Mr Dudumizi
JF-Expert Member
- Sep 9, 2020
- 6,880
- 12,319
Habari zenu wanaJF wenzangu, ama baada ya salam ningependa kuendelea na mada yangu hapa jukwaani.
Ndugu zangu kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Wakati raisi Samia alipoingia madarakani, haikupita hata miezi sita akaanza pangua pangua ya viongozi wakubwa pale ikulu akiwemo aliekuwa katibu mkuu kiongozi mhe Dr Bashiru ambae alikuwa amechukua nafasi hiyo muda mfupi tu baada ya aliekuwepo kufariki.
Wengi walianza kulalamika na kumlaumu Rais kwa hatua yake hiyo ya pangua pangua pale state house, mpaka wengine wakafikia hatua ya kusema kuwa raisi ana ugomvi sijui na sukuma gang, team Magufuli nk. Ila nyuma ya pazia hawakuwa wanajua ni kwanini raisi aliamua kufanya vile na kwa sababu gani.
Cheo cha katibu mkuu kiongozi ni cheo kikubwa sana kimamlaka, hivyo sio rahisi kuondolewa tu hivi hivi kienyeji bila kuwa na sababu ya msingi. Hivyo raisi kumuondoa mhe Bashiru katika nafasi ile ghafla bin vuu kulikuwa na sababu maalumu ambayo wengi hawakuijua.
Leo hii ukisikiliza kwa makini ile interview ya CDF mstaafu mhe Mabeyo, na kile kilichotokea baada ya mama kuingia (pangua pangua) utaona kabisa ni kina nani ambao walikuwa na mpango wa kupindisha katiba. Nakumbuka CDF Mabeyo wakati wa hotuba yake pale msibani alimwambia mhe raisi kuwa ana ujumbe wake ambao atamwambia pindi watapokuwa falagha kati yake na raisi.
Miezi kadhaa mbele baada ya msiba kuisha Rais Samia akaanza pangua pangua ambayo ilipelekea mhe Bashiru kuwa miongoni mwa waliotenguliwa, huku waziri mkuu na mawaziri wengine wakiendelea kubaki na vyeo vyao hadi leo.
So Rais anapotengua au kutea mtu huwa anafanya hivyo baada ya kupata taarifa za kutosha za anaeteuliwa au tenguliwa.
Leo niishie hapa.
Ndugu zangu kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Wakati raisi Samia alipoingia madarakani, haikupita hata miezi sita akaanza pangua pangua ya viongozi wakubwa pale ikulu akiwemo aliekuwa katibu mkuu kiongozi mhe Dr Bashiru ambae alikuwa amechukua nafasi hiyo muda mfupi tu baada ya aliekuwepo kufariki.
Wengi walianza kulalamika na kumlaumu Rais kwa hatua yake hiyo ya pangua pangua pale state house, mpaka wengine wakafikia hatua ya kusema kuwa raisi ana ugomvi sijui na sukuma gang, team Magufuli nk. Ila nyuma ya pazia hawakuwa wanajua ni kwanini raisi aliamua kufanya vile na kwa sababu gani.
Cheo cha katibu mkuu kiongozi ni cheo kikubwa sana kimamlaka, hivyo sio rahisi kuondolewa tu hivi hivi kienyeji bila kuwa na sababu ya msingi. Hivyo raisi kumuondoa mhe Bashiru katika nafasi ile ghafla bin vuu kulikuwa na sababu maalumu ambayo wengi hawakuijua.
Leo hii ukisikiliza kwa makini ile interview ya CDF mstaafu mhe Mabeyo, na kile kilichotokea baada ya mama kuingia (pangua pangua) utaona kabisa ni kina nani ambao walikuwa na mpango wa kupindisha katiba. Nakumbuka CDF Mabeyo wakati wa hotuba yake pale msibani alimwambia mhe raisi kuwa ana ujumbe wake ambao atamwambia pindi watapokuwa falagha kati yake na raisi.
Miezi kadhaa mbele baada ya msiba kuisha Rais Samia akaanza pangua pangua ambayo ilipelekea mhe Bashiru kuwa miongoni mwa waliotenguliwa, huku waziri mkuu na mawaziri wengine wakiendelea kubaki na vyeo vyao hadi leo.
So Rais anapotengua au kutea mtu huwa anafanya hivyo baada ya kupata taarifa za kutosha za anaeteuliwa au tenguliwa.
Leo niishie hapa.