a4afrika
JF-Expert Member
- Apr 13, 2012
- 1,389
- 1,330
WanaJF, inakuwaje pale mtu anapotokea kuhoji juu ya viongozi wa Chadema, basi wengi huja na majibu makali hata matusi? Je, wao ni malaika, hawakosei chochote? Msipokuwa makini, mtaifuga mijitu ambayo ni mamluki na wezi kama wale wa ccm, mwisho wake ushawishi wenu utashuka na kupotea kabisa. Lazima umakini ufanyike, msihoji mambo kwa kuongozwa na mapenzi na hisia, ila mantiki ya jambo..! Nadhani hata chadema wanapnda wanachama na mashabiki wao wawe hivyo (critical thinkers), na si wale wa kufuata mkumbo, kwani siku moja watageuka njiani. Nachukia sana siasa, na naumia sana inavyowafunga watu macho! Sio mbaya, piteni humo, mkishajua thamani halisi ya UTU, mtarudi na tutaungana na kupigania furaha ya kweli-UTU! Mungu wetu anaita!