Elections 2010 Unamuunga mkono Dr. Slaa kugombea URAIS mwaka 2010? Jiandikishe hapa

Arsene Wenger,
Mkuu katika kujadiliana mara zote ni hoja kama zako ndizo huongeza kima cha kufikiria, wala usijisikie vibaya kuandika fikra zako. Binafsi toka siku ya kwanza nilipozungumzia swala hili nilipima mengi sana na hasa hali halisi ya nchi za kiafrika..Kama ingekuwa Ulaya ama nchi zenye demokrasia ya kweli basiUbunge ungekuwa na nguvu zaidi lakini sivyo hapa kwetu.

Majuzi tu huko Holland na Uingereza tumeona jinsi bunge lilivyokuwa na nguvu hata kuvunja serikali iliyopo na kuitisha uchaguzi mpya.. hii haiwezekani nchi zetu, mbunge anachukua majukumu yasiyokuwa ya mbunge na kwa bahati mbaya Ubunge nje ya CCM wewe ni ADUI.. Wenzetu Zanzibar walikuwa hivyo hivyo, wakipingana kwa jina la vyama wakasahau kwamba wao ni Wazanzibar kwanza. Sasa hivi taratibu wanajitambua na wanaelewa kwamba kutengana kwao kisiasa kulizidi kuwatenganisha hadi Upemba na Ungazija ukarudi kama wakati wa Sultan.

Bara nako tunatakiwa kujipanga upya, swala sii kumwondoa JK madarakani isipokuwa kuwaondoa CCM na hakuna dawa ya kuua nyoka isipokuwa kumkata kichwa. Huko Zimbabwe kusimama kwa Morgan kugombea urais against Mugabe ndiko kulikobadilisha historia ya nchi ile baada ya vyama vikuu ZANU na ZAPU kuungana na kuondoa ushindani kwa muda mrefu sana. South Afrika tumeona mabadiliko yakianzia kiti cha Ikulu,Kenya, Zambia, Malawi you name it..ni kiti cha Ikulu ambacho kinaweza piganiwa zaidi ktk kuleta mabadiliko na Bunge limefuata mabadiliko ya kiti hicho..

Kumbuka tu kwamba mfumo mzima wa Popular vote unalenga zaidi ushindi wa Ikulu na sii Ubunge.. Kama tungekuwa tukitumia mfumo wa electral vote ambapo chama chenye wabunge wengi ndicho kinachukua Ikulu basi bila shaka tungeweka nguvu zetu zaidi ktk Ubunge zaidi. Hii ndio hali halisi ya nchi zetu mkuu wangu. Hata Nyerere aliyajua hayo na ndio maana aliweka picha ya mgombea yeye mwenyewe akipingana na Ukuta, hali ndani ya chama walikuwepo watu waliopingana naye. Hivyo miaka 23 ya Utawala wa Nyerere ulitokea tu kwa sababu ya mfumo uliokuwepo hivyo tusiendekeze sana akili ya kwamba mgombea wa CCM ni lazima akubalike..Mara zote ushindani unapotokea ndipo watu huamka, mkumbuke Augustine Mrema kama sii wao kuvugana na kufuatiwa kwa vyama CUF na Chadema ktk uchaguzi mwaka 2000 ingekuwa ngumu sana kwa Mkapa.

Makosa ya kutoungana vyama vya Upinzani yameisha fanyika lakini bado hatujachelewa ikiwa bado watakubaliana kumsimamisha mgombea mmoja ktk kiti hiki.. Pia swala la muda mfupi sii hoja kabisa...CCJ imevuma toka mwisho wa Desemba kufikia mwezi wa March tayari Tanzania nzima imeshikwa na homa. Hii ina maana wananchi wamechoka! wanasubiri nabii atakaye warudisha ktk ibada ya kweli. Watu walijiuliza CCJ ni kina nani hao! je, tumaini jipya limepatikana na mengi yalizungumzwa ingawa mimi binafsii naamini ilikuwa changa la macho kupunguza nguvu ya hoja za Ufisadi. Hata hivyo bungeni hapakukalika, Ikulu hadi mitaani hadithi ilikuwa CCJ tena basi habari zilisambaa kwa uharaka zaidi ilipofahamika kwamba ni Waasisi wa chama CCM..Kwa muda mfupi sana CCJ ilitingisha Taifa zima kisiasa, lakini kwa kuwa CCJ imekosa nguvu kwa sababu hadi sasa hivi hakuna jina maarufu ambalo wananchi walitegemea..

Dr.Slaa can, he is the right candidate isipokuwa anahitaji WATU na mkakati bomba nyuma yake..Ni rahisi sana kumshinda CCM kwa hoja. Ni rahisi sana kumshinda CCM tofauti na wengi wanavyofikiria na naposema dr.Slaa anahitaji watu inabeba uzito mkubwa wa hoja nzima ya mgombea. What he need ni support ya baadhi ya watu haswa toka ktk taasisi muhimu sana. Kifupi Dr.Slaa akitumia mbinu alizotumia mwalimu kutuletea Uhuru wetu. Akikaa na wazee waasisi wa Uhuru na Muungano wa jamii hizi mbili na kusikiliza ushauri wao..Ushindi unaweza patikana na kama hautapatikana basi Upinzani wa kweli utakuwa umezaliwa UPYA.
 
Muombeni mzee mwanakijiji aongeze majina yeye anayo mengi mwanakijiji, mwafrika, mwafrika wa kike, mgaya, david solomon, madilu, maxshimba et al
 
Labda huyu Dr. Slaa anatakiwa KUAMSHWA. Nimeona tufanye SENSA ya haraka haraka humu ndani ya JF. Kwa wale wote wanaoona DR SLAA agombee mwaka huu basi hebu jiandikishie jina lako tuone mwisho wa wiki tutakuwa wangapi. Tujitokeze kwa wingi ili kumuonyesha Dr. Slaa anavyohitajika.

Dr. Slaa, samahani nimeamua kuanzia jina lako kwa makusudi kabisa maana JEMADARI lazima awe mbele na wengine watafuata.

1. Dr. Slaa 2. MKANDARA 3. King of kings 4. Masanilo kugema 5. Fidel80

6. Bht 7. Tanzania 8. Ndege ya Uchumi 9. Jiwe 10. Jakathesi

11. Technician 12. Kilembwe 13. Ndjabu Da Dude 14. Bollo Yeng 15. Selous

16. Nyamizi 17. Mfwatiliaji 18. Sikonge 19. Ben 20.Lorah

21. Chief 22. Alpha 23. Malunde-Malundi 24. Muhindi 25. Nanu

26. Betina 27. Baija Bolobi 28. Epigenetics 29. Member 911 30. Mlalahoi

31. Mag3 32. Nndondo 33. Tai Ngwilizi 34. Sn2139 35. Shalom

36. Mc 37. Firstlady1 38. Henge 39. Nemesis 40. Mchili

41. Ngambo Ngali 42. Positive Thinker 43. Advocate Jasha 44. Zhule 45. Araway

46. Pasco 47. Mbu 48. The Invincible 49. Vivian 50. Daughter

51. Deo 52. Holowane 53. Kingi 54. Tzpride 55. Mzee Punch

56. Kiby 57. Mtangi 58. Birigita 59. 60. Rwabugiri

Tumeshakaribia 60 huraaa!!!!!, lengo ni 1,000 hadi wiki lijalo.

(Andika jina lako tu na mie nitaongeza kwenye listi)
7306

Nami 60. Rwabugiri
Dr. Slaa anafaa sana, cjui ile sheria inayo sema akipata asilimia kadhaa hata asipokuwa raisi awe mbunge ilipitishwa? Kinacho boa hapo kwamba asipo
pata ukulu hata mjengoni dom haendi, kwahiyo hofu ya wengi iko hapo kwani anfaa pote, na hatutamani asipate walau mojawapo kati ya hizo!
 
Rwagubira,
Kuna sheria nyingi za kikatiba zinatakiwa kubadilishwa. Binafsi sikubaliani na ule mpango wa mtu anayeshindwa kurudi bungeni kwa sababu ya asilimia alizopata isipokuwa mgombea yeyote kiti cha rais ndiye haswa anayetakiwa kutopoteza kiti cha Ubunge.
Muhimu sheria isistize tu kwamba mgombea kiti cha urais ni lazima awe mbunge aloshinda uchaguzi uliopita,hivyo akishinda kiti cha urais anaacha nafasi ya jimbo na uchaguzi utafanyika upya, akishindwa basi moja kwa moja anarudi kuwakilisha jimbo lake. Ni muhimu mihimili mitatu iwe huru pasipo kuchanganya viongozi wake. wabunge watabaki kuwa wabunge, rais na serikali (Mawaziri) nje ya bunge na Mahakama kujitegemea. Viongozi wa mikoa na wilaya (RC na DC) wachaguliwe na wananchi na lazima wawe wakazi wa majimbo husika.
Mwisho ni lazima tuwe na baraza la senate ambalo baada ya bunge kupitisha sheria ama matumizi, baraza hilo ndilo litakuwa na uamuzi wa mwisho kisheria na wenye nguvu ya kupitisha ama kupinga maazimio ya Utawala uliopo madakani kwa faida ya Taifa.
 
Mkandara,

Maelezo yako yametulia sana. Ili kuiondoa CCM kwenye madaraka kwa sasa, dawa ni kumuondoa mtu wao pale Magogoni na kupeleka mtu atakayeibadili katiba ya Tanzania. Bunge letu halina meno na labda akija mtu wa juu aanze kuwaondolea uvivu basi wataanza kutimiza wajibu wao. Sasa wanazidi kuliongeza bunge badala ya kulipunguza. Ila mishahara ya wafanyakazi hawawezi kuongeza maana hawana hela.

Jamaa wamejisagau sana na dawa ni kusubiri wakati wa kampeni ni ndiyo kuanza kuwaiga Wagiriki kwa asilimia fulani. Nisingelitaka kusikia watu wamepoteza maisha kama Greece kwa sasa ila ukweli ni kuwa watu wanaona na Watanzania huwa kwa kuiga tuko juu sana. CCM wanatakiwa kufahamu kuwa ukiona mwenzio ananyoa basi wewe tia maji. Ila wenzetu WANATIA PAMBA MASIKIONI.

Njooni tuendelee kujiandikisha. Tumeshafika tayari 60, si mbaya sana hadi leo hii. Nia ya kumpeleka Dr. Slaa Magogoni tunayo, Sababu tunayo na Uwezo tunao.
 
62. babaDesi + mamaDesi + Over 18 son and daughter. Dont worry, I am not a Dictator! I know their stand regarding Dr Slaa. so, we move to...
66.
 
MawazoMatatu

Nashukuru kwa ufafanuzi wako kwa nini tusikimbilie kumlazimisha Slaa agombee urais, nikitolea mfano wako wa makundi kundi la pili (the puppets) ndilo lenye matatizo makubwa na linajua athari za uongozi uliopo lakini kwa maslahi yao halitaki kukubali ukweli, kwa hiyo kuli convince kundi kama hili kuwa kuna shujaa kama Slaa ni kazi kubwa.

Makundi yaliyobaki la kwanza (vijijini) na la tatu (know how) ni rahisi kidogo ukilinganisha na la pili, kumuuza Slaa kwa kundi la kwanza inawezekana lakini inahitaji nyenzo kubwa na muda, Dr. Slaa anajulikana sana na kundi la tatu hata la pili (the puppets), sasa watu wa kumuuza watoke wapi au kundi lipi, tukisema watoke kundi la tatu ambalo ndilo walimo wanaJF kwa hali halisi itakuwa kazi na kusema kundi la pili walimo ma puppet wa chama tawala vile vile ni kazi kweli kweli.

Sasa kifanyike nini, tusijidanganye kuwa Slaa ameshakuwa maarufu kuliko Mrema, umaarufu wa Slaa ni wa utendaji kazi tofauti na umaarufu wa Mrema ambao ni wa propaganda(mdomo sana/na uongo ndani) ambao kwa siasa za Tanzania bado una play part kubwa hasa vijijini, ukiwaambia watu wa vijijini kuwa tumewaletea Slaa kwa vile alifichua wizi wa EPA sijui kama watakuelewa usikute wengine hata EPA hawajui ni nini, kwa hesabu ya haraka haraka ndiyo maana sisiem wanaomba usiku na mchana Slaa agombee, kwa hiyo mimi bado nasema tumsubiri mwenyewe aamue kwa vile nafikiri anajua uzito wa kazi ulio mbele yake.
Mkuu Luteni umenipata vizuri kabisa...
Mkuu kwa maneno niliyoyaweka nyekundu ..ni kama ulikua ndani ya kichwa changu....!
Umeeleza vizuri sana mkuu hakuna jinsi ningeweza yaeleza kuliko ulivyofanya... safi sana.
Nyongeza tu: ni kwamba hilo kundi la pili vilevile linajulikana kama la "wafuata upepo" na kwa mujibu wa mkuu wa kaya hawa ni 70% .
 
Ni wafanyakazi hao hao waliomfanya atambe kushinda kwa kishindo. ndiyo! hao hao, kwani vipi si ni nyie waalimu mliteuliwa kusimamia uchaguzi? si ni nyie mliokuwa mnahesabu kura? si ni nyie mliowadanganya wasioweza kusoma kuwa picha ya kikwete ndiyo picha ya lipumba? si ni nyie mliofanya hesabu za kinyumenyume kwa ajili yake?

Ninyi wafanayakazi ambao leo amesema hataki kura zenu, mkifunguka kidogo tu, Kikwete hatakuwa Raisi tena. Hesabu zake zimeishia kwenye wafanyakazi 350,000. tu. Lakini nyie ni wengi kuliko alivyofikiri. Fanyeni hivi.

1. Kila mafanyakazi mwenye mtoto mmoja ahakikishe hampigii kura kikwete. ( aliyefika umri)
2. Kila mfanyakazi mwenye marafiki wawili wanakunywa bia au wanachangiana kwenye shida na raha, washawishi wasimpigie kura kikwete.
3. Kila mfanyakazi ahakikishe baba na mama yake hawampigiii kura kikwete.
4. Kila mfanyakazi ahakikishe watu wawili anaosali nao hawampigii kura kikwete
5.Kila mafanyakazi ahakikishe kaka ama dada yake hampigii kura kikwete.
6. Kila mfanyakazi ahakikishe mtoto mmoja wa shangazi au mjomba hampigii kura kikwete
7. Kila mfanyakazi ahakikishe mtoto mmoja wa kaka yake au dada yake hampigii kura kikwete.

Sababu ya kuwapa ni kwamba. KAMA WATAMPA KIKWETE KURA, KIPATO CHAKO HAKITATOSHA TENA WEWE KUWASAIDIA AMA KUSHIRIKIANA NAO. NA WAO HAWATAKUWA TAYARI KUPOTEZA KILE WANACHOKIPATA KWAKO AU USHIRIKIANO WENU.

Kitakachotokea ni hiki. ( kwa uchache)
M+1+2+3+4+5+6+7
350,000+350,000+700,000+700,000+700,000+350,000+350,000+700,000= 4,200,000.

Kwa hesabu hii kikwete atakuwa amepoteza kura milioni nne na laki mbili kupitia kwenu. na hesabu hii inaendelea mbele.

Halafu baada ya hapo WAALIMU wahakikishe kuwa CCM hawaibi kura hata moja kwenye Kuhesabu kura, hata kama mtapewa pesa msikubali. Kazi yenu siku ya uchaguzi ni kuelimisha watu juu ya haki halisi ya wao kupiga kura.

Hebu soma hizi Point chini. Kama JAMII imekuchoka, wataanza kampeni za KIFAMILIA na hapo ufahamu kuwa utakwenda na maji. Hizi za watu kuambiana, basi hata utowe PILAU NA KHANGA, na mie nikaja kumwambia kaka, mjomba, shangazi, binamu nk kuwa MSIMPIGIE KURA, hapo mkuu wangu una hali mbaya.

Mkuu Luteni umenipata vizuri kabisa...
Mkuu kwa maneno niliyoyaweka nyekundu ..ni kama ulikua ndani ya kichwa changu....!
Umeeleza vizuri sana mkuu hakuna jinsi ningeweza yaeleza kuliko ulivyofanya... safi sana.
Nyongeza tu: ni kwamba hilo kundi la pili vilevile linajulikana kama la "wafuata upepo" na kwa mujibu wa mkuu wa kaya hawa ni 70% .
 
Mawazomatatu,
Ebu nikuulizeni nyie.. Wakati JK anapendekezwa kugombea Urais mwaka 2005, huko vijijini kina nani walimfahamu! Hivi kweli Kikwete alikuwa maarufu zaidi ya Mbowe, Mrema, Lipumba na wagombea wengine waliomtangulia toka mwaka 2000. Iliktokea nini akashinda kwa asilimia kubwa kuliko hata ile ya Mkapa ambaye pia tunajua fika kwamba Mrema alikuwa maarufu kuliko yeye. Hivyo kushinda kwa CCM hakutokani kabisa na umaarufu bali mbinu chafu wanazotumia.

Mkuu swala zima la uchaguzi linajulikana kwamba Takrima na ubabe ndio silaha kubwa ya CCM siku zote. Safari hii akisimamishwa mtu ni mnuhimu tuwe makini zaidi ya mwaka 2005 ndio kujifunza kwenyewe. Zanzibar waliibiwa kura mwaka 2000 na 2005 lakini kila siku ushindani unazidi kuwa mkubwa sana na CCM wanaishiwa mbinu. Mwaka huu kabla ya uchaguzi CCM hawakuona ndani zaidi ya kujisogeza karibu na Seif Sharrif Hamad, huyu ndiye kichwa cha CUF. Na wamekwisha msogeza marefu ya rungu lao, kilichobakia wanasubiri wakati muafaka wa kukikata kichwa hicho wakati wa uchaguzi.
 
Mawazomatatu,
Ebu nikuulizeni nyie.. Wakati JK anapendekezwa kugombea Urais mwaka 2005, huko vijijini kina nani walimfahamu! Hivi kweli Kikwete alikuwa maarufu zaidi ya Mbowe, Mrema, Lipumba na wagombea wengine waliomtangulia toka mwaka 2000. Iliktokea nini akashinda kwa asilimia kubwa kuliko hata ile ya Mkapa ambaye pia tunajua fika kwamba Mrema alikuwa maarufu kuliko yeye. Hivyo kushinda kwa CCM hakutokani kabisa na umaarufu bali mbinu chafu wanazotumia.

Mkuu Mkandara sijui unazifahamu kwa kiasi gani siasa za TZ lakini ni ukweli ulio dhahili kuwa kikwete alikua maarufu kuliko mbowe mwaka 2005 hilo halina ubishi
1. Kikwete alikua amekwisha fanya kazi serikalini miaka karibu 20 kabla ya kugombea tofauti na Mbowe ambae alikua mbunge kwa kipindi kimoja tu kabla ya kugombea urais(2005)
2.Kikwete tayari alikua amekwisha jaribu kugombea tiketi ya urais kupitia ccm mwaka 1995 tofauti na Mbowe ambae alikua amefanya hivyo kwa mara ya kwanza kwenye ngazi ya chama.
sababu ni nyingi mkuu...naweza kuendelea na kuendelea umesahau ile homa ya boyzIImen ya mwaka 1995.

Suala la Mkapa nalo lina sababu zake alibebwa na umaarufu wa Nyerere na ndio mana mwalimu alizunguka nae TZ nzima kumnadi..

CCM hata wakiweka mgombea mbovu bado wana advantage ya umaarufu wa chama ndugu yangu..! lazma tuwe na mgombea anayeweza kupambana na umaarufu wa CCM pia sisemi Dr.Slaa hawezi au mwingine yeyote yule ila inabidi tuwe na mikakati dhabiti ya kumtambulisha na kumuuza kwa wananchi


Mkuu swala zima la uchaguzi linajulikana kwamba Takrima na ubabe ndio silaha kubwa ya CCM siku zote. Safari hii akisimamishwa mtu ni mnuhimu tuwe makini zaidi ya mwaka 2005 ndio kujifunza kwenyewe. Zanzibar waliibiwa kura mwaka 2000 na 2005 lakini kila siku ushindani unazidi kuwa mkubwa sana na CCM wanaishiwa mbinu. Mwaka huu kabla ya uchaguzi CCM hawakuona ndani zaidi ya kujisogeza karibu na Seif Sharrif Hamad, huyu ndiye kichwa cha CUF. Na wamekwisha msogeza marefu ya rungu lao, kilichobakia wanasubiri wakati muafaka wa kukikata kichwa hicho wakati wa uchaguzi.
Suala la kulinda kura ni moja na suala la kuwa na mbinu za kumnadi mgombea wako akubalike ni suala lingine
 
Mkuu,
Mbona umenukuu Umaarufu wa Jk na Mbowe tu?..
Swala la kufanya kazi serikalini muda mrefu halizidishi Umaarufu wowote ktk kugombea kiti cha Urais. Wamegombea kina Warioba, Salim, Malecela na wengineo wenye record kubwa kuliko JK na walishindwa. Swala la kutoivua CCM madaraka ni swala la imani tu, hakuna uhalali wowote kwani Mkapa ktk kipndi cha pili mwaka 2000 Nyerere hakuwa nyuma yake. Lipumba na CUF ndio walichukua umaarufu mkubwa na kwa bahati mbaya mchezo mchafu ulichezwa ukichangiwa na mvutano baina ya NCCR,TLP na Chadenma pamoja na kwamba Chadema hawakusimamisha mgombea.

Zipo sababu nyingi za Upinzani kushindwa kuchukua Uongozi kuliko sababu za kuiwezesha CCM ushindi. Watu wengi hawana imani na vyama vya Upinzani kutokana na Uongozi uliopo. Chadema uchaguzi wa 2005 wangefanya vizuri isipokuwa swala la Udini na Ukabila lilipotumika kuviua vyama hivi viwili (CUF na Chadema) na kwa bahati mbaya zaidi vyama hivi vilibaki kujitetea hadi uchaguzi ulipofika. CCM siku zote hutafuta weakness ya vyama vya upinzani na kuanza mashambulizi yake...Na kwa bahati mbaya vyama hivi hujisahau wakashindwa ku counter attack badala yake wanajihami..Na siku zote sii rahisi kupata ushindi kwa kujihami wanaoweza ni Wataliani tu ktk mpira...

Hata hivyo, Dr Slaa anaweza kabisa kutoa ushindani mkubwa kwa JK maadam Chadema na CUF wasimame nyuma yake kama Chadema walivyoweza kusimama nyuma ya Lipumba mwaka 2000. Vyama hivi viwili tu vikisimama nyuma ya mgombea mmoja, trust me CCM watayumba na kama ushindi hautapatikana basi mwaka huu utayaweka mazingira safi kwa jmwaka 2015. Any changes za uongozi mwaka 2015 ni lazima zianze ktk uchaguzi huu na sii kusubiri mwaka 2015 kwani nina hakika vyama vilivyopo leo wakishindwa chaguzi za Ubunge ndio imetoka. Uhakika wa popular vote ni mgombea wa Urais siku zote. Mimi siwezi kukipigia kura Chadema ikiwa hakina mgombea Urais na siku zote watu wanaotaka Jk arudi madarakani hujikuta wakimpa kura mbunge wao kwa sababu yupo tiketi moja na rais mtarajiwa. Nitakukumbusha tena - Winner take all ndio mfumo wa popular vote.
 
Chadema lazima kiweke mgombea urais hilo halina ubishi, ubishi unakuja ni nani wa kupeperusha bendera ya Chadema. CCM hategemei umaarufu wa mgombea kwa sababu ina machinery kubwa ninaposema machinery sina maana ya sera nzuri hata kama wana sera nzuri au mbaya lakini wao wana dora, uwezo(pesa), mtandao, umri, watu(puppets), nyenzo nk, ndiyo maana Mkapa na Kikwete pamoja na kutojulikana sana walishinda kwa kishindo.

kitu kingine tusidanganyane kushinda urais bila wabunge (minolity government) ndiyo solution tunasahau kuwa huyo rais atakuwa anaelea juu juu bila mshiko wowote ataikuta katiba ile ile na sheria ni zile zile na mikataba ilishapitishwa na bunge kuibadilisha itakuwa kazi nzito, bills zake zikikataliwa na bunge mara mbili inabidi aziondoe au alivunje bunge hapo ndipo mwanzo wa kupigiwa kura za kutokuwa na imani mfano Japan, kama kweli sisi ni wapinzani wa kweli tujiimalishe huku chini kwenye mizizi bungeni ndipo tutakapojenga nyumba imara(urais).
 
62. babaDesi + mamaDesi + two over 18 son and daughter. Dont worry, I am not a Dictator! I know their stand regarding Dr Slaa. so, we move to...
66.

62. BabaDesi 63. MamaDesi. 64. Desison1. 65.Desison2. 66.Desidada 67.


Tunakaribia 70 huraaa!!!!!, lengo ni 1,000 hadi wiki lijalo.

(Andika jina lako tu na mie nitaongeza kwenye listi)
Sikonge

Mimi naona thread hii inakwenda vizuri iko kama serious vile, lakini ninavyoona mleta thread hayuko serious nilitegemea atamwambia BabaDesi asante kwa kura zako lakini nachukua kura yako moja tu na kushauri ai-convince familia yake nao wajitokeze personally badala yake amezichukua zote 5, atatokea mwingine atasema mfano mimi Luteni nawapigia wajomba wangu ishirini sijui nazo utaziongeza, usipoziongeza utaonekana uko biased huo ndio utakuwa mwanzo wa kuharibika kwa kura kama siyo thread kupungua maana yake. Am not offensive nia ni kuiboresha thread.
 
Luteni,

Uko sawa. Ntalifanyia kazi kesho kwa kuondoa majina ya watu wasio member wa JF. Nimechoka na naenda kulala. Kesho jamani.
 
Dr. Slaa asigombee Urais naye amekiri kwamba watu wake wa Jimbo lake la Karatu bado wanamhitaji.
Na sio rahisi kupata Urais katika Mizengwe ya CCM. Hivyo, aendelee vizuri katika monitoring ya uozo uliopo na utakaotokea.
 
Akagombee uaskofu huko kwa wakatoliki wenzake nchi hana ubavu...wowote poleni

Padre awe rais on my dead body!!!!

Nilikutegemea uje uandike tangu siku ya kwanza hayo maneno. Pole kwa matatizo yaliyokupata hadi umekuja kuandika siku ya tatu. Tumeshakuzoea kwa maneno kama hayo. Ndiyo uzuri na ubaya wa Demokrasia. Kama Dr. Slaa atashinda na awe Rais, wewe ukiamua KUJILIPUA na ufe na watu kadhaa nikiwemo mimi si mbaya sana. Ila nina uhakika Watanzania wengine wataanza kushi kwenye nchi inayofuata sheria. Yakikushinda na ukataka kuishi, unaweza kwenda Pakistan au Afghanistani na kama huna nauli, Somalia hiyoo hapo karibu. Ukienda Zenji, mhhh wala Samaki wale ahh. siku hizi wanakula bata.
 
Back
Top Bottom