SAGAI GALGANO
JF-Expert Member
- Nov 13, 2009
- 43,707
- 60,766
Jana tumeshudia mapovu mithili ya watu waliofakamia omo toka vinnywani wa wahafidhina wa CCM. Tuliaminishwa kuwa kikao cha bunge siku ya tarehe 10 June ni mahsusi kwa kujadili na kuelemisha umma juu sintofahamu iliyojitokeza juu ya mchakato wa ubinafsishaji wa bandari zetu.
Lakini kwa mshangao wa wengi mada kubwa ilikuwa ni kumshambulia Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe kanakwamba yeye amehusika kuandika waraka uliokuwa mezani kujadiliwa. Matusi, kashfa na kejeli nyingi zilielekezwa kwake binafsi na uhusika wake kwa maridhiano yanayoendela kati ya CCM na Chadema.
Ukweli lugha iliyokuwa inatumika ilikuwa ni tafsida tu ya kumnanga Rais Samia kuwa kiko wapi sasa ulichopata kufanya muafaka na wahuni.
Kwa muda mrefu kulikuwa na minong'ono ya wahafidhina wa CCM kuponda maridhiano hayo sasa jana ilikuwa golden chance ya kumpiga mawe Mweyekiti wao kwa kutumia mgongo wa Freeman Mbowe.
Kama kweli Samia alikuwa na dhamira ya kweli ya kuleta muafaka wa kisiasa basi atawaapuuza wahafidhina hawa wakiongizwa na Nape Nnauye kwani maridhiano hayakuwa na kipengele cha kutokosoa mapungufu ya serikali ya CCM.
Lakini kwa mshangao wa wengi mada kubwa ilikuwa ni kumshambulia Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe kanakwamba yeye amehusika kuandika waraka uliokuwa mezani kujadiliwa. Matusi, kashfa na kejeli nyingi zilielekezwa kwake binafsi na uhusika wake kwa maridhiano yanayoendela kati ya CCM na Chadema.
Ukweli lugha iliyokuwa inatumika ilikuwa ni tafsida tu ya kumnanga Rais Samia kuwa kiko wapi sasa ulichopata kufanya muafaka na wahuni.
Kwa muda mrefu kulikuwa na minong'ono ya wahafidhina wa CCM kuponda maridhiano hayo sasa jana ilikuwa golden chance ya kumpiga mawe Mweyekiti wao kwa kutumia mgongo wa Freeman Mbowe.
Kama kweli Samia alikuwa na dhamira ya kweli ya kuleta muafaka wa kisiasa basi atawaapuuza wahafidhina hawa wakiongizwa na Nape Nnauye kwani maridhiano hayakuwa na kipengele cha kutokosoa mapungufu ya serikali ya CCM.