Ukioa mwanamke unaempenda sana ni hatari? Wewe unasemaje?

ndoa cyo majaribio ts a lyftym commitment, so ni bora kuoa au kuolewa na m2 umpendaye sana coz ni rahic kumvumilia kuliko ucye mpenda sana.
 
Ni vema kuoa/kuolewa na mtu unayempenda sana na yeye anakupenda hiyo itasaidia sana kudumisha ndoa yenu ni rahisi kuvumiliana kwa sababu mnapendana!
Ukioa/olewa na mtu usiyempenda ni rahisi sana kumsaliti na hapo ndo matatizo yatakua hayaishi kwenye ndoa na mwisho wa siku mtaishia kutengana..
 
Mtizamo wangu ni kwamba oa au olewa na m2 anayekupenda kwa sababu ni rahis kujlazmisha kumpenda m2 usiyemfeel kuliko kumbadilisha acyekupenda akupende.

Mimi nakupenda sana, wewe upo upo tu; umeamua kunioa si ndio? Lkn formula yako nikiimiliki mimi, sitakubali kuolewa na wewe ambaye hunipendi kwani sitaweza kukubadilisha unipende. Nami nitatafuta anayenipenda ili nijifunze kumpenda!

One way traffic doesn't work!
 
ndoa sio kitu cha mchezo wala majaribio..... Unapaswa kuoa/olewa na mtu unayempenda......

Unadhani kuishi na mtu ambaye huna mapenzi nae kivile ni mchezo?

u answered it collect dear!
watu wanafayia ndoa majaribio enh??? seriosly?? acheni masihara mjue, how comes uishi na mtu ambae humpendi for the rest of ur life??
tuache masihara jaman!
 
@mkereketwa huyu,
kwanza kabisa hilo sikitiko lako lihifadhi ukampe mtu mwenye kulihitaji, mie sio aina ya watu wa kupelekeshwa, najitambua na najua nini ninahitaji kwenye maisha yangu, na fedha nina uwezo wa kuzitafuta, nina uwezo wa kupata chochote ninachokihitaji, nina uwezo wa kusimama mwenyewe bila kushikwa mkono,kwa hilo namshukuru Mungu. ila nipo kwenye ndoa kwa sababu mimi na mwenzangu tunapendana, tumeamua kuishi pamoja siku zote, na itakapotokea mapenzi yanaisha(of cousrse hatuombei) kila mmoja atashika hamsini zake, tumekutana kila mmoja ana meno 32, kila mtu atachukua time zake na meno 32. maisha ni vile unavyoyapanga, majumba, pesa na magari yanatafutwa, hasara roho tu.....

pili, uliyoyaongea inawezekana kabisa kutokea kwa upande wa pili, ila umewalenga wanawake na wanaume wa aina gani? kuna aina hiyo ya wanawake na wanaume wanaokubali kujilipua ili kupata material things,

ila hapo nimongelea wanaofall in love na kuoana, mwanamke na mwanaume mwenye heshima zake na malengo yake, anayejua kuwa kupanga ni kuchagua na mwenye kuthamini ndoa na maisha yake binafsi..... hivyo ukielewa kuwa kupanga ni kuchagua, ukijua na kuelewa kuwa ndoa ni kitu serious na kama unampenda mpenzi wako na kutamani kuishi nae siku zote za maisha yako.... utachagua unayempenda......

kumbuka maisha ni vile unavyoyapanga, ukipanga kuwa mtumwa wa fedha (ambazo huzitafuti na hujui jasho lake) utakuwa mtumwa, ukiamua kuwa mtumwa wa penzi utakuwa...
ukiamua kuzitumikisha fedha utazitumikisha...
ukiamua kuenjoy penzi, utaenjoy

ukiwa ni mwanaume au mwanamke unayependa mambo ya "mujini" ukaishi kimjini mjini uliyoyasema ni dhahiri kutokea...... ukikurupuka kwa mtu bila kumsoma na kumchunguza utapata jini mla fedha...... kumbuka ndege wafananao ndio warukao pamoja...





BadiliTabia...Sikubaliani nawe moja kwa moja kwa haya uyasemayo. Wasichana/wanawake wengi hapa Bongo siku hizi hawaolewi na mtu eti kwa sababu wanampenda; hapana, ila wanafuata material things. Haswa ukiangalia idadi kubwa ya wanawake wanao olewa na hawa vijana wa kuuza unga, unataka kuniambia they are there for the love? Heck no, but they'll do anything na watakubali kunyanyasika ili waonyeshe kuwa wako serious na ndoa zao. Mwanamke gani mwenye akili timamu anakubali kuwa a spare tyre? Nasema hivi kwa sababu vijana wengi wenye mahela machafu hapa Bongo, yaani asilimia 100 ni malaya na wake zao wanajua hivyo lakini wanavumilia because they are there for the ride. Kutoka kwenye ndoa zao hawawezi kwani walishatambia wenzao kabla ya kuolewa, na akitoka hapo ataenda wapi kwenye matanuzi kama aliyonayo? Binafsi, najua jamaa kama watatu hivi wameoa na wapigaji mademu hodari sana hapa jijini. Cha kusikitisha wake zao wote wanajua na mara nyingi huwa wanawambia waume zao mwenzangu tafadhali jichunge huko nje na kina mama, au utasikia shemeji tafadhali muonyeni rafiki yenu jamani kwani najuwa vitu vyake huko nje. Karne hii ya 21 hakuna love Bongo, kama wewe una mapenzi Mungu akubariki ila pia nakusitikia kwani kina mama wengi kama wewe ndio wanaopelekeshwa kwenye ndoa zao na huishia kujiua kwa kutovumilia manyanyaso ya ndoa. Pole sana yasije kukukuta dada yangu ila ukweli ndo huo.
 
Katika hali ya kawaida mtu huweza kushangaa hoja hii. Ukweli ni kuwa watu wengi wanafikiri wakioa au kuolewa na watu wanaowapenda sana maisha huwa ya furaha sana lakini wengi wamekuwa wakilazimika kufanya mambo hata nafsi zao hazipendi kwa kuwa tu wanaogopa wampendae atachukia au atamwacha. Ni vyema basi mtu kuoa au kuolewa na mtu umpendae wastani ili kuwa na kuambiana tunavyopenda na tusivyopenda vinginevyo tutaogopa kuwaudhi watu tunaowapenda kupita kiasi.
WEWE UNAONAJE? NI VYEMA AU SI VYEMA KUOA AU KUOLEWA NA MTU UMPENDAE KUPIATA KIASI?

Kupendana kwa kiasi tena, hee! Ya leo kali
 
.....ndoa ni tofauti kabisa na mapenzi. Ndoa ni Upendo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom