Ukweli Kuhusu CHADEMA na Harakati Zake

Ngoromiko

JF-Expert Member
Sep 15, 2011
554
175
Wana-JF, napenda kuwashirikisha alichosema Mzee Peter Kisumo kuhusu CHADEMA:

‘Tatizo kubwa kwenye Chadema kuna wanaharakati na si wanasiasa, na haiwezekani kuongoza serikali kwa kuwa na viongozi wanaharakati’.

“Hawa Chadema wanachokifanya ni kuvizia makosa madogo madogo ya serikali na kisha kuwashawishi wananchi wawe upande wao,”.

“Wapo viongozi wa Chadema na waasisi, kama Mzee Edwin Mtei na watu wengine makini ninaowafahamu ndani ya chama hicho, sijawahi kuwasikia wakiropoka hovyo kama wanavyofanya baadhi ya viongozi wa chama hicho.”

'Ikiwa hulka hiyo itandelea, kuna hatari ya kukosa sifa ya kushika dola vinginevyo watapata shida, kwani hakuna serikali inayoweza kwenda kwa kuendeshwa na wanaharakati'.

'Inatakiwa chama ambacho kitashinda kiwe na uwezo wa kuongoza katika hali ya amani na utulivu na si kuingia kwenye machafuko mara baada ya uchaguzi'.

'Ili Chadema ishike dola, ni lazima wajitahidi kujenga safu ya uongozi wa kutawala na si kuwa na viongozi ambao kila wakati wanahamasisha watu kuandamana, kugoma na kuvizia makosa ya serikali iliyopo madarakani'.

'Wanachokifanya Chadema ni sawa na wawindaji wanaokoka moto kwa ajili ya kuchoma nyama ili hali nyama yenyewe hawajaipata, ..... kazi ya kuing’oa CCM si rahisi kama inavyofikirika'.


CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
 
Yaani CCM mmejaa watu wapuuzi sijawahi kuona mzee mtei ndiyo msemaji wa chama, hivi chama gani kati ya CCM na chadema kina cho ropoka hovyo, hivi wewe maswala kama ya richmond ni madogo kwako..ina ele kea hajuai kazi ya chama cha siasa kuwa ni kuikosoa lakini namsikitikia kwa kuwa anaita ni maswala madogo madogo wakati sisi wananchi tunayaona ni matatizo makubwa mfano mfumuko wa bei, serikali imeshindwa kuuzuia waziri mkuu anatangaza bei ya sukali isiuzwe zaidi ya 1700 wafanya biashara wana uza zaidi ya 2200 harafu unaita matatizo madomado... hebu tuwekee matati makubwa kwako wewe...........
 
Ni mtanzania yupi mwenye akili timamu anayeweza kushawishika na maneno ya kipuuzi ya hawa Mafisadi wa CCM?
 
... hebu tuwekee matati makubwa kwako wewe...........[/QUOTE said:
Matatizo hayako Tz pekee na wala hayasababishwi na chama cha siasa bali mwenendo wa hali ya uchumi duniani.

Hivyo kuilaumu serikali kwa bei ya sukari au petroli si sahihi, mambo mengine ni nje ya uwezo wa serikali yeyote hata kama ingekuwa ya CHADEMA.
 
Wana-JF, napenda kuwashirikisha alichosema Mzee Peter Kisumo kuhusu CHADEMA:

‘Tatizo kubwa kwenye Chadema kuna wanaharakati na si wanasiasa, na haiwezekani kuongoza serikali kwa kuwa na viongozi wanaharakati’.

“Hawa Chadema wanachokifanya ni kuvizia makosa madogo madogo ya serikali na kisha kuwashawishi wananchi wawe upande wao,”.

“Wapo viongozi wa Chadema na waasisi, kama Mzee Edwin Mtei na watu wengine makini ninaowafahamu ndani ya chama hicho, sijawahi kuwasikia wakiropoka hovyo kama wanavyofanya baadhi ya viongozi wa chama hicho.”

'Ikiwa hulka hiyo itandelea, kuna hatari ya kukosa sifa ya kushika dola vinginevyo watapata shida, kwani hakuna serikali inayoweza kwenda kwa kuendeshwa na wanaharakati'.

'Inatakiwa chama ambacho kitashinda kiwe na uwezo wa kuongoza katika hali ya amani na utulivu na si kuingia kwenye machafuko mara baada ya uchaguzi'.

'Ili Chadema ishike dola, ni lazima wajitahidi kujenga safu ya uongozi wa kutawala na si kuwa na viongozi ambao kila wakati wanahamasisha watu kuandamana, kugoma na kuvizia makosa ya serikali iliyopo madarakani'.

'Wanachokifanya Chadema ni sawa na wawindaji wanaokoka moto kwa ajili ya kuchoma nyama ili hali nyama yenyewe hawajaipata, ..... kazi ya kuing’oa CCM si rahisi kama inavyofikirika'.


CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

Itafika mahali hata wapumbavu watanena pamoja na uhuni wao wote.
 
Wazee wengi wa CCM kwao uzee ni ugonjwa na si dawa. Matamshi kama haya yametolewa na Wasira nk. Ukweli ni kuwa uwezi kutenganisha siasa na harakati. Na mwanasiasa bora ni lazima awe mwanaharakati, awe na uwezo wa kupambana kwa mbinu za aina zote.
 
Ni bora wanaharakati wa chadema kuliko MAJIZI,MAUZA MADAWA YA KULEVYA,MAFISADI,WACHAWI NA WAPUMBAVU waliojaa CCM.na harakati ndio tunazotaka sio porojoporojo za kina mbayumbayu na nepi.
 
Matatizo hayako Tz pekee na wala hayasababishwi na chama cha siasa bali mwenendo wa hali ya uchumi duniani.

Hivyo kuilaumu serikali kwa bei ya sukari au petroli si sahihi, mambo mengine ni nje ya uwezo wa serikali yeyote hata kama ingekuwa ya CHADEMA.


Acheni kuwaadaa watanzania nyie wezi wa hii nchi, kazi yenu ni kung'ang'ania kuwa ni hali ya dunia. Hivi mikataba mibovu ya madini inayoipotezea nchi mabilioni ya shilingi ni hali ya dunia? Hivi mikataba mibovu kwenye sekta ya umeme inayoisababishia nchi kulipa mabilioni hewa ni hali ya dunia? Hivi misamaha ya kodi kwa kampuni za madini zinazoinyima nchi mabilioni ya shilingi ni hali ya dunia? Hivi usimamizi mbaya wa fedha za umma na kusababisha watu wachache kuchota pesa kama shamba la bibi ni hali ya dunia? Acheni kuleta siasa maji taka hapa.
 
Matatizo hayako Tz pekee na wala hayasababishwi na chama cha siasa bali mwenendo wa hali ya uchumi duniani.

Hivyo kuilaumu serikali kwa bei ya sukari au petroli si sahihi, mambo mengine ni nje ya uwezo wa serikali yeyote hata kama ingekuwa ya CHADEMA.

We kweli ngoromiko,na Richmond iko dunia nzima ,?epa,kagoda,wizi wa twiga na uchafu mwingine vyote viko dunia nzima? tukae kimya eti kwa sababu na kwingine yapo? kweli huo ndo upeo wako ulipoishia Great Sinker! aibu yangu mimi
 
Wazee wangu nchi hii tuna kila kitu isipokuwa tunachokosa ni kimoja tu uongozi bora na siasa safi.Tatizo hapa ni watawala ambao bila shaka ni ccm.Watawala hawa kwa miaka 50 wamekosa dira ya kuingoza nchi hii kuelekea kufaidi neema tuliyojaliwa na Mwenyezi Mungu.Wamekuwa ni wabinafsi, wamekosa uadilifu,sio wazalendo,wamekosa pia akili na uelewa wa masuala ya uchumi na hivyo kuachia raslimali za nchi hii kuchukuliwa na wageni bila huruma huku wao wakipewa kitu kidogo sana kwa ajili yao na famiilia zao.Tuache masihara ya kiitikadi ktk masuala nyeti kama haya.Ndugu zangu angalieni mfano wa vinchi vidogo kama Mauritius hawana rasilimali yeyote ni kisiwa kidogo ktk bahari ya Hindi,wanategemea utalii na kilimo cha miwa pekee,angalia walivyopiga hatua.Wana uchumi mzuri,ni mojawapo ya nchi pekee nne Africa zenye uchumi mzuri sana zingine ni Botswana,Gabon na Africa ya Kusini wana literacy rate 85% na ni moja ya nchi zenye utawala bora na democracy nzuri,wamewahi kupata nishani ya Ibrahim kuhusu utawala bora.Sasa sisi tuna tatizo gani hadi tuwe masikini kiasi hiki licha ya rasilimali lukuki na ardhi nzuri tuliyo nayo.
Tujiulize wananchi tunahitaji kuchukua hatua,na hatua nzuri kwa sasa ni kubadilisha uongozi wa nchi kabisa tuwaone na wengine watafanya nini badala ya kutegemea walewale ambao wametuangusha kwa muda wote huo.Mbona nchi za wenzetu hubadilisha utawala mara kwa mara na wanaendelea mbele,sisi tunaogopa nini?Ni wakati muafaka wa kubadilisha watawala kwani hata wengine wakifanya vibaya si tutawaondoa tu shaka ya nini?
 
wakubwa!naombeni kufahamishwa jamani,huyu mzee ni nani na yuko wapi anafanya nini,simjui kabisa.anyways yeye anapungukiwa nini ama kuongezewa nini chadema ikiongozwd kiharakati?aseme kipi viongozi wa chadema wametudanganya wananchi juu ya chochote walichosema kwa serikali iliyo oza ya CCM?
 
Haya maneno hayawezi kueleweka kwa hawa vijana wa cdm wasiojua siasa. Ukweli ndio huo, chadema ni wanaharakati na si wanasiasa.
 
Back
Top Bottom