Baraza la Madaktari lawajibu Madaktari Watarajali waliodai hawana imani na MCT

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,814
11,991
Wizara ya Afya.jpg

Kupitia mitandao ya kijamii kumeibuka mjadala unaosema kuwa 'Baraza la Madaktari Tanganyika lamgomea Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu kuhusu Madaktari Watarajali kuendelea na mitihani yao huku ikiwa Waziri Ummy ameunda Kamati ya kuchunguza malalamiko ya Watarajali hao'.

Mnamo Agosti 13, 2023, Waziri Ummy Mwalimu alitoa taarifa kwa Umma ya kueleza kuwa ameunda Kamati ya uchunguzi wa malalamiko ya mitihani ya Watarajali.

Kamati hiyo iliwasilisha ombi kwa Waziri Ummy la kuongezewa muda wa ziada kuendelea kufanya uchunguzi wa kina wa malalamiko ya Watarajali hao na Waziri Ummy alikubali ombi hilo.

Aidha, ikumbukwe kwenye tamko la Waziri Ummy Mwalimu alielekeza Baraza la Madaktari Tanganyika kuendelea kutekeleza majukumu na taratibu nyingine za mafunzo ya Watarajali kama ilivyoainishwa kwenye Sheria mpaka hapo itakavyoelekezwa vinginevyo.

Baraza la Madaktari la Tanganyika (MCT) limeundwa chini ya Kifungu cha 4 cha Sheria ya Udaktari, Udaktari wa Meno na Afya Shirikishi Sura Na. 152 na linatekeleza majukumu yake kuhakikisha jamii inapata huduma nzuri na salama kutoka kwa Wanataaluma wenye sifa. Kwa msingi huo Baraza lina wajibu wa kuhakikisha Wanataaluma wanakuwa na sifa za utendaji kazi unaotakiwa kwa kuzingatia mwenendo na maadili ya kitaaluma.

Tunaomba Watarajali wote wawe na subira na waendelee kufuata maelekezo ya Baraza la Madaktari Tanganyika.
 
Back
Top Bottom