Ukweli Kuhusu CHADEMA na Harakati Zake

Wazee wangu nchi hii tuna kila kitu isipokuwa tunachokosa ni kimoja tu uongozi bora na siasa safi.Tatizo hapa ni watawala ambao bila shaka ni ccm.Watawala hawa kwa miaka 50 wamekosa dira ya kuingoza nchi hii kuelekea kufaidi neema tuliyojaliwa na Mwenyezi Mungu.Wamekuwa ni wabinafsi, wamekosa uadilifu,sio wazalendo,wamekosa pia akili na uelewa wa masuala ya uchumi na hivyo kuachia raslimali za nchi hii kuchukuliwa na wageni bila huruma huku wao wakipewa kitu kidogo sana kwa ajili yao na famiilia zao.Tuache masihara ya kiitikadi ktk masuala nyeti kama haya.Ndugu zangu angalieni mfano wa vinchi vidogo kama Mauritius hawana rasilimali yeyote ni kisiwa kidogo ktk bahari ya Hindi,wanategemea utalii na kilimo cha miwa pekee,angalia walivyopiga hatua.Wana uchumi mzuri,ni mojawapo ya nchi pekee nne Africa zenye uchumi mzuri sana zingine ni Botswana,Gabon na Africa ya Kusini wana literacy rate 85% na ni moja ya nchi zenye utawala bora na democracy nzuri,wamewahi kupata nishani ya Ibrahim kuhusu utawala bora.Sasa sisi tuna tatizo gani hadi tuwe masikini kiasi hiki licha ya rasilimali lukuki na ardhi nzuri tuliyo nayo.
Tujiulize wananchi tunahitaji kuchukua hatua,na hatua nzuri kwa sasa ni kubadilisha uongozi wa nchi kabisa tuwaone na wengine watafanya nini badala ya kutegemea walewale ambao wametuangusha kwa muda wote huo.Mbona nchi za wenzetu hubadilisha utawala mara kwa mara na wanaendelea mbele,sisi tunaogopa nini?Ni wakati muafaka wa kubadilisha watawala kwani hata wengine wakifanya vibaya si tutawaondoa tu shaka ya nini?

Mabadiliko ya uongozi wa nchi yatafanywa na Watanzania kidemokrasia watakapoona kuna haja ya kufanya hivyo na muhimu zaidi watakapoona kuna chama kinachoweza kuaminika kukabidhiwa dola.

Kwa sasa hakuna chama makini cha upinzani kinachoweza kuaminika na kupewa ridhaa hiyo. Waliopo ni wanaharakati tu.
 
huwi mpumbavu kwa kuitwa,ni sifa uliyonayo,hata usipoitwa utabaki hivyo!

Matusi ndo yaliyojaza kichwa chako na unaonekana una uwezo mzuri wa kuyajengea hoja.
Unaonekana umejaa najisi na unataka kuliambukiza jamvi hili uozo wako.

Umeshashindwa, kama huna hoja kaa kimya.
 
Nchi kama botswana zilizopiga hatua kubwa kwa ajili ya madin hazikufanya hivyo kimiujiza,ni umakini wa serikali na uongozi bora.that's what our leaders lack,still they dont want 2 admit.
 
Wana-JF, napenda kuwashirikisha alichosema Mzee Peter Kisumo kuhusu CHADEMA:

‘Tatizo kubwa kwenye Chadema kuna wanaharakati na si wanasiasa, na haiwezekani kuongoza serikali kwa kuwa na viongozi wanaharakati'.

"Hawa Chadema wanachokifanya ni kuvizia makosa madogo madogo ya serikali na kisha kuwashawishi wananchi wawe upande wao,".

"Wapo viongozi wa Chadema na waasisi, kama Mzee Edwin Mtei na watu wengine makini ninaowafahamu ndani ya chama hicho, sijawahi kuwasikia wakiropoka hovyo kama wanavyofanya baadhi ya viongozi wa chama hicho."

'Ikiwa hulka hiyo itandelea, kuna hatari ya kukosa sifa ya kushika dola vinginevyo watapata shida, kwani hakuna serikali inayoweza kwenda kwa kuendeshwa na wanaharakati'.

'Inatakiwa chama ambacho kitashinda kiwe na uwezo wa kuongoza katika hali ya amani na utulivu na si kuingia kwenye machafuko mara baada ya uchaguzi'.

'Ili Chadema ishike dola, ni lazima wajitahidi kujenga safu ya uongozi wa kutawala na si kuwa na viongozi ambao kila wakati wanahamasisha watu kuandamana, kugoma na kuvizia makosa ya serikali iliyopo madarakani'.

'Wanachokifanya Chadema ni sawa na wawindaji wanaokoka moto kwa ajili ya kuchoma nyama ili hali nyama yenyewe hawajaipata, ..... kazi ya kuing'oa CCM si rahisi kama inavyofikirika'.


CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

Mkuu umesema kweli ila hawa washabiki wa CHADEMA wamekuwa vipofu hata hawataki kufukiria japo kidogo. Je CHADEMA ni kipi wanachofanya? Zaidi ya kulalamika kila wakati na kuwadanganya wananchi hukuwakiwajaza jazba ambayo matokeo yake ni machafuko.
 
Mzee Peter Kisumo alitaka kuzungumza jambo jema ila hakujua amueleze nani,

Kwanza ni vema angeenza kueleza maana ya Mwanasiasa na Mwanaharakati,

Pili angeeleza dhumuni la vyama vingi? au dhumuni la kuwepo kwa chama cha siasa mbadala au kuweo kwa vyama pinzani,

Kwa kifupi kwa kipengele cha pili, vyama vya upinzani vipo ili viikosea serikali pili inapotenda mabaya, wananchi watajua kuwa serikali yao imewaacha kupitia vyama vya upinzania, Vipi ili vionyeshe uwezo wao wa kuweza kuiongoza nchi kwa kuwa na katiba zao zilizo bora, mipango bora na endelevu ya maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla, mikakati ya kuwawezesha wananchi kujua Uraia wao,

Vyama vya upinzani vipo ili kuwasaidia wanachi kuweza kujua umuhimu wa rasilimali za nchi, zinaweza kutumikaje kimaendeleo, zinaibiwa na nani na vipi zinaibiwa, nini kifanyike ili wao wananchi wafaidike,

Chadema kwa sasa wanastahili pongezi, wameweza kuikosoa serikali kwa asilimia mia, wameweza kuwa na katiba yao nzuri, mipango yao inaonyesha ni endelevu, inarekebishika, wana think tank kubwa kuliko wenzao waliopo madarakani, wameweza kuwaita serikali mafisadi na kutuhakikishia hivyo...

Mzee Kisumo ni mtu wa Zamani ni vema akashauri yaliyo ya kweli mana nchi hii si ya CCM, yeye atapita na wengine na mimi pia lakini Tanzania hii itakuwepo tuuu hvyo hapa tunataka uhuni wa kula nchi uishe, ufe, tuwanyonge hawa wahujumu uchumi,
 
Mkuu umesema kweli ila hawa washabiki wa CHADEMA wamekuwa vipofu hata hawataki kufukiria japo kidogo. Je CHADEMA ni kipi wanachofanya? Zaidi ya kulalamika kila wakati na kuwadanganya wananchi hukuwakiwajaza jazba ambayo matokeo yake ni machafuko.

Achana na wanungunikaji wa kisiasa. Kiama chao ni kwenye sanduku la kura 2015, hapo ndo watajua kuwa Watz walio wengi wanajua kutofautisha vyama-pumba na vyama makini.
 
Ninaamini tunaweza kujadili bila ya kuitana wapumbavu.

Acha mkate uitwe mkate na kinyesi kiitwe kinyesi ili mataahira ambao nao ni sehemu ja jamii watofaitishe wasijekula kinyesi wenye akili timamu wakalaumiwa.
 
CCM wanashikwa na kiwewe, chama chao kinaelekea kufa. Wanaiogopa sana chadema kwani hawatapona cdm ikishika dola. Hawana nia yeyote njema kwa nchi hii bali uoga wa nafisi zao. Ukiwauliza tofuti ya siasa na uwanaharakati kwa chama cha upinzani watashindwa kueleza. Kwani lazima chadema wafanye siasa kama wao ccm? Kivipi ccm wanaweza kuelezea demokrasia? Kama wanachofanya chadema ni harakati naomba waendelee hivyo hivyo, ndo tunachotaka sis wananchi. Bora wao kuliko ccm na siasa za ufisadi. Inakera sana.
 
Haya maneno hayawezi kueleweka kwa hawa vijana wa cdm wasiojua siasa. Ukweli ndio huo, chadema ni wanaharakati na si wanasiasa.
Kwa hiyo wanasiasa ni akina nani, Lusinde, Nape au wassira???
 
Ilianza ukabila, ikaja udini, ukaja ukanda, hatimae harakati nayo ikawa kigezo!! Kwamba CDM ni chama cha harakati?? Vp udini, ukabila na ukanda vimekosa mshiko na sasa ni harakati?? Najuta kusoma ulichoandika!!
 
Wana-JF, napenda kuwashirikisha alichosema Mzee Peter Kisumo kuhusu CHADEMA:

‘Tatizo kubwa kwenye Chadema kuna wanaharakati na si wanasiasa, na haiwezekani kuongoza serikali kwa kuwa na viongozi wanaharakati’.

“Hawa Chadema wanachokifanya ni kuvizia makosa madogo madogo ya serikali na kisha kuwashawishi wananchi wawe upande wao,”.

“Wapo viongozi wa Chadema na waasisi, kama Mzee Edwin Mtei na watu wengine makini ninaowafahamu ndani ya chama hicho, sijawahi kuwasikia wakiropoka hovyo kama wanavyofanya baadhi ya viongozi wa chama hicho.”

'Ikiwa hulka hiyo itandelea, kuna hatari ya kukosa sifa ya kushika dola vinginevyo watapata shida, kwani hakuna serikali inayoweza kwenda kwa kuendeshwa na wanaharakati'.

'Inatakiwa chama ambacho kitashinda kiwe na uwezo wa kuongoza katika hali ya amani na utulivu na si kuingia kwenye machafuko mara baada ya uchaguzi'.

'Ili Chadema ishike dola, ni lazima wajitahidi kujenga safu ya uongozi wa kutawala na si kuwa na viongozi ambao kila wakati wanahamasisha watu kuandamana, kugoma na kuvizia makosa ya serikali iliyopo madarakani'.

'Wanachokifanya Chadema ni sawa na wawindaji wanaokoka moto kwa ajili ya kuchoma nyama ili hali nyama yenyewe hawajaipata, ..... kazi ya kuing’oa CCM si rahisi kama inavyofikirika'.


CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

Tatizo kubwa watu hawajui maana ya siasa ya vyama vingi na maana ya upinzani. Kwani mbona CHADEMA wakikosea CCM ndiyo wanachonga sana. Mzee Kisumo ajue kuwa Kosa la CCM ni mtaji wa CDM na kosa la CDM ni mtaji wa CCM. Namshauri ajifunze kwanza maana ya siasa ya vyama vingi ndipo aongee.
 
Peter Kisumo amesema maneno mazito. Wapenzi wa CDM mnamrukia bure ma kumtukana. Yeye amewashauri vizuri sana na hajasema kwamba CDM isiingie ikulu ama kushika dola ila amesema ili ushike dola na kutawala vyema CDM inatakiwa ifanye mambo kadhaa. Sasa kwa kuwa CDM wamekodolea macho Ikulu basi hawasikiii la mwadhini wala mnadi swala. Sikilizeni ushauri na kuufanyia kazi badala ya kuleta matusi.
 
Kwani Peter Kisumo ni nani? Yeye ni Malaika? aache zake hizo... Hizi ndizo zile Nguzo za CCM zilizo gizani kama kina shibuda.

Walikuwa wanasema Sugu Mwana Mziki atakuwaje Mbunge eti kwa sababu tu yuko CDM wanamsahau Komba...

Hawa ni wanafiki,,, CDM ikiingia madarakani itakuwa ni opportunity Nzuri kwa vijana maana hawa wazee inabidi wawe phased out kutokana na maneno yao na matendo yao.
 
Ninaamini tunaweza kujadili bila ya kuitana wapumbavu.
Kama mtu anasifa zote za upumbavu tumuiteje?Kama mzee anadhani chama cha upinzani kipo kukipamba chama tawala kinaposhindwa kuimarisha serikali yake na kuanza kulialia mzee huyo tumuiteje? Kama serikali ina subiri fedha za wanywa pombe na wavuta sigara huku madini yake yakichukuliwa kuwa neemesha wageni tuiiteje?
 
Mabadiliko ya uongozi wa nchi yatafanywa na Watanzania kidemokrasia watakapoona kuna haja ya kufanya hivyo na muhimu zaidi watakapoona kuna chama kinachoweza kuaminika kukabidhiwa dola.

Kwa sasa hakuna chama makini cha upinzani kinachoweza kuaminika na kupewa ridhaa hiyo. Waliopo ni wanaharakati tu.
Sasa kwa kauri kama hii ukiitwa mpumbavu utakasirika? Nenda kamuulize msajiri wa vyama akufafanulie swala hili. La si hivyo wewe na huyu kibabu wako wote ni wapumbavu wachumia tumbo!
 
Kwa hiyo anaona chama chenye siasa za wizi ni bora kuliko wanaharakati? Anazeeka vibaya na anajitia aibu kwa ubinafsi!
 
Itabidi tutafiti na shule ya huyo mzee, alidanganywa na siasa za chama kimoja, hajui malengo ya chama pinzani!
 
Back
Top Bottom