Ushauri kwa waliochaguliwa UDOM

Duh! Afadhali bwana umewaambia mimi ni mjasiliamali hapa maeneo ya jamatin!
labda kwa upande wangu sina kipya ila naomba Niongezee hapo kwenye ukibaka(wapga ndole) nikianza na wadada na mikoba yao ile mikubwa(hand bag) utakuta wadada wamesmama wanasubir coster anakuja kushtuka hana wallet kwa ndan au wallt ipo lkn tupu cha ajabu sjui wanatumia dawa hii nimeshudia mara 2 au 3 hivi dada analia wallet lkn tupu na imesachiwa ndan kwa ndani sasa hapo wamesmama skilizia kwenye kusukumana kwaajili ya kupanda hakuna 3rd wala 2nd year ambao haendi na move hapo kalia sasa hawa new 1st ndo mamaaaaa!

Sasa ukija kwa hawa masela wenzangu mtu anaamin kila mtu ni mwanachuo kaweka wallet,simu nk mfukoni hapa hamna 3rd wala (new entry) 1st year mchezo ule ule kama sehemu nyingne mnasukumana jitu linazuga linaingia huku linajbana na ku-push huku na vidole viko kazn na limependeza ka janafunzi vile! Sasa hapa u 1st na u 3rd utaonekana na protection ya mali zako! Tu! Otherwise!
Na ukimkamata mwizi wako na kidhibiti wewe na kampan yako muwe comfotable maana na wao wanakampani kubwa watkuzongazonga utasikia mwachie! Mwachie! Mara utaona hayupo!!
Na Makole utakubaliana na mimi kuwa wakishaiba wallet kituo chao ni kule shell kwa nyuma ndo dampo la IDs na kule public toilet
utasikia wamama wanaofagia "jamani watakaokuwa wantafuta vtambulisho vyao vko kwa fulan"

na niangalizo kwa woote!
 
Mawadern wapo Social na utakapofika waulizie utakaowakuta hapo na watafanya utaratibu wa Magodoro. Hata hivyo watakusaidia godoro kwa usiku huo tu kwa utaratibu maalum na kesho yake utalirudisha ili ufanye taratibu za usajili.
 
Safi saana!! bado tuna wabongo ambao wana maadili mema, huruma na uaminifu! keep it up bro Mungu atakulipa!!
 
Mawadern wapo Social na utakapofika waulizie utakaowakuta hapo na watafanya utaratibu wa Magodoro. Hata hivyo watakusaidia godoro kwa usiku huo tu kwa utaratibu maalum na kesho yake utalirudisha ili ufanye taratibu za usajili.

vp lakini mwana medicine ya hapo imetulia, pia huu ni mwaka wa ngapi wanatoa hyo kozi, hali ya maisha kwa ujumla iko vp, malecture wapo wa kutosha au niaje
 
5. Nauli kwa daladala ni Tsh 350 kwa safari yoyote ndani ya College, Kutoka Jamatini hadi Chuo ni 350 pia. Wahuni wanapiga hadi 1500/- kwani wanajua kuwa ni wageni hamjui kitu.

hapo kwenye red rekebisha mkuu ni 300/-.
Jamatini-Social/bondeni 300/-
Jamatini-Medicine 450/-
Jamatini-Education 350/-
Jamatini-Informatics 350/-
 
hapo kwenye red rekebisha mkuu ni 300/-.
Jamatini-Social/bondeni 300/-
Jamatini-Medicine 450/-
Jamatini-Education 350/-
Jamatini-Informatics 350/-

Mkuu me ntakuja na begi 1 kubwa vp nauli haitaongezeka? Lingine sijahesabia kwakua ni dogo la mgongoni.
 
Mawadern wapo Social na utakapofika waulizie utakaowakuta hapo na watafanya utaratibu wa Magodoro. Hata hivyo watakusaidia godoro kwa usiku huo tu kwa utaratibu maalum na kesho yake utalirudisha ili ufanye taratibu za usajili.
Yote 9 mbona hujawelezea kuhusu hali ya kisiasa na ushabiki wa vyama au migomo na kwa nini mwaka huu imepungua
Umenifurahisha zaidi kuhusu Canteen hasa ya Mwarabu na ubora wa vyakula vyake, na mm nawashauri waende vibanda vya mama Lishe kule chini ya uwanja Social na Vinywaji vipo waelezee
 
vp brother kuhusu college of social science, kwa upande wa hostel,mavazi na maisha kwa ujumla
 
Yote 9 mbona hujawelezea kuhusu hali ya kisiasa na ushabiki wa vyama au migomo na kwa nini mwaka huu imepungua
Umenifurahisha zaidi kuhusu Canteen hasa ya Mwarabu na ubora wa vyakula vyake, na mm nawashauri waende vibanda vya mama Lishe kule chini ya uwanja Social na Vinywaji vipo waelezee
, Nasikitika kuwaelezea vijana kwamba yale mavazi yetu na magwanda yetu tunayapenda saaaaaaaanaaa, ila dah, naogopa kusema kwamba tuyapumzishe tu nymbani, kwani hali ni mbaya sana. Ushabiki wa vyama vya siasa (Hasa vidole viwili) kwa Chuo chenu ni utata. Hata hivyo nisikukatisheni tamaa kwani hatujui mazingira yatakuwaje. We have to be situational sometimes
 
soccer vp viwanja vnatosha au?

tena vya kisasa sana, kwa uongozi ulioingia madarakani kwa sasa wamepania kuongeza kasi ya michezo chuon. Vipo viwanja vizuri kwa football, basket netball na volleyball. Hata hivyo nawe ukalete mabadiliko ktk soka. Pia yawezekana kwa presha ya masomo na ugeni usivione viwanja vyenyewe!
 
vp brother kuhusu college of social science, kwa upande wa hostel,mavazi na maisha kwa ujumla

Hapo wanapaita St social, (samahani kama ntawakwaza watu), hapo kuna mapinduzi ya mavazi, ndipo palikuwa panavaliwa vivazi. Ila kwa sasa nadhani ndio college inayoongoza kwa nidhamu ya mavazi. wanawashinda walimu kwa haiba hapo. Hostel za kumwaga sana, maisha ya hapo ndo ivyo tena, mtu pesaaaaa na watoto wa kishua. ingawa wapo watoto wa wakulima lakini nao wanabadilika wakifika hapo.

Ukiingia eneo hilo heshimu "pavement" usikate njia ukakanyaga nyasi kufuata njia zisizo rasmi, utakinukisha mapema, wako vijana wa SMA-JKT (SINA HAKIKA KAMA BADO WANALINDA ENEO HILO), unaweza kujikuta uapanda na kumwagilia hayo majani, Usimwage maji dirishani, usianike kitu chochote dirishani, utaingia matatani. Hapo ni sosho ndugu!
 
Back
Top Bottom