Mbu
JF-Expert Member
- Jan 11, 2007
- 12,752
- 7,846
...hivi,
inakuaje mtu anakubali kudhalilika na kunyanyasika kisa
mapenzi.Ni kweli hawezi kula, kulala wala maisha bila huyo mtu?
au ni false hopes kwamba atabadilika tabia?
...Unakuta mwanaume haipiti mwezi anakuja kazini amevimba jicho, halioni sawasawa na damu imevilia. Ukimuuliza anakwambia nimejigonga na mlango.
Kumbe, jana yake alichezea kipondo cha kumtosha toka kwa mkewe,
kosa; 'anajitia jeuri sana!'...
...au, unamkuta mwanamke kakondeana, hana raha yeye ni kilio tu
na misononeko... kisa; Mume wa mtu hamjali, wala hana muda naye, eti muda wote anashinda na Mkewe, anakuja kula uroda tu!
...au mtu ananyimwa unyumba bure bure tuuu, au kila siku ya mungu unanuniwa bure bure! Kama hiyo haitoshi, mtu huyo huyo anayekutenda linapokuja suala la 'chakula cha usiku', anataka ajipakulie ale halafu akimaliza hafuniki wala kupangusa chombo..
shida yote ya nini? Utumwa wa mapenzi ni; udhaifu wa maamuzi/kujiamini, ...au ndio; Mapenzi ya kweli ni kujishusha(?)
Jadili.
inakuaje mtu anakubali kudhalilika na kunyanyasika kisa
mapenzi.Ni kweli hawezi kula, kulala wala maisha bila huyo mtu?
au ni false hopes kwamba atabadilika tabia?
...Unakuta mwanaume haipiti mwezi anakuja kazini amevimba jicho, halioni sawasawa na damu imevilia. Ukimuuliza anakwambia nimejigonga na mlango.
Kumbe, jana yake alichezea kipondo cha kumtosha toka kwa mkewe,
kosa; 'anajitia jeuri sana!'...
...au, unamkuta mwanamke kakondeana, hana raha yeye ni kilio tu
na misononeko... kisa; Mume wa mtu hamjali, wala hana muda naye, eti muda wote anashinda na Mkewe, anakuja kula uroda tu!
...au mtu ananyimwa unyumba bure bure tuuu, au kila siku ya mungu unanuniwa bure bure! Kama hiyo haitoshi, mtu huyo huyo anayekutenda linapokuja suala la 'chakula cha usiku', anataka ajipakulie ale halafu akimaliza hafuniki wala kupangusa chombo..
shida yote ya nini? Utumwa wa mapenzi ni; udhaifu wa maamuzi/kujiamini, ...au ndio; Mapenzi ya kweli ni kujishusha(?)
Jadili.