Usaliti wa Wabunge wa CCM kwa wananchi...

Jackbauer

JF-Expert Member
Oct 28, 2010
6,038
2,199
Kizungumkuti kinachoendelea dodoma kimedhihirisha kuwa ccm ni chama kinachofuga viongozi wasioweza kuchukua hatua.

Juzi tulishuhudia wabunge karibu wote waliochangia hoja za kamati teule wakionyesha machungu,jazba na hasira dhidi ya serikali kwa manufaa ya umma.
Baadae mh. Zitto akawatia mtegoni na kuwaambia 'maneno matupu hayavunji mfupa' na pia 'kazi ya mbwa ni kuuma na sio kubweka tu'
kama tulivyotegemea jamaa wakanasa mtegoni, wameshindwa kusaini!!

Sababu ya kushindwa kutia sahihi ni moja tu(kwa tafsiri yangu)......nayo ni WOGA WA FISI.

Huwezi kumshutumu waziri eti hachukui maamuzi wakati wewe mwenyewe umepata fursa ya kufanana na hiyo ukaogopa kufanya hivyo.

Nasema kama kuna mbunge 'kidume' kutoka ccm ajiainishe rasmi kwamba anabariki baraza la mawaziri liendelee na kazi mpaka bwana mkubwa akijisikia kulibadilisha.nataka kumuona anakusanya sahihi za wabunge 50%+1 ili akae mkao wa kumuokoa pinda pindi zitto atakapowasilisha hoja.

Kama hakuna basi huu uwe mwanzo na mwisho wa kujidai mnarukia hoja za wapinzani wakati hamna guts za kusimamia.

Makamba,zambi,sendeka,kilango,lusinde n.k jitokezeni either mmoja wenu au kwa umoja wenu mpambane na zitto.kama ikishindikana basi jitokezeni na mseme mko neutral ili wananchi wajue nani ni nani kwenye kusimamia maslahi yao..............................

Tunataka kujua kati ya YES, NEY na NEUTRAL nyie wabunge wa ccm mko wapi?


UPDATES;sehemu ya maelezo ya mheshimiwa mbunge wa nzega Dr.Hamisi kigwangalla.
Tatu, msisahau kitu kimoja cha muhimu kabisa. Kwamba, mimi ni Mbunge kutokea CCM na kama walivyo wengi wenzangu hatukusaini kwa sababu hatuwezi kuiangusha serikali ya CCM kwa hoja inayoletwa na Mbunge wa Kambi ya Upinzani! Mbunge wa Chama Tawala kuamua kuiangusha serikali ya chama chako ni sawa na kuamua kukata tawi la mti uliokalia, kwa vyovyote vile utaanguka nalo! Simple logic! Mfumo wa Bunge letu ni wa Westminster, na hivyo kuna kambi ya Upinzani (yenye interest ya kutaka kuiangusha serikali inayotawala) na Kambi ya Serikali (ambayo ina interest ya kutaka kuilinda serikali yake). Kwa maana hiyo sisi wabunge wa CCM tuna jukumu la kuilinda Serikali inayopatikana kutokana na sisi kuwa majority. Serikali ni lazima i-enjoy majority status ndani ya Bunge ili nchi itawalike kwa amani na utulivu, japokuwa haimaanishi kuruhusu ubadhirifu na ndiyo maana kwenye Party Caucus wabunge wana nguvu na fursa ya kusema chochote dhidi ya serikali ya Chama Chao. Kuna wengine wanataka Bunge liwe Bunge huru (ama 'An Indipendent Power House') disregarding political opinions/inclinations/affiliations na serikali iwe serikali, hii haiwezekani kwa katiba tuliyonayo leo. Tubadilishieni kwanza katiba na mfumo wa kufanya kazi ndipo mtutake tufanye hayo mnayoyatamani.

Nadhani nimejiweka wazi bila unafiki, sasa tujadili kwa hoja siyo kwa hisia na matusi kama hatukwenda shule vile.
my take;hivi wananzega walikutuma bungeni kuitetea serikali au kuwatetea wananzega.nadhani kazi ya kuilinda serikali ni ya mawaziri na sio wabunge.mbunge ni muwakilishi wa wananchi bungeni na sio mtetezi wa serikali bungeni.ndio maana nimesema wabunge wa ccm(ukiondoa waliosaini) mumewasaliti wananchi.
Nawasilisha...
 
Mungu tuepushe na hii laana inaitwa CCM

nyakati za uongo kujitenga na ukweli zimefika.sioni wanapata hofu gani ya kuchagua upande?!
Upinzani(kasoro cheyo),wale wabunge watatu wa ccm wameshaweka msimamo wao wazi.
 
Kizungumkuti kinachoendelea dodoma kimedhihirisha kuwa ccm ni chama kinachofuga viongozi wasioweza kuchukua hatua.

Juzi tulishuhudia wabunge karibu wote waliochangia hoja za kamati teule wakionyesha machungu,jazba na hasira dhidi ya serikali kwa manufaa ya umma.
Baadae mh. Zitto akawatia mtegoni na kuwaambia 'maneno matupu hayavunji mfupa' na pia 'kazi ya mbwa ni kuuma na sio kubweka tu'
kama tulivyotegemea jamaa wakanasa mtegoni, wameshindwa kusaini!!

Sababu ya kushindwa kutia sahihi ni moja tu(kwa tafsiri yangu)......nayo ni WOGA WA FISI.

Huwezi kumshutumu waziri eti hachukui maamuzi wakati wewe mwenyewe umepata fursa ya kufanana na hiyo ukaogopa kufanya hivyo.

Nasema kama kuna mbunge 'kidume' kutoka ccm ajiainishe rasmi kwamba anabariki baraza la mawaziri liendelee na kazi mpaka bwana mkubwa akijisikia kulibadilisha.nataka kumuona anakusanya sahihi za wabunge 50%+1 ili akae mkao wa kumuokoa pinda pindi zitto atakapowasilisha hoja.

Kama hakuna basi huu uwe mwanzo na mwisho wa kujidai mnarukia hoja za wapinzani wakati hamna guts za kusimamia.

Makamba,zambi,sendeka,kilango,lusinde n.k jitokezeni either mmoja wenu au kwa umoja wenu mpambane na zitto.kama ikishindikana basi jitokezeni na mseme mko neutral ili wananchi wajue nani ni nani kwenye kusimamia maslahi yao..............................

Tunataka kujua kati ya YES, NEY na NEUTRAL nyie wabunge wa ccm mko wapi?

Nawasilisha...
Kwanini usiseme watanzania ndio wana woga wa fisi? Alipofariki kiumbe mmoja anayeitwa Kanumba walilundikana kwenye mazishi, lakini yanapokuja mambo ya maana kwa maisha yao wanakaa na kuangalia kama sinema.
 
Kwanini usiseme watanzania ndio wana woga wa fisi? Alipofariki kiumbe mmoja anayeitwa Kanumba walilundikana kwenye mazishi, lakini yanapokuja mambo ya maana kwa maisha yao wanakaa na kuangalia kama sinema.

umeona watanzania walivyoamua huko arumeru?
 
Kufuatia mchakato aliouanzisha Mhe. Zitto Kabwe, hadi sasa ni wabunge 71 tu walioweka saini zao kwa ajili ya kuruhusu uwasilishwaji wa hoja ya kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu. Katika hatua hiyo, ni wabunge wa wili tu wa CCM walioweka sahihi zao. Kama ulifwatilia majadiliano ya Bunge last week yalijikita kwenye kuishutumu serikali kwa kuupamba mfumo dokozi na kufurahia ubadhirifu wa mali za Umma, wabunge wengi sana wa CCM walitupa moyo kwa kuchangia hoja hiyo na kuonesha nia ya kutaka mawaziri husika wajiuzuru. Cha kushangaza, hatua inayopelekea ukamilifu wa msimamo wa kuitaka serikali iwajibshwe, unapofanyika. Wabunge wa CCM waliokuwa wanatoa povu wamekaa pembeni na wameogopa kuweka sahihi zao.
Hii maana yake nini hasa??

1) Wabunge wa CCM wanawahadaa wapiga kura wao kuwa wapo nao pamoja katika kutetea maslahi yao kumbe kimsingi wabunge hawa wanatetea maslahi ya chama na familia zao. Imagine familia zinazoteseka kwa kukosa madawa hospitalini wakati serikali imehifadhi madawa hadi yana expire, Imagine wakulima wa jembe la mkono wanavyovimba mashambani kulima na kununua mbolea Mbovu zilizoingizwa nchin na serikali ambazo mwisho wa siku zinapelekea wakulima kukosa chakula. Angalia ubadhirifu kila wizara. Ila wabunge wa CCM wanaona ni haki kuendelea na serikali ya aina hiyo. Wanaona CCM ni Bora kuliko wananchi waliowapa dhamana ya kuwawakilisha.

2) Rai yangu kwa wananchi ambao Mbunge wao hakuweka sahihi, wananchi wachukue hatua ya kumuita Mbunge wao na aeleze kwenye mkutano wa hadhara ni kwa nini hakuweka sahihi katika karatasi ile kwa lengo la kuonyesha nia ya kutokuwa na imani na waziri mkuu na serikali yake katika ubadhirifu ambao CAG wa serikali hiyo hiyi ameuwasilisha mbele ya Bunge. Lugha yoyote atayoitoa Mbunge ambaye hajaweka saini yake itakuwa ni kuwahadaa wananchi.

3) Vyama vya upinzani viitumie orodha hiyo vizuri katika kupoka majimbo ya wabunge wote ambao hawajaweka sahihi kwenye karatasi hilo kwani ni dhahiri kuwa wabunge hao hawapo kwa ajili ya kuwatumikia wananchi wanaoteseka majimboni mwao badala yake wabunge hao wanakiabudu chama na kutetea maslahi ya familia zao. Aidha, wananchi waambiwe kuwa wabunge wao ni wanafki maana wakiwa bungeni na wanapoonekana kwenye luninga huwa wanaongea kwa jazba hadi wanatoa povu kujifanya wapo pamoja na wananchi. Kumbe ile ni kuwabrain wash wananchi. Ukweli umejidhihirisha kupitia list hii hapa chini.

Nini kifanyike kuwapelekea wananchi ujumbe juu ya usaliti huu wa wabunge wao????




  1. 2. Rashid Ali Abdallah – CUF
  2. 3. Chiku Aflah Abwao- Chadema
  3. 4. Saluim Ali Mbarouk – CUF
  4. 5. Salum Khalfam Barwany – CUF
  5. 6. Deo Haule Filikuchombe- CCM
  6. 7. Pauline Philipo Gekul- Chadema
  7. 8. Asaa Othman Hamad- CUF
  8. 9. Prof.Kuliyokela Kahigi- Chadema
  9. 10. Naomi Mwakyoma Kaihula – Chadema
  10. 11. Sylvester Kasulumbayi- Chadema
  11. 12. Raya Ibrahim Khamis - Chadema
  12. 13. Mkiwa Hamad Kiwanga - CUF
  13. 14. Susan Limbweni Kiwanga- Chadema
  14. 15. Grace Sindato Kiwelu –Chadema
  15. 16. Kombo Khamis Kombo – cuf
  16. 17. Joshua Samwel Nassari – Chadema
  17. 18. Tundu Antiphas Lissu- Chadema
  18. 19. Aphaxar Kangi Lugola- CCM
  19. 20. Susan Anselim Lymo- Chadema
  20. 21. Moses Machali – NCCR Mageuzi
  21. 22. John Shibuda Magalle – Chadema
  22. 23. Faki Haji Makame- CUF
  23. 24. Esther Nicholas Matiko- Chadema
  24. 25. Joseph Osmund Mbilinyi- Chadema
  25. 26. Freman Aikaeli Mbowe- Chadema
  26. 27. Kurudhum Jumanne Mchuchuli – Chadema
  27. 28. Halima James Mdee-Chadema
  28. 29. John John Mnyika- Chadema
  29. 30. Augustino Lyatonga Mrema- TLP
  30. 31. Maryam Salum Msabaha- Chadema
  31. 32. Peter Msingwa-chadema
  32. 33. Christowaja Gerson Mtinda- Chadema
  33. 34. Philipa Geofrey Mturano- Chadema
  34. 35. Christina Lissu Mughwai- Chadema
  35. 36. Joyce John Mukya – Chadema
  36. 37. Mchungaji Israel Yohane Natse – Chadema
  37. 38. Philemon Ndesamburo- Chadema
  38. 39. Ahmed Juma Ngwali- CUF
  39. 40. Vincent Josephat Nyerere- Chadema
  40. 41. Rashid Ali Omar- CUF
  41. 42. Meshack Jeremiah Opulukwa- Chadema
  42. 43. Lucy Philemon Owenya- Chadema
  43. 44. Rachel Mashishanga- Chadema
  44. 45. Mhonga Said Ruhwanya – Chadema
  45. 46. Conchesta Rwamlaza – Chadema
  46. 47. Moza Abedi Saidy- CUF
  47. 48. Joseph Roman Selasini – Chadema
  48. 49. David Ernest Silinde- Chadema
  49. 50. Rose Kamili Sukum - Chadema
  50. 51. Cecilia Daniel Paresso- chadema
  51. 52. Kabwe Zuberi Zitto- Kigoma Kaskazini
  52. 53. Magdalena Sakaya – CUF
  53. 54. Rebecca Mngodo- CUF
  54. 55. Sabreena Sungura -Chadema
  55. 56. Hamad Rashid Mohammed- CUF
  56. 57. Rukia Kassim Ahmed- CUF
  57. 58. Mustapha Boay Akoonay -Chadema
  58. 59. Abdalla Haji Ali -CUF
  59. 60. Khatibu Said Ali -CUF
  60. 61. Hamad Ali Hamad -CUF
  61. 62. Riziki Omar Juma -CUF
  62. 63. Haji Khatibu Kai -CUF
  63. 64. Anna Marystella John Malack -Chadema
  64. 65. Hamad Rashid Mohamed -CUF
  65. 66. Rajab Mbarouk Mohamed -CUF
  66. 67. Thuwayba Idrissa Muhamed -CUF
  67. 68. Masoud Abdallah Salum -CUF
  68. 69. Muhamad Ibrahim Sanya -CUF
  69. 70. Ali Khamis Seif -CUF
  70. 71. Haroub Muhammed Shamis -CUF
  71. 72. Amina Amour Nassoro -CUF
 
Mkuu na;56na 65 kwenye list mbona mtu mmoja huyo? au hii list umeitengeneza mwenyewe?
 
yaani hata mbunge wangu Barwani wa cuf huku lindi ametusaliti?...ina maana maneno yote anayotuambia kuwa ana uchungu na haya maisha magumu tunayoishi huku lindi ni uongo mtupu? sitaamini kama kweli Barwani hajasaini...labda hakuwa huko mjengoni wakati hii inasainiwa..naweza kuamini kidogo...
 
orodha itumike kuwaadhibu wabunge mavuvuzela nashauri hiyo orodha ihifadhiwe na hao wabunge watambulike kama mashujaa wa karne hii wa tanzania na wapewe heshima ya pekee, pia naomba itafutie title hapa JF isiondolewe kama ilivyo ya dada Regia Mtema RP Tunakusanya kero ......" 2015 itolewe hukumu kwa waliobaki.
 
Mkuu na;56na 65 kwenye list mbona mtu mmoja huyo? au hii list umeitengeneza mwenyewe?
nimeiona pia, then naona dizaini kama namba moja hamna kwenye hiyo orodha yaani imetoholewa katika orodha, kuanzia namba 2, ikawekwa namba moja huku..
 
Ombi langu kwa watanzania wenzangu wakao nje na ndani ya nchi hebu tuungane kuona hawa wa bunge ambao hawaja saini majimbo yao tuanze kutafuta wapiganaji wakachukue majimbo hayo maana hawana uchungu na nchi yetu bali wapo kwa masirahi ya familia zao.
 
Huyo Zito wa chama gani mbona mmeandika jimbo tu bila chama ....inakujwaje

Kwa kuwa hufahamu, ninakwambia wewe tu! sogeza sikio nikunong'oneze, "thithiem" ukibisha utamaanisha wajua.
 
yaani hata mbunge wangu Barwani wa cuf huku lindi ametusaliti?...ina maana maneno yote anayotuambia kuwa ana uchungu na haya maisha magumu tunayoishi huku lindi ni uongo mtupu? sitaamini kama kweli Barwani hajasaini...labda hakuwa huko mjengoni wakati hii inasainiwa..naweza kuamini kidogo...

soma vizuri barwany yupo katika majina ya mwanzo
 
Back
Top Bottom