Katika hali isiyo ya kawaida tumekuwa tunakaa na watoto wetu nyumbani ambao wanasifa ya kujiunga chuo kikuu au ameisha chaguliwa kujiunga chuo kikuu tayari lakini hajawa na uhakika wa kupata mkopo utakaomuwezesha kujiunga kutoka bodi ya mkopo kwa wasiwasi mkubwa sana kwa sababu zifuatazo.
1) Mtoto anaishi na mzazi nyumbani bila kufanya maandalizi yoyote ya mtoto kwa kuwa hajawa na uhakika wa mkopo.
2) Inamsababishia mtoto kutojiamini na maombi aliyofanya ya mkopo.
3) Mtoto na mzazi wake wote wanakuwa watu wa kuuliza kila siku bila kujenga msingi wa kujiamini.
4) Hali hii imejengea familia nyingi zenye watoto wenye sifa kuwa na hali ya masikitiko makubwa wakati wa kusbiri kuona mkopo kama mtoto amepata.
5) Hali hii imefanya watoto wengi kusubiria mkopo wakati vyuo tayari vimefunguliwa na baadhi yao wakiwa wanaendelea na masomo.
USHAURi
1) Kwa kuwa bodi ya mkopo ni chombo cha umma kiwe kinaweka wazi majina ya wanafunzi ambao watapata mkopo na asilimia ngapi atapewa kwenye magazeti kuondoa sintofahamu hiyo.
2) kutoa mikopo mapema kwa wanaostahili kabla ya vyuo kufunguliwa.
3)Kutoa majina mapema kunamuwezesha mzazi kufanya maamuzi ya kufanya au kutafuta njia mbadala ya mtoto wake kuliko kuwa anachungulia kwenye mtandao kila siku bila kuwa na uhakika.
4)Mwisho kutaimarisha kujiamini kwa mtoto, mzazi na kuongeza ufaulu.
Ahsante.
1) Mtoto anaishi na mzazi nyumbani bila kufanya maandalizi yoyote ya mtoto kwa kuwa hajawa na uhakika wa mkopo.
2) Inamsababishia mtoto kutojiamini na maombi aliyofanya ya mkopo.
3) Mtoto na mzazi wake wote wanakuwa watu wa kuuliza kila siku bila kujenga msingi wa kujiamini.
4) Hali hii imejengea familia nyingi zenye watoto wenye sifa kuwa na hali ya masikitiko makubwa wakati wa kusbiri kuona mkopo kama mtoto amepata.
5) Hali hii imefanya watoto wengi kusubiria mkopo wakati vyuo tayari vimefunguliwa na baadhi yao wakiwa wanaendelea na masomo.
USHAURi
1) Kwa kuwa bodi ya mkopo ni chombo cha umma kiwe kinaweka wazi majina ya wanafunzi ambao watapata mkopo na asilimia ngapi atapewa kwenye magazeti kuondoa sintofahamu hiyo.
2) kutoa mikopo mapema kwa wanaostahili kabla ya vyuo kufunguliwa.
3)Kutoa majina mapema kunamuwezesha mzazi kufanya maamuzi ya kufanya au kutafuta njia mbadala ya mtoto wake kuliko kuwa anachungulia kwenye mtandao kila siku bila kuwa na uhakika.
4)Mwisho kutaimarisha kujiamini kwa mtoto, mzazi na kuongeza ufaulu.
Ahsante.