Ukweli wa uwepo wa Mungu na Makazi yake upo hapa

Mungu...alikuwepo kabla ya hivyo vitu ..yupo na atakuwepo...vyote vitapita....na uhai sio jua kwan kuna viumbe hai haviishi mwenye jua na vinasonga tu...
Sikatai yakupasa ujue Mungu roho nafsi takatifu ndiyo maana walio mwona Mungu walimwona kwa moto;
 
Kuanzia 1999 mpaka sasa zaidi ya miaka 16 nimekuwa nikifanya utafiti wapi yalipo makazi ya Mwenyezi Mungu Kisayansi na Kutumia Vitabu vitakatifu hasahasa Biblia Takatifu nimepata majibu pasina shaka kila mumoja wetu atakubaliana nayo.
Utafiti huu haulengi kumchafua mtu mtu yeyote kwa imani yake naomba atakayeshindwa kuelewa asiwe na jaziba maana ni utafiti wangu binafsi.
KISAYANSI; Mpangilio na Usanifu wa muundo wa Ulimwengu wetu ni mpangilio uliofanywa kwa usahihi ndio maana kila kitu kipo katika sehemu yake bila kuathiri kingine kwa mfano; Dunia na Sayari zote katika mfumo wa Jua letu zinalizunguka Jua kwa kasi lakini haziwezi kugongana Na katika Anga yetu kuna Nyota mamilioni na pia Kuna Majua Mengine yametengeneza mifumo mifumo ya Sayari kama tuliyo nayo katika Jua letu, Vitu hivi vinaonekana kwa mbali na haviwezi kufikika kwa urahisi kwa akili za Kibinadamu.
Nina hakika Mwenyezi Mungu anaishi katika mojawapo ya Nyota za Jua kwa kuwa hakuwezi kufikika kwakua kuna joto {moto} kali sana hakuna chochote kinaweza kukaribia hata kwa kilometa milioni moja.

Mpaka hapa nilipo fikia kusoma ,sina haja ya kuendelea uko chini,

Moja,

Katika Anga/sky yetu hakuna jua lingine,labda itokee wanasayansi wakaamua kuita nyota nyinginezo jua,,"NOTE-,Sun/Jua ni Jina/Name". Ila kuna Sun like Stars,either small,same even big, Jua letu ni moja kati ya 100 Bilion stars zilizopo kwa hii galaxy! kumbuka Jua ni Nyota kama nyota nyingine angani, kwenye hii milky way yetu na all over the universe,pia Katika Universe ndipo kuna Galaxy yetu na Galaxy zingine kama 'Andromeda' ambayo ndo jirani yetu, zenye anga zao ambapo pia kunaweza kuwa na Big stars or even Biggest Stars, kama ili la kwetu na pia kuna uwezekano wa kuwa na Solar system kama yetu,usichanganye mambo,Pia narudi tena,hakuna 'nyota za jua', bali kuna nyota ambazo zipo kama/ndogo/au zaidi ya Jua.Pia kuna other Solar System within our Galaxy,,and Solar System yetu is located in the Orion Spur kwenye hii Spiral Milky Way yetu..
Kwa nilivokuelewa,Huu unaosema uchunguzi,ume base kwenye our home Galaxy tu,ambapo wewe ndo unaita 'Universe'! embu rudia hiyo so called research yako tafadhali,kama umeshindwa kujua kua Galaxy na Universe achilia mbali uwezekano wa Universe na Universe nyingine ni vitu viwili tofauti,basi naweza sema ulikua unacheza,hii stori uliyoandika kamwe haiwezi kuchukua miaka 16 kuitunga ,achilia mbali kuwa na walakini mkubwa, ni stori ya dakika moja! Baada ya Dogo kusoma kitabu cha George's Secret Key to the Universe ambapo nauhakika dogo wa miaka mitano anayeanza kukisoma sahivi ataelezea vizuri zaidi yako unayedai umetumia miaka 16 kuelezea maelezo haya ya kitoto.

2nd,

Kitendo cha huyu mungu ku exist inside of this same Universe ,tena kwa maelezo yako tupo nae kwenye galaxy moja maana yake there is nothing special kuhusu yeye,kwa maelezo yako,u-special wake ni yeye kuishi ndani kwenye jua,very funny!kwa maana nyingine,mwanzo wetu ndio mwanzo wake,na yeye pia ni matokea ya Big Bang!sasa kama yeye pia ni matokeo ya mwanzo wa Ulimwengu/Universe,amewezaje kutuumba sisi?kwa maana nyingine,mungu hana mamlaka na hii universe,sasa kwanini unamuogopa na kumsujudu wakati nayeye pia anategemea nature?
Kwa mantiki hii,huna tofauti na Vikings waliokua wanaabudu Eclipse,tena bora wao,maana kwa karne hii ya 21 kuabudu kitu ambacho kipo ndani ya uwezo wako wa kukifikia na hata kukitawala ni utumwa mkubwa sasa,,Religion people mnafurahisha sana,alafu sasa hamna utofauti,hampo logical,kuna wenzio wengine wanaamini kuna jamaa kashikilia dunia kwenye mkono wake,kuna wengine wanaamini kuna lijamaa lipo nje ya Universe linamonitor Universe nzima,nothing you people say makes sense,Hakuna mtu anayemkataza mtu kuamini,tatizo linakuja mnapo jiona mpo very correct na kuchukulia wasio hamini mnacho amini ambacho hakina maana ni wapumbavu na watenda dhambi wakubwa mbele ya huyo mungu wenu,mnatuombea hadi moto :D (actually huo moto mlioundiwa sijui utawashwa wapi :D ),Long story short,siku nyingine usikurupuke kutumia jina la Sayansi kupost vitu visivo na mantiki,abudu ,sujudu , sifu hakuna hataye kuingilia,ila when it comes tu science,Logic first. We care when you use it wrong.
 
H
Kama hakuna anaemjua mungu kwa kutumia akili yake, ninyi mmemjuaje sasa wakati kila mtu anatumia akili yake?
Hakuna anaetumia akili ya simba, konokono, chura, mbwa, fisi nk
hata huko kusoma bible na quraan ni kutumia akili zao.hawajielewi watu wa dini
 
Endeleeni kujifunza msikae kusikiliza ngonjera za kisiasa mshindwe mambo mengine yakujua Dunia yenu na Ulimwengu kwa ujumla.
 
H
hata huko kusoma bible na quraan ni kutumia akili zao.hawajielewi watu wa dini
Tatizo lililopo kwenye dini hofu tupu watu hawatumii akili wanatishwa na kuamini Mungu ni kitu cha kutisha si kweli Mungu ni mwenye huruma ndio maana ametuumba na MEMA NA DHAMBI VYOTE VYATOKA KWAKE NDIYE ALIYE FANYA VIWEPO.
 
(Yohana 5:28, 29
Msistaajabie jambo hili, kwa sababu saa inakuja ambayo wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho+ wataisikia sauti yake.............

Yaja siku ambayo kila mtu atabashiri na kusema njooni mungu yupo uku
 
Kuanzia 1999 mpaka sasa zaidi ya miaka 16 nimekuwa nikifanya utafiti wapi yalipo makazi ya Mwenyezi Mungu Kisayansi na Kutumia Vitabu vitakatifu hasahasa Biblia Takatifu nimepata majibu pasina shaka kila mumoja wetu atakubaliana nayo.
Utafiti huu haulengi kumchafua mtu mtu yeyote kwa imani yake naomba atakayeshindwa kuelewa asiwe na jaziba maana ni utafiti wangu binafsi.
KISAYANSI; Mpangilio na Usanifu wa muundo wa Ulimwengu wetu ni mpangilio uliofanywa kwa usahihi ndio maana kila kitu kipo katika sehemu yake bila kuathiri kingine kwa mfano; Dunia na Sayari zote katika mfumo wa Jua letu zinalizunguka Jua kwa kasi lakini haziwezi kugongana Na katika Anga yetu kuna Nyota mamilioni na pia Kuna Majua Mengine yametengeneza mifumo mifumo ya Sayari kama tuliyo nayo katika Jua letu, Vitu hivi vinaonekana kwa mbali na haviwezi kufikika kwa urahisi kwa akili za Kibinadamu.
Nina hakika Mwenyezi Mungu anaishi katika mojawapo ya Nyota za Jua kwa kuwa hakuwezi kufikika kwakua kuna joto {moto} kali sana hakuna chochote kinaweza kukaribia hata kwa kilometa milioni moja.
Nina dharula nitaendelea Baadae..............................
Katika Jua ndimo kulimo uhai Jua ndicho kitu ambacho hakiwezi kusogelewa wala kuchunguzwa na kitu chochote hata kama utatumia kiona mbali utaishia kuvaa miwani ya kuzuia mwanga ili macho yako yasipofuke kwa miale mikali ya Mwanga wa jua.
Hata Uhai wa viumbe wote hai hutegemea Jua ndiyo maana katika Bara Antaktika uwezekano wa viumbe hai kuishi ni mdogo kwa sababu hupata kiasi kidogo cha jua katika msimu wa mzunguko wa Dunia Ni aina Flani ya Bakteria huweza kuishi katika eneo hilo na Samaki wanaositahimili baridi kari INAYOPELEKEA MAJI KUGANDA NA KUWA BARAFU, NA ENEO LOTE LA BARA ANTAKTIKA NI BARAFU NA MVUA INAYONYESHA NI KWA MARA MOJA KATIKA msimu wa Mwaka.
Jua haliwezi kukalibiwa na kitu chochote kwa maana hiyo Jua linatunza Nafsi Takatifu iliyo hai hakuna chochote chenye mwili au Kitu kinacho weza kusogelea jua kikawa salama kitaungua na kunasa katika Jua.
JUA ndio kitu Kitukufu ambacho mwanadamu kwa uelewa wake hawezi kufikia wala kujaribu kufanyia utafiti.
Katika utafiti wangu nimejifunza kwa kuwa Jua ndilo lina Uhai kwa Viumbe basi kuna uwezekana mkubwa wa 94.6% Muumba anaishi katika Jua Sehemu Tukufu isiyoweza kusogelewa na uchafu wa aina yoyote ya mwanadam.


BIBLIA TAKATIFU (UTAFITI)
Katika vitabu Agano la kale Mwenyezi Mungu anatolewa Sadaka za kuteketezwa, Wanafukiza ubani katika sehemu walizojenga Nyumba za Ibada kwaajiri ya MWENYEZI MUNGU.
Kwanini aunguziwe vitu apokee sadaka kwa moshi?
Kwanini asipewe ng'ombe au Kondoo mzima mpaka achomwe aunguzwe? Ni kwasababu Nafsi ya Mungu inaishi katika moto na Inapokea katika moto.
Kwanini makanisa Mengi yanachoma Ubani katika Nyumba zao za Ibada, Kwanini wasitengeneze Marashi yenye harufu ya Ubani?
Wanachoma kwa kuwa mlengwa Mtukufu anapokea Vitukufu katika moto mjue ya kuwa kila kitu kikichomwa kinatoka katika hali hali nzuri au mbaya hata Dhahabu ili Ing'ae ni lazima ichomwe katika moto.
Kutoka 19: 16-20
Inaelezea jinsi musa anapewa Amri 10 na Mungu na Mwenyezi Mungu anamwambia Musa watu wajitakase kabla ya kukalibia mlima na Mawinguni Kunatokea Radi, Ngurumo na Umeme na Mungu anashuka katika moto na kumpa amri Musa Mlima Sinai unatetemeka kwa utisho Unafuka moshi mkali kama moshi wa tanuu unafunika Mlima wote.
Kwanini Mungu atokee katika moto?
Nikwasababu anataka watu wajue Nafsi Tukufu ya Mungu inaishi katika Moto ANAKUJA KWA STAILI YA MAISHA YAKE KWA MAZINGIRA ANAYO ISHI LAKINI WANADAMU WANASHINDWA KULIJUA HILO.
KAMA MUNGU ANALETA AMRI 10 KWA STAILI YA MOTO BASI YEYE ANAISHI KATIKA MOTO KWA HIYO UTUKUFU WA MUNGU HATUWEZI KUUFIKIA BILA MWILI KUFA IKABAKI NAFSI.
Kwa hiyo KIFO NI FAIDA NA NDIO STAREHE YA PEKEE ALIYOTUZAWADIA MWENYEZI MUNGU KWA KUWA TUTAISHI KATIKA UTUKUFU KAMA NAFSI ILIYO KARIBU NA MUNGU BILA KUFA WEWE NI MTUMWA WA DUNIA.
Uwe TAJIRI, uwe MASIKINI wewe ni MTUMWA wa DUNIA hakuna RAHA UTAKULA KWA JASHO, UTALALA KWA KUJIGEUZA GEUZA USIUMIZE UPANDE MMOJA WA MWILI,
Duniani hapa tupo kwa ajili ya kuandaa Maisha ya Utukufu wa milele kama nafsi Katika Jua.
Utafiti wangu unaendelea kadiri Mungu atakavyonijalia ntawaletea ninayoendelea kujifunza Pia ninajitahidi kutafuta njia ya Kitaalamu ya kuweka Video katika kiona mbali ili niweze kuwashirikisha kwa yale ambayo mimi naendelea kuyavumbua kwa kutumia kiona mbali Ninazunguka sehemu mbali mbali kujifunza jinsi Dunia yetu ilivyo na ni kazi ngumu ila ninapata michango ya mawazo kwa watu wengi sana ambao ninawashirikisha sehemu mbalimbali za Dunia.
KARIBUNI KWA MAONI NA USHAURI
"Huitaji nguvu nyingi kupambana na hawa wabishi.. wakitafakar watakuelewa, na wakikuelewa watachukia"
 
Mtu anafanya utafiti wa kisayansi kwa kutumia biblia, seriously?

Hilarious.
 
Mtu anafanya utafiti wa kisayansi kwa kutumia biblia, seriously?

Hilarious.

inamaana biblia haiwezi kuwa rejeo la utafiti wa kisayansi? ivi wakat wakina thomas malthus na charles dwarin walipotoa ripoti yenye dhana iitwayo "Nature selection" miaka ile ya 1770s inamaana wao hawakusoma kabisa biblia kujua imeelezea nini juu ya uhai kama marejeo yao?
 
inamaana biblia haiwezi rejeo la utafiti wa kisayansi? ivi wakat wakina thomas malthus na charles dwarin walipotoa ripoti ya yenye dhana iitwayo "Nature selection" miaka ile ya 1870s inamaana wao hawakusoma kabisa biblia kujua imeelezea nini juu ya uhai kama marejeo yao?
Hawakusoma kabisa biblia maana yake nini?

Watu wamesoma biblia na wamenda kufanya research ya quantum physics.

Utasema wamefanya research ya quantum physics kwa kutumia biblia?

Biblia ina makosa na contradictions kibao, ni kitabu cha Imani, sayansi haitaki Imani, inataka ujuzi, utasemaje biblia inaweza kuwa kitabu cha kisayansi?
 
Hawakusoma kabisa biblia maana yake nini?

Watu wamesoma biblia na wamenda kufanya research ya quantum physics.

Utasema wamefanya research ya quantum physics kwa kutumia biblia?

Biblia ina makosa na contradictions kibao, ni kitabu cha Imani, sayansi haitaki Imani, inataka ujuzi, utasemaje biblia inaweza kuwa kitabu cha kisayansi?

Duh, we mshkaji noma kweli....unajipu la kiimani.Kifup siwez kuendelea kubishana na wewe usiye na imani wala hakuna chochote unachokiamini ktk maisha ya ulimwengu,upo upo tu kana kwamba weye ndiye super natural being.
 
Tatizo lililopo kwenye dini hofu tupu watu hawatumii akili wanatishwa na kuamini Mungu ni kitu cha kutisha si kweli Mungu ni mwenye huruma ndio maana ametuumba na MEMA NA DHAMBI VYOTE VYATOKA KWAKE NDIYE ALIYE FANYA VIWEPO.
Kweli tupu bro. Religion is the box people fail to think out of.. Mungu hapaswi kuogopwa kama ambavyo dini inaelekeza
 
Unaposema viumbe huishi kwa kutegemea jua tu hapa napata tabu kuelewa kidogo.

Je mvua hayana nafasi ktk hayo ya mwanadamu? Kama ni hvyo basi hata jangwani kungekuwa na makazi mengi sana ya wanadamu kwakuwa uhai wa viumbe unatokana na jua pekee!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom