Ukikuta begi limetelekezwa limejaa maburungutu ya pesa liache kama lilivyo, usijizidi akili kujiona mjanja ukimbie nalo

Uncle bright

JF-Expert Member
Feb 9, 2023
1,040
4,080
1709579455692.png
Begi ukilikuta njiani kuna uwezekano mkubwa wa uhalifu kuhusika, aidha limetupwa wakati majambazi yakimkimbiza mwenye nalo, majambazi waliiba ila wakalitupa kupoteza ushahidi hasa wakiwa suspects, wezi wameiba pesa na ghafla wanaona kuna ukaguzi barabarani, n.k.

Maisha ya hapo zamani mtu akikuta begi kama hili na kuliacha, watu walimshangaa sana kwamba kapitwa na bahati na bahati haiji mara mbili,

Ila kwa siku hizi mtu akiliacha begi kama hilo ana akili sana, wala si wa kumcheka.

1709579197941.png

Teknolojia ya GPS tracking imekuwa kubwa sana, Begi lenye maburungutu ya hela ni kawaida sana kuwekwa gps inayoonyesha movement zote za begi, Gps ndigo ya ziada inaweza kuwekwa kwa ustadi katikati ya pesa zilizobanana, hata begi likitupwa location ya mzigo inaonekana.

Gps trackers itaonyesha sehemu lilipo begi na movements zake, hivyo ukiliokota na kwenda nalo nyumbani kwako, watajua lilipo na kulifuata, kibongo bongo utapewa kipigo kikali sambamba na kupewa kesi ya ujambazi.

Watu wanaweka gps kwenye pikipiki na magari na yakiibiwa wanayapata sembuse mabegi yenye maburungutu ya hela ? hilo swali ujuilize sana.

Njia pekee ya kuiba hilo begi labda uwe na jammer wanazotumia majambazi wa kisasa kuiba pikipiki na magari, gps jammer ni kifaa maalum cha kublock mawimbi ya gps tracker.

Begi ukikimbia nalo kwa muda mfupi ukiwa na furaha utasema maisha umeyapata lakini kifuatacho baada ya hapo kinaweza kufanya maisha yako yawe ya majonzi sana.
 
Kuna babu yuko kwa mo aliwahi okota bag limejaa hela akalirudisha.

Baadae ikaja kugundulika lile bag lilikua la mfanyakazi wa kigeni.(mhindi) aliyehudumu kama muwasibu baadae akapigwa chini. Sasa alivyojaribu kutorosha mapesa aliyoiba ikashindikana akaamua kuyatekeleza kwenye majani.

Ndipo babu huyu alipokua on duty akayaona.

Ajabu alimrudishia meneja bag lote la pesa. Akapewa zawadi ya godoro.

Pia akapewa ajira ya kudumu mpaka atakapoona hawezi tena endelea na kazi (true story).
 

Maisha ya hapo zamani mtu akikuta begi kama hili na kuliacha, watu walimshangaa sana kwamba kapitwa na bahati na bahati haiji mara mbili,

Ila kwa siku hizi mtu akiliacha begi kama hilo ana akili sana, wala si wa kumcheka.


Teknolojia ya GPS tracking imekuwa kubwa sana, Begi lenye maburungutu ya hela ni kawaida sana kuwekwa gps inayoonyesha movement zote za begi, Gps ndigi ya ziada inaweza kuwekwa kwa ustadi katikati ya pesa zilizobanana, hata begi likitupwa location ya mzigo inaonekana.

Njia pekee ya kuiba hilo begi labda uwe na jammer wanazotumia majambazi wa pikipiki na magari kuharibu mawasiliano ya gps tracker zisitume location

Begi ukikimbia nalo kwa muda mfupi ukiwa na furaha utasema maisha umeyapata lakini kifuatacho baada ya hapo kinaweza kufanya maisha yako yawe ya majonzi sana.
Nyoosha maelezo mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom