WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,457
- 956
Unaweza kutumia vitu ulivyo navyo kutatua baadhi ya dharura zinazoweza kukukabili kwa kufanya yafuatayo:
1. Ushajikuta dukani unataka kununua suruali au sketi lakini huna jinsi ya kujua kama size ya kiuno itakutosha.Hii yaweza kukupata kama uko Tz kwenye maduka ambayo huwezi kujaribu nguo wala hayakubali urudishe ukisha inunua!Usikonde! Chukua nguo hiyo ( sketi au suruali) kama ilivyo kisha zungusha kwenye shingo yako mwenyewe! Ikiungana basi ujue itakutosha maana shingo yako ni nusu ya kipimo cha kiuno chako! Mfano kama unavaa shati size 16 basi most probably utavaa kiuno size 32-34.Maajabu hayo!Jaribu kujipima.
2.Nguo nyeupe zilizofubaa unaweza kuzirudishia weupe wake bila kutumia bleach.Ziloweke kwenye maji ya ndimu kwa muda wa kutosha kisha zisuuze ndipo uanike.
3. Harufu za vikwapa zisizoisha - hii ni kero maana hata upake perfume inaweza isikubali.Mtu mwenye tatizo hili anaweza kushauriwa kuloweka ukoko wa ugali na kisha kutumia maji yake kusugulia makwapa na kisha kuoga kama kawaida.Hii ni kiboko ya vikwapa!
More to come..
1. Ushajikuta dukani unataka kununua suruali au sketi lakini huna jinsi ya kujua kama size ya kiuno itakutosha.Hii yaweza kukupata kama uko Tz kwenye maduka ambayo huwezi kujaribu nguo wala hayakubali urudishe ukisha inunua!Usikonde! Chukua nguo hiyo ( sketi au suruali) kama ilivyo kisha zungusha kwenye shingo yako mwenyewe! Ikiungana basi ujue itakutosha maana shingo yako ni nusu ya kipimo cha kiuno chako! Mfano kama unavaa shati size 16 basi most probably utavaa kiuno size 32-34.Maajabu hayo!Jaribu kujipima.
2.Nguo nyeupe zilizofubaa unaweza kuzirudishia weupe wake bila kutumia bleach.Ziloweke kwenye maji ya ndimu kwa muda wa kutosha kisha zisuuze ndipo uanike.
3. Harufu za vikwapa zisizoisha - hii ni kero maana hata upake perfume inaweza isikubali.Mtu mwenye tatizo hili anaweza kushauriwa kuloweka ukoko wa ugali na kisha kutumia maji yake kusugulia makwapa na kisha kuoga kama kawaida.Hii ni kiboko ya vikwapa!
More to come..