Wafanya biashara wawili maarufu wakamatwa kwa tuhuma za kutumia viungo vya maalbino

Unaweza kukopi na kupaste hapa?

SAKATA la ununuzi wa viungo vya ulemavu wa gozi 'albino' jijini limechukua sura mpya baada ya wafanyabiashara maarufu jijini kunaswa na Polisi kwa tuhuma za kujihusisha na biashara hiyo akiwemo mganga wa kienyeji na kufanya idadi ya waliokamatwa kuwa watano.

Sakata hilo la kunusurika kutekwa watoto wawili wa familia moja Irine Stanclaus (10) na Gerald Stanclaus (4) wakazi wa Kipawa, jijini ambapo walinusurikwa kupelekwa kusikojulikana na watu wawili waliokamatwa ambao ni Juma Anthony Ndaigwa (26), mkazi wa Magomeni Makuti na Juma Mgai (21) 'Juma Chibuku', mkazi wa Msasani Macho.

Watuhumiwa hao walikiri kushiriki kwenye matukio mbalimbali ya mauaji yaliyotokea ufukweni mwa habari ya Hindi, Morogoro, Kigamboni na Tandale.

Watuhumiwa wengine wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi ni mganga wa kienyeji, Kulwa Herman mkazi wa Mbezi Matangini, Dar es Salaam, wafanyabiashara maarufu wanaofahamika kwa majina Ndama Mtoto wa ng'ombe na Juma Ally 'Kizaizai'.

Kukamatwa kwa watuhumiwa hao ni kutokana na juhudi za polisi kufanya msako mkali kutokana na watuhumiwa kuwataja wanaoshirikiana nao kwenye suala la biashara ya viungo vya albino.

Habari kutoka vyanzo vyetu zinaeleza kuwa, hadi sasa idadi ya waliokamatwa kuhusiana na tuhuma za kushiriki kwenye biashara hiyo ni watano.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile alisema juzi kuwa, jeshi lake linaendelea na juhudi za kuhakikisha kuwa wale wote wanaojihusisha na biashara hiyo wanakamatwa.

Alisema kazi ya kuwakamata watuhumiwa imekuwa ngumu kutokana na watuhumiwa kukimbia nyumba zao hata hivyo juhudi zinafanywa kwa kushirikiana na wasamaria wema ili kuweza kupata taarifa walipokimbilia.

"Biashara hiyo imeingia Dar es Salaam hivyo tutashirikiana kuhakikisha wale wote wanaojihusisha na biashara hiyo wanakamatwa, " alisema Shilogile.

Mama wa watoto hao Evodia Stanclaus alisema alipata taarifa za watoto wake kuwindwa na watu wawili waliokuwa wakirandaranda katika maeneo ya nyumbani kwake wakijifanya kutafuta simu ya mkononi yenye kamera.

Hata hivyo kwa ushirikiano na wananchi waliweza kuwakamata watuhumiwa hao baada ya jirani yake kusikia njama hizo zikipangwa kwenye simu ya mkononi na vijana hao kupitia dirishani na kutoa taarifa za siri kwa majirani wenzake.

Baada ya kuwekwa chini ya ulinzi na kupata kipigo kikali vijana hao waliweza kuokolewa na polisi waliofika eneo la tukio.

Katika operesheni hiyo tayari mfanyabiashara anayesadikiwa kuwa ni raia wa Burundi mwenye asili ya Kiarabu anashikiliwa na polisi wakiwemo watu wengine watatu kutoka maeneo ya Kimara, Ubungo na Magomeni jijini.
 
Hii habari ya kusikitisha sana. Inawezekana kabisa inahusisha wafanyabiashara wengi wakubwa. Huwa nashangaa sana watu wanatoa wapi hela za kugawa kwa band nzima kila weekend. Ningeshauri wanyofolewe nyeti zao then waachiwe.
 
wakulu,
kwa habari nilizo zipata muda huu huu,
Mkulu Ndama Shaaban na mwenzie KIzai zai wameachiwa na polisi kwa dhamana.
lakini hii stori ni zaidi ya hapa,tuwape pole wenzetu
 
wakulu,
kwa habari nilizo zipata muda huu huu,
Mkulu Ndama Shaaban na mwenzie KIzai zai wameachiwa na polisi kwa dhamana.
lakini hii stori ni zaidi ya hapa,tuwape pole wenzetu
Yaani wauwaji wanaachiwa kwa dhamana? Mtu anayepanga kuua hatakiwi kuachwa anatakiwa akae ndani tuu. Waandishi wa habari itabidi wafuatilie hii kitu na kuiweka hadharani.
 
Waua albino kibao wadakwa

2008-12-06 16:34:11
Na Badru Kimwaga, Jijini


Zaidi ya watu 57 wakiwemo waganga wa jadi na wafanyabiashara wa madini na uvuvi wamenaswa na kufunguliwa mashtaka kuhusiana na tuhuma za kuhusika na mauaji ya albino katika maeneo tofauti nchini.

Watuhumiwa hao wamedakwa katika jumla ya mikoa sita baada ya polisi kufanya msako mkali dhidi ya wahusika wa vitendo hivyo.

Mdhibiti Mkuu wa kitengo cha makosa dhidi ya wanadamu, Bi. Sidney Mkumbi, ametoa taarifa hiyo jana kupitia kipindi cha `Kipima Joto` kilichorushwa `live` na kituo cha ITV jana.

Akadai wengi wa watuhumiwa hao wanatoka katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Bi. Mkumbi amesema watuhumiwa hao wakiwemo wafanyabiashara ya uvuvi, madini na wengine wanaosaka utajiri kwa nguvu za giza, wamedakwa katika mikoa inayosifika kwa mauaji ya aina hiyo ya Mwanza, Shinyanga, Mara, Kigoma, Kagera na Mbeya.

``Watu wengi wanadhani sisi hatufanyi kazi dhidi ya matukio haya ya kikatili, juhudi zipo na mafanikio yake ni kukamatwa kwa watu zaidi ya 57 wakiwemo wafanyabiashara 13 miongoni mwao watano walikutwa na viungo vya binadamu amabvyo bado havijathibitishwa kama ni vya maalbino au la,`` amesema.

Akiungwa mkono na Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Kamishna Peter Kivuyo na msemaji wa jeshi la polisi nchini, Bw. Abdallah Msika, Bi. Mkumbi amesema jeshi lao liko bize katika kuhakikisha mauaji ya maalbino yanakoma nchini na kwamba sasa, wameongeza nguvu kwa kufanya upelelezi wao kimyakimya ili kutowastua wengine.

Makamanda hao wa Polisi wakasema jambo la muhimu ni kwa kila mmoja kuwa tayari kushirikiana na jeshi lao kwa kuwapa taarifa zitakazowasaidia katika kuwanasa wauaji hao.

SOURCE: Alasiri
NB: Mhe Masha ilibidi habari kama hizi ndio unazitoa wewe ili uonekane hata at least unafanya kazi, "Kalaghabaho!"
 
Hivi kweli anahusika na tuhuma za kuua maAALBINO au ndio kasingiziwa?

Kama sele-briti huyu kafikia huku basi NOMA!

mwenzie TALL je?
 
From what i heard ,GT those guys are aren't even close,baada ya kaupepo mbaya kupita kati yao so HAWAWEZI KUKAA PAMOJA KUSHIRIKIANA KWENYE ISSUE KUBWA KAMA HIYO.
LKabda kuna watu wanajaribu kuwa-frame kwa kitu ambacho hawajafanya.
 
Back
Top Bottom