Upeo Mdogo wa Wajumbe CUF ndio Tatizo- Profesa Safari

Bw. Balantanda- hapo ndipo lilipo tatizo la CUF. Hawana dira ya kupanua chama chao nje ya Pemba wanaridhika na support kubwa waliyonayo Pemba. Wanasahau kuwa hawana nguvu tena hata kidogo popote pale nje ya Pemba. Hivi Chama kama hicho vipi kitaweza kuongoza Dola (Zanzibar) na Tanzania kwa jumla kwa kutegemea nguvu yake iliyopo Pemba tu. CUF imeshindwa kusambaa Unguja sikwambii Bara. Eti halafu wanakaa na kupiga mayowe tu. sasa sijui wanataka tuvunje sheria zetu za Demokrasia na kukiruhusu hicho Chama ambacho siku zote kitakuwa hakipati ridhaa ya wananchi walio wengi- kiunde Serikali (Kiongoze Dola?)

Wewe Pakacha wacha kuvuja ,nani kakwambia kama CUf ipo Pemba tu au sapoti yake ni Pemba tu, hata Kikwete Mkubwa wa Chama Sultani CCM anafahamu fika kuwa sio Pemba tu bali Zanzibar nzima hakuna hata wacha mtu hata mdudu anampa sapoti sultani CCM vilevile mikoa ya Pwani yote halikadhalika mikoa ya Magharibi yote Sultani CCM hapendwi maana kama kupendwa wale waliosema watajitenga si Wapemba peke yao hata huko Kigoma Kagera walisema hivyohivyo. Watu wamechoka na utawala wa Sultani CCM.

Mnajua wazi leo hii WaZanzibari ukiwaamsha usiku wa manane au wacha hilo wawe wamekunywa ulevi wa tende ,muwaambie wapige kura basi hawamchagui Sultani CCM ni juzi tu mmerusha mapanga pale Magogoni yaani kama mnapendwa na mnajua mnawapenzi yanini kupiga watu mapanga na minyororo huoni kama Sultani CCM ameishiwa na hana wananchi wanaompa sapoti ,ndio maana yake na hapo sio Pemba ni Unguja ,nyie mnasema Unguja ni wafuasi wa Sultani CCM watupu sasa mapanga ya nini ,Kiteto ni wafuasi wa Sultani CCM watupu sasa sime za nini ?

Nyinyi dawa yenu ipo jikoni ,hao mnaowatumia kwenda kupiga watu minyororo na mapanga watakuja kupewa kibano cha mbwa koko mpite mkilia midomo juu.
 
Ndugu yangu Ngekewa Acha hiyo. Haifai staghafiru kidogo. Acha kuwadanganya wale wasioijua au wasiofika Zanzibar. Hivi Wapemba gani wanaodharauliwa? Ni pamoja na wale waishio maisha ya raha kabisa na kutembea na magari ya kifakhari, na kuendesha biashara kubwa kubwa, na kuwa na majumba mazuri mazuri ndani ya Mjini Zanzibar. Unajua adhabu ya watu wanaoshadidia ethnicity. Aste aste-Ndugu yangu.

PAKACHA nafikiri kama kumuogopa mungu basi ni wewe unaehitaji kufanya hivyo. Usiugope ukweli na huo ndio ukweli wenyewe kuwa mnawadharau Wapemba na huku wamekushindeni kwa mambo mengi. Pengine huko kuonekana kwa Wapemba wachache wakijifaharisha ndiko kunakowapa choyo juu ya Wapemba wote.
Mimi si shabikii Ethnic kama unavyodai lakini naumwa rohoni kwa watu kama nyie kuvigawa visiwa vyaZanzibar kwa maslaha ya wachache. Nitaorodhesha machache halafu unieleze nini maana ya hayo kama si kuutafuta huo unaojidai kuukemea.
_ Kauli isemayo "Karume (mkubwa) kasema Mpemba hatotawala maisha yake Zanzibar
_ Kuanzia Tomondo kupitia mpendae, magogoni hadi Mtoni kuitwa Ukanda wa Gaza.
_Kuundwa Janjawidi na kuwapiga watu fulani na kuwatia vilema na kushindwa kukamatwa hata muhusika mmoja.
_ Kuwepo Mpemba mmoja tu katika Baraza la Mawaziri.
Ndugu yangu PAKACHA si vizuri kuwa mnafiki kwa Mwenyezi Mungu kwani yeye anayajua yote, unaweza kutudanganya sisi lakini daima kama gazeti la Zanzibar wakati wa Karume lilivyosema "Ukweli ukidhihiri Uongo Hujitenga"
 
Halafu si wanajidanganya tu hivi hao wafuasi wa Sultani CCM wanaoongoza Zanzibar na kuikalia kimabavu wanaweza kusema kama hawajahusu Upemba ,basi ni kujifanya na kuwafanya wengine pia wapumbavu au wajinga kwa kauli zao za ajabu ajabu ili wazidi kukwiba.
 
Hujanikwaza ni kuwa una uelewa mdogo au finyu haswa pale panapotumika neno Sultani ,ingawa unaonekana kwa mbali kuifahamu maana halisi ya Sultani lakini unajifanya kuibadilisha maana na kuipotosha.

Nimefurahi kuwa umeelewa wale wanaoganda kwenye madaraka kwa muda mrefu pengine zaidi ya miaka mia huwa ni wenye cheo cha Usultani au Ufalme.

Kwa maana hiyo sitaki niende kwenye mtu mmoja mmoja kama tunavyowavamia mafisadi maana tukienda huko hata Nyerere nae atakuwa hatoki ,tokea hatujapata Uhuru mmpaka tumepata Uhuru hadi tumeupoteza Uhuru ni Nyerere tu ,yaani hata kwenye kugombania Uraisi akigombania peke yake ,kama si maajabu ni kitu gani unweka kura ya ndio ,ndio yeye hapana hapana isipokuwa yeye au vipi ,weka kando hilo na hivyo tuwache akina Seif na Lipumba waongoze Chama chao ,tatizo ambalo kwa upande wangu silioni huko kwengine kwa akina Chadema hali ni hiyo hiyo ila wenzetu wanamatatizo ya uongozi ndani au miongoi mwao ,kuna Mbatia kuna Mbowe kuna Mrema hawa wote ni viongozi wa vyama vya upinzani ambao sijaona kubadilishwa ,na kama kubadilika kumetokana na migogoro ,kupelekana mahakamani na kutibuana au kutimuana kwa kugawika makundi ndani yao au si kweli ? Mambo ambayo hayajapatikana katika safu ya uongozi wa CUF zaidi ya mtu kubwaga manyanga mwenyewe bila ya msuguano.

Halafu wacha kushindana na system ,katika Chama cha Sultan CCM wamejiwekea utaratibu ambao Raisi huwa ndie mwenyekiti wa Chama chao na raisi hupatikana kila baada ya miaka mitano au kumi hivyo mabadiliko kwa wao ni lazima kila baada ya miaka hiyo ,sasa sijui utaratibu huo utatumikaje ikiwa watapigwa na chini.Hayo ni yao.Sina uhakika kama wanapiga kura kumchagua Mwenyekiti na kwa misingi gani hata asiweze kuwa ni Raisi wa nchi.

Unafahamu maana ya kuweka Base ? Base ya CUF haipo Pemba, Pemba kuna wafuasi wengi tu walioamua kuukataa utawala wa Sultani CCM na ziko sehemu nyingi tu ambazo Sultani CCM amepoteza uhai na hatakiwi hata kuonekana.

Kuhusu CUF kuwa na wabunge wengi huko Pemba huo ni msimamo wa raia wa huko ambao waliamua kula sahani moja na nguvu za Sultani CCM na kuzishinda ,kumbuka Pemba waliamua kuzipiga na yeyote yule ambae ataonekana kumkingia kifua Sultani CCM ,hivyo nguvu na mbinu za Sultani CCM zilipigwa na chini katika utetezi wa mtu kugombania na kuilinda haki yeke.

WaPemba walisimama kidete kuona asiehusika haandikishwi katika kupiga kura katika maeneo asiyohusika.

Yaliyotokea Unguja na kwingineko yanajulikana na wananchi au wafuasi wa CUF walikosa nguvu kama zile za Wapemba katika kulinda haki zao na si vinginevyo jambo ambalo liliwafanya wafuasi wa Sultani CCM kuwa na uwezo wa kufanya hujuma kiurahisi na hata hivyo matokeo halisi yanajulikana kuwa Sultani CCM na wafuasi wake hawakushinda na kubakia kutangaza matokeo yasio kuwa ya kweli ,kama unakumbuka katika uchaguzi wa 1995 ,redio kibao zilisikika kutangaza matokeo ya kweli na ndipo hapo jeshi lilipotumwa kuudhibiti ushindi huo ,Sultani CCM alitumia nguvu za dola kupora ushindi ,halikadhalika 2000 polisi walikimbia na masanduku ya kura ili kumsitiri Sultani CCM na 2005 ndio hivyo hivyo jeshi lilivamia Zanzibar na kulazimisha ushindi kwa Sultani CCM.

Hivyo nikirudi sasa na kukuonyesha kwa nini Chama Cha CCM chama ambacho siku kitakapoanguka ndipo nitakapojiunga nacho, CCM tokea tupate uhuru ndio Chama kinachotawala tokea Tanu ,Asp na kuasisiswa kama CCM ambapo nilishiriki katika sherehe zile kama mgeni rasmi kufunga na kufungua vitabu pale mjini Tanga. Miaka yote hiyo CCM ipo madarakani na haitaki kuondoka ,uhakika imeshang'olewa huko Zanzibar lakini bado kwa kutumia nguvu za dola bado imejisimika madarakani.

CCM imekataa kubadilisha katiba kupitia kwa makada wake ambao ndio viongozi serikalini ,CCM imekataa kubadilisha tume ,CCM imekataa kubadili mahakama na yote kutokana na kuwa Sultani CCM amejikita katika sehemu zote muhimu za nchi hii,kila kona na pembe yupo.Kwa maana nyingine ambayo ni maarufu ameshika hatamu za nchi hii ,hatamu ni zile kama za farasi ambazo zinatumika kumuamurisha farasi aende wapi asimame wapi apinde wapi kwa ufupi ni control ,wengine hawana haki ya kufanya lolote lile zaidi ya kupiga makelele kuwa farasi anaendeshwa au anakwenda kutumbukia kwenye shimo.

Na ndio hapa tulipo tumekaza kupiga makelele kuwa nchi inaendeshwa kienyeji lakini hakuna anaetusikia na kama wakisikia basi hubadilishana dereva na kupewa kipofu mwengine.

Nchi imejaa vyama vya siasa ambavyo kila kimoja kinahitaji mabadiliko ya kweli ila Chama kiliopo madarakani kimeshika sukani na hakitaki kuachia kinajiona yeye ndio mtawala wa nchi hii,au mwenye haki miliki ya kutawala ,tumemwondoa Mzungu muarabu na wengineo ili kujenge maendeleo kwa wote kubadilishana madaraka kwa wote ,lakini Chama kimoja kinajiona ndio chenye haki ya kutumia vyombo vya dola kulazimisha wengine kutawaliwa na wao japo wameonekana hawana jipya zaidi ya kuididimiza nchi hii.

Hivyo kama ulivyoona kuwa akina Seif kukaa madarakani kwa muda ni Usultani na hawataki kuwapisha wengine kwa upande wa CCM ni zaidi ya hao akina Seif ,CCM wameua ili kubakia madarakani ,CCM wanatumia rasilimali za Nchi hii ili kubakia madarakani ,CCM anatumia vyombo vya dola ili kubakia madarakani nani anaeweza kufanya yote hayo kama si Sultani ?

Tatizo ni fikra ambazo zimeganda kichwani mwako(ambazo nina uhakika zitachukua muda mrefu kuyeyuka).Mie nilitoa ushauri tu wa bure kwenu(si lazima kuufuata).Otherwise(narudia tena) CUF mnapaswa kubadilika(rejea maelezo yangu ya awali)
 
Back
Top Bottom