Ben T
JF-Expert Member
- Sep 18, 2013
- 245
- 263
Ni sahihi hizo Application zinavurunda mambo mengi kwa mfano usipoingia tu siku moja lawama utakazokutana nazo ni balaaaHabarini ndugu!
Nina miezi miwili nimeachana na matumizi ya smartphone,al-mahsusi hizi app za whatsapp na instagram.
Nataka niwashirikishe watanzania wenzangu uzoefu wangu huu wa miezi miwili, nadhani inaweza kuwasaidia baadhi ya watu!
Pamoja na faida chache au nyingi za mitandao hii,nilikuja kugundua hizi app hasa whatsapp ilikuwa inanipotezea sana muda na kuniharibia concentration kwenye mambo ya msingi zaidi katika utafutaji hivyo kupunguza uzalishaji, na kupunguza kasi ya kufikiri!
Baada ya kuachana na matumizi haya ya whatsapp/smartphone nimejikuta nimekuwa effective sana kwenye kazi zangu kwa maana ya kuutumia vizuri muda wangu,napata muda wa kutosha kusoma vitabu,kufikiri,ku meditate nk,
Uwezo wangu wa kukumbuka umeongezeka, imagine, kwa sasa nikiangalia namba yoyote ya simu mara moja tu inakaa kichwani tofauti na kipindi cha nyuma.
Stress zimepungua,nimefakiwa kupunguza stress za aina mbalimbali ambazo zinasabishwa na chatting nyingi zisizo za msingi au picha na video za ajabuajabu,zimebaki stress za kusaka hela tu.
Mahusiano yameimarika;mahusino na watu wangu hayajatetereka tena, kwa sababu hatuwasiliani mara kwa mara hivyo hakuna makwazo yanayotokana na kuwasiliana mara kwa mara
Akiri imekuwa focused zaidi na kazi
Concentration kwenye kazi imeongezeka sana na kuondoa blockage za sms za whatsapp zinazoingia masaa 24.
Hizo ni baadhi tu, kuna nayaona matokeo makubwa zaidi baadae.
Hofu yangu,
Tunatengeneza taifa la mashabiki na watu wasioweza kufikiri tukiendekeza hili, watu wanachati tu hata wakiwa maofisini, tena wanachat umbeaumbea tu,mpira,ajali,picha za uchi nk
Taifa linaangamia,nani atalizuia au kulisemea hili, ni kitu chenye impact kubwa sana in the long run.
Taifa linaongeza watu wavivu,watu wenye tabia mbovu,wambea,walalamikaji nk.. where are we heading as a nation?
Tutegemee thinkers wachache sana baadae.
Najua wale addicts watapinga sana hili, lakini huu ndo ukweli mchungu.
Tafari..chukua hatua.
Pia huko Instagramu ndo shida tupu hatusemi matangazo ya kuuza Dawa za Kuongeza nguvu za Kiume, kuongeza Makalio na mambo mengi kama yale alokemea Mkuu wa Mkoa wa Dar ndo yamejazana, sasa tunajiuliza kuna nini Maana hata TCRA wako kimya tu sijui tunaelekea wapi Nchii hii baada ya miaka Mitano.