UDOM kuna tatizo! Ndani ya mwaka mmoja wanafunzi 890 watimuliwa chuo, JK walijua hili?

yeah halafu ni profesa aliyebobea kwenye kiswahili.

mbona mnajadili kwa utani suala nyeti kama hili? Mtu mmoja ajitolee kutoa maelezo ya kina ili rais alipate vizuri. Tuko kwenye wakati wa safisha serikali. Tuko serious na mambo yanayotuharibia hatutaki tena. Huyu mtu hawezi kutajwa kila siku kwamba ni tatizo halafu anaendelea kuwepo kuwa madarakani. Udom ni legacy ya rais kama kuna mtu anaiharibu kwa maslahi binafsi asiachwe hapo tena. Kikwete tembelea udom, tuma watu wako wa usalama, takukuru, polisi na cag kwa pamoja haraka pale kamuondoe huyo kidudu mtu. Hao ndio wanaotuletea shida nchi hii yenye kila neema kadiri ilivyojaliwa na subwana wa taala. Eee mungu umjalie kikwete uwezo wa kumwondoa mlacha. Au mpaka watoto wagomeeee kama madaktari kwa mponda? Au mpaka kamati kuu ya ccm ikushauri? Hapana kikwete inuka chukua hatua dhidi ya kiswahili specialist huyo wa udom.
 
Kumbe ni mtaalamu wa kiswahili tu fujo zote hizi? Kumbe hata 2X2 hawezi kujibu. Angesoma hata Jiografia tu si angesumbua zaidi. Mpeleke Bahrain akawe mkalimani, asaidie kukitangaza Kiswahili. Maprofesa kibao hawana kazi. Kwani Mwakyusa hawezi kuchukua nafasi kama yake. Mlachaaa, Mlachaaa, Mlachaaa, Mlachaaa ndio nani yeye nchi hii?
 
Kwa mlacha hang'oki two week ago Aliwauliza malecture hivi"MMEWAHI KUONA KUKU ANAYEATAMIA ANACHINJWA?" ndiyo sawa na mimi kufukuzwa hapa udom.
 
Shida la chuo chenyewe kilivyo kaa organization ni tatizo wanatumia mfumo wa divide and rule kutoka kozi moja hadi nyingine ni mpaka upande gari

Mie nimeenda pale mashangaa chakula 4,500/= kwa hela gani na wanafunzi wapo kimya mnatarajia nn sie kwetu twala kwa buku tu.

Huyo Mlacha mnamlea wenyewe vichwa vyote hapo mnashindwa kumtia adabu kweli?
 
Prof.Mlacha ni mungu mtu na ni fisadi wa kutupwa A.k.a MCHWA ANAYETAFUNA PESA ZA WANANCHI VIA CHUO.Na akikujua kuwa unamfatilia fahamu kuwa huna tena chuo.Ana mashushu wake wanaojifanya ni wanafunzi wanampelekea taarifa zote.YANI UDOM IMEKUWA NI SEHEMU YENYE UDIKTETA NA UTUMWA WA HALI YA JUU.Tatzo ni huyu MCHWA SHAABAN MLACHA MZEE WA NGELI BUT HANA LOLOTE.J.K asipomtoa huyu mchwa chuo hicho kitabaki majengo tu kwani hata malecturer wapo karibu kugoma kwani hata wao wanafukuzwa na kunyanyaswa kama WATUMWA.Wewe mlacha acha ufisadi unaelekea kubaya!
 
Kamati ya nidhamu ya Udom imeshindwa kuwa na nguvu na imemezwa na Mlacha,kuna kipindi ilesemekana huyu jamaa anapelekwa TCU,kwa mshangao mkumbwa aligoma kuondoka udom na jk akampotezea tu.Kikubwa hawa vijana wanaofukuzwa bila utaratibu ni watanzania tena watanzania maskini waliosoma kwa shida hadi kufikia pale na leo wanapotezewa future.Jk rudisha wanafunzi waliofukuzwa udom hawana hatia,mawazir wako ndio chanzo cha yote yaliyotokea udom,walienda kuwaahidi vijana vitu ambavyo vivitekelezeki na kisha kuingia mtini.Ukweli kuhusu UDOM pinda,shukuru kawambwa na Naibu wake Mlugo wanaujua,Vuhai Nahonda naye anajua alichoahidi Udom.vijana wanateseka nyie munaendelea kula bata.
 
Wanaotarajia kujiunga na vyuo mwaka huu,UDOM Sio sehemu salama hata kidogo.
 
mbona mnajadili kwa utani suala nyeti kama hili? Mtu mmoja ajitolee kutoa maelezo ya kina ili rais alipate vizuri. Tuko kwenye wakati wa safisha serikali. Tuko serious na mambo yanayotuharibia hatutaki tena. Huyu mtu hawezi kutajwa kila siku kwamba ni tatizo halafu anaendelea kuwepo kuwa madarakani. Udom ni legacy ya rais kama kuna mtu anaiharibu kwa maslahi binafsi asiachwe hapo tena. Kikwete tembelea udom, tuma watu wako wa usalama, takukuru, polisi na cag kwa pamoja haraka pale kamuondoe huyo kidudu mtu. Hao ndio wanaotuletea shida nchi hii yenye kila neema kadiri ilivyojaliwa na subwana wa taala. Eee mungu umjalie kikwete uwezo wa kumwondoa mlacha. Au mpaka watoto wagomeeee kama madaktari kwa mponda? Au mpaka kamati kuu ya ccm ikushauri? Hapana kikwete inuka chukua hatua dhidi ya kiswahili specialist huyo wa udom.

Huyo Mlacha ni copy ya kikwete hapo udom. Once alijibrag ati hawezi kuondolewa udom kwa maneno cuz hakuomba kazi bali JK alimbembeleza aje afanye kazi akitokea marekani.
 
Kumbe ni mtaalamu wa kiswahili tu fujo zote hizi? Kumbe hata 2X2 hawezi kujibu. Angesoma hata Jiografia tu si angesumbua zaidi. Mpeleke Bahrain akawe mkalimani, asaidie kukitangaza Kiswahili. Maprofesa kibao hawana kazi. Kwani Mwakyusa hawezi kuchukua nafasi kama yake. Mlachaaa, Mlachaaa, Mlachaaa, Mlachaaa ndio nani yeye nchi hii?

foolish,nani ka kwambia waliosoma Kiswahili hawajui 2x2? Dharau zitakudumbukiza kwenye shimo.
 
foolish,nani ka kwambia waliosoma Kiswahili hawajui 2x2? Dharau zitakudumbukiza kwenye shimo.

mimi nadhani tatizo si kusoma kiswahili,tajadili vitu critical vitakavyosaidia kuondoa tatizo Udom.
 
Udom ni janga la taifa,kwa kipindi kirefu tumekuwa tukifuatilia mambo yanavyoendelea chuo kikuu cha Dodoma(udom),kiukweli chuo hiki kimekuwa kikiendesha kibabe,kisiasa na ni chuo pekee Tanzania ambacho hakifuati haki za binadamu wala maazimio ya kimataifa kuhusiana na haki za wanafunzi na wanataaluma.Katika kipindi cha mwaka mmoja chuo kikuu cha dodoma kimewafukuza wanafunzi wasiopungua 800 bila ya kujitetea.Pale college of humanities and social science wanafunzi 511 walisimamishwa masomo tar 13/06/2011 na hadi hii leo vijana hao hawajarudishwa kuendelea na masomo.Tukijaribu kuangalia muda waliokaa vijana hawa nyumbani ni mwingi sana na wengine wamekata tamaa na hawana tena matumaini ya kuendelea kupata haki yao ya kimsingi ya elimu.Wengi wao wamekuwa waangaikaji mitaani na kwa upande wa akina dada wameamua kuolewa au kujiuza.College ya education wanafunzi 89 wametimuliwa,natural science 108 na infomatics ni wanafunz 66.Mzaz usimpeleke mwanao Udom hapafai kabisa,vijana wanafukuzwa kama mbwa na hakuna wa kuwatetea,wanafukuzwa hata bila kusikilizwa na maamuzi yote yanakuwa influenced na mtu mmoja anayeitwa Shabani Mlacha.vijana wanaosoma udom hivi sasa wamekuwa waoga na hawana ujasiri hata wa kuhoji mambo ya kawaida ambayo wao kama wasomi wana haki na niwajibu wao kuhoji na kudadisi.Kwa udom ikionekana umehoji tu kitu chochote basi unapewa barua ya kufukuzwa chuo. Vijana wanakufa udom na maumivu yao,hali imekuwa mbaya hivi sasa hata wahadhili wanafukuzwa bila utaratibu.Nitaendelea kuwaletea mengi yanayoendelea Udom ili muweze kuepukana na janga hili la taifa.Mh rais Jk tunakuomba uingilie kati suala la Udom vinginevyo taifa litakuwa limekula hasara pale Udom.Tunaomba vijana hawa waliokaa nyumbani kwa muda wa mwaka mzima warudishwe kuendelea na masomo na wahadhili wote waliofukuzwa bila utaratibu wapatiwe haki zao.Mungu ibariki Tanzania.

Poleni sana vijana! ila tatizo lenu hamna kitu cha kuwaunganisha, sisi enzi za ujana wetu tuliunganishwa na jeshi la kujenga taifa (JKT) kama walivyo vijana wa dunia yoote. nyinyi mmetenganishwa na siasa you will hate each other, na hamtakua na umoja wa kutetea haki zenu. polenei sana kwa matatizo yanayo wakabili huko UDOM i hope wahusika watawasoma!
 
Poleni sana vijana! ila tatizo lenu hamna kitu cha kuwaunganisha, sisi enzi za ujana wetu tuliunganishwa na jeshi la kujenga taifa (JKT) kama walivyo vijana wa dunia yoote. nyinyi mmetenganishwa na siasa you will hate each other, na hamtakua na umoja wa kutetea haki zenu. polenei sana kwa matatizo yanayo wakabili huko UDOM i hope wahusika watawasoma!

unadhani nini kinaweza kufanyika?
 
Udom ni chuo safi kilichotokana na serikali safi na kinachoongozwa na watu safi na makini. Kama wewe unaona UDOM sio pazuri ondoka waachie wenye njaa zao wakae. Watu mnaomba kazi Udom mkiwa mikono nyuma mkipewa mnaanza kelele. Kazi ni moja tu. Kuwaondoa wote wenye kelele ambao hata kujenga just CHOO hawawezi kisha wanabeza vya wenzao. Tena mwisho leo nisisikie kelele tutawafuata hukohuko mliko. Mnateswa na njaa zenu na bado hadi mkome. Mlacha ni presidentail appointee hajaandika barua yenye "wako mtiifu" kwa JK kuomba kazi. Mnakaa mnabeza Kiswahili mbona bwana mganga anakuwa waziri wa ulinzi? Acheni wivu nyie kudadadeki. Niwachane nisiwachaneeeeeeeeeeeeeeee....................wachaneeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Matatizo ya UDOM yanayoelezwa hapa ya kuwafukuza wanafunzi na walimu hovyo hovyo tu mimi nayaona kama dalili za nje tu za tatizo la msingi lililopo UDOM na vyuo vyetu vyote vya ndani. Yapo mambo mengi tu ambayo kama mdau wa elimu nikiambiwa yanatokea pale UDOM nawaza hivi sisi kama taifa tunazalisha wasomi wa namna gani? Hivi mnaweza kuamini pale UDOM, chuo kilichoanza miaka mitano hivi iliyopita tayari wanatoa PhD? Na kama vile haitoshi hawatoi PhD katika social sciences tu, ambazo unaweza ukasema kwamba haihitaji investment kubwa sana zaidi ya literature za kutosha na wahadhiri waandamizi katika hizo fani, wanatoa hata PhD kwenye natural sciences (kwenye masomo kama biology, chemistry na biochemistry) fani zinazohitaji si tu wahadhiri waliobobea bali hata maabara za viwango vikubwa sana.

Hata UDSM chuo kikongwe vile bado wanafunzi wanaosoma natural sciences PhD zao zinasuasua sana kumaliza kutokana na tatizo hilo hilo, sembuse UDOM? Siasa zitatumaliza sie wabongo. Hivi mbona tunapenda sifa kuliko ubora wa kweli kwenye elimu?

Napendekeza:
1. Ifike mwisho (of course ili lazima liwe kwenye katiba mpya) uongozi wa vyuo vikuu vya umma kuteuliwa na wanasiasa: Shabani Mlacha hakustahili hata kuwa head of department ya Kiswahili sasa inakuwaje anakuwa bosi wa juu kabisa katika chuo kikuu nchini? Mkandala naye vivyo hivyo. Viongozi wa vyuo lazima wapendekezwe na board za vyuo husika kutokana na CV zao na wateuliwe baada ya kushindanishwa.
2. Ifike wakati waadhiri wa vyuo vikuu wastahili nafasi zao baada ya kupikwa vya kutosha. Na kuajiriwa isiwe kama hisani tu ya kufahamiana. Pale UDOM kuna mchezo huo sana maana kuna wahadhiri wengi waliajiriwa pale kwa sababu ya kufahamiana na Gharib Bilal (VC wa chuo wakati huo) au na kiongozi mwingine wa juu pale. Madhara ya kuajiriwa kwa kufahamiana ni hayo, unaweza kufukuzwa tu hovyo hovyo maana nafasi yako uliipata, si kwa sababu ya CV yako, bali hisani.
3. Wanafunzi haki zao zitapuuzwa kama hawatakuwa na umoja. Wale wanafunzi 800 na ushee waliofukuzwa UDOM wangesharudi kama kunji la uhakika la kushinikiza usimamizi wa haki za wanafunzi waliofukuzwa lingeratibiwa. Si kwa fujo kuvunja vioo vya magari ya watu barabarani au kuandamana maana FFU kazi yao kubwa na kuchinja kuua na kuharibu, bali kimya kimya: mkiwa ndani mabwenini, no student's rights, no classroom sessions. Ndio watawapa summary dismissal, lakini mnakuwa dismissed wote kwa umoja ili mrudishwe chuoni wote kwa pamoja without leaving anyone home. Na please wasiwatishe kwa vimikopo vya loanboard, sisi kaka zenu tunakatwa hela nyingi sana (mimi binafsi nakatwa zaidi ya mshahara wa kima cha chini cha mwalimu wa diploma kila mwezi) kugharimia masomo yenu. Loan ni haki yenu si hisani. Pamoja kama taifa.
 
Hi WANA jf KAMA NI MENGI YAMEONGEWA KUHUSU HUYU BWANA MZEMBE MLACHA TUNAFANYAJE KUMUWAJIBISHA....JAMAA ANA TAWALA KIDIKTETA SANA PALE UDOM MPAKA LEO WANA UDOM HAWAJAPATA BUM WAKATI WALIPASWA KUPATIWA HAKI YAO TAREHE 3/05/2012,HADI LEO HAWAJA SIGN POSHO ZAO WAKATI YEYE KWA WIKI ANAINGIA ZAIDI YA VIKAO 2 NA KIKAO ANALIPWA SI CHINI YA LAKI 3....JAMANI HAYA MAMBO TUNAYOTOA UNAWEZA HISI TUNA MKASHIFU LAKINI NDIO HALI HALISI YA HUYU BWANA,CHUO HAKIFAI TENA LAITI NINGEJUA KAMA NTAKUA KWN HAYA MATATIZO NISINGE CHAGUA UDOM KAMA 1st CHOICE YANGU NA PATA MATESO SANA KAMA SIPO NDANI YA NCHI YANGU......NAOMBA KWA ANAEWEZA KUTUSAIDIA WANA UDOM KUFIKISHA UJUMBE HUU KWA JK AFIKISHE JAMAA HAFAI KABISA....UKIONEKANA KUDAI HAKI YAKO UNAITWA NA KUPEWA BARUA YA SUSPENSION ISIYO NA KIKOMO....NAOMBA WANA JF MTUSAIDIE KWA HILI,HALI ZETU NI MBAYA SANA.
 
Last edited by a moderator:
Udom ni chuo safi kilichotokana na serikali safi na kinachoongozwa na watu safi na makini. Kama wewe unaona UDOM sio pazuri ondoka waachie wenye njaa zao wakae. Watu mnaomba kazi Udom mkiwa mikono nyuma mkipewa mnaanza kelele. Kazi ni moja tu. Kuwaondoa wote wenye kelele ambao hata kujenga just CHOO hawawezi kisha wanabeza vya wenzao. Tena mwisho leo nisisikie kelele tutawafuata hukohuko mliko. Mnateswa na njaa zenu na bado hadi mkome. Mlacha ni presidentail appointee hajaandika barua yenye "wako mtiifu" kwa JK kuomba kazi. Mnakaa mnabeza Kiswahili mbona bwana mganga anakuwa waziri wa ulinzi? Acheni wivu nyie kudadadeki. Niwachane nisiwachaneeeeeeeeeeeeeeee....................wachaneeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Mhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh unatetea uozo loh
 
Back
Top Bottom