Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,148
'Uchuro' waingia CHADEMA
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimedaiwa kulenga kupanga safu mpya ya uongozi ikiongozwa na Freeman Mbowe na kumuingiza aliyewahi kuwa Mbunge wa Bukoba Mjini, Wilfred Lwakatare, kuwa makamu mwenyekiti, na kumn'goa Kabwe Zitto, kwenye nafasi yake ya Naibu Katibu Mkuu.
Hata hivyo, madai hayo yamekanushwa vikali na Mbowe, ambaye mbali na kushangazwa lakini alisisitiza kuwa wanaheshimiana sana na Zitto na kwamba binafsi wala chama hicho hakina mpango wowote wa kumng'oa kwa kuwa bado kinahitaji "Zitto" wengine wengi zaidi.
"Sijapanga safu yoyote ya uongozi, kwenye chama chetu tumekuwa na utamaduni rasmi wa kugombea na kupata uongozi. Najua kwamba kuna mbinu za kila namna kuisambaratisha CHADEMA. Mimi nitakuwa mwendawazimu kama nitakuwa sitambui mchango wa Zitto kwenye chama huwa hatukurupuki tu kugawana vyeo, taratibu zote hufuatwa kwa hiyo si uamuzi wa mwenyekiti.
"Nasema madai hayo hayana msingi wowote na ni jungu la kitoto. Viongozi tutakuwa wendawazimu kama tutakubali CHADEMA iangamizwe kwa majungu, na Watanzania ambao matumaini yao yameelekezwa kwetu hawatatusamehe daima. Zitto ni kamanda wangu, natambua mchango wake kwenye chama na tunamhitaji," alisema Mbowe.
Lwakatare hivi karibuni alihama kutoka Chama Cha Wananchi (CUF) ambako alikuwa Naibu Katibu Mkuu Tanzania Bara, na kujiunga CHADEMA na kushiriki kampeni za chama hicho katika uchaguzi mdogo Jimbo la Biharamulo Magharibi.
Nafasi ya Makamu Mwenyekiti ambayo kwa sasa iko wazi, awali ilikuwa ikishikiliwa na aliyekuwa Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe, aliyefariki dunia kwa ajali ya gari akiwa safarini kutoka Dodoma kuelekea Dar es Salaam.
Inaelezwa kuwa katika safu hiyo mpya anayodaiwa kuipanga Mbowe, John Mnyika ndiye anayaterajiwa kuchukua nafasi ya Kabwe Zitto, ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, huku Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa, akiendelea kuwa Katibu Mkuu.
Kwa mujibu wa habari zilizozagaa ndani na nje ya CHADEMA, uamuzi huo wa kumng'oa Zitto unaelezwa kuwa msingi wake ni kile kinachoelezwa kuwa ni "usumbufu" wa kiongozi huyo dhidi ya viongozi wakuu, akiwamo ya Mbowe.
"Mbowe anapanga kugombea ubunge na kuingia bungeni ikiwezekana kuongoza Kambi ya Upinzani Bungeni na atahakikisha anafanya kazi hiyo kwa nguvu zake zote ili umma umwamini, ataitikisa serikali na mwaka 2015 atashinda urais," inaeleza sehemu ya madai hayo ambayo yamekanushwa vikali na viongozi wote makini wa CHADEMA.
Madai hayo ambayo yameelezwa kuwakera baadhi ya viongozi hao yameelezwa kwamba mkakati mwingine unalenga kuhakikisha Zitto anapotea kwenye ramani ya siasa Tanzania "kwa gharama yoyote kwani ni tatizo."
Kwa upande wake, Zitto alipoulizwa kuhusu yeye kuwania uenyekiti alisema; "Mimi nasema sina mpango wala kufikiria kugombea uenyekiti. CHADEMA kina taratibu nzuri za kuachiana uongozi, ninaamini kama kuna mabadiliko yatakuwa ambayo yataacha chama salama. Mi bado mdogo, sitaki watu wanivurugie na kuvuruga chama. Nina imani na uongozi uliopo wa chama."
Katika hatua nyingine, akizungumzia madai ya kugombea ubunge Mbowe alisema; "Suala muhimu kwa sasa si kufikia nani anagombea ubunge au nani hagombei, jambo la msingi kufahamu kwa sasa ni kwamba CHADEMA tumejipanga kuongeza idadi ya wabunge ili kuipa nguvu zaidi za uamuzi Kambi ya Upinzani Bungeni kama unavyojua mara nyingi wabunge wa CCM wamekuwa wakitumia uchache wa wabunge wa upinzani kupitisha mambo yasiyokuwa na msingi."
Kwa upande wa madai ya kukusudia kuongoza Kambi ya Upinzani Bungeni na baadaye mwaka 2015 kugombea urais alisema; "Hivi mimi nimekuwa mpiga ramli? Na haya majungu yamepangwa kama vile mimi nina mkataba na Mwenyezi Mungu kwamba amenihakikishia kwa asilimia 100 nitakuwa hai hadi wakati huo. Nasema kila hatua ya kupata uongozi, na hasa uongozi wa umma inazo taratibu zake, mimi ni kiongozi mwanademokrasia ninayeheshimu taratibu."
Akizungumzia madai ya hivi karibuni kutoka kwa baadhi ya viongozi wa CUF kwamba CHADEMA ni CCM-B, Mbowe alisema ni utoto kuendesha siasa za kushambuliana kati ya chama kimoja cha upinzani na kingine na kwamba hayuko tayari kuingia katika malumbano ya namna hiyo.
"CHADEMA hatuwezi kuingia kwenye malumbano ya kupotezeana muda kiasi hicho, jukumu letu kubwa ni kutafakari kwa pamoja viongozi na wanachama tunakiandaaje chama chetu kuelekea Uchaguzi Mkuu 2010 kwa mafanikio makubwa katika historia yake nchini," alisema.
Historia ya vyama vya siasa vya upinzani nchini inaonyesha kuwa Chama Cha NCCR-Mageuzi ni chama kilichokuwa na nguvu kubwa za kisiasa mwaka 1995 na kufanikiwa kuwa na idadi kubwa ya wabunge, na kwa sasa chama nguvu hizo zimeshuka na chama hicho hakina mbunge hata mmoja.
Vyama vingine vilivyowahi kupoteza viti vya ubunge kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kushuka kwa nguvu za kisiasa ni pamoja na UDP pamoja na TLP. Kwa sasa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, linaundwa na Kambi ya Upinzani kutoka vyama vitatu, ambavyo ni CUF, CHADEMA na UDP, chenye mbunge mmoja.
Mwandishi Wetu
Julai 29, 2009CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimedaiwa kulenga kupanga safu mpya ya uongozi ikiongozwa na Freeman Mbowe na kumuingiza aliyewahi kuwa Mbunge wa Bukoba Mjini, Wilfred Lwakatare, kuwa makamu mwenyekiti, na kumn'goa Kabwe Zitto, kwenye nafasi yake ya Naibu Katibu Mkuu.
Hata hivyo, madai hayo yamekanushwa vikali na Mbowe, ambaye mbali na kushangazwa lakini alisisitiza kuwa wanaheshimiana sana na Zitto na kwamba binafsi wala chama hicho hakina mpango wowote wa kumng'oa kwa kuwa bado kinahitaji "Zitto" wengine wengi zaidi.
"Sijapanga safu yoyote ya uongozi, kwenye chama chetu tumekuwa na utamaduni rasmi wa kugombea na kupata uongozi. Najua kwamba kuna mbinu za kila namna kuisambaratisha CHADEMA. Mimi nitakuwa mwendawazimu kama nitakuwa sitambui mchango wa Zitto kwenye chama huwa hatukurupuki tu kugawana vyeo, taratibu zote hufuatwa kwa hiyo si uamuzi wa mwenyekiti.
"Nasema madai hayo hayana msingi wowote na ni jungu la kitoto. Viongozi tutakuwa wendawazimu kama tutakubali CHADEMA iangamizwe kwa majungu, na Watanzania ambao matumaini yao yameelekezwa kwetu hawatatusamehe daima. Zitto ni kamanda wangu, natambua mchango wake kwenye chama na tunamhitaji," alisema Mbowe.
Lwakatare hivi karibuni alihama kutoka Chama Cha Wananchi (CUF) ambako alikuwa Naibu Katibu Mkuu Tanzania Bara, na kujiunga CHADEMA na kushiriki kampeni za chama hicho katika uchaguzi mdogo Jimbo la Biharamulo Magharibi.
Nafasi ya Makamu Mwenyekiti ambayo kwa sasa iko wazi, awali ilikuwa ikishikiliwa na aliyekuwa Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe, aliyefariki dunia kwa ajali ya gari akiwa safarini kutoka Dodoma kuelekea Dar es Salaam.
Inaelezwa kuwa katika safu hiyo mpya anayodaiwa kuipanga Mbowe, John Mnyika ndiye anayaterajiwa kuchukua nafasi ya Kabwe Zitto, ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, huku Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa, akiendelea kuwa Katibu Mkuu.
Kwa mujibu wa habari zilizozagaa ndani na nje ya CHADEMA, uamuzi huo wa kumng'oa Zitto unaelezwa kuwa msingi wake ni kile kinachoelezwa kuwa ni "usumbufu" wa kiongozi huyo dhidi ya viongozi wakuu, akiwamo ya Mbowe.
"Mbowe anapanga kugombea ubunge na kuingia bungeni ikiwezekana kuongoza Kambi ya Upinzani Bungeni na atahakikisha anafanya kazi hiyo kwa nguvu zake zote ili umma umwamini, ataitikisa serikali na mwaka 2015 atashinda urais," inaeleza sehemu ya madai hayo ambayo yamekanushwa vikali na viongozi wote makini wa CHADEMA.
Madai hayo ambayo yameelezwa kuwakera baadhi ya viongozi hao yameelezwa kwamba mkakati mwingine unalenga kuhakikisha Zitto anapotea kwenye ramani ya siasa Tanzania "kwa gharama yoyote kwani ni tatizo."
Kwa upande wake, Zitto alipoulizwa kuhusu yeye kuwania uenyekiti alisema; "Mimi nasema sina mpango wala kufikiria kugombea uenyekiti. CHADEMA kina taratibu nzuri za kuachiana uongozi, ninaamini kama kuna mabadiliko yatakuwa ambayo yataacha chama salama. Mi bado mdogo, sitaki watu wanivurugie na kuvuruga chama. Nina imani na uongozi uliopo wa chama."
Katika hatua nyingine, akizungumzia madai ya kugombea ubunge Mbowe alisema; "Suala muhimu kwa sasa si kufikia nani anagombea ubunge au nani hagombei, jambo la msingi kufahamu kwa sasa ni kwamba CHADEMA tumejipanga kuongeza idadi ya wabunge ili kuipa nguvu zaidi za uamuzi Kambi ya Upinzani Bungeni kama unavyojua mara nyingi wabunge wa CCM wamekuwa wakitumia uchache wa wabunge wa upinzani kupitisha mambo yasiyokuwa na msingi."
Kwa upande wa madai ya kukusudia kuongoza Kambi ya Upinzani Bungeni na baadaye mwaka 2015 kugombea urais alisema; "Hivi mimi nimekuwa mpiga ramli? Na haya majungu yamepangwa kama vile mimi nina mkataba na Mwenyezi Mungu kwamba amenihakikishia kwa asilimia 100 nitakuwa hai hadi wakati huo. Nasema kila hatua ya kupata uongozi, na hasa uongozi wa umma inazo taratibu zake, mimi ni kiongozi mwanademokrasia ninayeheshimu taratibu."
Akizungumzia madai ya hivi karibuni kutoka kwa baadhi ya viongozi wa CUF kwamba CHADEMA ni CCM-B, Mbowe alisema ni utoto kuendesha siasa za kushambuliana kati ya chama kimoja cha upinzani na kingine na kwamba hayuko tayari kuingia katika malumbano ya namna hiyo.
"CHADEMA hatuwezi kuingia kwenye malumbano ya kupotezeana muda kiasi hicho, jukumu letu kubwa ni kutafakari kwa pamoja viongozi na wanachama tunakiandaaje chama chetu kuelekea Uchaguzi Mkuu 2010 kwa mafanikio makubwa katika historia yake nchini," alisema.
Historia ya vyama vya siasa vya upinzani nchini inaonyesha kuwa Chama Cha NCCR-Mageuzi ni chama kilichokuwa na nguvu kubwa za kisiasa mwaka 1995 na kufanikiwa kuwa na idadi kubwa ya wabunge, na kwa sasa chama nguvu hizo zimeshuka na chama hicho hakina mbunge hata mmoja.
Vyama vingine vilivyowahi kupoteza viti vya ubunge kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kushuka kwa nguvu za kisiasa ni pamoja na UDP pamoja na TLP. Kwa sasa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, linaundwa na Kambi ya Upinzani kutoka vyama vitatu, ambavyo ni CUF, CHADEMA na UDP, chenye mbunge mmoja.