Ufugaji wa ng'ombe wa maziwa; ushauri wa kitalaam, changamoto, mawazo na masoko

salmin siraj

Senior Member
Oct 10, 2017
198
204
1681032715619.png

Habari zenu ndugu zangu wajf leo nimeamua kuanzisha hii thread inayohusu ufugaji wa ng'ombe wa kisasa /maziwa kwa minajiri ya kujaribu kusolve changamoto mbalimbali zinazowakumba wafugaji wa sector hii kupitia uzoefu wangu mashambani na shuleni (SUA) hivo karibuni tusharee mawazo tupate kujifunza njia na namna tofauti ya kuzitatua hizi changamoto kitaalamuna kiasili ili ufugaji huu uweze kua yenye tija kwetu na jamii kiujumla.

Tuanze mwanzo kabisa kujua aina ya ng'ombe wa maziwa na sifa zake mbalimbali.

Friesian
Sifa
-Hawa ni wale wenye rangi meusi na nyeupe (rangi yeyote inaweza kutawala kuliko nyingine).
-Wana maumbo makubwa kuliko aina (breed) nyingine.
-Wanasifa ya kuwa na uwezo wa kutoa maziwa mengi kuliko aina nyingine zote za ng'mbe wa kisasa.
-Kutokana na kua na umbo kubwa wanafaa pia kutumika kama ngombe wa nyama.

Changamoto
-Sio wastahimilivu wa magonjwa hasa magonjwa ya kupe na ndorobo.
-Wanamahitaji makubwa ya chakula kutokana na kua na uzito mkubwa .
-Sio wastahimilivu kwenye mazingira ya joto sababu ni rangi nyeusi inaakisi joto zaid ya rangi nyingine.

Arshire
-Hawa wanamchanganyiko wa rangi nyekundu na nyeupe .
-Wanaumbo la wastani ukilinganisha na friesian (ni wakubwa kuliko aina ya jersey na guernsey.
-Ni wastahimilivu wa mazingira magumu mfano maeneo yenye joto.
-Kinga kwa maginjwa ipo juu ukilinganisha na fresian.
-Pia Wanatoa maziwa mengi yenye wastani asimilia 4% ya fatty(mafuta).

Changamoto
-Wanamatumizi makubwa ya chakula na maji.

Guernsey
-Hawa wanataka kufanana na arshire ila wao wanaumbo madogo na rangi zao ni kama njano hivi au red yenye brown ilochanganyika na rangi nyeupe

Sifa
  • Wanatoa maziwa ya wastani ukilinganisha na arshire na friesian
  • Maziwa yao yana asilimia ya fatty (mafuta ) 4.3%
  • Mahitaji ya chakula ni wastani

Changamoto
- Awatoa kiasi kikubwa cha maziwa kama friesian na arshire

Jersey
  • Sura zao ukiziangalia ni kama dish (sura kama imebonyea) na macho ya prominent (yametoka nje)
  • wanaumbo dogo zaid kuliko aina nyingine.
  • Wanatoa maziwa mazuri zaidi, mazito yenye kiasi kikubwa cha mafuta(fatty 4.8%)
  • wako very fertile (uwezo mkubwa wa kushika mimba na kuzaa kuliko aina nyingine .
  • Wanamature haraka sana (kupevuka).

Changamoto
-Wanatoa kiasi kidogo cha maziwa kuliko aina nyingine za ng'mbe wa waziwa

Aina nyingine zitumikazo ni
1. Brown swiss
2. Mpwapwa breed

Note
Ng'ombe wetu wengi Tanzania ni crossbreed yani ni mchanganyiko wa mbegu za kisasa na kitanzania sio pure breed.
 
Hongera Mkuu kwa maarifa mtambuka yenye mlengo wa kutujenga na kutuongezea maarifa ya ufugaji ws ng'ombe wa maziwa. Sambamba na hilo naomba uongezee uzi huu nyama upande wa soko na gharama za upatikanaji wake na mengineyo yanayoelekeana na hayo.
 
Habari zenu ndugu zangu wajf leo nimeamua kuanzisha hii thread inayohusu ufugaji wa ng'ombe wa kisasa /maziwa kwa minajiri ya kujaribu kusolve changamoto mbalimbali zinazowakumba wafugaji wa sector hii kupitia uzoefu wangu mashambani na shuleni (SUA) hivo karibuni tusharee mawazo tupate kujifunza njia na namna tofauti ya kuzitatua hizi changamoto kitaalamuna kiasili ili ufugaji huu uweze kua yenye tija kwetu na jamii kiujumla.

Tuanze mwanzo kabisa kujua aina ya ng'ombe wa maziwa na sifa zake mbalimbali.

Friesian
Sifa
-Hawa ni wale wenye rangi meusi na nyeupe (rangi yeyote inaweza kutawala kuliko nyingine).
-Wana maumbo makubwa kuliko aina (breed) nyingine.
-Wanasifa ya kuwa na uwezo wa kutoa maziwa mengi kuliko aina nyingine zote za ng'mbe wa kisasa.
-Kutokana na kua na umbo kubwa wanafaa pia kutumika kama ngombe wa nyama.

Changamoto
-Sio wastahimilivu wa magonjwa hasa magonjwa ya kupe na ndorobo.
-Wanamahitaji makubwa ya chakula kutokana na kua na uzito mkubwa .
-Sio wastahimilivu kwenye mazingira ya joto sababu ni rangi nyeusi inaakisi joto zaid ya rangi nyingine.

Arshire
-Hawa wanamchanganyiko wa rangi nyekundu na nyeupe .
-Wanaumbo la wastani ukilinganisha na friesian (ni wakubwa kuliko aina ya jersey na guernsey.
-Ni wastahimilivu wa mazingira magumu mfano maeneo yenye joto.
-Kinga kwa maginjwa ipo juu ukilinganisha na fresian.
-Pia Wanatoa maziwa mengi yenye wastani asimilia 4% ya fatty(mafuta).

Changamoto
-Wanamatumizi makubwa ya chakula na maji.

Guernsey
-Hawa wanataka kufanana na arshire ila wao wanaumbo madogo na rangi zao ni kama njano hivi au red yenye brown ilochanganyika na rangi nyeupe

Sifa
  • Wanatoa maziwa ya wastani ukilinganisha na arshire na friesian
  • Maziwa yao yana asilimia ya fatty (mafuta ) 4.3%
  • Mahitaji ya chakula ni wastani

Changamoto
- Awatoa kiasi kikubwa cha maziwa kama friesian na arshire

Jersey
  • Sura zao ukiziangalia ni kama dish (sura kama imebonyea) na macho ya prominent (yametoka nje)
  • wanaumbo dogo zaid kuliko aina nyingine.
  • Wanatoa maziwa mazuri zaidi, mazito yenye kiasi kikubwa cha mafuta(fatty 4.8%)
  • wako very fertile (uwezo mkubwa wa kushika mimba na kuzaa kuliko aina nyingine .
  • Wanamature haraka sana (kupevuka).

Changamoto
-Wanatoa kiasi kidogo cha maziwa kuliko aina nyingine za ng'mbe wa waziwa

Aina nyingine zitumikazo ni
1. Brown swiss
2. Mpwapwa breed

Note
Ng'ombe wetu wengi Tanzania ni crossbreed yani ni mchanganyiko wa mbegu za kisasa na kitanzania sio pure breed.
Shukran sana kwa elimu iliyonyooka mkuu. Ombi langu ni kama unaweza kuchimba zaidi utupe madini ya BEI ZA MANUNUZI (NDAMA AU MATURE), GHARAMA ZA MATUNZO KWA MWEZI, GHARAMA ZA DAWA NA CHANJO ,

Nakuomba tafadhali. Binafsi niko very very interested na hii industry ya ufugaji wa ngombe wa maziwa, usindikaji wa maziwa na utengenezaji wa jibini (cheese).

Nawasilisha salmin siraj
 
Namba zote wanatumika kwenye free range mkuu .
Kama project yako ni kuzalisha nyama sio maziwa naweza kukushauri fuga hao friesian (weusi na weupe) .wanakua kwa kasi sana kuliko ng'mbe wa asilli. Under good management madume yake yanaweza fikisha zaidi ya 400kg ndani ya 2yrs. Ukuaji wao ni wa haraka wanatoa nyama nzuri pia ila sio wastahimilivu so watahitaji chanjo/dawa zaidi kama dawa za kuogesha/minyoo/chanjo za ndorobo.

Ila kuna breed inaitwa boran hawa ni ng'ombe wa asilia na ni wastahimilivu wa mazingira wanakua haraka pia.
 
Tuelekeze tofauti zao ubira wao katika utoaji wa maziwa na madhaifu yao
Tofauti ni kama nlivoeleza hapo juu mkuu kuna wengine wananature ya kutoa maziwa mepesi mfano hao fresian maziwa yake mepesi yana asilimia za mafuta kwa uchache na wengine mazito /high quality yenye mafuta ya kutosha kama jesrsey ujue mara nyingi ubora wa maziwa unatofautishwa kwa asilimia za mafuta ndo maana hii aina ya ngombe na baadhi ya nchini zinazozalisha jibini au youghurt ni wafugaji wazuri wa jersey sjui nmejibu swali lako mkuu??
 
Shukran sana kwa elimu iliyonyooka mkuu. Ombi langu ni kama unaweza kuchimba zaidi utupe madini ya BEI ZA MANUNUZI (NDAMA AU MATURE), GHARAMA ZA MATUNZO KWA MWEZI, GHARAMA ZA DAWA NA CHANJO ,

Nakuomba tafadhali. Binafsi niko very very interested na hii industry ya ufugaji wa ngombe wa maziwa, usindikaji wa maziwa na utengenezaji wa jibini (cheese).

Nawasilisha salmin siraj
Kwa upande wa bei za manunuzi mkuu inategemea na mahali offcoz ni kwamba bei ya maeneo dar es salaam aiwezi kua sawa na huko mikoani yani zimetofautiana kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine ila wastani wa bei kwa ng'mbe mature 1.5M-3M.ndama pia 1.5 kushuka chini kutegemea na umri wake .

Gharama za matunzo pia zinatofautina na mahali mfano dar es salaam ni kubwa kuliko maeneo mengine kutoka upatikanaji mgumu wa nyasi bei kubwa ya pumba ,mashudu n.k .
Gharama za chakula zinakua 70%-80%

Upande wa tiba hio makadirio yake ni kwa mwaka maana zaid chanjo nyingi ni miezi mitatu na mwaka.mfano kuogesha ni kila baada ya mwezi au week mbili mpaka tatu kutegemea na sehem maana yametofautiana uwepo wa kupe, chanjo ndorobo ,minyoo ni miezi mitatu ila chanjo kama za magonjwa ya kwato na midomo(FMD),ugonjwa wa ngozi (LSD),blucella ,black quarter n.k ni mwaka

Note
project yako aitakiwi kuzidi 5% ya gharama za tiba. Under good management unatazidi kupunguza gharama za matibabu.

Kama unania ya kuanza project hii fuatilia gharama za mahala ulipo kuanzia
-Gharama ya chakula-utamlipa shingapi kwa mwezi mkata nyasi au mchungaji ,pumba kwa kg ,mashudu kwa kg madini na upatikanaji wa maji
-Gharama za ujenzi wa mabanda-mbao sementi ,mabati ,misumali n.k
-Gharama za tiba-dawa za kuogesha chanjo n.k
-Gharama umeme -tanesco au bayogesi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom