Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Kumtaka Rais kutoka CCM aingilie swala la wizi na uporaji wa mali za wananchi uliofanywa na CCM, chama ambacho hakioni aibu kumiliki mali hizo, ni ndoto za Alnacha.
Rais ni zao la chama hicho na anaingia madarakani baada ya kuwaridhisha waporaji wenzake ndani ya chama hicho kuwa atalinda na kutetea hizo sera za uporaji na dhulma.
CCM imejengwa kwenye misingi ya dhulma na ndio maana nguvu kubwa mno hutumika kuhakikisha Katiba itakayolinda uhuru wetu, haki na usawa katu haipatikani.
Kwa sababu hizo CCM haioni aibu kutumia mihimili ya dola na vyombo vya dola kung'ang'ania madaraka kwani inaamini hivyo ni vyombo vyake halali na ina haki kuvitumia.
Ndugu zangu tuache utani na tuukabili ukweli hata kama unauma kiasi gani, CCM haimiliki viwanja tu na serikali, CCM kwa sasa inatumiliki sisi wananchi, uhai wetu na mali zetu.
CCM ndio pekee inaamua wananchi tuishi vipi na wapi ndani ya taifa letu, tumiliki nini na tuseme nini kwa wakati gani. CCM imepora ardhi yote Tanzania na vyote vilivyoko chini na juu yake.
Nashangaa watu wanahoji viwanja kuporwa na CCM, je yaliyokuwa Majengo ya umma? Mashirika ya umma? Taasisi za umma? Magari ya umma? CCM ndiyo SMB (Serikali, Mahakama na Bunge)
La kusikitisha ni kwamba wale walioporwa mali zao, uhuru wao na haki zao wote kwa pamoja wanaonekana kuridhika na hali hiyo na kwa pamoja wimbo unaotesa hivi sasa ni kazi iendelee!
KIla baada ya miaka mitano au kumi, mamlaka yanaporwa na watu wale wale, chama kile kile, akili zile zile, uongo ule ule ila vinavyobadilika ni sura, rangi, kanda, dini na inapolazimu jinsia. Inasikitisha!
Ndugu zangu adui wa taifa letu si mwingine bali CCM. Nawatakia Jumanne njema.
Rais ni zao la chama hicho na anaingia madarakani baada ya kuwaridhisha waporaji wenzake ndani ya chama hicho kuwa atalinda na kutetea hizo sera za uporaji na dhulma.
CCM imejengwa kwenye misingi ya dhulma na ndio maana nguvu kubwa mno hutumika kuhakikisha Katiba itakayolinda uhuru wetu, haki na usawa katu haipatikani.
Kwa sababu hizo CCM haioni aibu kutumia mihimili ya dola na vyombo vya dola kung'ang'ania madaraka kwani inaamini hivyo ni vyombo vyake halali na ina haki kuvitumia.
Ndugu zangu tuache utani na tuukabili ukweli hata kama unauma kiasi gani, CCM haimiliki viwanja tu na serikali, CCM kwa sasa inatumiliki sisi wananchi, uhai wetu na mali zetu.
CCM ndio pekee inaamua wananchi tuishi vipi na wapi ndani ya taifa letu, tumiliki nini na tuseme nini kwa wakati gani. CCM imepora ardhi yote Tanzania na vyote vilivyoko chini na juu yake.
Nashangaa watu wanahoji viwanja kuporwa na CCM, je yaliyokuwa Majengo ya umma? Mashirika ya umma? Taasisi za umma? Magari ya umma? CCM ndiyo SMB (Serikali, Mahakama na Bunge)
La kusikitisha ni kwamba wale walioporwa mali zao, uhuru wao na haki zao wote kwa pamoja wanaonekana kuridhika na hali hiyo na kwa pamoja wimbo unaotesa hivi sasa ni kazi iendelee!
KIla baada ya miaka mitano au kumi, mamlaka yanaporwa na watu wale wale, chama kile kile, akili zile zile, uongo ule ule ila vinavyobadilika ni sura, rangi, kanda, dini na inapolazimu jinsia. Inasikitisha!
Ndugu zangu adui wa taifa letu si mwingine bali CCM. Nawatakia Jumanne njema.