Vigogo Dar wajiingiza orodha ya waathirika wa mafuriko... viwanja!

Chanzo cha habari (Mtanzania) kimedai majina ya vigogo hao kinayo ila kimeyahifadhi labda bado wanaendelea kufukunyua na mengine kama wadhani ni udaku basi kawaulize mtanzania
 
"Eti wanaiuliza serikali waende wapi? kwani sisi ndio tuliwapeleka mabondeni?" mh.mkuu wa mkoa.

Kwani wenye nyumba walipelekwa mabondeni?

Wote walifanya makosa, kama serikali inawajali wananchi wake, na imefanya uzembe kutokutekeleza sheria zake yenyewe basi wote wapewe viwanja.
 
Gazeti la mtanzania ni gazeti majeruhi la Rostam Aziz na Hussein Bashe tuwe makini kulifanya chanzo chetu makini cha taarifa. magazeti majeruhi wakati mwingine yanaumba taarifa bandia ili kukidhi haja ya kuwasafisha majeruhi wa kisiasa au kututoa kwenye agenda za msingi za kujadili madhambi ya waliohujumu uchumi wetu na kutufikisha hapa tulipo.

Wasomaji mahiri wanaweza kupitia lakini hawanunui magazeti kama mtanzania

Taarifa za mrengo moja inaweza kuwa na ujumbe lakini uliofinyangwa kwa manufaa ya mmiliki

Dawa yake kupotezea kiaina
 
Ili kuwe na uwazi inabidi majina ya walioathirika na kugawiwa viwanja yawekwe hadharani. vinginevyo kweli tutakuta waathirika wa narudi jangwani na viwanja vya mabwe pande wanapewa vigogo. Tumeyaona haya kumbuka miaka ya 90 waathirika wa Jangwani waliambiwa wanapewa viwanja kinyerezi lakini waliovipata ni wachache vingine vikaenda kwa vigogo! Nchi hii bwana kila kitu deal!

Taja mwathirika japo mmoja tu ambaye hakupata kiwanja. acha siasa kwenye mambo ya msingi viwanja 105 vyote walipewa na baadhi ya wakauza. Ndio sababu wanaogopa kujitokeza hadharani kwamba hawakupewa kwani wataumbuka. hicho ndio kisingizio chao cha kutotaka kutoka mabondeni.
 
Mkuu wa mkoa Sadiki alitangaza hadharani kwamba waathirika wanahitaji viwanja visivyozidi 1000 na vitakavyobaki 1800 watapewa wananchi wanaohitaji. sasa hapo tusichanganye kuwanyang'anya waathirika vyao 1000 na vigogo kujigawia viwanja 1800 ambavyo sio vya waathirika. hizi ni kesi mbili tofauti ziwapo mahakamani
 
Enzi za Jenelali Ulimwengu magazeti hayo yalikuwa maarufu sana lakini sasa ni magazeti ya fisadi namba moja hapa nchini na wakati mwingine yanataka kutuonyesha kwamba fisadi sio yeye tu bali wapo na wengine. Mbona wao hawataki kuandika mabaya yaoi? lini uliwahi kuona magazeti haya yakiandika kuhusu mmiliki wake yule mwizi mkuu?
 
Wewe kama sio dalali basi ni bepari mmojawapo mwenye nyumba nyingi hapa dar, hivyo unaogopa kukosa wapangaji. kwanini wasipewe viwanja? kwani wapangaji hawana haki ya kupata viwanja? wakirudi mabonddeni mtawalaumu?

hakika wewe unatumia masaburi kuwaza, kunena na kuona. wapangaji hawana haki hiyo ya kudai viwanja na hata wamiliki ni huruma tu itumike lakini uliona wapi mvunja sheria anafidiwa hasara? kitendo cha kujenga mabondeni ni uvunjaji wa sheria ya kutowajibika kujikinga na hatari. Hata matajiri waliliona bonde na wangeweza kujaza vifusi kuinua bonde lakini wameacha kufanya hivyo kukwepa hatari ndio ikawe maskini?
 
Mimi ndo maana sitaki kabisa kuchangia haya maafa coz unachangia maisho wa siku unachangia watu wanajineemesha watu wanaostahili hawapewi kwanza ndo wanafukuzwa, huu ni ukatili sijawahi ona, mkuu wa mkoa anajibu kwa kiburi wakati wao ndo wameidhinisha hizo nyumba zikajengwa zisingejengwa wasingepanga huko wangetafuta safe place. Ccm hawana akili hii ilikuwa nafasi ya kurudisha imani kwa wananchi sasa ndo wanaudhi wananchi. Poleni ccm.
 
Viongozi wa serikali wapo kwaajili ya matumbo yao na wala si kwaajili ya kutumikia wananchi, so kila dili lolote litakalo tokea lazima wao wawe wa kwanza kunufaika. Nawapongeza CDM misaada waliyotowa waliwapa waathirika moja kwa moja.

Mkuu, wewe ndio umejua hili leo? Kufa kufaana!
 
Enzi za Jenelali Ulimwengu magazeti hayo yalikuwa maarufu sana lakini sasa ni magazeti ya fisadi namba moja hapa nchini na wakati mwingine yanataka kutuonyesha kwamba fisadi sio yeye tu bali wapo na wengine. Mbona wao hawataki kuandika mabaya yaoi? lini uliwahi kuona magazeti haya yakiandika kuhusu mmiliki wake yule mwizi mkuu?

Umeshajiuliza Salva Rweyemamu alikwendaje Ikulu na anafanya nini pale? Alikuwa ni mmoja wa waandishi wa hayo magazeti.
 
viongozi wa serikali wapo kwaajili ya matumbo yao na wala si kwaajili ya kutumikia wananchi, so kila dili lolote litakalo tokea lazima wao wawe wa kwanza kunufaika. nawapongeza cdm misaada waliyotowa waliwapa waathirika moja kwa moja.


maafao ya wengine kwao ni dili! Very sad!
 
Wapo baadhi ya watanzania wenzetu wanafanya mambo maovu lakini baya zaidi ni idadi kubwa ya watanzania wema wanaoshuhudia maovu na kubaki kimya bila kuchukua hatua yoyote. Ni vema tukaamua kutowafumbia mambo waovu wote naamini tukimaanisha tuyasemayo haki itaishinda dhuluma.
 
Mimi hili la wapangaji nao kudai viwanja sili support ... Wapewe wenye nyumba tu ... Wapangaji wakatafute mahala pengine "sio bondeni kupanga "

Kichwa cha habari kinasomeka hivi: "Vigogo Dar wajiingiza orodha ya waathirika wa mafuriko...viwanj!"

Kama kuchomekea waathirika hewa inawezekana kuwapa viwanja inashindikana nini waathirika wa kweli ambao wengine ndio walikuwa wakazi pekee kwenye nyumba hizo kwa maana kwamba wenye nyumba hawakuwa wanaishi hapo.

Kwa tafsiri hapo muathirika wa mafuriko ni mwenye nyumba asiyeishi hapo? Kigogo aliyejichomeka ? Au wapangaji waliopanga nyumba mabondeni?
 
Back
Top Bottom