Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,893
- 16,319
S.hikamooni wakubwa zangu wote wa hapa JamiiForums.
Ndugu zangu Watanzania;
Kuna tofauti kubwa sana kati ya kusoma na kuwa na akili nyingi. Kuna watu waliishia darasa la (7) tu kwa sababu ya umasikini wa nyumbani kwao wakashindwa kuendelea na masomo.
Kuna watu hawajasoma sana (unakuta mtu ameishia darasa la saba tu mwaka 1991) ila wana akili sana hata ukikutana nao mtaani katika maisha ya kila siku.
Namna wanavyopangilia kazi zao au hata ratiba zao za kila siku, unajua kabisa huyu mwamba aliishia darasa la 7 kwa sababu ya umasikini tu na kama angesoma sana angekuwa mtu mmoja hatari kweli kweli.
Wewe jenga picha wale wezi wa pale kariakoo wanakuibia mfukoni bila hata wewe kujua kama kuna mkono umeingia ndani ya mfuko wako wa suruali na kuchukua pesa yako ya dagaa. Zile ni akili nyingi sana sema tu zimeelekezwa pahala pasipo stahili.
KISA KIDOGO CHA MIMI KUUZIWA KIPANDE CHA SABUNI KWA 20,000/= NIKIDHANIA NI SIMU
===========
Nikiwa kidato cha 6 miaka hiyo ya 2000 na kitu, niliwahi kuuziwa kipande kidogo cha sabuni nikidhani kuwa ni simu.
Nilikuwa ninatoka Tabata Segerea nyumbani mama yangu mkubwa nilienda kumtembelea siku ya ijumaa jioni sasa nikawa ninarudi jumapili mchana ili nifanye maandalizi ya usafi wa nguo kwa ajili ya shule kesho yake ambayo ni Jumatatu.
Baada ya kushuka kutoka katika daladala pale mtaa wa Kongo akatokea jamaa mmoja rika langu akiwa ameshika simu aina ya nokia zile za jeneza za zamani akawa ananioneshea kwa ukaribu basi mimi nikaichukua ile simu nikaikagua vema kisha nikamuuliza bei gani, yeye akasema ni 20,000/=. Nikasema kimoyomoyo poa ngoja nichukue hii ngoma ili na mimi nikatambe huko mitaani.
Alafu hiyo pesa yenyewe sasa ndio nilikuwa nimepewa kama pocket money ya mwezi mzima na huyo mama yangu mkubwa.
Yule jamaa rika langu kabisa akaniambia mwamba njoo huku hapo barabarani sana, basi mimi nikaenda, akanipa tena simu nikaikagua kwa mara ya pili, simu ipo sawa haina tatizo.
Sawa. Basi mwamba akaichukua simu akaiweka katika bahasha fulani hivi ya kaki kisha na mimi nikampa pesa yake 20,000/= huyo nikaondoka.
Kabla sijaenda mbali, baada ya kupanda daladala za kwenda home kwetu kurasini huku Dar, nikaona ngoja nifungue bahasha nitoe simu yangu walau nicheze hata game la nyoka niji-keep busy, halooooo!
Nilikutana na kipande cha sabuni ya kodrai hahahahahaaaaa size ile ile kama simu ya Nokia ya jeneza (3310) kikiwa kinaniangalia tu. Kwa kweli roho iliniuma sana.
Ukizingatia 20,000/= ni pesa nyingi sana kwa miaka ile alafu mimi bado mwanafunzi sina majukumu mengi.
Basi sikuwa na jinsi zaidi ya kuvumilia hasira nilizokuwa nazo na nilipofika home nikafua nguo zangu kwa kutumia sabuni ya kipande ya 20,000/= hahahahaa.
===========
Kuna watu wenye akili nyingi lakini hawajasoma sana hususan huko vijijini. Unakuta mwanakijiji yeye hawajawahi kuwa na njaa bomani kwake.
Miaka yote anavuna mahindi mengi, anafuga ng'ombe wake vizuri na anasomesha watoto kwa kuuza maziwa tu mpaka watoto wanamaliza form six. Siku akiamua kukuandikia barua, huo muandiko wake utadhani labda ni mwalimu wa secondary.
Kuna watu hawajasoma sana ila wana akili nyingi kweli. Je, ulishawahi kukutana nao (mbali na wizi) katika maisha yako?
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO. MUNGU IBARIKI NCHI YANGU.
Ndugu zangu Watanzania;
Kuna tofauti kubwa sana kati ya kusoma na kuwa na akili nyingi. Kuna watu waliishia darasa la (7) tu kwa sababu ya umasikini wa nyumbani kwao wakashindwa kuendelea na masomo.
Kuna watu hawajasoma sana (unakuta mtu ameishia darasa la saba tu mwaka 1991) ila wana akili sana hata ukikutana nao mtaani katika maisha ya kila siku.
Namna wanavyopangilia kazi zao au hata ratiba zao za kila siku, unajua kabisa huyu mwamba aliishia darasa la 7 kwa sababu ya umasikini tu na kama angesoma sana angekuwa mtu mmoja hatari kweli kweli.
Wewe jenga picha wale wezi wa pale kariakoo wanakuibia mfukoni bila hata wewe kujua kama kuna mkono umeingia ndani ya mfuko wako wa suruali na kuchukua pesa yako ya dagaa. Zile ni akili nyingi sana sema tu zimeelekezwa pahala pasipo stahili.
KISA KIDOGO CHA MIMI KUUZIWA KIPANDE CHA SABUNI KWA 20,000/= NIKIDHANIA NI SIMU
===========
Nikiwa kidato cha 6 miaka hiyo ya 2000 na kitu, niliwahi kuuziwa kipande kidogo cha sabuni nikidhani kuwa ni simu.
Nilikuwa ninatoka Tabata Segerea nyumbani mama yangu mkubwa nilienda kumtembelea siku ya ijumaa jioni sasa nikawa ninarudi jumapili mchana ili nifanye maandalizi ya usafi wa nguo kwa ajili ya shule kesho yake ambayo ni Jumatatu.
Baada ya kushuka kutoka katika daladala pale mtaa wa Kongo akatokea jamaa mmoja rika langu akiwa ameshika simu aina ya nokia zile za jeneza za zamani akawa ananioneshea kwa ukaribu basi mimi nikaichukua ile simu nikaikagua vema kisha nikamuuliza bei gani, yeye akasema ni 20,000/=. Nikasema kimoyomoyo poa ngoja nichukue hii ngoma ili na mimi nikatambe huko mitaani.
Alafu hiyo pesa yenyewe sasa ndio nilikuwa nimepewa kama pocket money ya mwezi mzima na huyo mama yangu mkubwa.
Yule jamaa rika langu kabisa akaniambia mwamba njoo huku hapo barabarani sana, basi mimi nikaenda, akanipa tena simu nikaikagua kwa mara ya pili, simu ipo sawa haina tatizo.
Sawa. Basi mwamba akaichukua simu akaiweka katika bahasha fulani hivi ya kaki kisha na mimi nikampa pesa yake 20,000/= huyo nikaondoka.
Kabla sijaenda mbali, baada ya kupanda daladala za kwenda home kwetu kurasini huku Dar, nikaona ngoja nifungue bahasha nitoe simu yangu walau nicheze hata game la nyoka niji-keep busy, halooooo!
Nilikutana na kipande cha sabuni ya kodrai hahahahahaaaaa size ile ile kama simu ya Nokia ya jeneza (3310) kikiwa kinaniangalia tu. Kwa kweli roho iliniuma sana.
Ukizingatia 20,000/= ni pesa nyingi sana kwa miaka ile alafu mimi bado mwanafunzi sina majukumu mengi.
Basi sikuwa na jinsi zaidi ya kuvumilia hasira nilizokuwa nazo na nilipofika home nikafua nguo zangu kwa kutumia sabuni ya kipande ya 20,000/= hahahahaa.
===========
Kuna watu wenye akili nyingi lakini hawajasoma sana hususan huko vijijini. Unakuta mwanakijiji yeye hawajawahi kuwa na njaa bomani kwake.
Miaka yote anavuna mahindi mengi, anafuga ng'ombe wake vizuri na anasomesha watoto kwa kuuza maziwa tu mpaka watoto wanamaliza form six. Siku akiamua kukuandikia barua, huo muandiko wake utadhani labda ni mwalimu wa secondary.
Kuna watu hawajasoma sana ila wana akili nyingi kweli. Je, ulishawahi kukutana nao (mbali na wizi) katika maisha yako?
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO. MUNGU IBARIKI NCHI YANGU.