaweza kufanya mbinu ya kuwainua na kuwapa fursa ya kuuliza wale ambao hurusha "friendly fire" kwa watawala. Huu utaratibu wa wahariri wetu kukubali "kuandikiana barua za mapenzi" na rais ukome maana unaidhalilisha tasnia ya habari. Kama rais anataka maswali yaliyoandikwa, basi na yeye ajibu kwa maandishi na awatumie waliouliza.
Kukosekana kwa umoja na mshikamano miongoni mwenu, kunawafanya muishi kwa matumaini ya kuteuliwa ua kuingia katika siasa ili muendeleze michezo michafu mnayoipiga hivi sasa mkiwa mmevaa glovu. Jamani mnashindwa kumwuliza Rais, ikiwa serikali haikumteka Dr. Ulimboka kwa nini haichunguzi utekaji huo? Mnakubaliana na kujiumauma kwake kuwa "maneno yako mengi na yataendelea kuwapo"!
MMENISIKITISHA SANA.