Upeo Mdogo wa Wajumbe CUF ndio Tatizo- Profesa Safari

CUF na CCM... ipi hasa ina asili ya Usultani?
Wacha ubarakala huo , ila kwa kukusaidia hakuna hata mmoja mwenye asili ya Usulutani ,halafu haiwezekani kuwepo na Masultani wawili au watatu katika Nchi moja ila anakuwepo mmoja na wengine kama wapo inakuwa sio masulutani bali Machifu ambao hawa hupatikana kama wapinzani.

Sasa hapa URT kuna Sultan mmoja tu ambae ni Sultani CCM na hawa vyama vingine vya upinzani akina CUF wanakuwa ni machifu kama akina Mkwawa na Mirambu , Tatizo tulilonalo hapa URT ,Sultani hasikilizi Machifu wala hataki kukaa nao wakapanga mstakbali wa Nchi ,Sultani CCM na wafuasi wake hawataki kubadilisha katiba wala tume ya Uchaguzi maana ndio utakuwa mwisho wa Takirima ya mabilioni na biashara ya kuuza vinoo.
 
Nilazima ujute maana itakuwa hakuna tena chauchau ,na kila kitu kitafuata mkondo wa sheria ,rushwa za mabilioni zitakuwa na grade ya uhaini ,polisi atakaejulikana kabambikiza kesi ataenda jela ,yaani kutakuwa na sheria uchwara kibao ambazo zitakufanya uogope hata kutupa karatasi,hapo ndipo utakapoona kuwa bora utawala wa Sultani CCM ukiweza kufungua dirisha kumwaga machicha.
Tatizo la mwiba ndio walewale anaowazungumza Prof Safari mgando mtupu.Kwenu usultani ni wa asili Maalim sefu miaka nenda rudi badilisheni viongoizi utaona maendeleo ya CUF yanavyobadilika kuelekea kuwa na mafanikio.Kuna jamaa yangu mmoja husema kama mtume Muhammad asingeelezwa kwenye Qur'an ni wa mwisho basi maalim Seif angekuwa ni mtume sasa mawazo kama haya ni mgando mtupu na ndiyo majority ya wana CUF wanayo bila maalim SEif au Prof Lipumba hakuna CUF.Kwa mtaji huo ushindi dhiidi ya SISIM wasahau.CHADEMA itajipatia ushindi2010 kilaini.Mfano mzuri uchaguzi uliopita Hivi karibuni mbeya pamoja na kupiga nyimbo za kwaya CUF na kumuweka menja wa kampeni askofu CUF ilishindwa kwa mbali sana.
 
Nadhani personality imemponza Dr. Safari, manake amekaa kama mlevi fulani!
 
CUF na CCM... ipi hasa ina asili ya Usultani?
Mwenye asili ni CUF manake wao wanauhusudu kweli kweli Hebu tazama kalenda za CUF ya mwaka 2000 jinsi Siff alivyoonekana sura yake na ndevu alvyozichonga hakuna tofauti na mfalme wa oman ili hali picha iko juu ya wananchi wa zanzibar kichekesho kingine huko zenji kila mwana CUF wakipeleka matangazo ya kifo humtaja maalim Seif apate taarifa swali linakuja hivi maalim Seif anawafahamu wanachama wake wote kwa majina
 
Tafuteni picha ya Sultan Jamsid, pembeni weka picha ya Maalim Seif, utapata uthibitisho wa nasaba bila hata kuhangaikia DNA.
Hakuna ubishi Maalim hushinda Zanzibar na kamwe hakabidhiwi nchi ng'o! Na hivi ndivyo itakavyokuwa 2010. Ni vilio CUF na vicheko CCM.

Kama tayari umeshajua mwaka 2010 utalia, na mwaka huo ukafika, ukalia kweli, ukitoka machozi ni machozi ya mamba!.
 
Mlimshangaa jenerali mboma akishindwa kura za maoni kwa mchungaji huko mbeya sasa prof. Anapokwama hata mbele ya koplo kazi kwelikweli wakuu!!!!!!
 
Najua nimewachoma ila ndio hivyo Sultani CCM lazima aondoke hakuna lugha mbadala hapa,nyie mvisheni vilemba vya ukoka Sultani CCM lakini ajue siku zake zinahesabika ,hilo sio la kulifanyia mzaha.
Na lazima mumtetee Sultani CCM maana siku akiangushwa ndio mwisho wenu wa kuonekana hapa JF :D
 
Najua nimewachoma ila ndio hivyo Sultani CCM lazima aondoke hakuna lugha mbadala hapa,nyie mvisheni vilemba vya ukoka Sultani CCM lakini ajue siku zake zinahesabika ,hilo sio la kulifanyia mzaha.
Na lazima mumtetee Sultani CCM maana siku akiangushwa ndio mwisho wenu wa kuonekana hapa JF :D
Tatizo CUF wamekariri hoja zao...na sasa zinakera masikioni mwa watu! Kwani hakuna jipya tokea walipomfukuza James Mapalala na hawato kuwa na jipya mpaka Maalim Seif aka Madevu(Sultan wa Ndotoni) atakapo ondolewa katika chama.

Ama kudai huu ndio mwisho wa CCM ni sawa na kuota mchana kweupe. Endelea na ndoto zako za Alinacha..
 
Ama kudai huu ndio mwisho wa CCM ni sawa na kuota mchana kweupe. Endelea na ndoto zako za Alinacha..

Na kufikiri Sultani CCM hawezi kuondoka utawalani ni mazoea ya kutawaliwa na kufanywa mtumwa ndani ya nchi yako.
 
Na kufikiri Sultani CCM hawezi kuondoka utawalani ni mazoea ya kutawaliwa na kufanywa mtumwa ndani ya nchi yako.

i14_k.jpg
Unanichekesha, mtumwa unamjua wewe?
Mtumwa ni huyo hapo kati mwenye madevu, yeye na jamaa zake wa kisiwa cha pili ndio watumwa... Na wataendelea kuwa watumwa mpaka pale watakapotia akili vichwani mwao.
 
Najua nimewachoma ila ndio hivyo Sultani CCM lazima aondoke hakuna lugha mbadala hapa,nyie mvisheni vilemba vya ukoka Sultani CCM lakini ajue siku zake zinahesabika ,hilo sio la kulifanyia mzaha.
Na lazima mumtetee Sultani CCM maana siku akiangushwa ndio mwisho wenu wa kuonekana hapa JF :D

Tatizo kauli yako hii ya kuwaita Masultani ndiyo inachanganya(labda utafute kauli mbiu nyingine) maana katika hali ya kawaida mimi CUF ndio daima mnaonesha chembe za usultani(mabandiko yako hapa yananifanya nikuhusishe moja kwa moja na CUF) tofauti na ilivyo kwa CCM,kwa mfano tangu mfumo wa vyama vingi umeanza mwaka 1992 naona hakuna mabadiliko sana ya kiuongozi katika CUF na wagombea wa urais katika uchaguzi mkuu ni walewale(S.S.Hamad na Prof.Lipumba),ina maana hakuna wana CUF wengine wenye sifa ya kugombea Urais(ama hawa ndo wameandikwa kwamba ni lazima wawe marais),je?,kuna demokrasia ndani ya CUF????(Hapa ndipo chembe mojawapo ya usultani inapojionesha ndani ya CUF)...Vilevile ile hali ya CUF kuweka base yake Pemba zaidi(ambako watu wengi wana asili ya Arabuni walikotokea Masultani) nayo inaonesha 'usultani' wa CUF...Jiulize kwa nini CUF ina wabunge na Wawakilishi wengi toka Pemba tofauti na ilivyo kwa Unguja na Tz Bara(Kumbukumbu zangu zanionesha hawana Mbunge wa kuchaguliwa Bara zaidi ya wale wawili wa kuteuliwa,kama nimekosea hapa nisahihishwe)...CCM yenyewe ina Wabunge toka Bara na Visiwani(japo haijaambulia kitu Pemba) kuwaita ni Masultani unakuwa hauwatendei haki,labda utupe sababu(zinazojitosheleza) za kuwaita wao Masultani...Otherwise nawashauri ninyi CUF mjipange upya kukifufua chama(nilitegemea mngeanza mkakati huu kwa kuwabadilisha viongozi wenu wa kitaifa lakini hola,kwangu mimi mtu kama Lipumba na Seif walitakiwa kupumzika wawapishe wengine nao wajaribu,wao wabaki kuwa wazee washauri tu wa chama),pia kukifanya kiwe cha kitaifa zaidi badala ya cha Kipemba zaidi...Aidha ifikie kipindi wewe Mwiba na wengine muache haya mambo ya kulialia na kushutumu kila wakati(siasa za jazba hazijengi zinabomoa) maana hili ndo linawafanya CHADEMA wawapige bao na kuwa chama kikuu cha upinzani(wamedhihirisha kuwa wana mikakati tofauti na ninyi CUF)...Inafikia kipindi kila nikiiona post ama thread yako mkuu Mwiba najihakikishia kuwa lazima nikutane na malalamiko ya kumwaga bila kusahau neno (ma)sultani CCM(na kweli nakutana nayo)...Anyways,huu ni mtizamo wangu tu mkuu,sorry kama nimekukwaza...Be blessed
 
Anyways,huu ni mtizamo wangu tu mkuu,sorry kama nimekukwaza...Be blessed

Hujanikwaza ni kuwa una uelewa mdogo au finyu haswa pale panapotumika neno Sultani ,ingawa unaonekana kwa mbali kuifahamu maana halisi ya Sultani lakini unajifanya kuibadilisha maana na kuipotosha.

Nimefurahi kuwa umeelewa wale wanaoganda kwenye madaraka kwa muda mrefu pengine zaidi ya miaka mia huwa ni wenye cheo cha Usultani au Ufalme.

Kwa maana hiyo sitaki niende kwenye mtu mmoja mmoja kama tunavyowavamia mafisadi maana tukienda huko hata Nyerere nae atakuwa hatoki ,tokea hatujapata Uhuru mmpaka tumepata Uhuru hadi tumeupoteza Uhuru ni Nyerere tu ,yaani hata kwenye kugombania Uraisi akigombania peke yake ,kama si maajabu ni kitu gani unweka kura ya ndio ,ndio yeye hapana hapana isipokuwa yeye au vipi ,weka kando hilo na hivyo tuwache akina Seif na Lipumba waongoze Chama chao ,tatizo ambalo kwa upande wangu silioni huko kwengine kwa akina Chadema hali ni hiyo hiyo ila wenzetu wanamatatizo ya uongozi ndani au miongoi mwao ,kuna Mbatia kuna Mbowe kuna Mrema hawa wote ni viongozi wa vyama vya upinzani ambao sijaona kubadilishwa ,na kama kubadilika kumetokana na migogoro ,kupelekana mahakamani na kutibuana au kutimuana kwa kugawika makundi ndani yao au si kweli ? Mambo ambayo hayajapatikana katika safu ya uongozi wa CUF zaidi ya mtu kubwaga manyanga mwenyewe bila ya msuguano.

Halafu wacha kushindana na system ,katika Chama cha Sultan CCM wamejiwekea utaratibu ambao Raisi huwa ndie mwenyekiti wa Chama chao na raisi hupatikana kila baada ya miaka mitano au kumi hivyo mabadiliko kwa wao ni lazima kila baada ya miaka hiyo ,sasa sijui utaratibu huo utatumikaje ikiwa watapigwa na chini.Hayo ni yao.Sina uhakika kama wanapiga kura kumchagua Mwenyekiti na kwa misingi gani hata asiweze kuwa ni Raisi wa nchi.

Unafahamu maana ya kuweka Base ? Base ya CUF haipo Pemba, Pemba kuna wafuasi wengi tu walioamua kuukataa utawala wa Sultani CCM na ziko sehemu nyingi tu ambazo Sultani CCM amepoteza uhai na hatakiwi hata kuonekana.

Kuhusu CUF kuwa na wabunge wengi huko Pemba huo ni msimamo wa raia wa huko ambao waliamua kula sahani moja na nguvu za Sultani CCM na kuzishinda ,kumbuka Pemba waliamua kuzipiga na yeyote yule ambae ataonekana kumkingia kifua Sultani CCM ,hivyo nguvu na mbinu za Sultani CCM zilipigwa na chini katika utetezi wa mtu kugombania na kuilinda haki yeke.

WaPemba walisimama kidete kuona asiehusika haandikishwi katika kupiga kura katika maeneo asiyohusika.

Yaliyotokea Unguja na kwingineko yanajulikana na wananchi au wafuasi wa CUF walikosa nguvu kama zile za Wapemba katika kulinda haki zao na si vinginevyo jambo ambalo liliwafanya wafuasi wa Sultani CCM kuwa na uwezo wa kufanya hujuma kiurahisi na hata hivyo matokeo halisi yanajulikana kuwa Sultani CCM na wafuasi wake hawakushinda na kubakia kutangaza matokeo yasio kuwa ya kweli ,kama unakumbuka katika uchaguzi wa 1995 ,redio kibao zilisikika kutangaza matokeo ya kweli na ndipo hapo jeshi lilipotumwa kuudhibiti ushindi huo ,Sultani CCM alitumia nguvu za dola kupora ushindi ,halikadhalika 2000 polisi walikimbia na masanduku ya kura ili kumsitiri Sultani CCM na 2005 ndio hivyo hivyo jeshi lilivamia Zanzibar na kulazimisha ushindi kwa Sultani CCM.

Hivyo nikirudi sasa na kukuonyesha kwa nini Chama Cha CCM chama ambacho siku kitakapoanguka ndipo nitakapojiunga nacho, CCM tokea tupate uhuru ndio Chama kinachotawala tokea Tanu ,Asp na kuasisiswa kama CCM ambapo nilishiriki katika sherehe zile kama mgeni rasmi kufunga na kufungua vitabu pale mjini Tanga. Miaka yote hiyo CCM ipo madarakani na haitaki kuondoka ,uhakika imeshang'olewa huko Zanzibar lakini bado kwa kutumia nguvu za dola bado imejisimika madarakani.

CCM imekataa kubadilisha katiba kupitia kwa makada wake ambao ndio viongozi serikalini ,CCM imekataa kubadilisha tume ,CCM imekataa kubadili mahakama na yote kutokana na kuwa Sultani CCM amejikita katika sehemu zote muhimu za nchi hii,kila kona na pembe yupo.Kwa maana nyingine ambayo ni maarufu ameshika hatamu za nchi hii ,hatamu ni zile kama za farasi ambazo zinatumika kumuamurisha farasi aende wapi asimame wapi apinde wapi kwa ufupi ni control ,wengine hawana haki ya kufanya lolote lile zaidi ya kupiga makelele kuwa farasi anaendeshwa au anakwenda kutumbukia kwenye shimo.

Na ndio hapa tulipo tumekaza kupiga makelele kuwa nchi inaendeshwa kienyeji lakini hakuna anaetusikia na kama wakisikia basi hubadilishana dereva na kupewa kipofu mwengine.

Nchi imejaa vyama vya siasa ambavyo kila kimoja kinahitaji mabadiliko ya kweli ila Chama kiliopo madarakani kimeshika sukani na hakitaki kuachia kinajiona yeye ndio mtawala wa nchi hii,au mwenye haki miliki ya kutawala ,tumemwondoa Mzungu muarabu na wengineo ili kujenge maendeleo kwa wote kubadilishana madaraka kwa wote ,lakini Chama kimoja kinajiona ndio chenye haki ya kutumia vyombo vya dola kulazimisha wengine kutawaliwa na wao japo wameonekana hawana jipya zaidi ya kuididimiza nchi hii.

Hivyo kama ulivyoona kuwa akina Seif kukaa madarakani kwa muda ni Usultani na hawataki kuwapisha wengine kwa upande wa CCM ni zaidi ya hao akina Seif ,CCM wameua ili kubakia madarakani ,CCM wanatumia rasilimali za Nchi hii ili kubakia madarakani ,CCM anatumia vyombo vya dola ili kubakia madarakani nani anaeweza kufanya yote hayo kama si Sultani ?
 
i14_k.jpg
Unanichekesha, mtumwa unamjua wewe?
Mtumwa ni huyo hapo kati mwenye madevu, yeye na jamaa zake wa kisiwa cha pili ndio watumwa... Na wataendelea kuwa watumwa mpaka pale watakapotia akili vichwani mwao.

Hili ndio tatizo kubwa Zanzibar. Mapinduzi yalipaswa kuwa ya kuleta usawa wa kijamii. Hata hivyo matokeo ya ni haya. Aliyekuwa MTUMWA/MTWANA wa jana akajigeuza BWANA wa leo na BWANA wa jana akajigezwa kuwa MTUMWA/MTWANA wa leo.

Halafu wote wanakaa wakibishana nani adui wa maendeleo ZANZIBAR....

Sasa kama umebomoa mantinki/misingi ya KIMAPINDUZI ni vipi ukategemea maendeleo na sio ushindani wa kihafidhina usio na maslahi kwa nchi na jamii yote kwa ujumla...

Sasa hapa ndugu yangu KIBUNANGO anajitumua kabisa kwa ustadi wote kuwa yeye yuko upande wa MABWANA wa leo na sio MTUMWA/MTWANA isipokuwa wao (mabwana wa jana) ndio WATUMWA..Wazanzibari wanahitaji kujikwamua kutoka katika .......huuuu amasivyo wataendelea kuwa MATEKA wa wanasiasa hovyohovyo milele amina na kuendelea kuchekwa/kudharauliwa na WATANGANYIKA.

omarilyas
 
...Otherwise nawashauri ninyi CUF mjipange upya kukifufua chama(nilitegemea mngeanza mkakati huu kwa kuwabadilisha viongozi wenu wa kitaifa lakini hola,kwangu mimi mtu kama Lipumba na Seif walitakiwa kupumzika wawapishe wengine nao wajaribu,wao wabaki kuwa wazee washauri tu wa chama),pia kukifanya kiwe cha kitaifa zaidi badala ya cha Kipemba zaidi...

Huu ni ushauri wenye nia njema kabisa. Laiti kama CUF wangeondokana na FALSAFA ya UKOMBOZI DAIMA ni wazi mawazo kama haya yangesaidia sana kusonga mbele badala ya kuendela kudumaa kama hali ilivyo sasa....

omarilyas
 
Last edited:
pia kukifanya kiwe cha kitaifa zaidi badala ya cha Kipemba zaidi...
Bw. Balantanda- hapo ndipo lilipo tatizo la CUF. Hawana dira ya kupanua chama chao nje ya Pemba wanaridhika na support kubwa waliyonayo Pemba. Wanasahau kuwa hawana nguvu tena hata kidogo popote pale nje ya Pemba. Hivi Chama kama hicho vipi kitaweza kuongoza Dola (Zanzibar) na Tanzania kwa jumla kwa kutegemea nguvu yake iliyopo Pemba tu. CUF imeshindwa kusambaa Unguja sikwambii Bara. Eti halafu wanakaa na kupiga mayowe tu. sasa sijui wanataka tuvunje sheria zetu za Demokrasia na kukiruhusu hicho Chama ambacho siku zote kitakuwa hakipati ridhaa ya wananchi walio wengi- kiunde Serikali (Kiongoze Dola?)
 
Tatizo kauli yako hii ya kuwaita Masultani ndiyo inachanganya(labda utafute kauli mbiu nyingine) maana katika hali ya kawaida mimi CUF ndio daima mnaonesha chembe za usultani(mabandiko yako hapa yananifanya nikuhusishe moja kwa moja na CUF) tofauti na ilivyo kwa CCM,kwa mfano tangu mfumo wa vyama vingi umeanza mwaka 1992 naona hakuna mabadiliko sana ya kiuongozi katika CUF na wagombea wa urais katika uchaguzi mkuu ni walewale(S.S.Hamad na Prof.Lipumba),ina maana hakuna wana CUF wengine wenye sifa ya kugombea Urais(ama hawa ndo wameandikwa kwamba ni lazima wawe marais),je?,kuna demokrasia ndani ya CUF????(Hapa ndipo chembe mojawapo ya usultani inapojionesha ndani ya CUF)...Vilevile ile hali ya CUF kuweka base yake Pemba zaidi(ambako watu wengi wana asili ya Arabuni walikotokea Masultani) nayo inaonesha 'usultani' wa CUF...Jiulize kwa nini CUF ina wabunge na Wawakilishi wengi toka Pemba tofauti na ilivyo kwa Unguja na Tz Bara(Kumbukumbu zangu zanionesha hawana Mbunge wa kuchaguliwa Bara zaidi ya wale wawili wa kuteuliwa,kama nimekosea hapa nisahihishwe)...CCM yenyewe ina Wabunge toka Bara na Visiwani(japo haijaambulia kitu Pemba) kuwaita ni Masultani unakuwa hauwatendei haki,labda utupe sababu(zinazojitosheleza) za kuwaita wao Masultani...Otherwise nawashauri ninyi CUF mjipange upya kukifufua chama(nilitegemea mngeanza mkakati huu kwa kuwabadilisha viongozi wenu wa kitaifa lakini hola,kwangu mimi mtu kama Lipumba na Seif walitakiwa kupumzika wawapishe wengine nao wajaribu,wao wabaki kuwa wazee washauri tu wa chama),pia kukifanya kiwe cha kitaifa zaidi badala ya cha Kipemba zaidi...Aidha ifikie kipindi wewe Mwiba na wengine muache haya mambo ya kulialia na kushutumu kila wakati(siasa za jazba hazijengi zinabomoa) maana hili ndo linawafanya CHADEMA wawapige bao na kuwa chama kikuu cha upinzani(wamedhihirisha kuwa wana mikakati tofauti na ninyi CUF)...Inafikia kipindi kila nikiiona post ama thread yako mkuu Mwiba najihakikishia kuwa lazima nikutane na malalamiko ya kumwaga bila kusahau neno (ma)sultani CCM(na kweli nakutana nayo)...Anyways,huu ni mtizamo wangu tu mkuu,sorry kama nimekukwaza...Be blessed[/QUOTE


Pengine neno usultani linakukera na hivyo unalihusanisha na UARABU. Kwako usultani maana yake mtawala wa Kiarabu. Usultani ni mamlaka yasiyo na mpinzani juu yake yaani kuendelea kutawala na kutawala kama sio wewe basi mwanao au mpwao au wa ukoo wako. Sasa chukulia utawala wa Zanzibar kwa vitendo na maneno umeshasema kuwa CCM ndiyo yenye haki ya kutawal maisha visiwa vya Zanzibar. Tafadhali nipe jina la utawala wa namna hiyo. Kwa Zanzibar ndugu yangu utapaa shida kuwabaguwa Waarabu na weusi. Naomba fanya utafiti au uulize kwani mfano mmoja tu Amani ni Mwarabu kuliko Seif Sharifu ikiwa rangi ndio kabila.
Kuhusu kuendelea kwa wale wale ndani ya chama cha CUF kipi cha kushangaza? Nakupa mifano na baadae utafakari kwanini hili linatokea. Mkumbuke Odinga Odinga wa Kenya. Jiulize Samuel Malecela alishakuwa Waziri Mkuu kwa nini alitaka Urais hata baada ya kupigwa muhuri na Nyerere? Fanya tafakuri na ujiulize huko CCM zaidi ya Mwenyekiti (anaebanwa na kofia ya Urais kuna mabadiliko gani? Mabadiliko ni wale wachache Rais(anapokuwa Mwenyekiti) anaopenda kuwa nao. Zaidi ya hapo lbda baada ya vifo wabunge wa CCM ni wale wale waliokuwa wakati wa Nyerere.
Lengo langu ni kukuonyesha kuwa siasa zetu WAAFRIKA/Watanzania ni biashara yenye tija na nani yuko tayari kuacha biashara yenye tija.Tusiongozwe na Chuki binafsi za ukabila au dini katika kuchanganua mambo.
Hebu nieleze kipi kinachokushangaza kuona chama fulani kina ngome pahala fulani na kwa upande wa CCM na CUF kule Zanzibar siri ni hii. Kule Unguja Tabaka la waliokuwa nacho walipinduliwa na walio wengi masikini na Mapinduzi hayo yaliwaletea mambo mengi mazuri kwa wakati ule. Elimu bure,ardhi,Matibabu bure na madaraka ambayo waliyakosa wakati wa usultani na kwa hivyo MAPINDUZI ni kila kitu kwao. Waroho wa madaraka kwa kupitia CCM wanalijuwa hilo na hivyo wanatumia propaganda(inayowafika hata nyinyi msiojua hali halisi ya visiwa vile) kuwa upinzani unahujumu Mapinduzi ingawa zile faida zote za Mapinduzi hayo hazipo sasa. Kwa Upande wa Pemba Watawala wa Zanzibar wanaizarau Pemba na watu wake wote na Hivyo mtu yeyote anaewatetea wanamuona kama nusu Mungu. Hapo ndipo CUF wanachukua advantage kwa kupiga kelele za uongo kuitetea Pemba na hivyo Wapemba wataendelea kuwapa sapoti.
Tabia ya kuwadharau wapemba imo ndani ya damu ya Waunguja hivyo inakuwa vigumu kubadilisha tabia yao na kuwaweka daraja sawa. Sasa niambie nini unachotegemea?
 
Bw. Balantanda- hapo ndipo lilipo tatizo la CUF. Hawana dira ya kupanua chama chao nje ya Pemba wanaridhika na support kubwa waliyonayo Pemba. Wanasahau kuwa hawana nguvu tena hata kidogo popote pale nje ya Pemba. Hivi Chama kama hicho vipi kitaweza kuongoza Dola (Zanzibar) na Tanzania kwa jumla kwa kutegemea nguvu yake iliyopo Pemba tu. CUF imeshindwa kusambaa Unguja sikwambii Bara. Eti halafu wanakaa na kupiga mayowe tu. sasa sijui wanataka tuvunje sheria zetu za Demokrasia na kukiruhusu hicho Chama ambacho siku zote kitakuwa hakipati ridhaa ya wananchi walio wengi- kiunde Serikali (Kiongoze Dola?)

PAKACHA unaelewa vizuri kuwa laiti kama si mbinu zakijasusi hao CUF unaowasema wangepata viti zaidi ya vitano Unguja. Kama umpenzi wa Mungu ungeshaungama namna ulivyoshiriki kuhakikisha CUF hawapati ushindi.
Usiwadanganye wasioelewa kuwa Unguja yenyewe ndio yenye tofauti iliyoletwa na Mapinduzi. Pemba hawkushiriki wala hawakuguswa na Mapinduzi bali nyie Waunguja ndio mliouwana wenyew kwa wenyewe. Hali inakuwa ngumu zaidi pale waroho wa madaraka wanpozidi kukumbusha mauwaji hayo kuwa ndiyo msingi wa kuendelea madarakani. Nguvu za CUF zinaletwa na huu mgawanyiko wa nyie Waunguja kwani Wazawa hao wa Unguja walopinduliwa ndio wanawapa nguvu CUF unguja na ndio maana hakuna lolote mnalopanga lisiwafike CUF. Kwa kutowaamini Wapemba Serikali yenu haina Wapemba lakini mnaloliamuwa linawafika haraka sababu ni kuwa miongoni mwenu madonda ya Mapinduzi yanatoneshwa kila wakati.
Naamini kelele na kejeli zenu kwa CUF zinatokana na kushindwa kuvunja nguvu zao.
USHAURI; Mapinduzi ni jambo la kihistoria lisiloepukika lisiwe kigezo cha kuleta umoja kati yenu kwani naamini hao Waunguja wanaotowa sapoti kwa CUF hawafanyi hivyo kwa mapenzi bali kwa kukata tamaa kuwa nyie ndugu zao hamok tayari kuacha kukumbusha yaliyopita.
 
Tabia ya kuwadharau wapemba imo ndani ya damu ya Waunguja hivyo inakuwa vigumu kubadilisha tabia yao na kuwaweka daraja sawa. Sasa niambie nini unachotegemea?

Ndugu yangu Ngekewa Acha hiyo. Haifai staghafiru kidogo. Acha kuwadanganya wale wasioijua au wasiofika Zanzibar. Hivi Wapemba gani wanaodharauliwa? Ni pamoja na wale waishio maisha ya raha kabisa na kutembea na magari ya kifakhari, na kuendesha biashara kubwa kubwa, na kuwa na majumba mazuri mazuri ndani ya Mjini Zanzibar. Unajua adhabu ya watu wanaoshadidia ethnicity. Aste aste-Ndugu yangu.
 
kwenye siasa hakuna elimu hata kidogo, ni jinsi watu walivyokudondokea, ukizingatia watanzania tuna dhana kwamba ukiwa na sura, shape nzuri basi umekwua rais.
 
Back
Top Bottom