Uhamisho watumishi wa Umma: Waziri Ummy Mwalimu acha usanii na siasa kwenye maisha ya watu

Kauli ya kukataza uhamisho kutoka vijijini/miji midogo kwenda mjini kaitoa Waziri Ummy Mwalimu na sio wasaidizi wake

Style ya kufanya kazi za serikali kwa matamko yasio ya kisheria iliasisiwa kwenye awamu iliyopita. Kila mtu alikua anatoa maagizo ili kumridhisha "Mkuu" ikiwemo ya ma DC na Ma RC kuweka watu ndani!

Wakurugenzi wa Manispaa na Halmashauri za Miji pamoja na baadhi ya Wakuu wa Mikoa na Wilaya nao wanatoa matamko kwa watumishi kwamba hakuna kwenda likizo mpaka wakamilishe ujenzi wa madarasa ambao unakadiriwa kuchukua hadi miezi saba!!!!

Ajabu ni kwamba hawawalipi hizo likizo zenyewe ambazo zipo kisheria. Inapotokea kufuta likizo ya mtumishi kuna taratibu zake ikiwa pamoja na kuinunua

Huyu Ummy Mwalimu hivi karibuni alitoa tamko la kuwazuia wakuu wa mikoa kutoka nje ya mikoa yao bila kibali cha Rais au Makamu au Waziri Mkuu!!! Hii haikubaliki na ni uvunjaji haki za binadamu na kanunu na taratibu za utumishi wa umma

Huku ni kudhalilishana kwakweli! Unamzuia mtu kutoka nje ya mkoa amekua ni mtuhumiwa ambaye yupo chini ya uangalizi wa mahakama au polisi?!!! Kwani isingetosha kuwapa malengo ya Wizara na wakawaacha na uhuru wao kama watu huru tena viongozi wa umma!!! Hizi ni athari mbaya kabisa za mind set za watawala zilizoachwa na awamu ile.

Acheni upotoshaji enyi vijana wa Ufipa. Hebu rudia kusikiliza ile speech yake vizuri. Ummy Mwalimu hajasimamisha Uhamisho amesitisha kwa muda tena ni Uhamisho kwenye Majiji, Miji na Manispaa kwa ajili ya kufanya msawazo wa watumishi.

Kilichopo ni kwamba kwenye Maeneo hayo Watumishi wamezidi ni wengi sana na wanaohitaji kuhamia huko bado ni wengi kitu kinachopelekea upungufu kwenye halmashauri za Pembezoni.

Hata Hivyo uhamisho wa kubadilishana unaruhusiwa
na ule wa kuhamia kwenye Halmashauri za Wilaya unafanyika kama kawaida. Kitaalamu wanaita kubalance Ikama.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Serikalini wafanyakazi wanadeka sana mkataba wa ajira kawaida Ni wa mtu binafsi mmoja tu na mwajiriwa lakini serikalini Ajabu eti mtu anajiamlia tu nataka kuhama nifuate mume wangu au mke wangu aiseeee!!! Private sector mleta mada ungepigwa makofi na mateke ndipo upewe barua ya kufukuzwa kazi moja kwa moja


Oeni full time house wife asiyefanya kazi ili muda wowote uhame naye bila shida na wanawake wafanyakazi serikalini oleweni na wanaume wasio na kazi muwe nao popote
Wewe utakua ummy...acha roho mbaya na kupangia watumishi waishi vipi..wewe mbona kwa mumeo unaenda bila kupangiwa.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acheni upotoshaji enyi vijana wa Ufipa. Hebu rudia kusikiliza ile speech yake vizuri. Ummy Mwalimu hajasimamisha Uhamisho amesitisha kwa muda tena ni Uhamisho kwenye Majiji, Miji na Manispaa kwa ajili ya kufanya msawazo wa watumishi.

Kilichopo ni kwamba kwenye Maeneo hayo Watumishi wamezidi ni wengi sana na wanaohitaji kuhamia huko bado ni wengi kitu kinachopelekea upungufu kwenye halmashauri za Pembezoni.

Hata Hivyo uhamisho wa kubadilishana unaruhusiwa
na ule wa kuhamia kwenye Halmashauri za Wilaya unafanyika kama kawaida. Kitaalamu wanaita kubalance Ikama.
Masawazisho upi..huko vijijini wanataka watumishi wafe kwa hali duni na kukosa huduma muhimi..mbona wao ofisi zipo mjini kwanini asihamishie wizara yake huko sitimbi..na sio wote wanahamia mjini kufuata wake au wamue zao wengine wakae karibu na huduma za kiafya.

Acheni roho mbaya hizo ofisi za umma ni mapito tu..tendeni kwa haki.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo Ummy hana tofauti na Kitila Mkumbo naye leo anakija na mambo eti siyo sera ya ccm kijengaviwandamia moja kilamkoa
 
ushauri wangu kwa vijana,Kama una Target ya kuajiliwa na serikali basi msioe/kuolewa kabla ya kuajiliwa!!, wake/waume zenu mtawakuta huko huko makazini !! kiherehere chenu Cha kuoana mapema kabla ya ajira ,mwisho wa siku mnakaa mbalimbali ,matokeo yake mnakuwa na familia mamluki ,unakuta mwal.anawatoto 3 wawili sio wake!! muwe mnatembelea makazini kwa wake zenu Mara moja moja mjionee sura zinazofanana na watotowenu!!
Naona utendaji wa kazi katika taasisi za umma utakuwa wa watu wenye umri mkubwa tofauti na malengo ya kimkakati ya sera ya vijana
 
Huyu mama nilimuona ana busara kumbe siyo,na sizani kama ana ndugu,mdogo wake au mtoto wake anayeishi mbali na mke au mme wake.
Na kwa kauli zake hizi ameumiza wengi ila Mungu ni wa wote nadhani ataweka mikono yake ikiwezekana hata amuonyeshe tu kuwa anayoyatamka kwa binadamu wenzake wanaotabika huko na ndoa zao siyo mazuri ili ajifunze maana siyo kwa kauli hizi za kuudhi na kunyanyasa watumishi.
Halafu unategemea watu wakufanyie kazi nzuri huku unawatengezea misongo ya mawazo sifikirii kama utapata zao lililo bora!...
 
Huyu mama nilimuona ana busara kumbe siyo,na sizani kama ana ndugu,mdogo wake au mtoto wake anayeishi mbali na mke au mme wake.
Na kwa kauli zake hizi ameumiza wengi ila Mungu ni wa wote nadhani ataweka mikono yake ikiwezekana hata amuonyeshe tu kuwa anayoyatamka kwa binadamu wenzake wanaotabika huko na ndoa zao siyo mazuri ili ajifunze maana siyo kwa kauli hizi za kuudhi na kunyanyasa watumishi.
Halafu unategemea watu wakufanyie kazi nzuri huku unawatengezea misongo ya mawazo sifikirii kama utapata zao lililo bora!...
Hii kuchelewa kutoa ajira ni chanzo cha mambo mengi sana ikiwa Separation of Family
 
Acha Upotoshaji wewe Waziri wa TAMISEMI Ummy Mwalimu Hajasimamisha uhamisho bali amesitisha kwa Muda uhamisho wa Watumishi kutoka Maeneo ya Vijijini kuja Mjini
Asilimia kubwa ya watumishi wanataka uhamisho kutoka Vijijini kuja Mjini inapelekea maeneo Mengi hasa ya Vijijini kukosa Watumishi wa kutosha. Waziri Ummy Mwalimu anafanya kazi kubwa na Nzuri Ofisi ya Rais TAMISEMI na ana nia Njema sana na watumishi. Tamisemi ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan ni TAMISEMI ya Wananchi.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Acha Upotoshaji wewe Waziri wa TAMISEMI Ummy Mwalimu Hajasimamisha uhamisho bali amesitisha kwa Muda uhamisho wa Watumishi kutoka Maeneo ya Vijijini kuja Mjini
Asilimia kubwa ya watumishi wanataka uhamisho kutoka Vijijini kuja Mjini inapelekea maeneo Mengi hasa ya Vijijini kukosa Watumishi wa kutosha. Waziri Ummy Mwalimu anafanya kazi kubwa na Nzuri Ofisi ya Rais TAMISEMI na ana nia Njema sana na watumishi. Tamisemi ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan ni TAMISEMI ya Wananchi.
Simpendi huyu mama since ile siku. Aliongea kwa dharau halafu by that moment nilikuwa nishakamirisha uhamisho wa mke wangu wa ndoa halali kabisa anifuate
 
Acheni upotoshaji enyi vijana wa Ufipa. Hebu rudia kusikiliza ile speech yake vizuri. Ummy Mwalimu hajasimamisha Uhamisho amesitisha kwa muda tena ni Uhamisho kwenye Majiji, Miji na Manispaa kwa ajili ya kufanya msawazo wa watumishi.

Kilichopo ni kwamba kwenye Maeneo hayo Watumishi wamezidi ni wengi sana na wanaohitaji kuhamia huko bado ni wengi kitu kinachopelekea upungufu kwenye halmashauri za Pembezoni.

Hata Hivyo uhamisho wa kubadilishana unaruhusiwa
na ule wa kuhamia kwenye Halmashauri za Wilaya unafanyika kama kawaida. Kitaalamu wanaita kubalance Ikama.
Kwanini unahusianisha hoja za watu na Ufipa?

Uhamisho wa kubadilishana upo miaka yote na wala hapakua na haja ya yeye kutolea tamko

Kuhusu kurekebisha ikama pia ni uongo uliotukuka. Kwa mfano kwenye sekta ya elimu naweza kukupa mifano ya shule za Dar tena mjini kuna baadhi ya masomo wanafunzi hawafundishwi kwa kukosa mwalimu wa somo husika

Dharura zipo kila mahali na kila wakati. Kitendo cha kuzuia uhamisho ni kibaya na cha kibaguzi.

Ummy ni anatabia ya kutoa matamko ya kujipendekeza aonekane anafanya kazi. Uliona wapi Ma RC eti wanapigwa marufuku wasitoke nje ya mikoa yao!!!! Ni haki kweli hiyo?
 
Ummy Mwalimu hajasimamisha Uhamisho amesitisha kwa muda tena ni Uhamisho kwenye Majiji, Miji na Manispaa kwa ajili ya kufanya msawazo wa watumishi.

Kilichopo ni kwamba kwenye Maeneo hayo Watumishi wamezidi ni wengi sana na wanaohitaji kuhamia huko bado ni wengi kitu kinachopelekea upungufu kwenye halmashauri za Pembezoni.

Hata Hivyo uhamisho wa kubadilishana unaruhusiwa
na ule wa kuhamia kwenye Halmashauri za Wilaya unafanyika kama kawaida
Kwa sheria ipi mkuu???
 
Kwanini unahusianisha hoja za watu na Ufipa?

Uhamisho wa kubadilishana upo miaka yote na wala hapakua na haja ya yeye kutolea tamko

Kuhusu kurekebisha ikama pia ni uongo uliotukuka. Kwa mfano kwenye sekta ya elimu naweza kukupa mifano ya shule za Dar tena mjini kuna baadhi ya masomo wanafunzi hawafundishwi kwa kukosa mwalimu wa somo husika

Dharura zipo kila mahali na kila wakati. Kitendo cha kuzuia uhamisho ni kibaya na cha kibaguzi.

Ummy ni anatabia ya kutoa matamko ya kujipendekeza aonekane anafanya kazi. Uliona wapi Ma RC eti wanapigwa marufuku wasitoke nje ya mikoa yao!!!! Ni haki kweli hiyo?
Anajisahau sana, analeta pigo za wizara ya afya, kule alikuwa anadili na huduma zaidi kwa watu, huku yeye anadeal na watoa huduma hasa kwa matamko yake yasiyo na utafiti.
Unakataaje uhamisho, eti kama ndoa ndoa wote wanazo.
Itoshe kusema Ummmi kafeli
 
Point inabaki palepale huu sio utawala wa mabavu ule uliokoma march 17
Unasema sio utawala wa mabavu wakati unalialia hapo sababu ya hayohayo mabavu
Tz viongozi mazuzu na walalamikaji nao ni mazuzu square!
 
Acha Upotoshaji wewe Waziri wa TAMISEMI Ummy Mwalimu Hajasimamisha uhamisho bali amesitisha kwa Muda uhamisho wa Watumishi kutoka Maeneo ya Vijijini kuja Mjini
Asilimia kubwa ya watumishi wanataka uhamisho kutoka Vijijini kuja Mjini inapelekea maeneo Mengi hasa ya Vijijini kukosa Watumishi wa kutosha. Waziri Ummy Mwalimu anafanya kazi kubwa na Nzuri Ofisi ya Rais TAMISEMI na ana nia Njema sana na watumishi. Tamisemi ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan ni TAMISEMI ya Wananchi.
Ni sawa lakini kwenye hili kapotoka sana,kuonekana kuwa kazi bure kabisa na pengine kuleta matabaka kwa wananchi walio wengi,watoe ajira wapeleke watu kule kuliko na upungufu na mtu akitimiza masharti ya kuhama aruhusiwe siyo kumzuia au la sivyo watoe waraka mwingne kuwa mtumishi harusuwi kuhama pindi anapoajiliwa mbona zamani watu walihama na hapakuwa na haya makandokando ya enzi hizi.
Mtumishi katimiza matakwa ya kuhama kituo tena wengi wanajiombea wawahamishe wakaishi na waume/wake zao kama walivyo wao hadi wanasafiri na waume/wake zao mchana kutwa,je huyu mtumishi wa chini anakosa nini yeye hadi mme akae Mtwara na mke yuko Kagera miaka nenda rudi hii sawa!?
 
Mbona Unajitoa Akili Mkuu
Hujasikia Ummy Alisema Hakuna Uhamisho
Hujui unachokitetea na hujui kinachoumiza wenzio. Nahisi kuna kitu hukuelewa, hicho ambacho hukukielewa ndicho kinachotugusa wenzio. So piga kinywa mzee. Tuliza gorori tuongee tuliopo kwenye majiji tunaoguswa na tamko, wewe wa Mbinga huko Makete vunga tu.
 
Back
Top Bottom