UPDATE: Wizara ya Afya yaunda Kamati kuchunguza Malalamiko ya Madaktari Watarajali

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,813
11,991
UPDATE:
WIZARA YA AFYA YAUNDA KAMATI KUCHUNGUZA MADAI YA MADAKTARI WATARAJALI

1692004207972.png


1692004229643.png


1692004246376.png


Madaktari Tarajali wanatoa malalamiko yao dhidi ya Baraza la Madaktari Tanganyika (MCT)
Akizungumza katika mkutano huo wa Wanahabari, Dkt. Warsha Wilson ambaye ni mmoja wa waathirika wa matokeo mabaya ya mitihani ya madaktari Nchini, amesema:

Baada ya matokeo kutoka na kuonekana idadi kubwa ya Madaktari wamefeli katika mitihani tulifuata njia za kawaida kuwasilisha malalamiko yetu lakini tulipuuzwa.

Tuliwasilisha changamoto tunazopitia kwa Baraza la Madaktari (MCT) na waliahidi kulishughulikia suala letu lakini haikufanyika hivyo, kilichofuata tukawasilisha suala letu kwa Naibu Waziri, Dkt Moleli ambaye alilipokea na kulikabidhi kwa Mkurugenzi wa Tiba wa Wizarara ya Afya.

Mkurugenzi akasema ameunda Tume kulishughulikia suala hilo, lakini haikuwa hivyo, kwani baada ya zaidi ya miezi miwili tulipoenda kufuatilia mrejesho kwake na kwa MCT, tukagundua kuwa MCT haijui hata kama kuna Tume imeundwa.

Baada ya hapo tukaandika barua ya wazi kwenza kwa Rais, tulifanya hivyo na nakala ikaenda Wizarani, lakini zaidi ili Rais apate maombi yetu tukaamua tuandae taarifa hii kwa Wanahabari, ili Mheshimiwa Rais apate maombi.

Hoja ni mazingira ya tata ya mitihani
Tunaamini taratibu za mtihani baada ya mafunzo ya vitendo (Post internship) ni chanzo cha kupoteza umahiri kuliko kuweka uratibu mzuri.

Kwanza ni muda wa mitihani, kawaida baada ya mafunzo ya vyuoni kukamilika utaratibu unaofuata ni kuwa tunafanya mtihani kabla ya kwenda kwenye mafunzo ya vitendo (internship) kisha tunaenda kujifunza chini ya Madaktari Bingwa katika vituo vya Afya.

Baada ya mafunzo ya vitendo Daktari anakaa nyumbani kwa zaidi ya miezi 8, 9 hadi zaidi kisha anakutana na mtihani mwingine wa pili wa nadharia, hiyo inataegeneza mazingira ya kumpotezea ubora wake, hata akifanya mtihani akafaulu anakuwa ni daktari wa nadharia na sio vitendo.

Kwa nini fani yetu ina kelele nyingi?
Mitihani yetu imekuwa na kelele nyingi kwa kuwa fani yetu inahusisha vitendo zaidi kuliko nadharia, hivyo tunapotaka kumhukumu au kutegemea kumpata Daktari kwa njia ya nadharia unadhani atafanya vizuri?

Changamoto nyingine, mitihani haina uwazi, Wanafunzi au wafanya mitihani hawajui matokeo yao kwa maana ya alama, hakuna uwazi ili utambulike umefaulu unatakiwa upate alama ngapi, hakuna kitu kama hicho, wanasema tu wewe umefaulu au umefeli.

Hata kuambiwa ulifanya mtihani fulani haukupata matokeo mazuri katika somo fulani na kufaulu somo fulani, hilo halipo na huwezi kujua.

Wadau Msajili wa Madaktari amewadharau
Kupitia Gazeti la Mwananchi, Msajili wa Madaktari, Dkt. Mnzava alisema Madaktari wanafeli kwa kuwa wana uwezo mdogo wa darasani, hatukufurahishwa na hiyo kauli kwa sababu kwa muundo wa utaratibu wa Udaktari, ni sawa ametudharau sisi Madaktari wenzake, pia ni sawa na kuwadharau wakufunzi wetu.

Kwani kabla ya kufika hatua tuliyopo sisi tunakuwa tumepitishwa na TCU, tumepitishwa na Wakufunzi wa ngazi ya chuo na katika taasisi za afya ambazo wanatufundisha, hivyo kauli yake ni kama amedharau mamlaka zote hizo na ametudharau sisi ambao ni Madaktari wenzake.

Mbali na hapo amesema Madaktari wanafeli masomo ya upasuaji, sisi inajulikana wazi kuwa fani yetu ni vitendo zaidi kuliko nadharia, lakini mazingira yaliyopo wanatupima kwa njia za nadharia.



Pia soma: Madaktari wataraji wamekuwa ombaomba Mtaani kisa leseni, wamuangukia Waziri Ummy Mwalimu na Rais Samia
 
Zamani tulikuwa na vyuo vichache vya utabibu, hivyo waliodahiliwa walikuwa the best of the best. Tulikuwa na uhaba wa madaktari lakini walikuwa na ubora wa juu

Siki hizi vyuo vimeongezeka lakini ubora umeshuka. Sasa wanaanza kulialia ili magoli yapanuliwe kwa ajili yao.
 
Mimi kama mdau wa afya, naona hawa Madaktari wanaonewa sana, miaka mitatu iliyopita hakukua na hii mitiani, hii ilianza tu baada ya kuona watu wameanzisha ugumu Law school wakasema why not in Medical school, so ilivyoanzishwa hakukua na utaratibu mzuri wala research nzuri iliyofanywa.

Hivyo bhas kama umefatilia hii press, MCT waliamua kupush kutoa license despite walikua wanafeli sana, nasikitika kuona mtu anacomment anasema kua nilifanya ilo paper na nikafaulu, hawajui walikua wanafaulu kwa ngapi, hii ndo ikawa kigezo kua wakawa hawaonyeshi matokeo yao kwenye system, nimefanya kazi na interns wengi na najua uwezo wao na weledi wao, na nilichoona kua hawa Madaktari bado ni wadogo na bado wanandoto kubwa ebu tusiwakatishe tamaa.

Wewe unayelalamika kua uwezi tibiwa na Doctors waliofeli unajidanganya kama hujui historia ya hawa. Unaweza ukaenda hospital ukajua umekutana na specialist mkubwa kumbe ata hao wangepata huo mtiani enzi zao wasingetoboa.

Ushauri sasa, kwakua wanasema wamekaa mda mrefu sana nyumbani tusipoteze skills zao wapewe nafasi, wapewe license maana ni haki yao kwa hoja kubwa ya kua wameshafanya pre internship ya MCT wakafaulu, wakafanya one year internship pia wakapitishwa na maspecialist na kupata grades nzuri.

Wakakaa first on calls na kufanikisha mgonjwa anapona ivyo bhas post internship examination has no part on giving them license, huku naomba baraza likishirikiana na MCT plus wadau wa afya wenye sense na utu, wachakatue huu mtiani upya, ili ukirudi usilete malalamiko kama haya kwenye jamii, hili ni anguko.

NB: Hawa ni watoto maskini wa vidumu na fagio waliojitoa mhanga kwenye jamii, Medicine has never been easy.
 
Miaka mi5 ya Medical school halafu mmoja wa internship halafu mtihani wa masaa ma3 unaamua hatma ya mtu hyu dah sometimes tukubali kuna mambo hayakuwekwa sawa. Hivyo kwa kunyima leseni na yeye kukaa nyumbani ndo kunamuongezea uwezo? Hapana
 
Miaka mi5 ya Medical school halafu mmoja wa internship halafu mtihani wa masaa ma3 unaamua hatma ya mtu hyu dah sometimes tukubali kuna mambo hayakuwekwa sawa. Hivyo kwa kunyima leseni na yeye kukaa nyumbani ndo kunamuongezea uwezo? Hapana
Kwani form 4 ikoje? Mtihani wa masaa mawili kupima elimu uliyoipata kwa miaka minne. Huko mlipitaje?

Kama unajua unajua tu, hivyo vingine ni visingizio.
 
Madaktari Tarajali wanatoa malalamiko yao dhidi ya Baraza la Madaktari Tanganyika (MCT)
Akizungumza katika mkutano huo wa Wanahabari, Dkt. Warsha Wilson ambaye ni mmoja wa waathirika wa matokeo mabaya ya mitihani ya madaktari Nchini, amesema:

Baada ya matokeo kutoka na kuonekana idadi kubwa ya Madaktari wamefeli katika mitihani tulifuata njia za kawaida kuwasilisha malalamiko yetu lakini tulipuuzwa.

Tuliwasilisha changamoto tunazopitia kwa Baraza la Madaktari (MCT) na waliahidi kulishughulikia suala letu lakini haikufanyika hivyo, kilichofuata tukawasilisha suala letu kwa Naibu Waziri, Dkt Moleli ambaye alilipokea na kulikabidhi kwa Mkurugenzi wa Tiba wa Wizarara ya Afya.

Mkurugenzi akasema ameunda Tume kulishughulikia suala hilo, lakini haikuwa hivyo, kwani baada ya zaidi ya miezi miwili tulipoenda kufuatilia mrejesho kwake na kwa MCT, tukagundua kuwa MCT haijui hata kama kuna Tume imeundwa.

Baada ya hapo tukaandika barua ya wazi kwenza kwa Rais, tulifanya hivyo na nakala ikaenda Wizarani, lakini zaidi ili Rais apate maombi yetu tukaamua tuandae taarifa hii kwa Wanahabari, ili Mheshimiwa Rais apate maombi.

Hoja ni mazingira ya tata ya mitihani
Tunaamini taratibu za mtihani baada ya mafunzo ya vitendo (Post internship) ni chanzo cha kupoteza umahiri kuliko kuweka uratibu mzuri.

Kwanza ni muda wa mitihani, kawaida baada ya mafunzo ya vyuoni kukamilika utaratibu unaofuata ni kuwa tunafanya mtihani kabla ya kwenda kwenye mafunzo ya vitendo (internship) kisha tunaenda kujifunza chini ya Madaktari Bingwa katika vituo vya Afya.

Baada ya mafunzo ya vitendo Daktari anakaa nyumbani kwa zaidi ya miezi 8, 9 hadi zaidi kisha anakutana na mtihani mwingine wa pili wa nadharia, hiyo inataegeneza mazingira ya kumpotezea ubora wake, hata akifanya mtihani akafaulu anakuwa ni daktari wa nadharia na sio vitendo.

Kwa nini fani yetu ina kelele nyingi?
Mitihani yetu imekuwa na kelele nyingi kwa kuwa fani yetu inahusisha vitendo zaidi kuliko nadharia, hivyo tunapotaka kumhukumu au kutegemea kumpata Daktari kwa njia ya nadharia unadhani atafanya vizuri?

Changamoto nyingine, mitihani haina uwazi, Wanafunzi au wafanya mitihani hawajui matokeo yao kwa maana ya alama, hakuna uwazi ili utambulike umefaulu unatakiwa upate alama ngapi, hakuna kitu kama hicho, wanasema tu wewe umefaulu au umefeli.

Hata kuambiwa ulifanya mtihani fulani haukupata matokeo mazuri katika somo fulani na kufaulu somo fulani, hilo halipo na huwezi kujua.

Wadau Msajili wa Madaktari amewadharau
Kupitia Gazeti la Mwananchi, Msajili wa Madaktari, Dkt. Mnzava alisema Madaktari wanafeli kwa kuwa wana uwezo mdogo wa darasani, hatukufurahishwa na hiyo kauli kwa sababu kwa muundo wa utaratibu wa Udaktari, ni sawa ametudharau sisi Madaktari wenzake, pia ni sawa na kuwadharau wakufunzi wetu.

Kwani kabla ya kufika hatua tuliyopo sisi tunakuwa tumepitishwa na TCU, tumepitishwa na Wakufunzi wa ngazi ya chuo na katika taasisi za afya ambazo wanatufundisha, hivyo kauli yake ni kama amedharau mamlaka zote hizo na ametudharau sisi ambao ni Madaktari wenzake.

Mbali na hapo amesema Madaktari wanafeli masomo ya upasuaji, sisi inajulikana wazi kuwa fani yetu ni vitendo zaidi kuliko nadharia, lakini mazingira yaliyopo wanatupima kwa njia za nadharia.



Pia soma: Madaktari wataraji wamekuwa ombaomba Mtaani kisa leseni, wamuangukia Waziri Ummy Mwalimu na Rais Samia

Kuna waliofaulu? Kama wapo hawana uhalali wa kulalamika
 
Mimi kama mdau wa afya, naona hawa Madaktari wanaonewa sana, miaka mitatu iliyopita hakukua na hii mitiani, hii ilianza tu baada ya kuona watu wameanzisha ugumu Law school wakasema why not in Medical school, so ilivyoanzishwa hakukua na utaratibu mzuri wala research nzuri iliyofanywa.

Hivyo bhas kama umefatilia hii press, MCT waliamua kupush kutoa license despite walikua wanafeli sana, nasikitika kuona mtu anacomment anasema kua nilifanya ilo paper na nikafaulu, hawajui walikua wanafaulu kwa ngapi, hii ndo ikawa kigezo kua wakawa hawaonyeshi matokeo yao kwenye system, nimefanya kazi na interns wengi na najua uwezo wao na weledi wao, na nilichoona kua hawa Madaktari bado ni wadogo na bado wanandoto kubwa ebu tusiwakatishe tamaa.

Wewe unayelalamika kua uwezi tibiwa na Doctors waliofeli unajidanganya kama hujui historia ya hawa. Unaweza ukaenda hospital ukajua umekutana na specialist mkubwa kumbe ata hao wangepata huo mtiani enzi zao wasingetoboa.

Ushauri sasa, kwakua wanasema wamekaa mda mrefu sana nyumbani tusipoteze skills zao wapewe nafasi, wapewe license maana ni haki yao kwa hoja kubwa ya kua wameshafanya pre internship ya MCT wakafaulu, wakafanya one year internship pia wakapitishwa na maspecialist na kupata grades nzuri.

Wakakaa first on calls na kufanikisha mgonjwa anapona ivyo bhas post internship examination has no part on giving them license, huku naomba baraza likishirikiana na MCT plus wadau wa afya wenye sense na utu, wachakatue huu mtiani upya, ili ukirudi usilete malalamiko kama haya kwenye jamii, hili ni anguko.

NB: Hawa ni watoto maskini wa vidumu na fagio waliojitoa mhanga kwenye jamii, Medicine has never been easy.
Bwana Dokta principle ya DEMAND and SUPPLY ndio inayofanya kazi hapo.
Utitiri wa wahitimu unawachuja vipi? Madkta tuna amini mmesoma nambo mengi mbona unatuangusha.
Wahasibu wana CPA walimu nao mtihani unakuja,i wanashetia, injinia nao wanao muda mrefu tu.
Binadamu kukubali mabadiriko huwa ni ngumu. Ukweli ni kwamba serikali inahitaji madokta na wale weledi watafaulu walevwazembe watachujwa wakarafute maisha mengine.
Dr. Huku makazini ukanjanja ni mwingi sana serikali inataka smart people na hii iwe kila sekta.
Poleni sana madokta.
Nawashukuru vilevile kwa kutuhudumia afya zetu, endeleeni na moyo huo huo japo mnakutana na changamoto nyingi.
 
Miaka mi5 ya Medical school halafu mmoja wa internship halafu mtihani wa masaa ma3 unaamua hatma ya mtu hyu dah sometimes tukubali kuna mambo hayakuwekwa sawa. Hivyo kwa kunyima leseni na yeye kukaa nyumbani ndo kunamuongezea uwezo? Hapana
Mwana saikolojia akikuuliza maswali matatu tu, anapata A to Z kuhusu wewe.
Mtihani ndio njia rahisi kumpima mtu.
Kwa jawaida mwanafunzi au muhitimu anakuwa na kumbukumbu nyingi sana kuliko aie hitimu zamani.
Kama una deal na mwili wa binadamu na una sahau sahau uoni ni hatari.
Hata hivyo majibu ya wanafunzi hayawagi sahihi 100% ndio maana kuna grade.
Kuna min requirenent na max, Watafaulu tu na wabovu watachujwa.
Naunga mkono mitihani.
 
Kwani form 4 ikoje? Mtihani wa masaa mawili kupima elimu uliyoipata kwa miaka minne. Huko mlipitaje?

Kama unajua unajua tu, hivyo vingine ni visingizio.
Yan unalinganisha form 4 na chuo cha afya em acha hzo ww. Hapa ni mkufunzi wa hali ya juu anatumika,mwanafunzi pia na yeye anajiadjust kila miaka ili kutoka kuwa kwenye vitabu na kuwa na clinical skills
 
Mwana saikolojia akikuuliza maswali matatu tu, anapata A to Z kuhusu wewe.
Mtihani ndio njia rahisi kumpima mtu.
Kwa jawaida mwanafunzi au muhitimu anakuwa na kumbukumbu nyingi sana kuliko aie hitimu zamani.
Kama una deal na mwili wa binadamu na una sahau sahau uoni ni hatari.
Hata hivyo majibu ya wanafunzi hayawagi sahihi 100% ndio maana kuna grade.
Kuna min requirenent na max, Watafaulu tu na wabovu watachujwa.
Naunga mkono mitihani.
Mm sijapinga mtihani ila nasema bado sio kigezo sahihi. Unadhan kutibu ni kufanya mtihan tu? Inategemea na exposures pia. Ushaona mtihani huo maswali yake? Unajua yamebase wap? Level ya hospitali husika? Decision-making ya kujib swali husika unaeielewa kua inadepend na mambo meng?
 
Bwana Dokta principle ya DEMAND and SUPPLY ndio inayofanya kazi hapo.
Utitiri wa wahitimu unawachuja vipi? Madkta tuna amini mmesoma nambo mengi mbona unatuangusha.
Wahasibu wana CPA walimu nao mtihani unakuja,i wanashetia, injinia nao wanao muda mrefu tu.
Binadamu kukubali mabadiriko huwa ni ngumu. Ukweli ni kwamba serikali inahitaji madokta na wale weledi watafaulu walevwazembe watachujwa wakarafute maisha mengine.
Dr. Huku makazini ukanjanja ni mwingi sana serikali inataka smart people na hii iwe kila sekta.
Poleni sana madokta.
Nawashukuru vilevile kwa kutuhudumia afya zetu, endeleeni na moyo huo huo japo mnakutana na changamoto nyingi.
The issue here huu mtiani haujafanyiwa research ya kutosha, other countries within EAC wanafanya only pre intern examination for license na baada ya hapo wakishafanya intern hawapewi exam kwasababu washakua pitishwa na panel assessment ya kila idara tena zinazoongozwa na specialists, kuna manguli na maprofessor wa Medicine wako kila kona Tanzania unafikiri hawakuliona hili kitambo? Other point ni 100 times better to retain a person in internship centers if they do not meet the criteria to become a doctor, for example, in terms of ethics and academic excellence until they reform and become fit for the job. This is better than the current approach used by MCT (Medical Council of Tanzania), which may not be an accurate filter, as it could prevent smart doctors from practicing while allowing ignorant individuals to obtain practicing licenses📌📌📌
 
The issue here huu mtiani haujafanyiwa research ya kutosha, other countries within EAC wanafanya only pre intern examination for license na baada ya hapo wakishafanya intern hawapewi exam kwasababu washakua pitishwa na panel assessment ya kila idara tena zinazoongozwa na specialists, kuna manguli na maprofessor wa Medicine wako kila kona Tanzania unafikiri hawakuliona hili kitambo? Other point ni 100 times better to retain a person in internship centers if they do not meet the criteria to become a doctor, for example, in terms of ethics and academic excellence until they reform and become fit for the job. This is better than the current approach used by MCT (Medical Council of Tanzania), which may not be an accurate filter, as it could prevent smart doctors from practicing while allowing ignorant individuals to obtain practicing licenses📌📌📌
Do you want to tell me the filter will biased out the smart and leave non smart Doctor?
Always good filter filt out all unwanted and achieve high results.
The issue is if the exam is not valid the board/council should think of standard exam but not reject it.
Why we Tanzanian we have developed a habit of opposing and rejecting any change proposed by experts or government?
We critisize everything even if the agenda/issue has positive impact!
The exam has more benifit.
Imposter Syndrome: this is what the doctors face and many experts.
 
Mm sijapinga mtihani ila nasema bado sio kigezo sahihi. Unadhan kutibu ni kufanya mtihan tu? Inategemea na exposures pia. Ushaona mtihani huo maswali yake? Unajua yamebase wap? Level ya hospitali husika? Decision-making ya kujib swali husika unaeielewa kua inadepend na mambo meng?
Mtihani si utatungwa na baraza? Halafu si kuna vigezo vya kutunga mtihani?
Hata wakiajili bila mtihani bado personal interest hazikwepeki na lawama zitakuwepo sababu hao ni binadamu tu. Hata wewe akija bibi yako kutibiwa huko hispital utamfanyia upendele tu.
Si busara kuacha mambo ya maana kwa sababu ya personal interest za mtu mmoja.
Nadhani mngejadili zaidi ubora wa mtihani au upimaji ufanyikeje sio kutupilia mbali.
Serikali sio wajinga wanajua wengine wamepata vyeti kiujanja ujanja huko vyuoni.
Kumbuka hivi vyuo maadili vinatofautiana.
Ibawezekana mwenye second ckass yuko vizuti kuliko wa first class.
Mi ningependa sana Tanzsnua tuwe na fsir competion kwenye kila jambo.
Hsta wakuu na mabos wa idara mbali mbali wawe waba compete sio kuteuliwa kiushkaji tu kisa mnafahamuana.
 
Some of the so called experts leave a lot to be desired! Wanafunzi wakifeli wengi, mwalimu lazima uljiulize! I'm not a medical doctor, lakini kwa udesaji wa siku hizi wa TZ, wataalamu wengi pia ni feki!

Pia si sahihi wahitimu kukaa muda mrefu mtaani bila practice afu ghafla unawashtua na mtihani. The whole system need to be revisited! Hospitali nyingi madokta hawatoshi, wale wa Muhimbili wanarukaruka kama njiwa from one hospital to another kusaka pesa! Serikali iweke mifumo bora! Madakatari walipwe vizuri, watulie mahali pamoja, kusudi na hawa vijana wapate nafasi! Maana taarifa za kuaminika ni kwamba, the so called wataalam, hugombania hizo nafasi na vijana; na kijana akigang'ania, basi kufeli kunamuhusu. Ethics za wataalamu pia zimeshuka!

Mfumo mzima uangaliwe na wale wataalam credible, kusudi haki itendeke. Si sahihi kudharau malalamiko, kiongozi mzuri huangalia malamiko na kuyatathmini, kisha kuyafanyia kazi. Kufeli kwa wingi pia kunaashiria ubovu wa walimu! Mjitathmini!
 
Mtoto wa kaka yangu kakosa chuo kisa leseni .maana chuo usika walitaka .
Hawa MCT wawaangalie vijana wetu hata kwa wale wanao takanda kujiendeleza maana hao wamechagua kusoma zaidi wawape hata scholar license.
Hapa ndo tutakuwa tunakuza hii fani ya afya...tuweke categories mbalimbali.
Na kwawale ambao kazi zao azikutani na wagonjwa kama walimu na wamaofisini ie NHIF, na baadhi ya taasisi.
Wapewe leseni kila mtu anameans yake aliyochagua..
Sasa wao kuzani kila mtu hatibu..vijana wetu wameishia kufapa kupata sonona.
 
Kwani form 4 ikoje? Mtihani wa masaa mawili kupima elimu uliyoipata kwa miaka minne. Huko mlipitaje?

Kama unajua unajua tu, hivyo vingine ni visingizio.
I
Do you want to tell me the filter will biased out the smart and leave non smart Doctor?
Always good filter filt out all unwanted and achieve high results.
The issue is if the exam is not valid the board/council should think of standard exam but not reject it.
Why we Tanzanian we have developed a habit of opposing and rejecting any change proposed by experts or government?
We critisize everything even if the agenda/issue has positive impact!
The exam has more benifit.
Imposter Syndrome: this is what the doctors face and many experts.
Hey, I understand your concerns, and I agree that the policy should be revised again. While filters can be useful to achieve high results, it's essential to ensure that they are fair and not biased against smart doctors. The current exam may not be valid, but that doesn't mean we should reject it entirely. Instead, the board should consider creating a standard exam that truly evaluates a doctor's skills and knowledge. It's true that sometimes we tend to oppose and criticize changes proposed by experts or the government. However, constructive feedback is essential to ensure that policies and decisions are in the best interest of everyone involved. The exam's revision can have a positive impact, and it's crucial to address the issue of Imposter Syndrome that doctors and experts face. Ultimately, the goal should be to create a fair and effective exam that allows all qualified doctors to practice, while also upholding high standards of medical care in Tanzania📌📌🙏🏼
 
Kuna waliofaulu? Kama wapo hawana uhalali wa kulalamika
Ninaweza kuelewa wasiwasi wako, lakini ni muhimu kutofautisha masuala ya mitihani ya sekondari na mitihani ya udaktari. Mitihani ya sekondari inaweza kutofautiana na mitihani ya udaktari kwa kiwango cha utata na ugumu. Ni haki kwa wale waliofaulu kufurahia mafanikio yao, lakini tunapaswa pia kutambua kuwa kuna masuala yaliyojitokeza katika mitihani ya udaktari ambayo yanahitaji kushughulikiwa. Kupaza sauti si tu kuhusu wale waliofaulu au kushindwa, bali ni juu ya kuhakikisha kuwa mchakato wa mitihani ni wa haki, uwazi, na unaendana na viwango vya kitaaluma. Kuna masuala kama vile utungwaji wa maswali ambao hauendani na viwango vya matibabu, ukosefu wa uwazi katika kutoa matokeo, ambayo yanaweza kuathiri uwezo wa madaktari kufanya kazi zao kwa ufanisi.
Kwa kuunganisha sauti zao, tunataka kuhakikisha kuwa madaktari wote wenye uwezo wanapata nafasi ya kuonyesha ujuzi wao na kutoa huduma bora za afya. Hii inahusu si tu wale waliofaulu au kushindwa, bali ni juu ya kuboresha mfumo mzima wa mitihani ili kuwa na madaktari bora na wenye ujuzi ambao watasaidia kuboresha huduma za afya na ustawi wa jamii yetu.

Ni muhimu kuzingatia masuala yanayohusu haki na uwazi katika mchakato wa mitihani ili tuweze kujenga mfumo thabiti na wa kuaminika ambao unathamini na kukuza talanta ya madaktari wetu na kuboresha afya ya jamii yetu 📌
 
Back
Top Bottom