Ndagullachrles
Member
- Jun 20, 2023
- 55
- 52
Harakati za chini kwa chini za kuwania jimbo la Moshi vijijini zimeanza kwa kasi ya kutisha huku zikizongwa na siasa za kuchafuana kwenye mitandao ya Kijamii.
Mbunge wa Sasa wa jimbo Hilo ,Profesa Patrick Ndakidemi anazongwa na upinzani mkali kutoka kwa makada wenzake ambao wameanza kujijenga kisiasa kuelekea 2025.
Baadhi ya madiwani (CCM)wametangaza wazi wazi kujitenga na mbunge wao hasa wanaotoka jimbo la Moshi Vijijini Hali ambayo inatajwa kuleta mgawanyiko mkubwa.
"Kama chama hakitakemea hii tabia nakuambia 2025 jimbo tunalikowa,haiwezekani huu uasi ndani ya chama uangaliwe bila watu kuchukuliwa hatua"anaonya kada wa CCM.
Kwa upande wake Ndakidemi anakili kuwepo kwa mpasuko huo ambao inadaiwa unafadhiliwa na kigogo mwenye ushawishi mkubwa wa kisiasa katika jimbo Hilo ambaye anadaiwa kuwaweka mfukoni aslimia kubwa ya madiwani.
Anasema ni Bora wenye Nia ya ubunge waache wabunge walioko madarakani watimize majukumu yao ya kuwatumikia wananchi na wakati ukifika nafasi itatolewa kila mwenye Nia achukue fomu",anasema.
Anasema si jambo lenye afya kuanza kuchafuana kwa sababu ya kusaka ubunge na kwamba jambo Hilo halikijengi chama Bali linakibomoa akidai badala ya kuwaza kuwapa watu maendeleo watu wanavurugana wenyewe kwa wenyewe kwa kujitengenezea nafasi.
"Tusubi wakati ufike kila mmoja atoke kuomba nafasi hiii kama viongozi wetu wa chama wanavyosema wapltupe muda wabunge tulioko madarakani tutekeleze majukumu yetu kwani wote ni CCM na tunajenga nyumba moja"anasema.
Mbunge wa Sasa wa jimbo Hilo ,Profesa Patrick Ndakidemi anazongwa na upinzani mkali kutoka kwa makada wenzake ambao wameanza kujijenga kisiasa kuelekea 2025.
Baadhi ya madiwani (CCM)wametangaza wazi wazi kujitenga na mbunge wao hasa wanaotoka jimbo la Moshi Vijijini Hali ambayo inatajwa kuleta mgawanyiko mkubwa.
"Kama chama hakitakemea hii tabia nakuambia 2025 jimbo tunalikowa,haiwezekani huu uasi ndani ya chama uangaliwe bila watu kuchukuliwa hatua"anaonya kada wa CCM.
Kwa upande wake Ndakidemi anakili kuwepo kwa mpasuko huo ambao inadaiwa unafadhiliwa na kigogo mwenye ushawishi mkubwa wa kisiasa katika jimbo Hilo ambaye anadaiwa kuwaweka mfukoni aslimia kubwa ya madiwani.
Anasema ni Bora wenye Nia ya ubunge waache wabunge walioko madarakani watimize majukumu yao ya kuwatumikia wananchi na wakati ukifika nafasi itatolewa kila mwenye Nia achukue fomu",anasema.
Anasema si jambo lenye afya kuanza kuchafuana kwa sababu ya kusaka ubunge na kwamba jambo Hilo halikijengi chama Bali linakibomoa akidai badala ya kuwaza kuwapa watu maendeleo watu wanavurugana wenyewe kwa wenyewe kwa kujitengenezea nafasi.
"Tusubi wakati ufike kila mmoja atoke kuomba nafasi hiii kama viongozi wetu wa chama wanavyosema wapltupe muda wabunge tulioko madarakani tutekeleze majukumu yetu kwani wote ni CCM na tunajenga nyumba moja"anasema.