Ukweli wa uwepo wa Mungu na Makazi yake upo hapa

impongo

JF-Expert Member
Feb 18, 2015
8,732
7,611
Kuanzia 1999 mpaka sasa zaidi ya miaka 16 nimekuwa nikifanya utafiti wapi yalipo makazi ya Mwenyezi Mungu Kisayansi na Kutumia Vitabu vitakatifu hasahasa Biblia Takatifu nimepata majibu pasina shaka kila mumoja wetu atakubaliana nayo.

Utafiti huu haulengi kumchafua mtu mtu yeyote kwa imani yake naomba atakayeshindwa kuelewa asiwe na jaziba maana ni utafiti wangu binafsi.

KISAYANSI; Mpangilio na Usanifu wa muundo wa Ulimwengu wetu ni mpangilio uliofanywa kwa usahihi ndio maana kila kitu kipo katika sehemu yake bila kuathiri kingine kwa mfano; Dunia na Sayari zote katika mfumo wa Jua letu zinalizunguka Jua kwa kasi lakini haziwezi kugongana Na katika Anga yetu kuna Nyota mamilioni na pia Kuna Majua Mengine yametengeneza mifumo mifumo ya Sayari kama tuliyo nayo katika Jua letu, Vitu hivi vinaonekana kwa mbali na haviwezi kufikika kwa urahisi kwa akili za Kibinadamu.

Nina hakika Mwenyezi Mungu anaishi katika mojawapo ya Nyota za Jua kwa kuwa hakuwezi kufikika kwakua kuna joto {moto} kali sana hakuna chochote kinaweza kukaribia hata kwa kilometa milioni moja.

Katika Jua ndimo kulimo uhai Jua ndicho kitu ambacho hakiwezi kusogelewa wala kuchunguzwa na kitu chochote hata kama utatumia kiona mbali utaishia kuvaa miwani ya kuzuia mwanga ili macho yako yasipofuke kwa miale mikali ya Mwanga wa jua.

Hata Uhai wa viumbe wote hai hutegemea Jua ndiyo maana katika Bara Antaktika uwezekano wa viumbe hai kuishi ni mdogo kwa sababu hupata kiasi kidogo cha jua katika msimu wa mzunguko wa Dunia Ni aina Flani ya Bakteria huweza kuishi katika eneo hilo na Samaki wanaositahimili baridi kari INAYOPELEKEA MAJI KUGANDA NA KUWA BARAFU, NA ENEO LOTE LA BARA ANTAKTIKA NI BARAFU NA MVUA INAYONYESHA NI KWA MARA MOJA KATIKA msimu wa Mwaka.

Jua haliwezi kukalibiwa na kitu chochote kwa maana hiyo Jua linatunza Nafsi Takatifu iliyo hai hakuna chochote chenye mwili au Kitu kinacho weza kusogelea jua kikawa salama kitaungua na kunasa katika Jua.

JUA ndio kitu Kitukufu ambacho mwanadamu kwa uelewa wake hawezi kufikia wala kujaribu kufanyia utafiti.

Katika utafiti wangu nimejifunza kwa kuwa Jua ndilo lina Uhai kwa Viumbe basi kuna uwezekana mkubwa wa 94.6% Muumba anaishi katika Jua Sehemu Tukufu isiyoweza kusogelewa na uchafu wa aina yoyote ya mwanadam.

BIBLIA TAKATIFU (UTAFITI)

Katika vitabu Agano la kale Mwenyezi Mungu anatolewa Sadaka za kuteketezwa, Wanafukiza ubani katika sehemu walizojenga Nyumba za Ibada kwaajiri ya MWENYEZI MUNGU.

Kwanini aunguziwe vitu apokee sadaka kwa moshi?

Kwanini asipewe ng'ombe au Kondoo mzima mpaka achomwe aunguzwe? Ni kwasababu Nafsi ya Mungu inaishi katika moto na Inapokea katika moto.

Kwanini makanisa Mengi yanachoma Ubani katika Nyumba zao za Ibada, Kwanini wasitengeneze Marashi yenye harufu ya Ubani?

Wanachoma kwa kuwa mlengwa Mtukufu anapokea Vitukufu katika moto mjue ya kuwa kila kitu kikichomwa kinatoka katika hali hali nzuri au mbaya hata Dhahabu ili Ing'ae ni lazima ichomwe katika moto.

Kutoka 19: 16-20 Inaelezea jinsi musa anapewa Amri 10 na Mungu na Mwenyezi Mungu anamwambia Musa watu wajitakase kabla ya kukalibia mlima na Mawinguni Kunatokea Radi, Ngurumo na Umeme na Mungu anashuka katika moto na kumpa amri Musa Mlima Sinai unatetemeka kwa utisho Unafuka moshi mkali kama moshi wa tanuu unafunika Mlima wote.

Kwanini Mungu atokee katika moto?

Ni kwa sababu anataka watu wajue Nafsi Tukufu ya Mungu inaishi katika Moto ANAKUJA KWA STAILI YA MAISHA YAKE KWA MAZINGIRA ANAYO ISHI LAKINI WANADAMU WANASHINDWA KULIJUA HILO.

KAMA MUNGU ANALETA AMRI 10 KWA STAILI YA MOTO BASI YEYE ANAISHI KATIKA MOTO KWA HIYO UTUKUFU WA MUNGU HATUWEZI KUUFIKIA BILA MWILI KUFA IKABAKI NAFSI.

Kwa hiyo KIFO NI FAIDA NA NDIO STAREHE YA PEKEE ALIYOTUZAWADIA MWENYEZI MUNGU KWA KUWA TUTAISHI KATIKA UTUKUFU KAMA NAFSI ILIYO KARIBU NA MUNGU BILA KUFA WEWE NI MTUMWA WA DUNIA.
Uwe TAJIRI, uwe MASIKINI wewe ni MTUMWA wa DUNIA hakuna RAHA UTAKULA KWA JASHO, UTALALA KWA KUJIGEUZA GEUZA USIUMIZE UPANDE MMOJA WA MWILI,

Duniani hapa tupo kwa ajili ya kuandaa Maisha ya Utukufu wa milele kama nafsi Katika Jua.

Utafiti wangu unaendelea kadiri Mungu atakavyonijalia ntawaletea ninayoendelea kujifunza Pia ninajitahidi kutafuta njia ya Kitaalamu ya kuweka Video katika kiona mbali ili niweze kuwashirikisha kwa yale ambayo mimi naendelea kuyavumbua kwa kutumia kiona mbali Ninazunguka sehemu mbali mbali kujifunza jinsi Dunia yetu ilivyo na ni kazi ngumu ila ninapata michango ya mawazo kwa watu wengi sana ambao ninawashirikisha sehemu mbalimbali za Dunia.

KARIBUNI KWA MAONI NA USHAURI..
 
Aisee Hi hatari!

Unawezaje kutumia miaka 16 tu kukamilisha Extraordinary research kama hiyo?

NASA wana taarifa yako?

Scientific research ndiyo,Methodology ipi uliyotumia?

Kifaa kipi ulichotumia kuchunguza hiyo nyota?Hubble space telescope?

"Nina hakika mwenyezi Mungu anaishi katika mojawapo ya Nyota za Jua"

'Nyota za Jua' ndiyo kitu gani kaka yangu?

Mkuu,Mungu hachunguziki.
 
B
Kwa sababu ni tafiti kisayansi Kama ulivyodai tunaomba methodology uliyotumia kufikia hilo hitimisho lako pia bila kusahau proofs.[/QUOT Naendelea kuleta nilichojifunza kuhusu mungu bado mada ni ndefu kila ntapopata muda ntajitahidi kuelezea kwa kina Kisayansi na Kimungu
 
Aisee Hi hatari!

Unawezaje kutumia miaka 16 tu kukamilisha Extraordinary research kama hiyo?

NASA wana taarifa yako?

Scientific research ndiyo,Methodology ipi uliyotumia?

Kifaa kipi ulichotumia kuchunguza hiyo nyota?Hubble space telescope?

"Nina hakika mwenyezi Mungu anaishi katika mojawapo ya Nyota za Jua"

'Nyota za Jua' ndiyo kitu gani kaka yangu?

Mkuu,Mungu hachunguziki.
Mkuu Mungu ametupa akili inamaana tumjue tumchunguze bila hivo tungekuwa mbuzi na ng'ombe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom