Uchambuzi wa matokeo ya ufaulu form four 2023 channel ya ITV

proton pump

JF-Expert Member
Apr 30, 2017
5,363
6,903
Mara nyingi nimekua nikiandika hili suala humu kuwa elimu ibadilishwe kwan haifai kabisa. Mwaka huu hawajatangaza shule Bora Wala mwanafunzi Bora.

Wachambuzi wa ITV wengi wametoa mawazo mazuri Sana kama vile;

Kubadilisha lugha ya kufundishia iwe ya Moja kwa Moja kuanzia msingi hadi chuo kikuu. Hapa ni vizuri kwa sababu aliyesoma shule za kiingereza mwanzo mwisho huwezi kumshindanisha na aliyesoma kwa KISWAHILI msingi, halafu Kiingereza sekondari ambaye ndio kwa anapambana kujua lugha kwanza ndio aendelee.

Naunga mkono Tena kwa sababu shule ya mjini huwezi kuishindanisha na ya kule kijijini Monduli ambapo shule Ina walimu wawili na watoto hawana muamko wa elimu, watoto wanatoka mbali, umasikini unawadumaza, japokua hata mjini pia umasikini upo.

Shule binafsi huwezi kuishindanisha na shule za serikali kwa sababu serikalini hakuna vifaa vya kutosha na idadi ya wanafunzi ni wengi kuliko shule binafsi.

Narudi kwa Huyu mchambuzi anayeitwa (BANTE) ajifikirie Sana kuwaita walimu vilaza (mambumbu) huku akijisifia alipata ONE form four, huyu huyu mwalimu aliyemfundisha ndiye aliyemtoa BANTE. Hiyo lugha anayotumia sio nzuri. Kama yeye alifundishwa na mbumbumbu sijui Leo hii angekaa hapo ITV aongee hicho anachozungumza saa hivi.

Hao wanaojiita Tanzania one ni Nini walichobadilisha au jipya lipi wamegundua? Wengi wao ndio wameharibika katika JAMII zetu chunguza vizuri utanijulisha.

Narudia huyu BANTE atafakari anayoyaongea unaweza ukawa na Elimu lakini hujaelimika.
 
Sikuona cha maana walichochambua, walikuwa wanajikanganya tu kwa hoja za hovyo zisizo na mashiko juu ya maboresho ya elimu.

Kuna wengine walijikita kwenye matumizi ya lugha ndiyo chanzo cha ufaulu mbaya, mwingind akawashushia rungu zito walimu kuwa ni mafelia.

Mwingine akaona ufundi wa veta ndiyo suluhisho, kwa kifupi wachangiaji wengi hawana upeo mpana wa namna ya kuboresha matokeo mazuri ya mitihani.

ITV nayo inaokoteza watu wa kujadili masuala ya elimu wasiyokuwa na ujuzi nayo matokeo yake hakuna hoja maridhawa zinazowagusa watunga sera ya elimu pamoja na serikali kwa ujumla
 
Sikuona cha maana walichochambua, walikuwa wanajikanganya tu kwa hoja za hovyo zisizo na mashiko juu ya maboresho ya elimu.

Kuna wengine walijikita kwenye matumizi ya lugha ndiyo chanzo cha ufaulu mbaya, mwingind akawashushia rungu zito walimu kuwa ni mafelia.

Mwingine akaona ufundi wa veta ndiyo suluhisho, kwa kifupi wachangiaji wengi hawana upeo mpana wa namna ya kuboresha matokeo mazuri ya mitihani.

ITV nayo inaokoteza watu wa kujadili masuala ya elimu wasiyokuwa na ujuzi nayo matokeo yake hakuna hoja maridhawa zinazowagusa watunga sera ya elimu pamoja na serikali kwa ujumla
Hao ndio wasomi wenyewe sasa
 
Kwamba ni rahisi kuwabadilisha walimu zaidi ya 200,000 wabadilishe lugha waliyozoea?
Kubadilisha mtaala wa kiingereza ni Rahisi kwani watacopy wa English medium, kwenye suala la walimu mbona wataozea tu, mbona wanaleta vitabu vipya hata mtu kama sio familiar with anakua na experience baada ya mda? Inawezekana tu japo sio overnight
 
mtihani wa mwisho usihukumu hatma ya mtoto, kuwe na mfumo wa assessment ya maendeleo ya mtoto, mtihani wa mwisho uwe ni sehemu tu ya matokeo, kama vyuoni, lugha iwe uniform from chekechea tu university, serikali iwe na mpango serious wa kuboresha mazingira ya kusomea, miundombinu, na waalimu. Uhai wa Taifa ni elimu, kama output ni mambumbumbu tutegemee taifa la hovyo sana.
 
mtihani wa mwisho usihukumu hatma ya mtoto, kuwe na mfumo wa assessment ya maendeleo ya mtoto, mtihani wa mwisho uwe ni sehemu tu ya matokeo, kama vyuoni, lugha iwe uniform from chekechea tu university, serikali iwe na mpango serious wa kuboresha mazingira ya kusomea, miundombinu, na waalimu. Uhai wa Taifa ni elimu, kama output ni mambumbumbu tutegemee taifa la hovyo sana.
Shida wanasiasa wabongo wanaua elimu ili watawale milele, ukitaka kuongoza watu usiwape elimu ifaayo
 
Back
Top Bottom