Waziri Ummy Mwalimu, Mfuko wa Bima ya Afya unawatesa Wagonjwa wasio na hatia na unakiuka kanuni za utawala bora

Mama Amon

JF-Expert Member
Mar 30, 2018
2,021
2,478
1686636978600.png

Mheshimiwa Waziri Ummy Mwalimu,

Napenda kukufahamisha matatizo matatu kuhusu Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF), kama ifuatavyo:

Mosi, mikataba yote kati ya NHIF na vituo vya Afya inacho kifungu kinachovunja sheria ya mikataba, kanuni za utawala bora, na heshima ya utu wa wamiliki wa vituo. Kinasomeka hivi:

"24.2.5. The Fund also may terminate Agreement if: the Fund in its sole discretion and for any reason whatsoever decides to terminate this Agreement."

Ushauri
: Mwagize Mkurugenzi Mkuu kurekebisha dosari hii. Tanzania ni Jamhuri ya Kidemokrasia, na Katiba yake inataja kanuni za utawala bora ambazo haziruhusu ulevi wa madaraka wa kiwango hiki, hata kama NHIF wanayo monopoly katika sekta ya bima ya afya.

Pili, NHIF inatumia kifungu nilichokitaja hapo juu kuwatesa wagonjwa wasio na hatia pale inapovifungia vituo vya Afya kiholela. Kuna orodha ya vituo vya afya vilivyofungiwa inasambaa mitandaoni. Nimeambatanisha.

Baadhi ya vituo vinatoa huduma za kibingwa, kiasi kwamba wagonjwa husika wasopokwenda kwenye vituo hivyo, ama watakufa au watalazimika kwenda kwenye hospitali zinazowataka kugusa mfukoni, lakini wanakwama kwa sababu ya kukosa fedha taslimu.

Ushauri: Adhabu ya kufungia vituo kiholela zikomeshwe, na zitafutwe adhabu mbadala kwa vituo vinavyokiuka utaratibu. Kufungiwa huduma ya NHIF iwe hatua ya mwisho.

Ukweli ni kwamba, siwatetei wamiliki wa vituo vya afya wakorofi. Ninachosema ni kwamba, uwepo mfumo wa udhibiti usiowaumiza watu wasio na hatia. Kwa mfano, uwepo mfumo wa kusimamia nidhamu ufuatao:
  • Kwanza, onyo kwa mmiliki.
  • Pili, mmiliki apigwe faini ya kifedha,
  • Tatu, mmiliki apigwe faini ya kupunguziwa baadhi ya huduma zilizosajiliwa na NHIF kwa muda
  • Nne, mmiliki apigwe faini ya kufungiwa kwa muda,
  • Na hatimaye, tano, mmiliki apewe adhabu ya kufungiwa kabisa.
Mara zote kipaumbele kiwe ni huduma kwa wagonjwa. Lakini pia, haki ya wamiliki wa vituo kusikilizwa uzingatiwe.

Makosa mengine katika mfumo wa kompyuta yanatokea inadvertently kwa sababu ya computer iliteracy.

Na tatu, ni kuhusu service delivery cycle: Uongozi wa NHIF unafanya kazi kwa kasi ya konokono.

Tangu kituo kinapopeleka maombi ya kuingia mkataba hadi mkataba huo upatikane inachukua muda mrefu, jambo ambalo pia ni mzigo kwa wagonjwa. Kuna shida mbili hapa.

Kwanza, NHIF wanafanya kazi ya kukagua hospitali kana kwamba wao ni "health service regulator," yaani District Medical Officer (DMO), badala ya kufanya kazi ya "health insurance service provider," ambaye anafanya maamuzi kwa kuzingatia maamuzi ya DMO.

Hata ukisoma mikataba kati ya NHIF na vituo vya afya utaona tatizo hili. Neno "ukaguzi" limerudiwa zaidi ya mara 20.

NHIF Wakiacha ukiritimba, kazi ya NHIF inaweza kufanyika "remotely" kwa kutumia "NHIF service portal" na maombi kukamilishwa ndani ya masaa 24 pekee.

Ushauri: Waziri komesha huu ukiritimba na uporaji wa madaraka ya DMO. Watanzania wanataka huduma, sio ubabe na hali ya kutotabirika inayoighubika NHIF kwa sasa.

Nawasilisha.

Ukipita "Sumbawanga Town" tuwasiliane jamani.

1686635692680.png
 
Wenye vituo vya Afya wanacheza michezo michafu mno ndo mana wanapelekea NHIF kuwa wakali sana.

Kuhusu kukagua huduma lazima NHIF wajiridhishe kuwa wanapatner na watu wanaotoa huduma bora.

Kuhusu mchakato kuchukua muda mrefu hapo hata mm nashindwa kuwatetea, inshort wanazingua, wangejitahidi isizidi mwezi mmoja
 
View attachment 2655692
Mheshimiwa Waziri Ummy Mwalimu,

Napenda kukufahamisha matatizo matatu kuhusu Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF), kama ifuatavyo:

Mosi, mikataba yote kati ya NHIF na vituo vya Afya inacho kifungu kinachovunja sheria ya mikataba. Kinasomeka hivi:

"24.2.5. The Fund also may terminate Agreement if: the Fund in its sole discretion and for any reason whatsoever decides to terminate this Agreement."

Ushauri
: Mwagize Mkurugenzi Mkuu kurekebisha dosari hii. Tanzania ni Jamhuri ya Kidemokrasia, na Katiba yake inataja kanuni za utawala bora ambazo haziruhusu ulevi wa madaraka wa kiwango hiki, hata kama NHIF wanayo monopoly katika sekta ya bima ya afya.

Pili, NHIF inatumia kifungu nilichokitaja hapo juu kuwatesa wagonjwa wasio na hatia pale inapovifungia vituo vya Afya kiholela. Kuna orodha ya vituo vya afya vilivyofungiwa inasambaa mitandaoni. Nimeambatanisha.

Baadhi ya vituo vinatoa huduma za kibingwa, kiasi kwamba wagonjwa husika wanakwama kujihudumia kwa kulipa fedha taslimu.

Ushauri: Adhabu ya kufungia vituo kiholela zikomeshwe, na zitafutwe adhabu mbadala kwa vituo vinavyokiuka utaratibu. Kufungiwa huduma ya NHIF iwe hatua ya mwisho.

Na tatu, ni kuhusu service delivery cycle: Uongozi wa NHIF unafanya kazi kwa kasi ya konokono.

Tangu kituo kinapopeleka maombi ya kuingia mkataba hadi mkataba huo upatikane inachukua muda mrefu, jambo ambalo pia ni mzigo kwa wagonjwa. Kuna shida mbili hapa.

Kwanza, NHIF wanafanya kazi ya kukagua hospitali kana kwamba wao ni "health sector regulator" badala ya kufanya kazi ya "health insurance service regulator".

Hata ukisoma mikataba kati ya NHIF na vituo vya afya utaona tatizo hili. Wakiacha ukiritimba, kazi ya NHIF inaweza kufanyika "remotely" kwa kutumia "NHIF service portal" na maombi kukamilishwa ndani ya masaa 24.

Ushauri: Komesha huu ukiritimba. Watu wanataka huduma, sio ubabe na hali ya kutotabirika inayoighubika NHIF kwa sasa.

Nawasilisha.

Ukipita "Sumbawanga Town" tuwasiliane jamani.

View attachment 2655679
Hii Tanzania ikiwa na watu kama wewe tutafika mbali mnooo. Mungu akubariki sana
 
Wenye vituo vya Afya wanacheza michezo michafu mno ndo mana wanapelekea NHIF kuwa wakali sana.

Kuhusu kukagua huduma lazima NHIF wajiridhishe kuwa wanapatner na watu wanaotoa huduma bora.

Umeandika: "Wenye vituo vya Afya wanacheza michezo michafu mno ndo mana wanapelekea NHIF kuwa wakali sana."

Najibu: Hata mie siwatetei wamiliki wa vituo vya afya wakorofi. Ninachosema ni kwamba, uwepo mfumo wa udhibiti usiowaumiza watu wasio na hatia. Kwa mfano:
  • Kwanza, mmiliki apigwe faini ya kifedha kabla ya kufungiwa,
  • Kisha apigwe faini ya kupunguziwa kwa muda huduma zilizosajiliwa na NHIF,
  • Halafu apigwe faini ya kufungiwa kwa muda,
  • Na hatimaye adhabu ya kufungiwa kabisa.
Mara zote kipaumbele kiwe ni wagonjwa, na pia haki ya kusikilizwa uzingatiwe. Makosa mengine katika mfumo wa kompyuta yanatokea inadvertently kwa sababu ya computer iliteracy.

Umeandika: Kuhusu kukagua huduma lazima NHIF wajiridhishe kuwa wanapatner na watu wanaotoa huduma bora.

Najibu: Kazi ya "kukagua ubora wa hudumua" inafanywa na DMO. NHIF wanachopaswa kuangalia ni uwepo wa kibali/idhini ya DMO. Lakini wao wanarudia mchakato mzima uliokwishafanywa na DMO tayari. It is illogical, funciful and absurd!
 
View attachment 2655692
Mheshimiwa Waziri Ummy Mwalimu,

Napenda kukufahamisha matatizo matatu kuhusu Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF), kama ifuatavyo:

Mosi, mikataba yote kati ya NHIF na vituo vya Afya inacho kifungu kinachovunja sheria ya mikataba, kanuni za utawala bora, na heshima ya utu wa wamiliki wa vituo. Kinasomeka hivi:

"24.2.5. The Fund also may terminate Agreement if: the Fund in its sole discretion and for any reason whatsoever decides to terminate this Agreement."

Ushauri
: Mwagize Mkurugenzi Mkuu kurekebisha dosari hii. Tanzania ni Jamhuri ya Kidemokrasia, na Katiba yake inataja kanuni za utawala bora ambazo haziruhusu ulevi wa madaraka wa kiwango hiki, hata kama NHIF wanayo monopoly katika sekta ya bima ya afya.

Pili, NHIF inatumia kifungu nilichokitaja hapo juu kuwatesa wagonjwa wasio na hatia pale inapovifungia vituo vya Afya kiholela. Kuna orodha ya vituo vya afya vilivyofungiwa inasambaa mitandaoni. Nimeambatanisha.

Baadhi ya vituo vinatoa huduma za kibingwa, kiasi kwamba wagonjwa husika wasopokwenda kwenye vituo hivyo, ama watakufa au watalazimika kwenda kwenye hospitali zinazowataka kugusa mfukoni, lakini wanakwama kwa sababu ya kukosa fedha taslimu.

Ushauri: Adhabu ya kufungia vituo kiholela zikomeshwe, na zitafutwe adhabu mbadala kwa vituo vinavyokiuka utaratibu. Kufungiwa huduma ya NHIF iwe hatua ya mwisho.

Ukweli ni kwamba, siwatetei wamiliki wa vituo vya afya wakorofi. Ninachosema ni kwamba, uwepo mfumo wa udhibiti usiowaumiza watu wasio na hatia. Kwa mfano, uwepo mfumo wa kusimamia nidhamu ufuatao:
  • Kwanza, onyo kwa mmiliki.
  • Pili, mmiliki apigwe faini ya kifedha,
  • Tatu, mmiliki apigwe faini ya kupunguziwa baadhi ya huduma zilizosajiliwa na NHIF kwa muda
  • Nne, mmiliki apigwe faini ya kufungiwa kwa muda,
  • Na hatimaye, tano, mmiliki apewe adhabu ya kufungiwa kabisa.
Mara zote kipaumbele kiwe ni huduma kwa wagonjwa. Lakini pia, haki ya wamiliki wa vituo kusikilizwa uzingatiwe.

Makosa mengine katika mfumo wa kompyuta yanatokea inadvertently kwa sababu ya computer iliteracy.

Na tatu, ni kuhusu service delivery cycle: Uongozi wa NHIF unafanya kazi kwa kasi ya konokono.

Tangu kituo kinapopeleka maombi ya kuingia mkataba hadi mkataba huo upatikane inachukua muda mrefu, jambo ambalo pia ni mzigo kwa wagonjwa. Kuna shida mbili hapa.

Kwanza, NHIF wanafanya kazi ya kukagua hospitali kana kwamba wao ni "health service regulator," yaani District Medical Officer (DMO), badala ya kufanya kazi ya "health insurance service provider," ambaye anafanya maamuzi kwa kuzingatia maamuzi ya DMO.

Hata ukisoma mikataba kati ya NHIF na vituo vya afya utaona tatizo hili. Neno "ukaguzi" limerudiwa zaidi ya mara 20.

NHIF Wakiacha ukiritimba, kazi ya NHIF inaweza kufanyika "remotely" kwa kutumia "NHIF service portal" na maombi kukamilishwa ndani ya masaa 24 pekee.

Ushauri: Waziri komesha huu ukiritimba na uporaji wa madaraka ya DMO. Watanzania wanataka huduma, sio ubabe na hali ya kutotabirika inayoighubika NHIF kwa sasa.

Nawasilisha.

Ukipita "Sumbawanga Town" tuwasiliane jamani.

View attachment 2655679
NHIF ni tatizo kubwa,
Pale kuna shida ya management, Kuanzia Mkurugenzi mkuu ameonyesha incompetence kubwa, hakuna ubunifu,
Maamuzi yao na mipango hasa kuhusu vituo binafsi yanaendeshwa na wivu na chuki, kituo binafsi kinachotoa huduma vizuri kwa wagonjwa na kusubmit madai wao wakiona tu kituo kinaclaim hela nyingi kidogo wanakurupuka kutafuta sababu za kukiongezea makato,

Wanamshauri vibaya Waziri wa afya mpaka sasa na yeye ana mtizaomo hasi na vituo vya private, sasa mtu unajiuliza vituo vya private vikifungwa au kutokuwa na huduma za bima vituo vya serikali pekee vina uwezo wa kuhudumia wagonjwa wote? wanataka kuturudisha enzi za msongamano mkubwa mahospitalini?

Mfano pale Dodoma, NHIF wameweka station yao Hospitali ya Benjamin Mkapa eti wanaverify details za wagonjwa kabla ya kumuona daktari tena manually unakuta asubuhi foleni ndefu hatari wanachelewesha utoaji huduma kliniki zinaanza saa nne mpaka saa tano, sasa mtu unajiuliza katika level ya technology ya dunia ya leo hakuna njia ya kufanya hizi verification kwa njia nyingine mpaka Staff wa NHIF aende kwenye kituo physically? hii ni indication ya kukosa ubunifu na incompetence kwa uongozi wa NHIF.

Badala hao Staff wakae maofisini kuprocess claims za watoa huduma ili kulipa in time kuendeleza ubora wa huduma wao staff wamehamia kwenye vituo wanafanya kazi za reception na masijala.
Matokeo yake kuna vituo vya kutoa huduma hawajalipwa claims zao tangu mwaka huu uanze hapo Dodoma.
Na hapo unategemea huduma za hizo facilities ziwe nzuri? watanunuaje dawa na vipimo hujalipa claims tangu February na leo ni August?

Waziri Ummy, inabidi utafute independent advisors wa kuwa wanakupa taarifa sahihi, kuna vitu vingi watu wakaribu hata hao madaktari mfano kuhusu NIHIF hawakwambii ukweli na hivi wanajua wewe sio daktari!
 
Back
Top Bottom