Elections 2010 Upinzani wa kweli aujafika bandari ya tanzania

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,149
Wapendwa kwanza nawasalimu kwa jina la bwana wetu kristu alie hai..pili polen sana na shuguli za kila siku hasa wakati huu ukifikiria jinsi ya kwenda kugongana bams na watu huku wengine wakitoa masalio yao ya mchana mkiwa mmejaa na huku EPHRAAAAAAAAAAIMU KIBONDE akiwachekesha sana pasipo kuamini unasikia Mwisho wa GARI JAMANI ...si mbaya kuelezana ukweli wapendwa najua wachache watkaokuwa hapa jamvini baada ya uchaguzi

MI ni mmoja wa wapenda mageuzi lakini simbaya kusema ama kuelezana ukweli jamani hatuna upinzani zaidi ya kutumia fedha za wananchi kwenye uchaguzi na kuwahadaa watanzania ....nasema hivi kwa moyo mmoja pengine naahatarisha maisha lakini la hasha inaniuma pesa tunayotumia kwa ajili ya vyama vya upinzani ambavyo viko kama viko na vingine vinafikia kuwahadaa watu maofisini...si mbaya kusema hivi ila ndugu naomba mjue si wana CHADEMA/NCCR MAGEUZI/TLP wote ni wanachama wa hivyo vyama ama kwa kusema si wote wanaoshangilia UPINZANI ni wapinzani

Hili ni kuwajulisha wale waliojitwika kwa moyo mmoja wakitaraji mageuzi ya kweli yapo kwenye porojo .ndugu anguni kweli yawezekana tukawa na wabunge wapinzani lakini ukweli bado upinzani wa kweli aujafika tanzania..na kama kweli sijaona kwa nini wameshindwa kuungana na kumchagua mmpja kugombea urais..ukitaka kujua hizi chaguzi ni dili we jiulize hilo kabla aujaambiwa sh ngapi hivi vyama vinapewa kila mwezi ati kujiendeleza na huku shule zikikosa madawati....anyway wana mapinduzi tuwe makini na hawa wanaotushabikia na kurusha nguo zao ama vikanga vyao ovyo si wote wanamapinduzi wengine wametumwa na wamo umo humo ndani

Kila la kheri
 
Hizo ni hoja laini ambazo hazina uchambuzi wa maantiki, hivi hujui maana ya kuunguna? kwa Tanzania sheria hairuhusu vyama kuungana. Kwa kuungana maana yake ni kusajili chama kipya tena kipitie mchakato wote wa usajili wa muda na baadaye wa kudumu msajili akiridhika, vinginevyo inakuwa kama CCJ. Kwa hiyo dhana hii inatolewa na watu ambao mtazamo wao ni wafuasi wa CCM, na ndiyo walitunga sheria hii kiufundi zaidi kama ile ya mgombea binafsi.

Pia kila chama kina katiba yake na malengo yake sasa vitakuwa vinaungana ili kufanya biashara gani?. Mimi nafikiri mazingira ya siasa Tanzania na hapa ni upuuzi kivilaumu vyama kwa kushindwa kuungana. Labda ndugu unazungumzia kushirkiana hilo linawezekana , lakini ikumbukwe kuwa kuungana na kushirikiana ni vitu viwili tofauti.
 
bORA HATA TUNGEIKUBALI CCJ LABDA BAMBO YANGEKUWA POA WAKURU DUUUUU MBONA MBOMBO NGAFU FIIIJO!
 
Back
Top Bottom