Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,641
- 46,298
Jambo mojawapo kubwa na la muhimu katika siasa za kushika dola ni kuweza kuwasiliana na kufikisha ujumbe wako kwa kwa wakati kwa wananchi walio wengi. Hiyo ni bila kujali ujumbe wako ni sahihi au sio sahihi.
Tatizo mojawapo kubwa la upinzani Tanzania ni kukosa vyombo vya habari vya kuusapoti na kusema mambo yake kwa nguvu.Hili ni jambo ambalo lina uweka upinzani kwenye nafasi mbaya "disadvantageous" kuwafikia wananchi.
Ukiangalia vyombo karibia vyote vya habari nchi hii 99% vimeegemea upande wa chama tawala cha CCM .Pia juu ya ziada ya hilo chama tawala kina TV na redio zake na gazeti lake. Pia kinatumia faida ya kuwa katika dola kutumia shirika la utangazaji la umma TBC.Kuna wakati upinzani ulikuwa na mahezeti yake yakapotezwa, ITV ilikuwa inajaribu kuwapa nafasi kubwa nayo ikawekwa kwapani ikatulia tuli.
Tanzania ya watu milion 60 ni vigumu sana kufikiwa kwa Twitter, Instagram au Facebook. Hilo ni kwa kuzingatia pia kwamba raia wengi wa vijijini hawajawahi kusikia hata baadhi ya hii mitandao ya kijamii. Wachache wenye Smartphone wanaishia WhatsApp.
Pia ni vigumu kufanya mikutano ya hadhara kuwafikia watu wote kwa sababu ya ukubwa wa eneo la nchi na gharama. Redio, TV, magazeti(kama enzi za Tanzania Daima, Mwanahalisi na Mawio) bado zinabaki njia kuu za kuufikia umma mkubwa na kupenyeza agenda za kisiasa za kudumu na zinazoibuka kila siku.
Upinzani ufanye mpango wa kuwa na media zao na pia wafanye mikakati ya kuonekana zaidi katika vituo binafsi vya sasa japo hili ni jambo gumu kwa sababu wamiliki wengi wa vyombo hivi wasingetaka kusuguana mabega na serikali ya chama tawala ili waendelee kulamba asali. Upinzania una kazi kubwa ya kufanya kuwa katika media kubwa.
Tatizo mojawapo kubwa la upinzani Tanzania ni kukosa vyombo vya habari vya kuusapoti na kusema mambo yake kwa nguvu.Hili ni jambo ambalo lina uweka upinzani kwenye nafasi mbaya "disadvantageous" kuwafikia wananchi.
Ukiangalia vyombo karibia vyote vya habari nchi hii 99% vimeegemea upande wa chama tawala cha CCM .Pia juu ya ziada ya hilo chama tawala kina TV na redio zake na gazeti lake. Pia kinatumia faida ya kuwa katika dola kutumia shirika la utangazaji la umma TBC.Kuna wakati upinzani ulikuwa na mahezeti yake yakapotezwa, ITV ilikuwa inajaribu kuwapa nafasi kubwa nayo ikawekwa kwapani ikatulia tuli.
Tanzania ya watu milion 60 ni vigumu sana kufikiwa kwa Twitter, Instagram au Facebook. Hilo ni kwa kuzingatia pia kwamba raia wengi wa vijijini hawajawahi kusikia hata baadhi ya hii mitandao ya kijamii. Wachache wenye Smartphone wanaishia WhatsApp.
Pia ni vigumu kufanya mikutano ya hadhara kuwafikia watu wote kwa sababu ya ukubwa wa eneo la nchi na gharama. Redio, TV, magazeti(kama enzi za Tanzania Daima, Mwanahalisi na Mawio) bado zinabaki njia kuu za kuufikia umma mkubwa na kupenyeza agenda za kisiasa za kudumu na zinazoibuka kila siku.
Upinzani ufanye mpango wa kuwa na media zao na pia wafanye mikakati ya kuonekana zaidi katika vituo binafsi vya sasa japo hili ni jambo gumu kwa sababu wamiliki wengi wa vyombo hivi wasingetaka kusuguana mabega na serikali ya chama tawala ili waendelee kulamba asali. Upinzania una kazi kubwa ya kufanya kuwa katika media kubwa.