IsayaMwita
JF-Expert Member
- Mar 9, 2008
- 1,127
- 140
mmh.. yamekuwa haya sasa! just ignore me please.
Ilikuwa mwaka 2008, wakati huo JF ikijulikana kama Jambo forums, hapa ndipo nilipoanza kumfahamu huyu Mzee Mwanakijiji, nilibandika PM yangu hapa jamvini, kwa kweli haikuwa na mtiririko mzuri, nilikuwa nasimuliwa kisa cha Mzee Maganya wa kule kwetu Mara.
Unajua aliniambia nini Mzee Mwanakijiji?
Akasema hivi......
Mwita una hoja nzuri ila elimu yako inatia shaka.
Nilijisikia vibaya sana, nikawaza moyoni mwangu hebu huyu mtu kajuaje kuwa elimu yangu ni ya kubahatisha? tena 4m 6 ya kutafuta tafuta?kadiploma ka graphics?
Lakini wachangiaji wengine siku zile wakaniponda, wakanikejeli sana, kwake yeye Mzee Mwanakijiji akanishauri nitie bidii ili niweze kuwakilisha hoja kwa usahihi. Mwaka ule ule nikaamua kutafuta chuo(university) na kuendelea kusaka maarifa.
Mzee Mwanakijiji ana busara, hekima.
Mungu amuongezee siku za kuishi, ili watanzania walio wengi wafaidi kisima hiki cha busara na hekima na pia tunamuomba sasa arudi nyumbani tuikomboe nchi yetu.