Just Distinctions
JF-Expert Member
- May 5, 2016
- 2,728
- 5,365
Habari za wakati huu,
Hili suala la usaili kufanyika Dodoma lizingatiwe tena na tena, sikatai lengo lilikuwa ni jema ila changamoto zimekuwa ni nyingi unakuta mtu anaitwa usaili wa kuandika tarehe 25 kisha ukipita hapo wa vitendo tarehe 28 ama mahojiano 29, sasa ukiangalia kwa haraka, asie na ndugu wala rafiki (ambao ndio asilimia nyingi) gharama ni kubwa kwani guest sio chini ya siku 5, japo mchakato unafanyika ili kupoza na waomba ajira wafanyie katika kanda zao.
Kwa wakati uliopo basi wajitahidi kama wa kuandika ukifanyika tarehe 25 kwa mfano basi wa mahojiano au vitendo uwe siku inayofata, vinginevyo ni kupeana gharama zisizoepukika.
Ukifika pale Nyerere Square ndio balaa, wanaosaka ajira kama wote maana ndio sehemu ya kupotezea muda na huu mji ulivyo hakuna pa kwenda kuzuga hivyo unakuta kwenye kimbweta wasailiwa kama wote wana-buy time, ukifanya ka-survey kadogo utakuta wengi ambao wanazuga hapa ukiacha wazawa ni watu waliokuja kwenye usaili, utaenda wapi tena wakati mji hauna vipengele vingi?
Kila la heri kwa wote ambao bado wanapambania kombe, one day Yes.
Je wewe ulikumbana na changamoto ipi kwenye hizi saili za Dodoma?
Karibu
Pia soma: Kikwete: Mfumo wa usaili wa ajira sasa kufanyika online. Hakuna tena kwenda Dodoma kwa usaili
Hili suala la usaili kufanyika Dodoma lizingatiwe tena na tena, sikatai lengo lilikuwa ni jema ila changamoto zimekuwa ni nyingi unakuta mtu anaitwa usaili wa kuandika tarehe 25 kisha ukipita hapo wa vitendo tarehe 28 ama mahojiano 29, sasa ukiangalia kwa haraka, asie na ndugu wala rafiki (ambao ndio asilimia nyingi) gharama ni kubwa kwani guest sio chini ya siku 5, japo mchakato unafanyika ili kupoza na waomba ajira wafanyie katika kanda zao.
Kwa wakati uliopo basi wajitahidi kama wa kuandika ukifanyika tarehe 25 kwa mfano basi wa mahojiano au vitendo uwe siku inayofata, vinginevyo ni kupeana gharama zisizoepukika.
Ukifika pale Nyerere Square ndio balaa, wanaosaka ajira kama wote maana ndio sehemu ya kupotezea muda na huu mji ulivyo hakuna pa kwenda kuzuga hivyo unakuta kwenye kimbweta wasailiwa kama wote wana-buy time, ukifanya ka-survey kadogo utakuta wengi ambao wanazuga hapa ukiacha wazawa ni watu waliokuja kwenye usaili, utaenda wapi tena wakati mji hauna vipengele vingi?
Kila la heri kwa wote ambao bado wanapambania kombe, one day Yes.
Je wewe ulikumbana na changamoto ipi kwenye hizi saili za Dodoma?
Karibu
Pia soma: Kikwete: Mfumo wa usaili wa ajira sasa kufanyika online. Hakuna tena kwenda Dodoma kwa usaili