Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
WABUNGE 3 (CCM) WALIOISALITI BAJETI YA SERIKALI YAO
KWA MANUFAA YA WAPIGA KURA WAO.
Kinyongo cha serikali ya CCM kubana bajeti ya maendeleo majimbo ya wabunge machachari wanaoinyoshea vidole serikali ili iwe na ari ya uwajibikaji ni dalili tosha ya CCM kuishiwa pumzi, na kwamba sikio la kufa halisikii dawa. Hakuna ajabu wengi wako mguu pande kwa sasa kusubiria muda ufike, kwani ukombozi wa vyombo mahsusi kama hivyo ni kuyakumboa majimbo yao. Tunajua fika hawa walivyozikonga nyoyo za wapiga kura wao na baadhi kusema kokote mbuge wetu utakakoamua kwenda tutakufuata tu maana yake mbunge huyu akiamua kwenda anakoona kunamfaa ataenda na wapiga kura wake.
Mchezo wa karata za siasa Tanzania ndo unazidi kukomaa. Wenye kuendekeza kujikomba kwa chama na serikalini ni wale wenye mwono mfupi sana, kwani wenye upeo mkubwa wapo kwa wananchi waliowapigia kura, kwani chama na serikali vitapita lakini wapiga kura watabaki wale wale wenye kuunda chama wakitakacho na serikali wanayoiridhia.