Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Ushauri umetolewa Bungeni kwamba JK amtoe Pinda kwenye U-PM kwa sababu inaonekana Pinda ni kikwazo katika mambo mengi. Mie nashauri kwamba kama Prof. Mwandosya amepona, basi JK afikirie kwa makini sana juu ya kumteua Professor Mwandosya kuwa Waziri Mkuu mpya. Mwandosya anaonekana kuwa mtendaji makini sana, na anaheshimika ndani na nje ya CCM, na ndani na nje ya nchi. Kama afya yake sio tatizo basi katika kipindi hiki kilichobaki cha uongozi wa JK ingekuwa busara sana kwa JK kumteua Prof Mwandosya kama Waziri Mkuu.
Nyongeza: Tunahitaji PM mwenye sifa muhimu zifuatazo:
1. Mtu aliyethibitika kuwa mchapa kazi, makini (asiyekurupuka kuongea au kutenda) na mwenye uwezo wa kuelewa changamoto za utendaji wa serikali
2. Mtu anaeheshimika si tu ndani ya CCM, bali na nje pia kwa vyama vingine vya siasa, na ndani ya Bunge
3. Mtu ambae ana uwezo wa kuwakemea mawaziri na wakamheshimu anachosema, wakijua ni mtu serious na kazi
4. Mtu ambae kuteuliwa kwake kuwa PM kutasaidia sana kuziba nyufa ndani ya CCM za huko nyuma zilizotokana na kugombea uraisi, hasa katika pindi hii ya lala salama ya JK.
5. Mtu atakaetoa ushauri mzuri kwa JK katika mambo ya kila siku yanayohusu Baraza la Mawaziri na utendaji wake
6. Mtu atakaesaidia kurudisha hadhi na heshima ya cheo cha Waziri Mkuu katika macho ya wananchi kwa ujumla
Nyongeza: Tunahitaji PM mwenye sifa muhimu zifuatazo:
1. Mtu aliyethibitika kuwa mchapa kazi, makini (asiyekurupuka kuongea au kutenda) na mwenye uwezo wa kuelewa changamoto za utendaji wa serikali
2. Mtu anaeheshimika si tu ndani ya CCM, bali na nje pia kwa vyama vingine vya siasa, na ndani ya Bunge
3. Mtu ambae ana uwezo wa kuwakemea mawaziri na wakamheshimu anachosema, wakijua ni mtu serious na kazi
4. Mtu ambae kuteuliwa kwake kuwa PM kutasaidia sana kuziba nyufa ndani ya CCM za huko nyuma zilizotokana na kugombea uraisi, hasa katika pindi hii ya lala salama ya JK.
5. Mtu atakaetoa ushauri mzuri kwa JK katika mambo ya kila siku yanayohusu Baraza la Mawaziri na utendaji wake
6. Mtu atakaesaidia kurudisha hadhi na heshima ya cheo cha Waziri Mkuu katika macho ya wananchi kwa ujumla