Optimists
JF-Expert Member
- Oct 17, 2021
- 278
- 686
Nimeangalia hii video kwa umakini Mkubwa na pia nimefatilia mjadala kuhusu mfalme zumaridi nimejikuta nashangaa na kujiuliza vitu vingi sana. Hiyo video hapo chini inamuonesha mfalme Zumaridi akimuamuru Michael Jackson aingie kupitia mtumishi wake atoe show kanisani 😂😂😂, na kuna watu wanashangilia wanaona huyu nabii anatupiga na kitu kizito.
Hivi kwa kupitia shuhuda hizi za uongo tena uongo wa wazi wazi nadhani uhitaji kua na degree wala elimu ya form four kujua kabisa huyu Mchungaji ni Muongo na anatupiga.
Kwa matukio kama haya yanayoendelea kwa watumishi wetu tunaowaita "wapakwa mafuta" watu wanaendeleaje kukaa kanisani kila jumapili kushuhudia maigizo kama haya?.
Zamani kidogo niliangalia YouTube nikipata hiyo link ya video nitaituma humu, inahusu yule Mwanahabari Mohammed ambae sasahivi ni Member of parliament alifichua maovu ya mchungaji mmoja huko Kenya jinsi alivyokua anawapanga waumini wake waseme ushuhuda wa uongo.
Nimejaribu kufungulia hizi channel za hawa wachungaji sioni kama wakihubiri kuhusu wokovu, toba, msamaha, kuwasaidia wajane naona wanahubiri sana kuhusu mafanikio na uponyaji yani utasikia toeni sadaka ya mavuno, bahasha ya kufunguliwa n.k
Dini safi isiyo na shaka mbele ya za Mungu ni kuwasaidia wajane na wenye uhitaji kutembelea wagonjwa na kufanya matendo ya huruma.
Hivi kwa kupitia shuhuda hizi za uongo tena uongo wa wazi wazi nadhani uhitaji kua na degree wala elimu ya form four kujua kabisa huyu Mchungaji ni Muongo na anatupiga.
Kwa matukio kama haya yanayoendelea kwa watumishi wetu tunaowaita "wapakwa mafuta" watu wanaendeleaje kukaa kanisani kila jumapili kushuhudia maigizo kama haya?.
Zamani kidogo niliangalia YouTube nikipata hiyo link ya video nitaituma humu, inahusu yule Mwanahabari Mohammed ambae sasahivi ni Member of parliament alifichua maovu ya mchungaji mmoja huko Kenya jinsi alivyokua anawapanga waumini wake waseme ushuhuda wa uongo.
Nimejaribu kufungulia hizi channel za hawa wachungaji sioni kama wakihubiri kuhusu wokovu, toba, msamaha, kuwasaidia wajane naona wanahubiri sana kuhusu mafanikio na uponyaji yani utasikia toeni sadaka ya mavuno, bahasha ya kufunguliwa n.k
Dini safi isiyo na shaka mbele ya za Mungu ni kuwasaidia wajane na wenye uhitaji kutembelea wagonjwa na kufanya matendo ya huruma.