Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,893
- 16,319
Habari zenu jamiiforums
Kwa wale msiomfahamu vema Infantry Soldier ni kwamba, mimi ni mkristo tena mkatoliki ila ninafahamu fika ya kuwa uislamu si ugaidi na si dini ya wizi na wala waislamu si magaidi na wala sio wezi bali wahalifu wachache hujificha katika kivuli cha uislamu ili kutenda uhalifu wao.
Dini ya uislamu ni dini safi sana tena ya watu waungwana kweli inayohubiri amani na upendo kama ilivyo dini ya kikristo. I love and respect all my muslim brothers and sisters out there.
Tanzania ililazimika kupigana vita ya Kagera mwaka 1978 kwa lengo la kuikomboa ardhi yetu na kumtoa nduli Idd Amin Dada na genge la wahuni wenzie. Uamuzi wa kuivamia ardhi ya mkoa wa ziwa Magharibi (Kagera) haukuwa na ridhaa ya waganda hata kidogo bali ni maamuzi ya kipuuzi na kichokozi yaliyofanywa utawala wa kidhalimu wa dikteta Amini dada.
Kwanini uhalifu alioufanya Salum Yusuph wa kwenda kuiba nguruwe uhusishwe na nafasi ya ungozi wa kidini (Imam) ilhali kitendo hicho (wizi) sio muongozo sahihi wa dini ya kiislam? Je, hii ni sahihi? Je, haya ndio maadili ya taaluma ya uandishi wa habari?
Je, mnafahamu kuwa vyombo vya habari visipotumika ipasavyo vinaweza kuleta vurugu za kidini au hata kikabila ndani ya jamii ya watanzania? Mmesahau yaliyotokea nchini Rwanda mwaka 1994? Leo hii mmesahau yaliyotokea nchini Kenya mwaka 2007? Ni njia zipi zilitumika katika kusambaza chuki kama sio vyombo vya habari?
Kulingana na Quran Tukufu, wizi umekatazwa katika Uislamu na ni dhambi kubwa sana. Inachukuliwa pia kuwa ni Haraam kulingana na maneno ya mtume Muhammad (SAW - peace be upon him). Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema amelaani wizi na ameamuru adhabu ya kisheria kupitia sheria ya Kiislam (Sharee’ah) kwa mwizi ni kukata mkono wa wake.
Mimi Infantry Soldier kabila langu ni mjaluo. Endapo itakuja siku moja kuonekana nimetoka msalani pasipo kunawa kabisa na kwenda moja kwa moja kwenye meza ya chakula kwa ajili ya kujiandaa na kula, Je itakuwa ni sahihi kusema kwamba, wajaluo wana tabia ya kula pasipo kunawa wakitoka msalani? Je, ni sahihi kutumia uovu wa mmtu mmoja katika kuhukumu wengine wa jamii yake?
Kabla ya mtu kufanya uhalifu, huwa anapanga kwanza mikakati kichwani mwake. Kitendo cha kupanga mikakati ovu kichwani tayari kinatosha kumvua mtu nafasi aliyonayo katika dini hata kabla hajatenda uovu husika.
Kitendo cha Imam mstaafu kupanga kuiba nguruwe kinamvua wadhifa ule hata kabla hajatenda tukio hilo la wizi. Alitenda tukio la wizi akiwa sio Imam tena kwa maana dini inakataza mtu wa hadhi yake kuwaza kutenda uovu wa namna ile.
Ninatambua na kuheshimu mchango wa wanataaluma wa tasnia ya habari katika kujenga jamii yenye umoja na mshikamano, lakini katika hili la uchochezi wa kidini ni lazima tulikemee sote kwa pamoja.
Maoni ya wadau;
==========
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Kwa wale msiomfahamu vema Infantry Soldier ni kwamba, mimi ni mkristo tena mkatoliki ila ninafahamu fika ya kuwa uislamu si ugaidi na si dini ya wizi na wala waislamu si magaidi na wala sio wezi bali wahalifu wachache hujificha katika kivuli cha uislamu ili kutenda uhalifu wao.
Dini ya uislamu ni dini safi sana tena ya watu waungwana kweli inayohubiri amani na upendo kama ilivyo dini ya kikristo. I love and respect all my muslim brothers and sisters out there.
Tanzania ililazimika kupigana vita ya Kagera mwaka 1978 kwa lengo la kuikomboa ardhi yetu na kumtoa nduli Idd Amin Dada na genge la wahuni wenzie. Uamuzi wa kuivamia ardhi ya mkoa wa ziwa Magharibi (Kagera) haukuwa na ridhaa ya waganda hata kidogo bali ni maamuzi ya kipuuzi na kichokozi yaliyofanywa utawala wa kidhalimu wa dikteta Amini dada.
Kwanini uhalifu alioufanya Salum Yusuph wa kwenda kuiba nguruwe uhusishwe na nafasi ya ungozi wa kidini (Imam) ilhali kitendo hicho (wizi) sio muongozo sahihi wa dini ya kiislam? Je, hii ni sahihi? Je, haya ndio maadili ya taaluma ya uandishi wa habari?
Je, mnafahamu kuwa vyombo vya habari visipotumika ipasavyo vinaweza kuleta vurugu za kidini au hata kikabila ndani ya jamii ya watanzania? Mmesahau yaliyotokea nchini Rwanda mwaka 1994? Leo hii mmesahau yaliyotokea nchini Kenya mwaka 2007? Ni njia zipi zilitumika katika kusambaza chuki kama sio vyombo vya habari?
Kulingana na Quran Tukufu, wizi umekatazwa katika Uislamu na ni dhambi kubwa sana. Inachukuliwa pia kuwa ni Haraam kulingana na maneno ya mtume Muhammad (SAW - peace be upon him). Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema amelaani wizi na ameamuru adhabu ya kisheria kupitia sheria ya Kiislam (Sharee’ah) kwa mwizi ni kukata mkono wa wake.
Mimi Infantry Soldier kabila langu ni mjaluo. Endapo itakuja siku moja kuonekana nimetoka msalani pasipo kunawa kabisa na kwenda moja kwa moja kwenye meza ya chakula kwa ajili ya kujiandaa na kula, Je itakuwa ni sahihi kusema kwamba, wajaluo wana tabia ya kula pasipo kunawa wakitoka msalani? Je, ni sahihi kutumia uovu wa mmtu mmoja katika kuhukumu wengine wa jamii yake?
Kabla ya mtu kufanya uhalifu, huwa anapanga kwanza mikakati kichwani mwake. Kitendo cha kupanga mikakati ovu kichwani tayari kinatosha kumvua mtu nafasi aliyonayo katika dini hata kabla hajatenda uovu husika.
Kitendo cha Imam mstaafu kupanga kuiba nguruwe kinamvua wadhifa ule hata kabla hajatenda tukio hilo la wizi. Alitenda tukio la wizi akiwa sio Imam tena kwa maana dini inakataza mtu wa hadhi yake kuwaza kutenda uovu wa namna ile.
Ninatambua na kuheshimu mchango wa wanataaluma wa tasnia ya habari katika kujenga jamii yenye umoja na mshikamano, lakini katika hili la uchochezi wa kidini ni lazima tulikemee sote kwa pamoja.
Maoni ya wadau;
==========
mjibu hoja nakupongeza , hii ni taabu ya kuwa na waandishi wasio waandishi. TAALUMA HII IMEVAMIWA . na biashara ya magazeti imekuwa ngumu kwa sasa kutokana na teknolojia. huyo muandishi uchara anatakiwa kujua KUNA UISLAMU , NA MUISLAMU.
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.