Ufahamu kuhusu nyota za angani

Mkuu Kifyatu mi naomba unifafanulie kidogo kuhusu ulimwengu ulivyo,maana tunaambiwa ulimwenguni kuwa hakuna juu wala chini,japo sisi tunaliangalia jua kwa juu,mwezi kwa juu na sayari zote na vikorokoro vyote tunaviangalia kwa juu hapo ndipo ninapotatizwa ufafanuzi tafadhari.
Hakuna juu wala chini. Popote ulipo ule upande unaovutwa na gravity ya dunia ndio chini (kwa sababu vitu vinaanguka kuelekea chini) na ule upande mwengine ndio juu. Mfano, kama kuna watu wawili, mmoja yuko north pole na mwengine yuko south pole. Upande anaouita juu alieko north pole basi utakuwa ni chini kwa alie south pole.

Watu wanavutwa kuelekea katikati ya dunia. Kwa hiyo popote ulipo duniani upande unaoelekea katikati ya dunia ndio chini na ule mwengine ndio juu.
 
Swali ni kwanini jua linapoanza kuchomoza huwa halina mwanga mkali na jinsi linavyozidi ndio mwanga huwa mkali na pia likaanza kuishia huwa linaanza kupungua ule mwanga mkali????
Jua linapotoka au kuzama mionzi ya mwanga wake inagusa dunia katika angle ndogo (karibu na sifuri). Kadri siku inavyoendelea mpaka kufika mchana (saa sita, hasa kama uko karibu na equator) basi hii mionzi inatua ardhini katika angle ya 90 degrees. Sasa, nishati (energy) ya jua inayoangukia duniani inategemea hii angle (tuiite A).

Kwa mfano, kama jua linatoa nishati (tuiite) N kwa ujumla, basi nishati inayobakia ardhini ni N*Sin(A). (Sin(A) ni sine ya angle A.) [Kama hukufanya trigonometry utakuwa hujui sine ni nini. Cha muhimu ni kujua kuwa Sin(0) = 0 na Sin(90) = 1). ] Kwa hiyo asubuhi na jioni wakati hii angle ni karibu na sifuri, nishati ya jua inayotua duniani ni karibu na sifuri wakati mchana - saa sita, nishati yote toka kwenye jua tunaipata.
 
Napenda sana watu wenye fikra tofauti na mimi. Hii ndio njia ninayotumia kujifunza. Nakusubiri.
Asante mkuu, mimi pia napenda challenge na mawazo tofauti kutoka kwa mtu aliye open minded, kama wewe.
1. Uwepo wa Mungu: Sijajuwa tuzungumzie Mungu yupi hapa kwa sababu Miungu ni mingi. Lakini wacha tubase kwenye Mungu wa "wengi", Mungu anayezungumziwa kwenye maandiko ya dini kubwa mbili...yaani Biblia na Qur'an. Ukimsoma Mungu as potrayed in the Bible unapata kwamba sisi binadamu "ametuumba" kwa mfano wake, kwa maana alijiangalia akatuumba, isipokuwa alitunyima mambo ambayo ni makubwa akajibakizia yeye ili aendelee kuwa mkuu pekee. Kwa maana hiyo basi, he is NOT a particle, he is rather a guy, with supernatural powers. Kusema kwamba the "god" particle huenda ni dalili za Mungu ni irrelevant, utakuwa unajaribu kumtengeneza Mungu mwingine tofauti na yeye mwenyewe anavyojitanabahisha au anavyotanabahishwa na mitume yake kwenye vitabu "vyake". Ukisoma maandiko unaona kwamba mungu alikuwa anatokea dhahir mbele ya baadhi ya waja wake, au wakati mwingine kuongea nao kwa sauti tu....thats the God we need to confirm his existence, siyo particle. That God doesn't exist.

2. Spirituality: Umetafsiri neno hili kama hali ya kuwa na "imani" kwamba utafanikiwa. Sijajua kwa nini umetafsiri hivyo, maana kuna neno sahihi zaidi ambalo ni HOPE! Spirituality linatokana na neno "Spirit", ambalo kwa kiswahili linamaanisha Mzimu, as in Holy Spirit, Holy Ghost, yaani kwa kiswahili Mzimu Mtakatifu. Unaponunua ticket ya bahati nasibu una-HOPE kwamba utashinda, ukitaka kuingiza spirituality inamaana uombe mizimu (spirits of all sorts, holy and "unholy").

My take; Ukishakuwa Spiritual inamaana tayari una imani kwa some deity ndani yako, kwamba ukiomba hao/huyo deity anaweza kutenda miujiza. Kusema kwamba wewe ni Agnostic na Spiritual ni lugha laini tu inayotumika ili Atheists wasikushangae na Theists wasikushangae pia. Scientifically God doesn't exist, uzuri wa sayansi ni kwamba kukitokea mtu akaprove kwa credible evidence basi wanasayansi watampigia saluti na kukubali uwepo wa Mungu na goti watapiga ikibidi, na ubaya wa Spiritualism ni kwamba evidence ziko "moyoni" zaidi, yaani mtu hahitaji solid evidence za uwepo wa Mungu, badala yake anahitaji kitabu kimoja tu cha kale atachokisoma kwa msisimko mkubwa...na baada ya hapo hautaweza kumbadili mawazo hata kwa evidence.
Asante.
 
Ukisafiri kwa kasi yoyote ile muda wako unatembea taratibu kuliko sisi tuliokaa. Ukiweza kusafiri katika kasi ya mwanga basi muda wako unasimama. Ni kama uliegandishwa (yaani wenzio wanaendelea kukua lakini wewe unabaki na umri wako uleule). Kwa hiyo kama ukisafiri kwa kasi ya mwanga kwa miaka 50, kwako wewe utakuwa hujabadilika (itakuwa ni kama kufumba na kufumbua) lakini ukisimama (hapa duniani) basi itakuwa ni miaka 50 ya mbele. Uliotuacha hapa duniani tulikuwa tunapwaga tu kama kawaida na tunazeeka lakini wewe ulikuwa umedumaa na umri uleule ulioondokea nao. Hii ndio maana ya kusafiri into the future. Sasa kama kasi yako ni ndogo kuliko ya mwanga basi utazeeka lakini kwa rate ndogo kuliko uliotuacha.

Dhana ni kuwa ukiweza kusafiri kwa kasi kubwa kuliko kasi ya mwanga basi unaweza kurudi into the past. Hii sidhani kama itatokea au kuwezekana.
Subiri kwanza kwahio kama nna miaka ishirini ntarudi nyuma umri niwe mtoto mdogo kabisa?? Mifupa irudi ya kitoto??
 
Swali lako ni fupi lakini naona linahitaji maelezo ya kina kulijibu. Kama kawaida maelezo mengi ya kitaalamu unaweza kuyapata kwenye mitandao. Hapa ngoja nijaribu kueleza kimatumbi.

Sayansi kavu kavu:
Kuna uhusiano wa karibu sana kati ya umeme (electricity au flow of electrons) na smaku (magnetism). Kama ukiwa na smaku yenye nguvu halafu ukaleta charged particles kama protons au electrons basi hizi charged particles zitakamatwa na kubaki katika magnetic field ya hii smaku. Hii, kwa kifupi, ndiyo sayansi ya van Allen belts.

Sayari zenye nguvu za smaku:
Sayari nyingi, kama dunia yetu, zina smaku (magnet) kubwa sana katikati yake (hii husababishwa na chuma kilichoyeyuka ndani ya dunia kwa moto na kuzunguuka kama uji unaochemka kutoka kaskazini kwenda kusini). Hii smaku katikati ya dunia yetu (au sayari nyingine) inaipa dunia mionzi ya smaku (magnetic field) kutoka kasikazini mpaka kusini. Ni hii magnetic field ndiyo inayoweza kutufanya tutumie dira (campus) kujua kaskazini au kusini ni wapi. Ni hii hii magnetic fields ndio inayokamata charged particles angani na kutengeneza hizi van Allen belts.

Van Allen Belt(s):
Jua letu linatoa mionzi na upepo wa hii mionzi (radiations & radiation storms) kuelekea pande zote. Sasa kama ilivyo radi inavyotengeneza plasma (ionized gas - rejea mabandiko kuhusu plasma humu kwenye huu uzi) hii mioinzi kutoka kwenye jua ikifika hapa duniani basi inazaba hewa yetu na hii hewa inakuwa ionized (charged particles kama protons na electons). Huu ukanda wenye hizi charged particles (kuanzia 1,000 mpaka 60,000 km kwenda juu) ndio unaojulikana kama van-Allen belt (uligunduliwa 1958 na mwanasayansi wa kiMarekani mwenye hili jina). Kila sayari yenye ukanda wa mionzi ya smaku (magnetic field) basi utakuwa na hizi van-Allen belts.

Faida /Athari ya hizi van Allen radiation fields.
Sisi hapa duniani tuna bahati sana kuwa na hizi van-Allen belts kwa sababu mionzi mingi ya hatari kwa maisha yetu inamezwa au kuelekezwa kuizunguuka dunia na kuendelea na safari yake nje ya dunia yetu kwa sababu ya hizi van-Allen belts au zones. Tusingekuwa na smaku aridhini na hizi van Allen belts basi hewa yote ingepeperushwa nje ya dunia yetu na huu upepo wa jua na maisha hapa duniani yasingekuwepo kabisa.

Kwa sababu van Allen belt ina charged particles, basi chombo kinachokuwa kwenye hii belt lazima kijikinge (shield) ama sivyo mitambo yao ya ki-elektroniki inaweza kuharibiwa. Kuna wakati hii belt inaweza kukuwa mpaka kufikia orbits za satelite zetu na kuleta madhara. Vyombo vyote vinavyotumwa angani (wanajua uwepo wa huu ukanda hatarishi na) hujikinga ipaswavyo.

I hope hii imesaidia.

Mkuu Kifyatu shukran sana, tuko pamoja .
 
Hakuna juu wala chini. Popote ulipo ule upande unaovutwa na gravity ya dunia ndio chini (kwa sababu vitu vinaanguka kuelekea chini) na ule upande mwengine ndio juu. Mfano, kama kuna watu wawili, mmoja yuko north pole na mwengine yuko south pole. Upande anaouita juu alieko north pole basi utakuwa ni chini kwa alie south pole.

Watu wanavutwa kuelekea katikati ya dunia. Kwa hiyo popote ulipo duniani upande unaoelekea katikati ya dunia ndio chini na ule mwengine ndio juu.
Hapo nimekupata,lakini bado hujaniambia kama hata leo hii tukienda sayari ya Mars kwa mfano je, tukiwa kule nako tutaiangalia Dunia kwa juu kama leo hii tunavyoiangalia sayari ya Mars kwa juu ........???
 
Asante mkuu, mimi pia napenda challenge na mawazo tofauti kutoka kwa mtu aliye open minded, kama wewe.
1. Uwepo wa Mungu: Sijajuwa tuzungumzie Mungu yupi hapa kwa sababu Miungu ni mingi. Lakini wacha tubase kwenye Mungu wa "wengi", Mungu anayezungumziwa kwenye maandiko ya dini kubwa mbili...yaani Biblia na Qur'an. Ukimsoma Mungu as potrayed in the Bible unapata kwamba sisi binadamu "ametuumba" kwa mfano wake, kwa maana alijiangalia akatuumba, isipokuwa alitunyima mambo ambayo ni makubwa akajibakizia yeye ili aendelee kuwa mkuu pekee. Kwa maana hiyo basi, he is NOT a particle, he is rather a guy, with supernatural powers. Kusema kwamba the "god" particle huenda ni dalili za Mungu ni irrelevant, utakuwa unajaribu kumtengeneza Mungu mwingine tofauti na yeye mwenyewe anavyojitanabahisha au anavyotanabahishwa na mitume yake kwenye vitabu "vyake". Ukisoma maandiko unaona kwamba mungu alikuwa anatokea dhahir mbele ya baadhi ya waja wake, au wakati mwingine kuongea nao kwa sauti tu....thats the God we need to confirm his existence, siyo particle. That God doesn't exist.
Hapa hutapata upinzani toka kwangu. Kila dini inaamini kivyake. Dini tatu, yaani Ukristu, Uislamu na Judaism (Abrahamic religions) zinapaswa kuamini Mungu wa aina moja lakini ukiwasikiliza viongozi wa dini hizi wanavyovutia kwao unaweza kufikiri wanaabudu miungu tofauti.

Mimi ni agnostic kwa hiyo sitampinga mtu na imani yake. Nitawasikiliza waumini wa dini zote wakimtafsiri Mungu wao lakini sitatia neno. Imani ni kitu personal sana. Sio busara kumwambia mtu kuwa imani yake ni potofu.

2. Spirituality: Umetafsiri neno hili kama hali ya kuwa na "imani" kwamba utafanikiwa. Sijajua kwa nini umetafsiri hivyo, maana kuna neno sahihi zaidi ambalo ni HOPE! Spirituality linatokana na neno "Spirit", ambalo kwa kiswahili linamaanisha Mzimu, as in Holy Spirit, Holy Ghost, yaani kwa kiswahili Mzimu Mtakatifu. Unaponunua ticket ya bahati nasibu una-HOPE kwamba utashinda, ukitaka kuingiza spirituality inamaana uombe mizimu (spirits of all sorts, holy and "unholy").
Nadhani hatutofautiani hapa. Nimesema kuwa Spirituality ni yale matumaini....... Sasa matumaini ndio HOPE. Unapo-HOPE unamaanisha (intrinsically) kuwa kuna higher power itakayoingilia. Hii higher power inaweza kuwa Mungu, mizimu, maruhani, n.k. Cha muhimu hapa ni kuwa binaadam wote wanayo hii hali ya matumaini (HOPE), hasa wanapokuwa katika matatizo.

My take; Ukishakuwa Spiritual inamaana tayari una imani kwa some deity ndani yako, kwamba ukiomba hao/huyo deity anaweza kutenda miujiza. Kusema kwamba wewe ni Agnostic na Spiritual ni lugha laini tu inayotumika ili Atheists wasikushangae na Theists wasikushangae pia. Scientifically God doesn't exist, uzuri wa sayansi ni kwamba kukitokea mtu akaprove kwa credible evidence basi wanasayansi watampigia saluti na kukubali uwepo wa Mungu na goti watapiga ikibidi, na ubaya wa Spiritualism ni kwamba evidence ziko "moyoni" zaidi, yaani mtu hahitaji solid evidence za uwepo wa Mungu, badala yake anahitaji kitabu kimoja tu cha kale atachokisoma kwa msisimko mkubwa...na baada ya hapo hautaweza kumbadili mawazo hata kwa evidence.
Asante.

Ukiwa spiritual (hopeful) ina maana una imani kuwa kuna higher power (sio lazima awe mungu au deity). Hii ndiyo broader definition ya spirituality. Agnostics are searchers of knowledge. Please do not pigeon hole me into the other two categories.

Scientifically, creation happened (refer to Higgs boson story). Now if only God creates then Higgs boson must be a god-particle because it accomplishes what only God does.

You see, the question of whether or not GOD exists is not resolved by science. What science has done is to prove that some of the things that only God can do (like creation) can actually be explained scientifically. If you already believe in God (Theist) this will be an affirmation that "YOU SEE, WE TOLD YOU THERE IS GOD". If you don't believe in the existence of God (Atheist) then this scientific proof of creation further affirms to you that "YOU DO NOT NEED GOD TO CREATE".

Now probably you understand why I am Agnostic.
 
Hapo nimekupata,lakini bado hujaniambia kama hata leo hii tukienda sayari ya Mars kwa mfano je, tukiwa kule nako tutaiangalia Dunia kwa juu kama leo hii tunavyoiangalia sayari ya Mars kwa juu ........???
Ukiwa Mars basi muelekeo wa katikati ya Mars (center) ndio chini na upande mwengine ndio juu kama hapa duniani. Sasa wakati Mars ikitokea usiku (yaani tunaiona) basi itakuwa juu yetu wakati wa usiku na chini yetu wakati wa mchana. Hivyo hivyo ndivyo itakavyokuwa kama tuko Mars na tunaiangalia dunia yetu.
 
1477634005070.jpg

kuna swali huwa najiulizaga kuhusu hizi black holes kitako chake kipo wapi hasa (bottom yake inaishia wapi)
 
Asante mkuu. Jibu langu litakua refu kidogo. Ni matumaini yangu sitawapoteza watu.

Kwa anaetaka kujua kwa kitaalam zaidi kuhusu Neutrinos anaweza kupata taarifa hizi kwenye internet (search for it). Hapa nitajaribu kuelezea kwa lugha rahisi haya yafuatayo:
  • Neutrino ni nini?
  • Neutrino zinatengenezwaje?
  • Neutrino zina faida gani kwetu?
  • Je neutrino zina madhara kwetu?
Neutrino ni nini?
Tulijifunza kwenye sayansi ya sekondari kuwa atom ina viambata vitatu navyo ni:
  1. Protons (+ve charged na zina uzito),
  2. Neutrons (haina chaji na zina uzito), na
  3. Electrons (-ve charged na karibuni hazina uzito - lakini zinao kidogo).
Ukweli ni kuwa kuna chembe chembe (sub-atomic particles) nyingi zaidi kuliko hizo tatu tulizojufunza.

Neutrino (ziko za aina 3) ni moja ya hizo chembe (sub-atomic particles) ambazo hazina chaji kabisa na uzito wake ni mdogo sana kuliko hata wa electrons (uzito wa neutrino milioni moja ni sawa na uzito wa electron moja).

Neutrino zinatengenezwaje?
Kukiwa tu na mlipuko wa ki-nyuklia (kama vile kwenye jua letu, nyota, super nova, mabomu au mitambo ya nyuklia) basi neutrino zinatengenezwa. Popote pale atom zinapopasuliwa (fission, kama mabomu ya nyuklia) au atom zinapounganishwa (fusion, kama kwenye jua au nyota) basi neutrinos zinatengenezwa. Jua letu linatumwagia neutrino billion 65 kwa sekunde katika kila eneo la sentimita moja ya mraba hapa duniani.

Tofauti na mwanga wa kawaida au hata ultra-violet na X-rays, neutrinos hazizuiwi na chochote kile. Zikitua hapa aridhini basi hupita moja kwa moja mpaka upande wa pili wa dunia kwa kasi ya mwanga na kuendelea. Kwa hiyo hata wewe hivi tunavyosema unalabuliwa na neutrino 65 billion kwa sekunde katika kila eneo la sentimita moja ya mraba ya mwili wako (na hiyo ni kutoka kwenye jua tu - na kuna za ziada kutoka sehemu nyingine).

Usifikirie kuwa usiku utakuwa salama, la hasha. Jua likiwa upande mwengine wa dunia hizo neutrino zake zitapenyeza mpaka upande wa pili ambako ni usiku na kukuzaba tu. We kaa mkao wa kula tu mkuu.

Neutrino zina faida gani kwetu?
Kwa kuwa neutrino hazina chaji basi haziathiriwi na nguvu za smaku (electromagnetic fields). Wakati hatuwezi kutumia mwanga wa kawaida kuchunguza kilichopo ndani ya jua letu au nyota na galaxies nyingine, tunaweza kutumia hizi neutrinos kama kurunzi (tochi) ya kuchungulia pasipoweza kuchungulika kwa sasa. Bado utafiti unaendelea wa kutengenezea hizi kurunzi za neutrinos.

Pia kama hizi kurunzi zitapatikana inawezekana tukaachana na upigwaji picha hatarishi wa matibabu kama vile X-rays, MRI (wanasema sio hatarishi lakini sijui), n.k. na tutumie neutrino-scans badala yake?

Unaona utamu huo mkuu.

Je neutrino zina madhara kwetu?
Hili sina uhakika nalo bado lakini nawaza tu. Kama neutrino nyingi kama hizi zinapita kwenye miili yetu, ya wanyama, miti, na viumbe hai vyote, je inawezekana kutubadilishia (mutations) maumbile ya DNA zetu? Kama ni kweli je tunaweza kutengeneza ngao au mwemvuli (neutrino shields) wa kujikinga nazo?

Sijui, lakini hapa ndio tunapofikia utamu wa sayansi.
mkuu hizi neutrinos zina utofauti gani na photons?
 
Mkuu wa Egypt ya kale kwenye swala la astronomy na hesabu hawa jamaa walikuwa vizuri kuna baadhi hata ya formula za hesabu zina mizizi yake huko.
kwanini egypt ya sasa wasiweze kutengeneza mapyramid kama hayo? ninahisi hiyo kazi haikufanywa na watu wa kawaida
 
Photons ni light particles (chembe chembe za mwanga) na zina electric charge. Neutinos azina electric charge na hazihusiani na mwanga.
sasa mkuu ukiacha hizi kuna zile tatu tulizojifunza ndani ya atom(electon proton neutron) kuna uwezekano yeyote kati ya hizo kutoka au kuwa nje ya atom? ma ka zikiwa nje zinaweza kuleta madhara yeyote
 
sasa mkuu ukiacha hizi kuna zile tatu tulizojifunza ndani ya atom(electon proton neutron) kuna uwezekano yeyote kati ya hizo kutoka au kuwa nje ya atom? ma ka zikiwa nje zinaweza kuleta madhara yeyote
Protons na neutrons zinashikiliwa kwa nguvu kubwa sana (Strong Nuclear Force). Kuzitawanya unahitaji atom iliyo unstable kama za Uranium au plutonium. Hii ndio njia inayotumiwa kutengeneza mabomu ya nyuklia au mitambo ya umeme ya nyuklia.

Electrons, kwa upande mwengine, ni rahisi kuziyumbisha (au kuzipukusa) hasa zile zilizoko kwenye ulingo wa nje wa atom. Radi hufanya hivi kila inapopiga. Huondoa electrons chache kwenye atom (ya Nitrogen, Oxygen au hewa yeyote angani). Radi ikifanya hivi hii hewa inakuwa ionized na inaitwa plasma. Rejea mazungumzo yetu kuhusu plasma.
 
Photons ni light particles (chembe chembe za mwanga) na zina electric charge. Neutrinos azina electric charge na hazihusiani na mwanga.
Mkuu nilikuwa na google Leo lakini cha kushangaza naambiwa kutoka duniani mpk Venus ni mbali zaidi kuliko kutoka duniani mpk kwenye jua hii imekaaje
 
Back
Top Bottom