USHAURI: Kuhusu kukata rufaa HESLB

The thinker27

Senior Member
Sep 15, 2023
123
131
WA-IMG-20231020-7c99790d.jpg

Habari za wakati huu wadau wa elimu

Kama picha inavojieleza hicho ndicho kiasi ambacho nimepangiwa na HESLB kwa mwaka wa masomo 2023/2024....
Nahitaji ushauri, maoni, faida na hasara za kukata rufaa pamoja na utaratibu wake unavyokuwa

Sababu kuu ya kuomba kukata rufaa ni kutokana na mfumo wa bodi kukataa kusave taarifa za TASAF wakati nilipokuwa nafanya application.
Mzazi wangu ni mnufaika wa TASAF na jina langu lipo katika mfumo wake wa malipo anaopokea kutoka TASAF na hata wakati najaza namba ya utambulisho ya kaya ya TASAF katika mfumo wa maombi ya mkopo jina langu lilikua likionekana pia na nilipokuwa naliclick dashbnard ikawa inaload then inaonesha kuwa "TASAF details saved succesfully" na katiki ka kijani. ila ikawa nikienda kupreview my details kwenye kipengele cha TASAF sponsored inaandka "NO" nikawa najaribu kuwapigia bodi wakawa wananiambia kuwa ni tatizo la kimtandao tu hivyo basi nikawa najaribu kujaza namba ya TASAF mara kwa mara .nikajaribu kurudia kwa takribani mwezi mzima bila mafanikio yoyote mpaka ikawa imebaki wiki 1 dirisha kufungwa ikabidi tu nisubmit taarifa maana hakukuwa na ahueni yoyote

Sasa majibu yametoka kama hivyo katika kiwango hicho na ada yangu inayotakiwa ni 1.6M. Kwa sasa baada ya majibu nimejaribu kuangalia kile kipengele cha "TASAF sponsored lakini bado imeandikwa NO, na hiyo inamaana kuwa bado HESLB HAINITAMBUI KAMA MLENGWA WA TASAF. je tatizo hili lilitokea kwangu tu au pia na kwa wengine?

Pia naomba kufahamu faida na hasara za kukata rufaa na pia je navyokata rufaa kiwango nilichopewa mwanzo kinakuwa stopped kwa muda au kinakua kishalipwa?

Naomba kuwasilisha wakuu na samahani kwa kutumia lugha ndefu ni katika hali tu kujenga kueleweka. Nawatakia majukumu mema katika ujenzi wa taifa
 
View attachment 2789175
Habari za wakati huu wadau wa elimu

Kama picha inavojieleza hicho kiasi ambacho nimepatiwa na HESLB kwa mwaka wa masomo 2023/2024.Nahitaji ushauri, maoni, faida na hasara za kukata rufaa pamoja na utaratibu wake unavyokuwa

Sababu kuu ya kuomba kukata rufaa ni kutokana na mfumo wa bodi kukataa kusave taarifa za TASAF wakati nilipokuwa nafanya application.Mzazi wangu ni mnufaika wa TASAF na jina langu lipo katika mfumo wake wa malipo anaopokea kutoka TASAF na hata wakati najaza namba ya utambulisho ya kaya ya TASAF katika mfumo wa maombi jina langu pia lilikua pia linatokea na kuliclick na ikawa inaonesha kuwa "TASAF details saved succesfully" ila ikawa nikienda kupreview my details kwenye kipengele cha TASAF sponsored inaandka "NO" nikawa najaribu kuwapigia bodi wakawa wananiambia ni mtandao tu so niwe najaribu mara kwa mara .nikajaribu kurudia kwa takribani mwezi mzima bila mafanikio mpaka ikawa imebaki wiki 1 dirisha kufungwa ikabidi tu nisubmit taarifa na majibu yametoka kama hivyo na nikienda kuangalia kipengele cha "TASAF sponsored imeandikwa NO, je hili lilitokea kwangu tu au pia na kwa wengine?

Pia naomba kufahamu faida na hasara za kukata rufaa na pia je navyokata rufaa kiwango nilichopewa mwanzo kinakuwa stopped kwa muda au kinakua kishalipwa

Naomba kuwasilisha wakuu na samahani kwa kutumia lugha ndefu ni katika kufanya maelewano.
Rufaa unaweza kukata ila kuongezewa mkopo unaweza kuongezewa au ikabaki vilevile then kuhusu mkopo wako wa awali hauwezi kuathirika so Cha muhimu Kama upo DSM nenda ofisini na details zako kipindi Cha rufaa


Then inawezekana umepewa Ada 230k lakini mnaweza kuja kuongezewa ikawa full hii imefanyika kwa wanafunzi was mwaka wa masomo 2022/2023
 
Rufaa unaweza kukata ila kuongezewa mkopo unaweza kuongezewa au ikabaki vilevile then kuhusu mkopo wako wa awali hauwezi kuathirika so Cha muhimu Kama upo DSM nenda ofisini na details zako kipindi Cha rufaa


Then inawezekana umepewa Ada 230k lakini mnaweza kuja kuongezewa ikawa full hii imefanyika kwa wanafunzi was mwaka wa masomo 2022/2023
Ahsante mkuu kwa ushauri wako ,kwa sasa niko tabora na chuo nimepata iringa so kwa kwenda sidhani kama itawezekana
 
Ahsante mkuu kwa ushauri wako ,kwa sasa niko tabora na chuo nimepata iringa so kwa kwenda sidhani kama itawezekana
Kama Hali nyumbani ni ngumu na ukawa hujaongezewa ada ,tumia boom kulipa Ada kulipa

Maisha ya iringa yapo chini katika vyakula hiyo laki sita unaweza kutenga laki tatu ukawa unaongezea Ada then laki tatu unatumia katika chakula .

Kumbuka MAARIFA ni utajiri mkubwa
 
Kijana sikushauri kukata rufaa kwa sasa kwani hali hiyo unayoiona sio kwako tu tena shukuru mungu umepata batch ya kwanza hujui wenzio huko batch za mwisho watawekewa ngapi.
Serikali inajua inachokifanya.
Wewe kuwa na subira na mambo mazuri hayataki papara.
Mwisho
 
Kama Hali nyumbani ni ngumu na ukawa hujaongezewa ada ,tumia boom kulipa Ada kulipa

Maisha ya iringa yapo chini katika vyakula hiyo laki sita unaweza kutenga laki tatu ukawa unaongezea Ada then laki tatu unatumia katika chakula .

Kumbuka MAARIFA ni utajiri mkubwa
Hivi Unaweza kukata rufaa ukanyanganywa na hiyo uliyonayo?.
 
Kama Hali nyumbani ni ngumu na ukawa hujaongezewa ada ,tumia boom kulipa Ada kulipa

Maisha ya iringa yapo chini katika vyakula hiyo laki sita unaweza kutenga laki tatu ukawa unaongezea Ada then laki tatu unatumia katika chakula .

Kumbuka MAARIFA ni utajiri mkubwa
Nakushukuru sana mkuu kwa kunipa matumaini ambayo binafsi nilikua nishaanza kuyapoteza
 
Kijana sikushauri kukata rufaa kwa sasa kwani hali hiyo unayoiona sio kwako tu tena shukuru mungu umepata batch ya kwanza hujui wenzio huko batch za mwisho watawekewa ngapi.
Serikali inajua inachokifanya.
Wewe kuwa na subira na mambo mazuri hayataki papara.
Mwisho
Ahsante mkuu kwa mawazo yako ,ila nimesikia kwamba wanufaika wa TASAF huwa wanapewa kipaumbele hata kama sio kwa hali ya kiwango cha juu
 
Ahsante mkuu kwa mawazo yako ,ila nimesikia kwamba wanufaika wa TASAF huwa wanapewa kipaumbele hata kama sio kwa hali ya kiwango cha juu
Ilikuwa hivyo zamani kipindi watu hawafaulu sana.
Lakini sasa zama zimebadilika na mambo yamekuwa tofauti kabisa.
 
Jitahidi upambane kwenye Tuition feee kijana 100%siku hizi ni ndotooo nasikia Hela za field na research pia hakunaa siku hizii so Komaa kijanaaa bumu na ada kidogo hiyo inatoshaa.. Kukataa rufaaa maana yake Upangiwe Upyaaa na kupangiwa upyaaa means unaweza kupata au kukosaa.
 
Enzi nzetu kuna kijana aliingia Top 10 tena yeye ni yatima hakuwa na wazazi kabisa alisomeshwa shule za msaada na wazungu.. Yule kijana bila CRDB kumdhamini wao asome alishaacha chuo hii kuonesha Heslb wana mioyo migumu mno so dont temper aisee unaweza juta.
 
The thinker27

1.Muda wa kukata rufaa ukifika wewe kata rufaa , mwaka jana ilitokea maajabu karibia first year wote ambao wamepata kiasi kidogo cha Fedha(sio wale waliokosa kabisa)na kukata waliokata rufaa walipata tena 100% wale waliokata tamaa na kutokata rufaa wakajutia baadae.Muda ukifika jaribu kuwa kuwa hata ukikosa kiasi cha mwanzo kinabaki hivyo hivyo.

2. Panga mikakati mapema ya kujikwamua kama ukikosa na rufaa ,kwa kuomba ndugu wakuwezeshe nk.
 
The thinker27

1.Muda wa kukata rufaa ukifika wewe kata rufaa , mwaka jana ilitokea maajabu karibia first year wote ambao wamepata kiasi kidogo cha Fedha(sio wale waliokosa kabisa)na kukata waliokata rufaa walipata tena 100% wale waliokata tamaa na kutokata rufaa wakajutia baadae.Muda ukifika jaribu kuwa kuwa hata ukikosa kiasi cha mwanzo kinabaki hivyo hivyo.

2. Panga mikakati mapema ya kujikwamua kama ukikosa na rufaa ,kwa kuomba ndugu wakuwezeshe nk.
Ni gharama kiasi gani kukata rufaa
 
Ni gharama kiasi gani kukata rufaa
Bodi ya Mkopo haulipii kiasi chochote ,gharama inategemea na stationery uliyopo ila kwa chuo kwa vile zipo nyingi kuna ushindani bei zinakuwa rahisi sana haizidi buku 5 .Ukiwa na PC na mzoefu wa kazi hizo unaweza ukafanya mwenyewe stationery ukaenda kuaattach na kuprint inakuwa gharama kama 1500 au 1000.
 
Back
Top Bottom