Ukiona wanakung'ang'ania wakupe utajiri wa haraka jua wamekuona akili yako ni chenga

Feb 4, 2024
67
206
UkIONA WANAKUNG'ANG'ANIA WAKUPE UTAJIRI WA HARAKA JUA WAMEKUONA AKILI YAKO NI CHENGA 😔

Umewahi kusikia watu wakijinadi kutoa utajiri wa HARAKA? Yaani kulala maskini na kuamka tajiri?

Taarifa isiyopendeza ni kuwa kama nawe ni mmoja wa wateja wao basi jua kuna kitu kwako hakipo sawa na tayari wamekiona ndio maana wanakulazimisha uingie kwenye hiyo fursa hiyo.

Wale watu wana akili sana na wapo vizuri kuisoma akili yako hasa kwenye maamuzi yako na utulivu wako na wakiona una maamuzi ya haraka yasiyo na subira basi wanajua wewe ni mteja wao mzuri katika fursa hiyo.

Tangazo lenye lengo la kutoa utajiri wa haraka huwa linawahusu watu wenye sifa hizi:

1.Wasio na utulivu, kama huna utulivu basi utakuwa mteja wao kwa sababu ukikosa utulivu utakuwa mtu wa kufanya mambo bila kufikiria kwa kina, kwa lugha rahisi unakuwa mvivu wa kupima matokeo na matendo ndio maana akija mtu akikwambia jambo fulani ukilifanya leo tu basi kesho utakuwa bilionea unaliendea kwa haraka sana bila kufikiria kuwa kama hilo jambo lingekuwepo si tungekuwa wote mabilionea.

2 Kupenda matokeo ya haraka, kama unapenda matokeo ya haraka basi nawe ni mteja kwa sababu ukiambiwa utajiri utakuja kesho haraka utaamini ila ukiambiwa utakuja baada ya miaka kumi utaona ni utapeli. Kwa lugha nyepesi hawa ni watu ambao hawana subira bali wanataka kila kianzacho leo basi kesho kilete matokeo chanya.

3.Waliokata tamaa, mkata tamaa ni mtu ambaye haamini tena kwenye kushinda hivyo amebaki kusubiria miujiza tu , kama umekata tamaa kiwango cha mwisho basi nawe utakuwa mteja.

4.Wanaokimbizana na umri, kuna watu ambao kwa namna moja ama nyingine wanajiona kama wameachwa na umri hivyo hawataki tena kitu cha kusubiri bali wanataka tu jambo lianze leo na kesho lije na matokeo, kama upo kundi hili basi nawe ni mteja.

Matangazo haya ya kujinadi kuwa kuna utajiri wa haraka yanzidi kushia kasi kwa sababu watoaji matangazo wamegundua kuwa watu wengi sasa hivi wanataka sana mambo ya miujiza na hawataki tena kusubiria hivyo wapo tayari kulipa gharama ya kupewa utajiri wa haraka usio na uhalisia kuliko kutumia pesa hiyo kutafuta utajiri wenye uhalisia.

Mwanasayansi Saul kalivubha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom