Ufugaji wa Samaki: Pata ushauri, mawazo na michango kuhusu ufugaji samaki. Jifunze changamoto, utaalamu na masoko ya Samaki

Toa mail address yako nikusukumie manual za jamaa wa Kenya na Uganda ambao wanafuga.

Kambale kwa mazingira ya kisasa ( yaani ukitengeneza bwawa kisasa mara nyingi hawazai, ni sawa na Kanga), wanataka mazingira asili zaidi.

Nimepata kambale ( Wild african cat fish ) kama 470 hivi, 20 july nimewapata 230 na 22july nimewapata 240 wakiwa wakubwa size ya kidole gumba,nimewaweka ktk ponds mbili tofauti, hakuna aliyekufa mpaka mchana huu. Nitawalisha vizuri kwa miezi sita nione ukuaji wake. Naanda pond ya tatu ili nifikie kambale 700 kwa kuanzia.

Nitayafanya (ponds) mabwawa haya yapate uasili kidogo hata kwa kuchelewa ili niweze kuzalisha fingerlings za mbegu pia. Hawa kambale nimewapata ktk mazingira asilia kabisa kwa kukausha vidimbwi kando ya mto Mduzi huko Shungubweni. Mpango ni kuhamisha kambale wote ktk vidimbwi vile kila baada ya msimu wa mafuriko/mvua unapopita. Kwa kufanya hivi nitaokoa gharama za kwenda Mbegani,kinguluira kuwanunua.

Naamini wengi watapata mbegu toka kwangu ya kambale asilia.
kaka tayari nimekutumia Email kupitia PM


kuhusu hao kambale pia mimi huku nimewaona wengi sana tena nimetaambua kuwa kuna aina mbili ya kambale kuna wengine aambao hawakui kabisa wenyeji wa huku wana waita shingugu.
 
kaka tayari nimekutumia Email kupitia PM


kuhusu hao kambale pia mimi huku nimewaona wengi sana tena nimetaambua kuwa kuna aina mbili ya kambale kuna wengine aambao hawakui kabisa wenyeji wa huku wana waita shingugu.

Huku mitaa ya Pwani wanaitwa ndobe, hawa ndobe hata uwawekee mrija wa lishe hawakui kabisa,ila ndevu zao ndio zinakua teheeeeee.

Naamini nikiwatunza ktk pond/bwawa lenye vionjo asilia watazaa bila shida.Nilishawahi kumshawishi Kanga kwa kumpa vionjo vya porini hadi akataga ndani ya banda.

Nilimuuliza jamaa wa Kinguluira swali hili, kwa nini hawauzi vifaranga/fingerlings vya Kitoga? Jibu lilikuwa;bado utafiti unafanyika. Nadhani hata sisi wafugaji wachanga,tujaribu kufuga samaki wa asili ktk mazingira ya kiasili tuone matokeo yake kisha tuwajulishe hawa jamaa tuone nini matokeo yake.
 
Wadau nina mpango wa kufuga samaki kwa ajili ya kula na biashara,nina eneo la heka moja mkoani Morogoro ambalo nafanya ujenzi,ila nimetenga robo heka kwa ajili ya zoezi la ufugaji wa samaki,me sina utaalamu kabisa na ufugaji wa samaki,kwa hiyo naomba kujua yafuatayo: je robo heka itatosha kweli kwa ufugaji wa samaki kwa ajili ya kitoweo na biashara,pili je ni aina gani ya samaki mbali ya kambare na perege, wanaweza stawi na kukua vizuri kwa hali ya hewa ya Morogoro?asanteni wadau
 
Wadau nina mpango wa kufuga samaki kwa ajili ya kula na biashara,nina eneo la heka moja mkoani Morogoro ambalo nafanya ujenzi,ila nimetenga robo heka kwa ajili ya zoezi la ufugaji wa samaki,me sina utaalamu kabisa na ufugaji wa samaki,kwa hiyo naomba kujua yafuatayo: je robo heka itatosha kweli kwa ufugaji wa samaki kwa ajili ya kitoweo na biashara,pili je ni aina gani ya samaki mbali ya kambare na perege, wanaweza stawi na kukua vizuri kwa hali ya hewa ya Morogoro?asanteni wadau

Mie nipo ktk hatua za mwisho kulikamirisha bwawa langu la pili.

Kifupi samaki aina ya sato niwanyama wenye maajabu sana huzaana sana wanapokuwa na maisha magumu ndani ya bwawa Kwa bwawa la 30mx30m anashauriwa mtu aweke samaki kulingana na uwezo wake wa kulisha. mfano mtu mwenye kufanyakazi ya ufugaji ktk kiwango cha biashara na ana chakula kizuri kama pellet au punje za chakula kilichotengenez wa rasmi kwa ajili ya samaki, unaweza kumshauri aweke samaki 4 kwa mita 1 ya mraba na hivyo bwawa la 900 m2 kama hili unaweka samaki 900 x 4 = 3,600 kujumlisha tahadhari ya 5% ambao ni sawana samaki 180.

Hivyo jumla unaweka samaki 3600 180 = 3780. Pia mabwawa hutiwa mbolea ya samadi iliyofungwa ktk viroba ili isichafue maji. kwa wastani mbolea ya kilo 1 hutiwa ktk mita 10 za mraba na hivyo bwawa kama hili langu la 900 m za mraba ni sawa na kilo90 za samadi ya ngombe,mbuzi kwa wiki 2 (yaani baada ya wiki 2 unaondoa mbolea na kujiandaa kwa kuweka nyingine tena).

Utajua kuwa bwawa lako lina chakula cha asili kwa kuangalia rangi ya kijani ndani ya bwawa lako kwakuwa wewe unahitaji kujua zaidi ya perege na kambare basi uwe na subira watakuja wadau.
 
Mfano mtu mwenye kufanyakazi ya ufugaji ktk kiwango cha biashara na ana chakula kizuri kama pellet au punje za chakula kilichotengenez wa rasmi kwa ajili ya samaki, unaweza kumshauri aweke samaki 4 kwa mita 1 ya mraba na hivyo bwawa la 900 m2 kama hili unaweka samaki 900 x 4 = 3,600 kujumlisha tahadhari ya 5% ambao ni sawana samaki 180.

Nichangie kidogo hapo pekundu, ni kweli inatakiwa samaki 4 kwa kila kila mita ya mraba iwapo tu, moja umefuga samaki wa jinsia moja kwa maana idadi yao haitaongezeka au umefuga kambale, kambale hawazaliani ktk mazingira ambayo sio ya kiasili. Sato wanaweza kuanza kuzaana baada ya siku 90, je kanuni ya samaki 4 kwa kila mita ya mraba itafanya kazi?

Nadhani tujaribu kufuga hata samaki wengine walioko ktk mazingira yetu,tatizo la jamii zingine za samaki ni namna ya kupata mbegu, kwa mfano wewe uko hapo moro, je waweza kupata mbegu ya kitoga, au mkunga? na walio pale mafinga mnaweza kupata mbegu ya black bassa ( spelling) pale Igowole na tukawafuga. Black bassa wanazaliana vizuri na wanakuwa haraka sana, ni wa maji baridi.

Nenda hapo FAO Kinguruila kawaone watalaam ili wakupe ujuzi bure bila urasimu.
 
Habari za leo wana JF
naomba msaada kwa anaefuga ama kujua ufugaji wa samaki maji baridi.
Na uandaaji wa mabwawa unakuwaje?
asanteni sana
 
Habari za leo wana JF
naomba msaada kwa anaefuga ama kujua ufugaji wa samaki maji baridi.
Na uandaaji wa mabwawa unakuwaje?
asanteni sana

Mkuu Strawberry, samaki maarufu sana wa maji baridi wanaofugwa hapa Tanzania ni Sato (Tilapia).
Labda, kwa kuanzia, hebu angalia article hii naona itafaa kuwa mwongozo wa mwanzo katika azma yako hii.
 

Attachments

  • Tilapia Fish_Farming (TZ).pdf
    1.8 MB · Views: 1,411
Habari za leo wana JF
naomba msaada kwa anaefuga ama kujua ufugaji wa samaki maji baridi.
Na uandaaji wa mabwawa unakuwaje?
asanteni sana

Strawberry, mimi ni mdau wa ufugaji samaki, nafuga samaki sato.
Nina bwawa dogo, nimefuga sato tangu mwanzoni mwa mwaka jana.
Samaki wangu wanaendela vizuri sana.

Kwa utaalamu zaidi wa ufugaji sato, angalia document hii hapa.
Tupo pamoja katika ufugaji sato.
 

Attachments

  • Tilapia Fish Farming.doc
    88 KB · Views: 1,187
Asante sasa ndugu yangu jamani wewe uo wapi?
kama ni dar naomba unikaribishe nije kutembelea bwawa lako.
 
Mkuu Strawberry, samaki maarufu sana wa maji baridi wanaofugwa hapa Tanzania ni Sato (Tilapia).
Labda, kwa kuanzia, hebu angalia article hii naona itafaa kuwa mwongozo wa mwanzo katika azma yako hii.

Kweli kabisa,

Ila avumaye ni Sato lakini African cat fish wapo, na hata wild african cat fish wanafugwa.
 
Kweli kabisa,

Ila avumaye ni Sato lakini African cat fish wapo, na hata wild african cat fish wanafugwa.

Hawa cat fish nasikia kuwa hawazaliani kirahisi kwenye bwawa. Sasa kuna mbinu gani za kuwafanya wazaliane wakiwa kwenye bwawa ?
Pia kuna samaki wanaitwa 'kitoga', hawa pia ni jamii ya cat fish ?
 
Hawa cat fish nasikia kuwa hawazaliani kirahisi kwenye bwawa. Sasa kuna mbinu gani za kuwafanya wazaliane wakiwa kwenye bwawa ?
Pia kuna samaki wanaitwa 'kitoga', hawa pia ni jamii ya cat fish ?

Kwenye bwawa la kujenga kama haya yetu hawazaliani, lakini ktk bwawa la asili wanazaliana sana. Nimewakamata cat fish watoto toka ktk vidimbwi kando ya mto na nimeviweka pamoja ktk bwawa ili nione kama hawatazaliana. Hiki kibwawa kinazidi kupata uasili fulani kwa sababu sitaki kukitibua kabisa ili nione haya maneno kama ni kweli.

Kitoga wapo zaidi Morogoro, sina hakika kama generation ni moja, pia kuna samaki anaitwa Mjonga, huyu hupatikana Kilombero huko Moro pekee duniani. Tatizo hawa samaki ( kitoga, mjonga,mkunga na wengine wa asili ni) wagumu kufugika na kuzaliana. Majaribio yanaendelea juu ya samaki aitwae black basa ( spelling sijui), huyu anazaliana na growth rate ni kubwa, ni wa maji baridi, anafugwa sana Igowole Mufindi, alitokea Songea ni mtamu sana.
 
Habari wanaJF
Naombeni msaada wa ushauri na maelezo ya kina juu ya ufugaji wa samaki kwa yeyote anayejua kuhusu hili.
1.Ningependa kujua kiasi/mtaji wa kuanza nao.
2.Ni aina gani ya samaki wanalipa wakifugwa.
3.Upatikanaji wa mbegu au samaki wenyewe.
4.Ujenzi wa mabwawa
 
Kwenye bwawa la kujenga kama haya yetu hawazaliani, lakini ktk bwawa la asili wanazaliana sana. Nimewakamata cat fish watoto toka ktk vidimbwi kando ya mto na nimeviweka pamoja ktk bwawa ili nione kama hawatazaliana. Hiki kibwawa kinazidi kupata uasili fulani kwa sababu sitaki kukitibua kabisa ili nione haya maneno kama ni kweli.

Kitoga wapo zaidi Morogoro, sina hakika kama generation ni moja, pia kuna samaki anaitwa Mjonga, huyu hupatikana Kilombero huko Moro pekee duniani. Tatizo hawa samaki ( kitoga, mjonga,mkunga na wengine wa asili ni) wagumu kufugika na kuzaliana. Majaribio yanaendelea juu ya samaki aitwae black basa ( spelling sijui), huyu anazaliana na growth rate ni kubwa, ni wa maji baridi, anafugwa sana Igowole Mufindi, alitokea Songea ni mtamu sana.

Kuna jamaa huko south america wanafuga tilapia kwa kuchanganya maji baridi na maji ya bahari (fresh water and sea water) !!!
Wanasema kuwa kwa kuchanganya maji hayo, tilapia wanatoka 'mchicha' wakiwa na 'unique taste' !!!
Wazalisha tilapia kwa large scale na kuuza Marekani na Ulaya.
Huu ndio ufugaji samaki wa ukweli !!

Angalia hapa: Welcome | Tropical Aquaculture Products
 
Back
Top Bottom