Uvamizi wa Eneo Meru na Mahojiano na Aloyce Kimaro (MB)

Hamjawasikiliza WANANCHI waliovamia shamba hilo wanasemaje. Haiwezekani watu wote wale wakavamia tu bila sababu. Jamani waambieni MATAJIRI wetu hawa wafungue mashamba mapya mbali na walalahoi.
 
Kwa kweli hali hii ya kujichukulia sheria mikononi inabidi idhibitiwe kabla maafa hayajawa makubwa. Kama leo wameru wamefanya hivi tukakaa kimya na kesho wakafanya wazigua kule Tanga si tutakuja jikuta watu wanafukuzwa katika mikoa ambayo si yao?

Mwanajamiione,
Sidhani kama hawa vijana wamejichukulia sheria mikononi mwao. Ni wazi kabisa kuwa kuna aliyewaamrisha kumshambulia Mbunge Kimaro.
  1. Hebu tujiulize, ni lini walalahoi wanathubutu kuharibu mali ya kiongozi wa juu serikalini kiasi hicho tena mchana mbele ya wanahabari?
  2. Viongozi kama EL, kwao vurugu zikitokea na watu wakachinjana, sidhani kama wao wanajali, ili mradi tu vurugu hizo ziwe zinawasaidia wao na familia zao kuendelea kuitafuna nchi.
 
Utitiri na ukubwa wa mashamba haya wanayonunua viongozi wetu tena kwenye maeneo jirani na watu wetu masikini kabisa ndio inayonisikitisha mimi. Bado tuna mapori makubwa tu nchi hii yanayohitaji kuendelezwa. Viongozi wetu hawayaoni hayo. Wananunua ambayo tayari yameendelezwa pamoja na ukweli kuwa wanao uwezo mkubwa tu wa kufungua mashamba mapya kuliko hao wananchi. Tupunguze UROHO na UBINAFSI wa Viongozi wetu vinginevyo milipuko ya aina hii baadaye itageuka kuwa vita kamili. Kimaro hawezi kuililia KIWIRA ambayo haina hata eka 20 wakati yeye anamiliki maekari mengi kiasi hiki.
Mkuu WildCard, kumiliki shamba au mali yoyote si kosa. Liwe limeendelezwa na mmiliki wa awali au lilikuwa pori. Kinachohitajika ni uhalali wa umiliki wa shamba au mali hiyo.

Ardhi ni kubwa nchini (kweli kabisa). Ila ardhi zote nchini zina thamani tofauti kutegemea na udongo wake, mahali ilipo (umbali kutoka kwenye njia kuu za uchumi) na madhumuni ya ardhi yenyewe katika mipango iliyopo kiuchumi na kimaendeleo (hata kwa uwezekano wa kupatia mikopo) n.k.

Mkuu katika maisha siku zote binadamu hutafuta njia za kujikwamua kwa kila hali. Haiwezekani leo ukadhani mtu kwa kuwa ni kiongozi, atakimbia ardhi nzuri ambayo anaweza kuipata kwa makusudio ya uendelezaji anaokusudia na kukimbilia ardhi zilizopo maporini (ili eti wananchi wamuelewe). Nadhani tutasubiri kwa muda mrefu sana kuwa na viongozi wajinga kiasi hicho. Hasa baada ya kubadilika hawa ambao hata kisicho halali kinahalalishwa.
 
Ni kweli wananchi hawatakiwi kujichukulia sheria mkononi na kitendo walichofanya si kizuri lakini nini chimbuko la tatizo? Inaonyesha wazi kuwa wananchi wanao zunguka eneo hilo hwana ardhi ya kutosha. Shamba limevamiwa na karibu wanakijiji 80, nadhani kuna tatizo la msingi. Lazima ifahamike kuwa ubinafsishaji wa ardhi ni tofauti sana na ubinafsishaji wa biashara nyingine.
 
Wajumbe,

Napenda kutoa mchango wangu kama ifuatavyo.


  1. Kwa mtazamo wangu, kinachotokea leo, suala la wananchi (soma "fukara") kujichukulia sheria mikononi, haswa kwenye migogoro ya ardhi, ni mwendelelezo wa mlolongo mrefu ambao umetokana na kuwepo kwa mazingira tatanishi kwenye uwekezaji unaotumia ardhi. Wananchi wanaona kwamba wao wametelekezwa na ardhi wanayoihitaji (ni mtaji mkubwa kwao) kwa ajili ya kilimo, n.k., kupewa kwa watu ambao TAYARI WANA UWEZO. Je, tumejiuliza iwapo wananchi hao wa Arumeru hawakuandika barua za maombi kwa Serikali yao, wakitaka (si kuomba) kupewa ardhi hiyo ili waitumie kujiendeleza kwa shughuli za kilimo, elimu, n.k.? Je, kwa nini walikataliwa na ardhi hiyo kupewa mtu mwingine, MWENYE UWEZO MKUBWA, Mbunge wa CCM, Aloyce Kimaro?
  2. Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliwahi kutabiri kwamba, itafika siku wale ambao hawana watashika mapanga, sime na mikuki na kuwatafuta wale walio-nacho, na kuwataka wawape sehemu ya kile walichonacho, ama kwa hiari yao au kwa nguvu. Kilichotokea kwa shamba la Kimaro ni dhihirisho na utimilifu wa utabiri huu.
  3. Wananchi wametambua hadaa kubwa waliyotendewa na watawala. Sasa wameamua kudai mapema haki yao. Suala ni, je, watawala watakuwa tayari kuwa waadilifu na wakweli kwa wananchi ambao ndio wamewapa dhamana ya kuitawala nchi hii, au wananchi wataamua kuitwaa (kwa njia ya demokrasia ama - God forbid - kwa njia ya silaha) na kuirejesha mikononi mwao?
  4. Yaliyotokea Busanda na yanayotarajiwa kutokea Biharamulo yanatudhihirishia kwamba watawala hawako tayari kuiachia nchi hii itawaliwe na wananchi wengine zaidi yao wenyewe. Watawala wamejimilikisha nchi hii yenye utajiri lukuki, si kwa maendeleo ya wananchi wote ila kwa ajili yao wenyewe, at least kwa kiwango kikubwa.
  5. Ndio, wapo baadhi ya viongozi wa chama tawala ambao ni waadilifu na wenye kutimiza wajibu wao. Lakini hawa wanaharibiwa na wengi walio wachafuzi. Hali ikiendelea, vita itatokea, whether or not we want the situation. Je, nani ataanza kumvika paka kengele kwenye suala hili la uadilifu na kupiga vita ya UKWELI dhidi ya ufisadi?
  6. Nisiwe quoted vibaya kwamba watu wote WENYE UWEZO ni mafisadi, ila, wawaachie wananchi ardhi yao, waiendeleze.
  7. Kimaro, hujatosheka?
Wabilah Tawfiq!

./Mwana wa Haki
 
Mh. Kimaro awe fisadi asiwe fisadi tukio hili lina jambo na ni la aibu sana kwa Taifa letu. Kama ni suala la wananchi kudai/kutaka ardhi, je, ardhi hiyo ya Ndugu Kimaro ambayo ameiendeleza kwa miaka kadhaa wananchi hao wameiona hivi punde tu? Siku zote walikuwa wapi kupanga na kufanya uvamizi?

Kuna mawili ninayoyaona mie, Mh. Kimaro amekuwa akisikika kupiga vita ufisadi. Yawezekana hiyo ndiyo nongwa. La pili, uchaguzi waja, uko kwenye kona tu, yawezekana kwamba kuna mtu anawania kiti cha Mh. Kimaro bungeni na yuko radhi kugeuka ibilisi wa kushawishi wananchi watende maovu; kwa hiyo, ameanza mchezo mchafu ili kummaliza Ndugu Kimaro.

Ni aibu sana kwamba sasa nchi yetu ambayo miaka yote tumekuwa tukiimba wimbo wa 'Amani na Utulivu' imefikia mahali kama hapa. Kitendo hicho cha uvamizi kama kimesukwa na mwanasiasa ama mwananchi wa kawaida, ni dhahiri kinawaweka pabaya wanasiasa wote wapenda/watenda haki na kinatuweka pabaya sisi wananchi wa kawaida wapenda amani maana hatuwezi tena kusimama jukwaani, vijiweni, hata nje ya mipaka ya nchi yetu na kutamba kwamba Tanzania ni nchi ya amani na utulivu kama tulivyokuwa tukifanya huko nyuma. Itakuwa ni uongo!

Wakulu, Mwenyezi Mungu hapendi maovu. Vyovyote vile ilivyo, kama uvamizi huo umepangwa na binadamu basi adhabu ataipata hapahapa duniani wala si mbinguni. Mwenyezi Mungu hatasubiri jamaa huyo/hao waende mbinguni kuipata adhabu yao. Mark my words!
 
Mbona wananchi walipojichukulia sheria kwa Ballali hamkulaani? Ndio maana wengine tunaipenda JF, rahisi kweli kweli kuona unafiki mkubwa ulioko hapa.

Kama tunalaani hizi tabia mbaya za wananchi kujichukulia madaraka mikononi mwao basi tulaani kwa kila mtu; tulaani hata pale hizo tabia zinapotumika kuchoma vibaka.

wananchi sio polisi, sio mahakama, hizi tabia za kuvamia na kuharibu mali za watu hazifai. Tusipoangalia tutaishia kuwa kama Zimbabwe.

Lakini pia wanasiasa nao waelewe kwamba kadri wanavyofanya deals mbalimbali za kuwaibia wananchi kwa kutumia system, kuna siku wananchi watashutuka na kuwafuata.
Mtanzania,
Umenena Mkuu.watu wanaangalia ambao wapo upande wao na wakati mwingine mwanakijiji huwa anafanya mambo kwa pupa kwa kuona flani ni bora kuliko mwingine kisa tu anajidai kupigania ufisadi(SERA MPya) ial kama tukiamua kuchimbua historia ya mambo basi unaweza ukashtushwa.

Mwanakijiji hajatenda haki sababu kahoji upande mmoja .Kimsingi inabidi aende akawahoji na hao wanakijiji waseme wanachokifahamu na siyo kumwamini kimaro peke yake.Kwanini ajimilikishe ardhi yote hiyo na wananchi wengine wakose??

Hii inatoafuti gani na mtu kujilimbikizia pesa kiunjanja ujanja??Naye ni Fisadi Period!.Haiwezekani kabisa watu 3000 wakaweza kukusanywa kumuonea mtu mmoja!

Mwanakijiji wahoji na wananchi na pia naomba huyo mhe kimaro awagawie baadhi ya maeneo hao wanakijiji!


 
Wananchi haohao wakimzomea Mkapa au wakipiga mawe msafara wa JK baadhi yetu tunawaona kama mashujaa wa aina fulani hivi. Wakichukua ardhi yao.....Kimaro anapinga ufisadi! Amiin nawambia hakuna ufisadi mbaya kama wa kujilundikia ARDHI huku ukiwaacha walio wengi kuwa wapangaji kwenye nchi yao. Moja ya Mambo ya msingi kabisa yaliyotufanya tudai UHURU wetu ni ARDHI. Mwalimu alilisimamia vizuri sana hili. Sasa limeanza kuvurugwa na akina Kimaro, Sumaye, Mkapa, Mramba, Yona,.....
 
Mwanajamiione,

Sidhani kama hawa vijana wamejichukulia sheria mikononi mwao. Ni wazi kabisa kuwa kuna aliyewaamrisha kumshambulia Mbunge Kimaro.
  1. Hebu tujiulize, ni lini walalahoi wanathubutu kuharibu mali ya kiongozi wa juu serikalini kiasi hicho tena mchana mbele ya wanahabari?
  2. Viongozi kama EL, kwao vurugu zikitokea na watu wakachinjana, sidhani kama wao wanajali, ili mradi tu vurugu hizo ziwe zinawasaidia wao na familia zao kuendelea kuitafuna nchi.
Makaayamawe nakubaliana kabisa na hoja yako ila bado nasisitiza kuwa walichokifanya si kitendo cha ujasiri na hata huyo aliyewatuma kama unavyosema ni kunguru mwoga ambaye hafai kuwa johari wa taifa letu changa. Kama wananchi hawa wanatatizo na Mh. Kimaro kuna njia nyingi tu za kutatua tatizo hili ikiwemo ya kumface na kumtamkia wazi kile wanachokitaka hata kama ni kuandamana na kumfungia njia asitoke ndani mwake.

Kwa hawa wameshindwa hata na wale wastaafu wa Jumuiya ya Africa Mashariki waliofunga barabara pale Salender Bridge. Sijui ingekuwaje kama wazee wale wangeamua kurushia mawe magari ya waheshimiwa yanayopita njia ile!!

Whether wametumwa au ni utashi wao bado wamekosea na tukiendelea kuyafumbia macho haya basi tusijeshangaa siku tukisikia watanzania wameingia mjengoni na kupasua vioo vyote na samani au hata wamevamia wizara flani au BOT na kuvinja vunja jengo lote.

Hawa wameanzia kwa Mh. kama kiongozi binafsi, kitu gani nitazuia watu kujioganiza na kuvamia bunge kwa jina la kupambana na mafisadi?
 
Wananchi haohao wakimzomea Mkapa au wakipiga mawe msafara wa JK baadhi yetu tunawaona kama mashujaa wa aina fulani hivi. Wakichukua ardhi yao.....Kimaro anapinga ufisadi! Amiin nawambia hakuna ufisadi mbaya kama wa kujilundikia ARDHI huku ukiwaacha walio wengi kuwa wapangaji kwenye nchi yao. Moja Mambo ya msingi kabisa yaliyotufanya tudai UHURU wetu ni ARDHI. Mwalimu alilisimamia vizuri sana hili. Sasa limeanza kuvurugwa na akina Kimaro, Sumaye, Mkapa, Mramba, Yona,.....

Tatizo isiwe ukubwa wa ardhi mtu anayo miliki tatizo iwe kama kapata kihalali au la. Ardhi nayo ni uwekezaji. Kama mtu ana uwezo wa kununua ekari 1000 au zaidi na akaendeleza hiyo ardhi asi nunue? Ardhi ni kama mali yoyote ile na kamwe watu hawawezi kumiliki kiwango sawa. Kama bwana Kimaro haku jipatia hiyo ardhi kihalali basi hilo ni swala jingine ila kama kaipata kihalali basi hana kosa.
 
Wananchi haohao wakimzomea Mkapa au wakipiga mawe msafara wa JK baadhi yetu tunawaona kama mashujaa wa aina fulani hivi. Wakichukua ardhi yao.....Kimaro anapinga ufisadi! Amiin nawambia hakuna ufisadi mbaya kama wa kujilundikia ARDHI huku ukiwaacha walio wengi kuwa wapangaji kwenye nchi yao. Moja Mambo ya msingi kabisa yaliyotufanya tudai UHURU wetu ni ARDHI. Mwalimu alilisimamia vizuri sana hili. Sasa limeanza kuvurugwa na akina Kimaro, Sumaye, Mkapa, Mramba, Yona,.....

Ni kweli kabisa WildCard unayoyasema yana ujumbe mzito but kuzomea si sawa na kuharibu mali!! Ni njia moja wapo ya kuonyesha kuwa umekerwa kupita kiasi!! Kitendo chao wameru kimeweza kikasababisha maafa kama angetokea mtu wa kupingana nao shambani mule!! Isitoshe mtu kuwa na ardhi si kosa unless ardhi hiyo awe ameipata kwa njia za panya kitu ambacho hatuna uhakika nacho kwa Mh. Kimaro.

Sijui utaelezea vipi wale wakazi wa Lindi, Mtwara na hata maeneo ya Kisarawe wanaouza maeneo ya mashamba yao kwa wageni. Nao ikifika muda waje waharibu mali na mazao yaliyomo katika maeneo hayo?.
 
Mbona wananchi walipojichukulia sheria kwa Ballali hamkulaani? Ndio maana wengine tunaipenda JF, rahisi kweli kweli kuona unafiki mkubwa ulioko hapa.

Kama tunalaani hizi tabia mbaya za wananchi kujichukulia madaraka mikononi mwao basi tulaani kwa kila mtu; tulaani hata pale hizo tabia zinapotumika kuchoma vibaka.

wananchi sio polisi, sio mahakama, hizi tabia za kuvamia na kuharibu mali za watu hazifai. Tusipoangalia tutaishia kuwa kama Zimbabwe.

Lakini pia wanasiasa nao waelewe kwamba kadri wanavyofanya deals mbalimbali za kuwaibia wananchi kwa kutumia system, kuna siku wananchi watashutuka na kuwafuata.

Balali alisha bainika ni mwizi na rais alikwisha mfukuza kazi lakini kwa kimaro ni njama tu za mafisadi wamewachochea wananchi (wahuni).
 
Ni kweli kabisa WildCard unayoyasema yana ujumbe mzito but kuzomea si sawa na kuharibu mali!! Ni njia moja wapo ya kuonyesha kuwa umekerwa kupita kiasi!! Kitendo chao wameru kimeweza kikasababisha maafa kama angetokea mtu wa kupingana nao shambani mule!! Isitoshe mtu kuwa na ardhi si kosa unless ardhi hiyo awe ameipata kwa njia za panya kitu ambacho hatuna uhakika nacho kwa Mh. Kimaro.

Sijui utaelezea vipi wale wakazi wa Lindi, Mtwara na hata maeneo ya Kisarawe wanaouza maeneo ya mashamba yao kwa wageni. Nao ikifika muda waje waharibu mali na mazao yaliyomo katika maeneo hayo?.

Ni kweli kabisa. Watanzania tuna bidi tuondokane na dhana ya kwamba kila aliye na mali ni mwizi. Hakuna kati yetu asiye penda kujiendeleza na kuji patia mali tatizo ni jinsi gani tuna jipatia mali. Tunapo elekea sasa ni kubaya. Watu bila kuchunguza mtu kaji patiaje mali wata taka kuhujumu mali za wengine. Tuwe wakweli bwana we all want to make money and we all want to become rich if we can. Tupinge ufisadi na si utajiri.
 
Wajumbe,

Napenda kutoa mchango wangu kama ifuatavyo.


  1. Kwa mtazamo wangu, kinachotokea leo, suala la wananchi (soma "fukara") kujichukulia sheria mikononi, haswa kwenye migogoro ya ardhi, ni mwendelelezo wa mlolongo mrefu ambao umetokana na kuwepo kwa mazingira tatanishi kwenye uwekezaji unaotumia ardhi. Wananchi wanaona kwamba wao wametelekezwa na ardhi wanayoihitaji (ni mtaji mkubwa kwao) kwa ajili ya kilimo, n.k., kupewa kwa watu ambao TAYARI WANA UWEZO. Je, tumejiuliza iwapo wananchi hao wa Arumeru hawakuandika barua za maombi kwa Serikali yao, wakitaka (si kuomba) kupewa ardhi hiyo ili waitumie kujiendeleza kwa shughuli za kilimo, elimu, n.k.? Je, kwa nini walikataliwa na ardhi hiyo kupewa mtu mwingine, MWENYE UWEZO MKUBWA, Mbunge wa CCM, Aloyce Kimaro?
  2. Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliwahi kutabiri kwamba, itafika siku wale ambao hawana watashika mapanga, sime na mikuki na kuwatafuta wale walio-nacho, na kuwataka wawape sehemu ya kile walichonacho, ama kwa hiari yao au kwa nguvu. Kilichotokea kwa shamba la Kimaro ni dhihirisho na utimilifu wa utabiri huu.
    [*]Wananchi wametambua hadaa kubwa waliyotendewa na watawala. Sasa wameamua kudai mapema haki yao. Suala ni, je, watawala watakuwa tayari kuwa waadilifu na wakweli kwa wananchi ambao ndio wamewapa dhamana ya kuitawala nchi hii, au wananchi wataamua kuitwaa (kwa njia ya demokrasia ama - God forbid - kwa njia ya silaha) na kuirejesha mikononi mwao?
  3. Yaliyotokea Busanda na yanayotarajiwa kutokea Biharamulo yanatudhihirishia kwamba watawala hawako tayari kuiachia nchi hii itawaliwe na wananchi wengine zaidi yao wenyewe. Watawala wamejimilikisha nchi hii yenye utajiri lukuki, si kwa maendeleo ya wananchi wote ila kwa ajili yao wenyewe, at least kwa kiwango kikubwa.
  4. Ndio, wapo baadhi ya viongozi wa chama tawala ambao ni waadilifu na wenye kutimiza wajibu wao. Lakini hawa wanaharibiwa na wengi walio wachafuzi. Hali ikiendelea, vita itatokea, whether or not we want the situation. Je, nani ataanza kumvika paka kengele kwenye suala hili la uadilifu na kupiga vita ya UKWELI dhidi ya ufisadi?
  5. Nisiwe quoted vibaya kwamba watu wote WENYE UWEZO ni mafisadi, ila, wawaachie wananchi ardhi yao, waiendeleze.
  6. Kimaro, hujatosheka?
Wabilah Tawfiq!

./Mwana wa Haki

Mwana wa Haki, nakubaliana nawe, dalili ya moto ni moshi!

Pamoja na kuyaafiki kwa asilimia mia maneno ya Baba wa Taifa kuhusu wananchi wenye dhiki kuchoshwa na tabaka la walionacho na wasionacho linaloendelea kujengeka nchini bila udhibiti wowote. Bado uwezekano upo wa hujuma za makusudi na zilizopangwa dhidi ya wale wanaotoa sauti zao kushutumu ufisadi.

Pia, ninapenda niongeze kwa kusema kwamba hakuna mahala popote ambapo Baba wa Taifa alisema hataki kuona watu wakijiendeleza na kuwa na hali nzuri kimaisha. Wala hakuwahi kutangaza ama kuruhusu watu wasio na ardhi wakavamie mashamba/ardhi za wengine zilizopatikana kwa kufuata utaratibu.

Mnaofuatilia jambo hili, je Mkuu wa Mkoa wa eneo husika ametoa tamko gani kuhusu wananchi kujichukulia sheria mkononi, au ndio amewaachia Polisi wafanye kazi yao, basi imetosha? Baadhi ya wakuu wa mikoa wamekuwa hawasikiki wakihofu 'kuharibu' na wengine wamekuwa 'ceremonial figures' wanaopenda kuonekana kwenye TV na kusikika kwenye vyombo vya habari bila tija. Wengi hawafanyi kazi yao ya kumsaidia Rais kwa umakini na utimilifu unaostahili katika kushughulikia masuala mbalimbali ya ukiukwaji wa sheria na maadili ya Taifa letu. Uzembe na kutowajibika ipasavyo ndiyo mambo yanayosababisha kutoweka kwa Amani na Utulivu nchini kama ilivyofanyika Arumeru.

Nimesoma kuna aliyesema kwamba tumeanza kuwa kama Zimbabwe. Kama matukio haya hayakemewi na kushughulikiwa ipasavyo, ni kweli, twendako tutakuwa kama Zimbabwe.

Nikiongezea maneno ya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu J.K. Nyerere aliwahi kusema: "Mvisavisa uburweri ikiriro kiza kumbura". Tafsiri isiyo rasmi: "Mfichaficha maradhi kilio kitamuumbua!" Tuendelee kufumbia macho na kufutika maovu chini ya uvungu badala ya kuyashughulikia ipasavyo, matokeo tutayaona kama hatujaanza kuyaona. Tunaliteketeza Taifa, moshi ulioanza, iwe kwa sababu yoyote ile, usipodhibitiwa tutashindwa kuuzima huo moto utakapopamba moto!
 
Tatizo isiwe ukubwa wa ardhi mtu anayo miliki tatizo iwe kama kapata kihalali au la. Ardhi nayo ni uwekezaji. Kama mtu ana uwezo wa kununua ekari 1000 au zaidi na akaendeleza hiyo ardhi asi nunue? Ardhi ni kama mali yoyote ile na kamwe watu hawawezi kumiliki kiwango sawa. Kama bwana Kimaro haku jipatia hiyo ardhi kihalali basi hilo ni swala jingine ila kama kaipata kihalali basi hana kosa.
Ekari 1000 za nini kwa mtu mmoja? Mbaya zaidi karibu kabisa na makazi ya watu wa kawaida. Yapo mapori Nchi hii yanahitaji kuendelezwa waende huko akina Kimaro.
 
Ekari 1000 za nini kwa mtu mmoja? Mbaya zaidi karibu kabisa na makazi ya watu wa kawaida. Yapo mapori Nchi hii yanahitaji kuendelezwa waende huko akina Kimaro.

Kwa nini mtu asiwe na ekari 1000? Mtu kama una pesa yako kwa nini usi nunue kitu unacho taka? Kwa hiyo una taka kusema iwekwe limit ya kiasi cha ardhi mtu anayo weza kumiliki? una taka kusema iwekwe limit ya kiasi cha mali mtu anacho weza kumiliki? Watu kama wakina Bill Gates wana net worth zaidi ya $50 billion jiulize zote hizo za nini. We are a capitalist economy and everyone is guaranteed by law to own any amount of property as long as it is legal.
 
Balali alisha bainika ni mwizi na rais alikwisha mfukuza kazi lakini kwa kimaro ni njama tu za mafisadi wamewachochea wananchi (wahuni).

1.Nani alibaini balali ni mwizi?

2.Aliiba shilingi ngapi?

3.Kwanini hawakumfungulia Kesi?

Vitu vingine muwe mnakaa kimya kama haujui kuhusiana na hilo,kwa taarifa yako Balali ndiyo alikuwa wa kwanza kuachia ngazi na mambo mengine yalikuw ani zuga tu ila Balali alijiuzuru kabla hajafutwa kazi!

Suala la Kimaro siyo njama za Mafisadi.Tutajie ni mafisadi gani hao siyo kubwabwaja tu...
 
lol nitafute nini? wananchi kujichukulia sheria mikononi dhidi ya balalli? kuna thread nyingi za balalli.....


Mtanzania tutendee haki kama unakumbuka kwa nini usikumbushe wenzio? A u kuna ugomvi.

Kwa mimi kwa Mzalendo yoyote aliyewekeza nchini kuvamiwa ni vibaya tena sana. Jirani na kimaro kuna wazungu wenye maeneo makubwa sana wananchi hawajaenda huko why?
 
Kwa nini mtu asiwe na ekari 1000? Mtu kama una pesa yako kwa nini usi nunue kitu unacho taka? Kwa hiyo una taka kusema iwekwe limit ya kiasi cha ardhi mtu anayo weza kumiliki? una taka kusema iwekwe limit ya kiasi cha mali mtu anacho weza kumiliki? Watu kama wakina Bill Gates wana net worth zaidi ya $50 billion jiulize zote hizo za nini. We are a capitalist economy and everyone is guaranteed by law to own any amount of property as long as it is legal.
Endeleeni kumiliki pesa kiasi mnachotaka hata kama ni kwa njia ya UFISADI, WIZI, UBADHIRIFU.... lakini sio ARDHI. Ardhi ni bidhaa ya aina yake. Tangu mwaka 1967, Watanzania tunajua ardhi ni mali yetu sote. Tugawane hii ardhi yetu kwa utaratibu unaokubalika, unaozingatia maslahi ya WENGI. Sio Kimaro peke yake.
 
Nionavyo mimi wananchi wamechoka na wamechoshwa na tabia za viongozi wetu, jamani hivi vilio vya mafisadi kila siku tunavisikia si mitaani si JF lakini hakuna hatua hakuna sheria, na wananchi wamechoshwa na wamekosa imani na viongozi hivyo kila mmoja anaonekana fisadi na ndio hapo sheria mkononi msije tu sikia siku kiongfozi kachomwa moto..tulisikia mkapa kuzomewa, kikwete kupigwa mawe, balali kuvamiwa leo hii kimaro bado mengi yatakuja, serikali na viongozi wetu wabadilike, hakuna kiongozi asiyejilimbikizia mali wakati mwananchi anaishi kwa chini ya dola moja na hana hata nusu eka wakati tunadanganywa eti ardhi ni mali ya serikali!!! unakuta mheshimiwa ana ekari 1000 amezungusha senyenge au ukuta hakuna maedeleo yoyote hata umeme unashindwa kuwafikia wananchi waliopo maeneo ya mbele yake kwa kuangalia gharama za nguzo amabzo zitapita kwenye hilo eneo na kama tujuavyo nguzo wananchi mnanunua au kuchangia ili muwekewe umeme, kwani watu wasivamie kupunguza!!! na je

tujiulize kwanini wananchi hao waende hapo tu hakuna wawekezaji wengine hapo, kipo kilichowasibu wanatakiwe wasikilizwe sio kuchukuliwa hatua, na pia kama serikali inajua kuchukua hatua ianze na mafisadi wanaofanya wananchi kukosa amani na kuikiria vitendo vya namna hiyo,
 
Back
Top Bottom