sembuli
JF-Expert Member
- Feb 3, 2012
- 757
- 383
Kwa wafuatiliaji wazuri wa historia, mtakumbuka vizuri kilichotokea algeria kuanzia tarehe januari 3 2011 mpaka februari 2011. Serikali ya rais Abdelaziz bouteflika ilifanya kosa kwa kumnyanyasa kijana msomi MOHAMED BOUAZIZ, (Kama serikali ya tanzania inavofanya kwa Dr ulimboka ). Manyanyaso hayo yalisababisha kijana huyo kujiteketeza kwa moto (self immolation), hali iliyochochea hasira za wananchi wa Algeria waliokuwa na dukuduku na hasira za muda mrefu za ugumu wa maisha, kupanda kwa bei ya vyakula na ukosefu wa ajira , hivyo kuamua kuingia mitaani na kufanya maandamano yaliyoing'oa madarakani serikali "dhaifu" ya bouteflika.
kwa maono yangu, yaliyotokea Algeria ndio naona yananukia kutokea tanzania ya leo. wakati watanzania wakiwa na msongo wa mawazo kutokana na ugumu wa maisha ,bei mbaya ya nishati, kupanda kwa bei ya chakula, ukosefu wa ajira , mgomo wa madaktari, na mengine mengi. serikali ya tanzania imeshindwa kujifunza kutoka algeria kwa "kumteka" na kumtesa vibaya DR STEVEN ULIMBOKA.
Siombei yaliyotokea algeria yatokee na tanzania, ila kama mtanzania naiona hatari kubwa ianayoinyemelea taifa letu ya kuweza kuzuka kwa vurugu kutokana na hasira ya wananchi kwa jinsi wanavyoona picha za dr ulimboka aliyeumia vibaya kutokana na kuteswa kupigwa kipindi hiki cha hali ngumu ya maisha nchini.
kwani kumchokoza binadamu yeyote kipindi ambacho anakabiliwa na hali ngumu ya maisha na amekata tamaa humfanya binadamu apoteze uvumilivu na subira na kufanya jambo lolote baya likiwemo riots. Algeria ilikuwa na ugumu wa maisha kwa muda mrefu uliovumiliwa , lakini kitendo cha kujiteketeza kwa moto mohamed bouaziz kutokana na kunyanyaswa na serikali yao kuliwafanya waalgeria wafikie kikomo cha uvumilivu (threshold ), wasiwe na cha kupoteza hivyo kuamua kuingia mitaani bila kuogopa risasi za moto wala mabomu ya machozi, kushinikiza kung"oka rais boteflika hadi kikaeleweka februari 2011.
Mzalendo ,mpambanaji na daktari wa binadamu steven ulimboka yu taabani kutokana na mateso aliyosababishiwa na serikali kwa kosa la kudai haki yake na ya madaktari wenzie. sina hakika ni hasira kiasi gani watanzania wengine wanayo kwa kuyashuhudia haya kipindi ambacho wanakabiliwa na magumu ya maisha. tumwombe mungu atupe uvumilivu kama ninaoshindwa kuupata kipindi hiki kigumu.
mungu ibariki africa mungu ibariki tanzania.
kwa maono yangu, yaliyotokea Algeria ndio naona yananukia kutokea tanzania ya leo. wakati watanzania wakiwa na msongo wa mawazo kutokana na ugumu wa maisha ,bei mbaya ya nishati, kupanda kwa bei ya chakula, ukosefu wa ajira , mgomo wa madaktari, na mengine mengi. serikali ya tanzania imeshindwa kujifunza kutoka algeria kwa "kumteka" na kumtesa vibaya DR STEVEN ULIMBOKA.
Siombei yaliyotokea algeria yatokee na tanzania, ila kama mtanzania naiona hatari kubwa ianayoinyemelea taifa letu ya kuweza kuzuka kwa vurugu kutokana na hasira ya wananchi kwa jinsi wanavyoona picha za dr ulimboka aliyeumia vibaya kutokana na kuteswa kupigwa kipindi hiki cha hali ngumu ya maisha nchini.
kwani kumchokoza binadamu yeyote kipindi ambacho anakabiliwa na hali ngumu ya maisha na amekata tamaa humfanya binadamu apoteze uvumilivu na subira na kufanya jambo lolote baya likiwemo riots. Algeria ilikuwa na ugumu wa maisha kwa muda mrefu uliovumiliwa , lakini kitendo cha kujiteketeza kwa moto mohamed bouaziz kutokana na kunyanyaswa na serikali yao kuliwafanya waalgeria wafikie kikomo cha uvumilivu (threshold ), wasiwe na cha kupoteza hivyo kuamua kuingia mitaani bila kuogopa risasi za moto wala mabomu ya machozi, kushinikiza kung"oka rais boteflika hadi kikaeleweka februari 2011.
Mzalendo ,mpambanaji na daktari wa binadamu steven ulimboka yu taabani kutokana na mateso aliyosababishiwa na serikali kwa kosa la kudai haki yake na ya madaktari wenzie. sina hakika ni hasira kiasi gani watanzania wengine wanayo kwa kuyashuhudia haya kipindi ambacho wanakabiliwa na magumu ya maisha. tumwombe mungu atupe uvumilivu kama ninaoshindwa kuupata kipindi hiki kigumu.
mungu ibariki africa mungu ibariki tanzania.