Ushauri: Kwako Waziri wa Nishati, Tumia mkakati huu kama mpango wa dharula kipindi hiki cha uhaba wa mafuta

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Apr 10, 2019
2,590
4,603
Kwa kuwa Waziri wa Nishati umepewa na jukumu la kuratibu shughuli za serikali ukiwa kama Naibu Waziri mkuu, ninaamini jukumu hilo limekuja kipindi sahihi na linaweza kukusaidia katika majukumu yako kama Waziri wa nishati hususani kipindi hiki cha uhaba wa mafuta.

Kwanza ninakushauri, katika dharula hii ya uhaba wa mafuta uanze na kuratibu matumizi ya magari ya Serikali kwa viongozi ambayo mengi yanatumia mafuta mengi. Katika kipindi hiki cha mpito viongozi watumie usafiri wa Umma.

Pili, misafara mikubwa ya viongozi pia iratibiwe. Katika kipindi hiki cha mpito cha uhaba wa mafuta tumia madaraka yako kuratibu matumizi ya mafuta yanayotumika katika misafara.

Tatu, ili kubaini uhalisia wa mafuta yaliyopo tafuta Teknolojia ya kubaini kiwango ambacho kimeingizwa na kilichobaki kutoka hapo wizarani. Hiyo itakuwa rahisi kuwabaini wanaoficha mafuta.

Nne, matumizi ya magari binafsi pia yadhibitiwe na kuratibiwa kipindi hiki. Utaratibu maalumu uwekwe ili wenye usafiri binafsi watumie usafiri wa Umma.
 
Hivi hamjasikia yupo kwenye majukumu ya Unaibu Waziri Mkuu kufanya Coordination ya Ofisi ya Waziri Mkuu na kujichotea uzoefu wa kazi hio yaan Naibu Waziri wa Nishati hamumjui au tuwape jina lake Stephen Byabato hamumjui?
 
Mtoa post kuna point umehimiza matumiz yaa usafiri wa umma ..naomba nkwambie tz n moja ya nchi yenye magari machache sana hapaa dunian...
 
Kwa kuwa Mhe.Waziri wa nishati umepewa na jukumu la kuratibu shughuli za serikali ukiwa kama Naibu Waziri mkuu, ninaamini jukumu hilo limekuja kipindi sahihi na linaweza kukusaidia katika majukumu yako kama Waziri wa nishati hususani kipindi hiki cha uhaba wa mafuta...
Yawezekana una hoja but ni mamb kibongobongo hayatekelezeki cz c tawala ya kuishi kwa precautions na kubana matumiz!!
 
Mtoa post kuna point umehimiza matumiz yaa usafiri wa umma ..naomba nkwambie tz n moja ya nchi yenye magari machache sana hapaa dunian...
Pia, ni nchi yenye wasafiri wachache ,magari yaliyopo yakiratibiwa vizuri yanatosheleza katika kipindi hiki
 
Duniani huko mafuta yapo kibao, BoT wanasema wanazo dolar za kutosha, uhaba wa mafuta unatoka wapi??

Dawa ni kutafuta chanzo halisi cha tatizo na kukiweka bayana. Tujue mvhawi ni nani na kwa namna gana tunakomesha tatizo hili lisijirudie tena.
 
Back
Top Bottom