Kauli ya CDF mstaafu kuhusu waliotaka kupindisha katiba ili Rais Samia asiapishwe inanipa picha halisi ya kwanini Bashiru na wenzake walitenguliwa

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Sep 9, 2020
6,880
12,319
Habari zenu wanaJF wenzangu, ama baada ya salam ningependa kuendelea na mada yangu hapa jukwaani.

Ndugu zangu kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Wakati raisi Samia alipoingia madarakani, haikupita hata miezi sita akaanza pangua pangua ya viongozi wakubwa pale ikulu akiwemo aliekuwa katibu mkuu kiongozi mhe Dr Bashiru ambae alikuwa amechukua nafasi hiyo muda mfupi tu baada ya aliekuwepo kufariki.

Wengi walianza kulalamika na kumlaumu Rais kwa hatua yake hiyo ya pangua pangua pale state house, mpaka wengine wakafikia hatua ya kusema kuwa raisi ana ugomvi sijui na sukuma gang, team Magufuli nk. Ila nyuma ya pazia hawakuwa wanajua ni kwanini raisi aliamua kufanya vile na kwa sababu gani.

Cheo cha katibu mkuu kiongozi ni cheo kikubwa sana kimamlaka, hivyo sio rahisi kuondolewa tu hivi hivi kienyeji bila kuwa na sababu ya msingi. Hivyo raisi kumuondoa mhe Bashiru katika nafasi ile ghafla bin vuu kulikuwa na sababu maalumu ambayo wengi hawakuijua.

Leo hii ukisikiliza kwa makini ile interview ya CDF mstaafu mhe Mabeyo, na kile kilichotokea baada ya mama kuingia (pangua pangua) utaona kabisa ni kina nani ambao walikuwa na mpango wa kupindisha katiba. Nakumbuka CDF Mabeyo wakati wa hotuba yake pale msibani alimwambia mhe raisi kuwa ana ujumbe wake ambao atamwambia pindi watapokuwa falagha kati yake na raisi.

Miezi kadhaa mbele baada ya msiba kuisha Rais Samia akaanza pangua pangua ambayo ilipelekea mhe Bashiru kuwa miongoni mwa waliotenguliwa, huku waziri mkuu na mawaziri wengine wakiendelea kubaki na vyeo vyao hadi leo.

So Rais anapotengua au kutea mtu huwa anafanya hivyo baada ya kupata taarifa za kutosha za anaeteuliwa au tenguliwa.

Leo niishie hapa.
 
..Mabeyo anastahili lawama.

..Kwanini MAKAMU WA RAIS hakuwa mtu wa kwanza kupewa taarifa kuwa Rais amefariki?

..Nimemsikia Mabeyo akisema eti kulikuwa na mjadala wa nani atangaze kifo cha Rais.

..Hivi Mabeyo na usomi wake, kutumikia jeshini kwa miongo kadhaa, na kutembelea nchi mbalimbali, hajui nani ana mamlaka ya kutangaza kifo cha Raisi? Kwamba walihitaji majadiliano?
 
..Mabeyo anastahili lawama.

..Kwanini MAKAMU WA RAIS hakuwa mtu wa kwanza kupewa taarifa kuwa Rais amefariki?

..Nimemsikia Mabeyo akisema eti kulikuwa na mjadala wa nani atangaze kifo cha Rais.

..Hivi Mabeyo na usomi wake, kutumikia jeshini kwa miongo kadhaa, na kutembelea nchi mbalimbali, hajui nani ana mamlaka ya kutangaza kifo cha Raisi? Kwamba walihitaji majadiliano?
Hilo hata mimi limenishangaza. Lkn hata kama alikuwa hajui hilo, ina maana alishindwa kuwa na mwanasheria ambae angemwambia ni nani mwenye jukumu la kutangaza kifo cha raisi au kiongozi mkuu wa serikali.

Toka lini kifo cha mkuu wa nchi kikatangazwa na katibu mkuu kiongozi au waziri mkuu huku makamu wa raisi akiwa nchini!
 
..Mabeyo anastahili lawama.

..Kwanini MAKAMU WA RAIS hakuwa mtu wa kwanza kupewa taarifa kuwa Rais amefariki?

..Nimemsikia Mabeyo akisema eti kulikuwa na mjadala wa nani atangaze kifo cha Rais.

..Hivi Mabeyo na usomi wake, kutumikia jeshini kwa miongo kadhaa, na kutembelea nchi mbalimbali, hajui nani ana mamlaka ya kutangaza kifo cha Raisi? Kwamba walihitaji majadiliano?
Nawe zuzu.

Sijui unauliza maswali gani!
 
Hilo hata mimi limenishangaza. Lkn hata kama alikuwa hajui hilo, ina maana alishindwa kuwa na mwanasheria ambae angemwambia ni nani mwenye jukumu la kutangaza kifo cha raisi au kiongozi mkuu wa serikali.

Toka lini kifo cha mkuu wa nchi kikatangazwa na katibu mkuu kiongozi au waziri mkuu huku makamu wa raisi akiwa nchini!
Hiyo ni meseji kua Makamu wa Rais hakuaminiwa hata na Rais mwenyewe.
 
..Mabeyo anastahili lawama.

..Kwanini MAKAMU WA RAIS hakuwa mtu wa kwanza kupewa taarifa kuwa Rais amefariki?

..Nimemsikia Mabeyo akisema eti kulikuwa na mjadala wa nani atangaze kifo cha Rais.

..Hivi Mabeyo na usomi wake, kutumikia jeshini kwa miongo kadhaa, na kutembelea nchi mbalimbali, hajui nani ana mamlaka ya kutangaza kifo cha Raisi? Kwamba walihitaji majadiliano?
Kama umeskiliza vzuri CDF Mabeyo alijua nani anatakiwa atangaze na aliweka msimamo huo. Na tumpongeze kwamba katika ile tension na kujadili ilijulikana wazi wazalendo na waasi ni wapi. Kazi yake aliifanya vzuri sana. Angeweza kutumia nguvu za kijeshi lakini busara ilitumika ili wanafiki wajikaange
 
Habari zenu wanaJF wenzangu, ama baada ya salam ningependa kuendelea na mada yangu hapa jukwaani.

Ndugu zangu kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Wakati raisi Samia alipoingia madarakani, haikupita hata miezi sita akaanza pangua pangua ya viongozi wakubwa pale ikulu akiwemo aliekuwa katibu mkuu kiongozi mhe Dr Bashiru ambae alikuwa amechukua nafasi hiyo muda mfupi tu baada ya aliekuwepo kufariki.

Wengi walianza kulalamika na kumlaumu Rais kwa hatua yake hiyo ya pangua pangua pale state house, mpaka wengine wakafikia hatua ya kusema kuwa raisi ana ugomvi sijui na sukuma gang, team Magufuli nk. Ila nyuma ya pazia hawakuwa wanajua ni kwanini raisi aliamua kufanya vile na kwa sababu gani.

Cheo cha katibu mkuu kiongozi ni cheo kikubwa sana kimamlaka, hivyo sio rahisi kuondolewa tu hivi hivi kienyeji bila kuwa na sababu ya msingi. Hivyo raisi kumuondoa mhe Bashiru katika nafasi ile ghafla bin vuu kulikuwa na sababu maalumu ambayo wengi hawakuijua.

Leo hii ukisikiliza kwa makini ile interview ya CDF mstaafu mhe Mabeyo, na kile kilichotokea baada ya mama kuingia (pangua pangua) utaona kabisa ni kina nani ambao walikuwa na mpango wa kupindisha katiba. Nakumbuka CDF Mabeyo wakati wa hotuba yake pale msibani alimwambia mhe raisi kuwa ana ujumbe wake ambao atamwambia pindi watapokuwa falagha kati yake na raisi.

Miezi kadhaa mbele baada ya msiba kuisha Rais Samia akaanza pangua pangua ambayo ilipelekea mhe Bashiru kuwa miongoni mwa waliotenguliwa, huku waziri mkuu na mawaziri wengine wakiendelea kubaki na vyeo vyao hadi leo.

So Rais anapotengua au kutea mtu huwa anafanya hivyo baada ya kupata taarifa za kutosha za anaeteuliwa au tenguliwa.

Leo niishie hapa.
Mbona Bado wapo na Wana Vyeo vingi tuu?
 
Hilo hata mimi limenishangaza. Lkn hata kama alikuwa hajui hilo, ina maana alishindwa kuwa na mwanasheria ambae angemwambia ni nani mwenye jukumu la kutangaza kifo cha raisi au kiongozi mkuu wa serikali.

Toka lini kifo cha mkuu wa nchi kikatangazwa na katibu mkuu kiongozi au waziri mkuu huku makamu wa raisi akiwa nchini!
Nani sasa alimwambia kuwa makamu ndiyo anastahili kutangaza kifo Cha Rais?
 
Back
Top Bottom