Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,018
- 144,377
Rais Samia kama unavyopenda kutumia mtandao wa X kuelezea mambo yanayohusu nchi na Watanzania ikiwemo kutoa taarifa mbalimbali za Serikali yako, nakushauri utumie mtandao huo kupata maoni ya wananchi ni namna gani wameupokea mkataba wa Bandari ambao umekuwa gumzo kuu hapa nchini.
Rais Samia ,mijadala mingi inaibuka na kupita, ila huu wa Bandari ni wazi umekuwa na utakuwa endelevu, hivyo fanya jambo la tofauti ,na hili si lingine bali kuitisha kura ya maoni isiyo rasimi kupitia mitandao na hapa napendekeza utumie mtandao wa twitter au ukiweza kupitia hapa JamiiForums vile vile.
Au ikiwezekana, jukumu hilo wape wasaidizi wako kama vile Msemaji wa Serikali ambae nae ana akaunti X
Swali la msingi liwe ni je, unaunnga mkono mkataba huu wa uwekezaji kwenye bandari zetu?
Majibu yawe ni ya kuchagua kati ya haya yafuatayo:
1. NDIO
2.HAPANA
3.SIJUI
Hilo swali mnaweza kuliuiza kwa kuliandika mnavyoona inafaa, ila ujumbe uwe ni huo huo.
Mhe. Rais, nukuu hii hapa chini ya Baba wa Taifa ikuongoze.
Julius Nyerere: Hatuwezi kutatua matatizo yetu kwa kujidanganya kuwa hayapo.
Rais Samia ,mijadala mingi inaibuka na kupita, ila huu wa Bandari ni wazi umekuwa na utakuwa endelevu, hivyo fanya jambo la tofauti ,na hili si lingine bali kuitisha kura ya maoni isiyo rasimi kupitia mitandao na hapa napendekeza utumie mtandao wa twitter au ukiweza kupitia hapa JamiiForums vile vile.
Au ikiwezekana, jukumu hilo wape wasaidizi wako kama vile Msemaji wa Serikali ambae nae ana akaunti X
Swali la msingi liwe ni je, unaunnga mkono mkataba huu wa uwekezaji kwenye bandari zetu?
Majibu yawe ni ya kuchagua kati ya haya yafuatayo:
1. NDIO
2.HAPANA
3.SIJUI
Hilo swali mnaweza kuliuiza kwa kuliandika mnavyoona inafaa, ila ujumbe uwe ni huo huo.
Mhe. Rais, nukuu hii hapa chini ya Baba wa Taifa ikuongoze.
Julius Nyerere: Hatuwezi kutatua matatizo yetu kwa kujidanganya kuwa hayapo.